Uzalendo ni nini?

Uzalendo ni nini?

Kwa upande Fulani nakubaliana na wewe maana jeshi wanafundishwa kulipenda na kulilinda taifa! Na hawashabikii chama chochote (kwa mujibu wa katiba), Uraiani huku mzalendo anatambulikaje?
Wanajeshi wa Tz wengi wana kadi ya ccm.
 
Habari za Jumapili wananchi wenzangu, nimekuwa nikijiuliza maana halisi ya uzalendo.

Tumekuwa tukisikia viongozi mbalimbali wakisisitiza wananchi kuwa wazalendo, na wakati mwingine wakilalamikia kinachoitwa "kupungua kwa uzalendo."

Kwakuwa JF ni home of Great thinkers iwapendeze kunijibu, je uzalendo ni nini haswa?

a) Je, uzalendo ni kuvaa tai yenye bendera ya taifa?
b) Au uzalendo ni kuwa kada wa Chama Cha Mapinduzi?
c) Je, ni mambo yapi hayapaswi kufanywa na mzalendo?
d) Je, mzalendo wa taifa letu ana haki zipi?
e) Au uzalendo ni kuzishabikia timu zetu katika mashindano ya kimataifa?
f) Je, uzalendo wetu unapimwaje?
g) Viongozi wetu wanaohubiri uzalendo, wanakidhi vigezo vya kuitwa wazalendo??

Nawakaribisha nipate kufahamishwa kwa kina maana halisi ya uzalendo na mzalendo.
Tatizo ni kuwa watanzania wengi hatuna tabia ya kupenda kusoma, kudadisi na kutafiti. Uzalendo au mzalendo ni term ambayo iko wazi sana na sidhani hata kama inahitaji mjadala. Ni sawa na mtu aje kuulizia hapa fisadi ni nani. Anyways hapa tupo watu wa backgrounds tofauti hivyo mtu anaweza kuuliza chochote.
 
Kwenye post yangu nimeuliza je kuvaa tai yenye bendera ya Tanzania ni kipimo tosha cha uzalendo?
Una-complicate mambo bure kwa kitu kinachojulika wazi. Kuvaa tai yenye bendera ya Taifa siyo uzalendo.
 
Tatizo ni kuwa watanzania wengi hatuna tabia ya kupenda kusoma, kudadisi na kutafiti. Uzalendo au mzalendo ni term ambayo iko wazi sana na sidhani hata kama inahitaji mjadala. Ni sawa na mtu aje kuulizia hapa fisadi ni nani. Anyways hapa tupo watu wa backgrounds tofauti hivyo mtu anaweza kuuliza chochote.
Mkuu hiyo maana inayosemwa kwenye kamusi unaiona kwa viongozi wetu?
 
Mkuu hiyo maana inayosemwa kwenye kamusi unaiona kwa viongozi wetu?
Najua kabisa unachokoza wajinga fulani ila tatizo ni kuwa walengwa wa mijadala kama hii hupenda sana kupoteza muda wa kujadili mambo mazito kwa kupotosha mambo yaliyo wazi. Hizi ndizo level zao na wakipata mijadala kama hii hupenda sana kupotosha.
 
Habari za Jumapili wananchi wenzangu, nimekuwa nikijiuliza maana halisi ya uzalendo.

Tumekuwa tukisikia viongozi mbalimbali wakisisitiza wananchi kuwa wazalendo, na wakati mwingine wakilalamikia kinachoitwa "kupungua kwa uzalendo."

Kwakuwa JF ni home of Great thinkers iwapendeze kunijibu, je uzalendo ni nini haswa?

a) Je, uzalendo ni kuvaa tai yenye bendera ya taifa?
b) Au uzalendo ni kuwa kada wa Chama Cha Mapinduzi?
c) Je, ni mambo yapi hayapaswi kufanywa na mzalendo?
d) Je, mzalendo wa taifa letu ana haki zipi?
e) Au uzalendo ni kuzishabikia timu zetu katika mashindano ya kimataifa?
f) Je, uzalendo wetu unapimwaje?
g) Viongozi wetu wanaohubiri uzalendo, wanakidhi vigezo vya kuitwa wazalendo??

Nawakaribisha nipate kufahamishwa kwa kina maana halisi ya uzalendo na mzalendo.
Wakati wa utawala wa magufuli/ utawala wa giza na ghiriba palikuwa na kikundi kilichoitwa VIJANA WAZALENDO. ni kama usalama ndani ya Usalama. kiliongozwa na msemaji mkuu wa serikali anaitwa MSIGWA. Kilikuwa pale syansi. Hawa ndiyo walimpa kazi Musiba na wanahusika na kuua na kutesa wwote walioenda kinyume na jiwe
nashangaa kumuona msigwa bado yu serikalini
Ilikuwa ni MIRADI BUBU YA WAZALENDO HAIKUKAGULIWA
 
Back
Top Bottom