Uzalendo ni nini?

Uzalendo ni nini?

Uzalendo ktk taifa hili masikini duniani ni kuishabikia CCM na Rais wao!!
Ni kukubali chochote anenacho mkulu hata kama baada ya mwaka moja inalitia taifa madeni yenye kusababisha umaskini!!
Uzalendo ktk taifa hili fukara ni kusifu na kuabudu
 
Uzalendo maana yake ni Kumwita Mtu Fisadi akiwa Chama Pinzani lakin akijiunga na Chama chako unakanusha kuhusu Ufisadi wa hiyo Mtu ulikuwa ukimtamgaza ni Fisadi
 
"Kuzaliwa Tanzania sio kigezo cha wewe kuwa mzalendo lakini kama uzalendo upo ndani yako huo ndio uzalendo kamili
 
Uzalendo ni kufata katiba na kuilinda,bali kufata amri badala ya katiba huko ni kuliangamiza taifa.
 
Hbr wapendwa
Nimekuwa nikiona jitihada zinazofanyika kurudisha umoja, ushirikiano na upendo miongoni mwa Watanzania na kwa nchi yao.
Ni jambo zuri na lenye kuhitajika sana.Kinachonipa shida ni
Njia tunazozitumia ktk ujenzi mpya wa uzalendo.
Uzalendo ni zao la hamasa.Hamasa hutokana na kujifunza na kutenda.

Hebu Turejee nyuma na kuona jinsi ya hatua za awali za Mwl ktk kujenga uzalendo.
Kwanza
Aliondoa uasili kwa vijana wadogo.
Elimu ilitumika kuwakusanya na kuwajenga ktk maadili ya Taifa. Na ndio sababu ya uwepo wa shule za bweni zilizowakusanya vijana wa maeneo mbalimbali ktk Tanzania na kufunzwa maadili na kuishi pamoja.
Pili
Kufunzwa kazi nje ya masomo. Kama vile ufugaji na kilimo. Hii iliwajenga vijana kwa kuwapa ujuzi na pia kuona kilimo kama sehemu ya maisha.
Tatu
Elimu ya siasa ,maisha halisi na historia za kila eneo zilijadiliwa kwa uhuru na uwazi hivyo vijana waliweza kujua nini Taifa lao lilihitaji kutoka kwao. Liliwapa ujasri wa kujifunza na kujenga hoja zilizozaa wanasiasa kwa asili na sio wababaishaji.
JKT
Baada ya kufunzwa yote,waliwekwa makambini kuivishwa ujasiri ili kuwajengea uwezo wa kujiamini na kusimamia wanachokiamini.
Leo vyote tunaharibu kwa sababu ya pesa lkn tunataka wasanii wawaimbishe watanzania ili wawe wazalendo.
Tujitafakari.
 
Hivi hili neno "Uzalendo" maana yake nini hasa!? Mtu anaweza tu kusema simply "ni mtu kuipenda nchi yake" lakini mtu kuipenda nchi yake maana yake nini hasa?

Je! Hivi tunawezaje kujua na kuwa na uhakika kama mtu anaipenda nchi au haipendi? Lakini kwani hats hivyo tunapaswa kufahamu hilo? Au suala la mtu kuipenda au kutoipenda nchi linabakia kuwa siri yake mwenyewe ndani ya kichwa chake?
 
ni ile hali ya mtu kuipenda na kuithamini nchi yake na kuweka maslahi ya taifa lake mbele.
 
Uzalendo unakuwa mkubwa viongozi wanapounganisha watu na kutekeleza majukumu yao kwa maslahi ya watu.
 
Habari wana JF,

Nimechanganyikiwa hapa na mambo yanayoendelea katika nchi yangu. Naomba nijuzwe maana ya neno uzalendo na yapi ni matendo ya kizalendo.

Asanteni
 
Maana halisi ni mtu kuipenda, kuithamini na kujitoa kwa ajili ya nchi yake.
 
Back
Top Bottom