Uzalendo wa ajabu wa Watanzania: Nchi inatukanwa, Rais anatukanwa, tumenyamaza. Huu ni Uzalendo gani?

Uzalendo wa ajabu wa Watanzania: Nchi inatukanwa, Rais anatukanwa, tumenyamaza. Huu ni Uzalendo gani?

Hoja za huu uzalendo wa ajabu wa baadhi ya Watanzania wenzetu, bado unaendelea, sasa uzalendo huu umehamia Twitter, watu wanafurahia hadi kushangilia wakati siri za ndani kwenu, nyumbani na chumbani kwa baba na mama, zinaanikwa hadharani!.

Baadhi ya siri hizi za taifa letu zinazomwagwa Twitter ni classified information, nyingine ni secrets, na hali hii ikiachwa iendelee hivi hivi inavyoendelea, kuna siku folder la top secrets za ile Idara yetu, zitakujashuka kwenye public domain!, kiti ambacho ni threat to our national security, mfano itokee yule jamaa akute kumbe wale 'jamaa', waliofanya kile kitendo cha lile shambulio, pale 'mahali' ni inside job!, kutakuwa na usalama, amani na utulivu?.

Kitendo cha kupublish taarifa classified information kuhusu nchi yako, hivyo kuzifanya zionekane nje ya nchi, ni uhaini, ila uhaini huu sio wa kusambaza tuu, bali hata wale wanafurahia taarifa hizo, ni kuufurahia uhaini, hivyo huu uhaini wa kufurahia uhaini kwa nchi yako, japo haina any criminal liability lakini it has something to do with uzalendo wako.

Huu ni uzalendo wa aina gani?.
P
Ndugu umekuwaje nowadays tangu uitwe kikaoni na nduGUY asee umekuwa toothless... siri gani hataki zijulikane au hizi za watu kugawama mabilioni ya hela
 
Wengi wanataka uliberali lkn nchi na ccm wanang'ang'ania ujamaa uliopitiliza
Uliberali hats trump hautaki ndiyo maana anahaha lkn Democratic wanafurahi na kutia mafuta kwenye moto

Watz nawe ukiwemo hujui falsafa hizi zinavyofanya kazi ndiyo maana ni rahisi kulaumu

Iliberali ni umungu ( Mungu katika ubinadamu) hivyo haulengi kuumiza wala matokeo Bali chanzo (mfumo ulioleta changamoto iliyopo na sio kumaliza changamoto ktk mifumo ile ile kwani isiloshughulikiwa litarudi kama majani ya shamba yanayowasumbuliwa wakulima> ndago, kidila, lusaragasi nk majina ya kilugha


Wewe na paschall mnataka matokeo ya kuisha tatizo na ndiyo kazi ya wahafidhina na mafashisti

Hata chadema na act si waliberali

Kiufupi tz tunasafari ndefu but paschal atatusaidia na wewe tukiwa mrengo wa kati
Ni kweli CHADEMA siyo liberals ni Social democrats zao la the Paris Commune, lakini wanafuata the NORDIC MODEL.

Liberals pekee hapa nchini walikuwa ni CUF ambao kwa sasa wamepoteza mwelekeo wa kujenga itikadi yao hiyo toka mauaji ya mwaka 2001.

Hakuna popote CHADEMA waliwahi kutangaza itikadi ya uliberali haipo hata kwenye katiba yao itikadi yao imesemwa wazi wazi.

Unajua nini maana ya kuwa social democrats ( Center Party) juu ya haki za watu na sera za kiuchumi.
 
Ndio ujuwe kuwa tumefika kubaya inamaana kwa upeo rahisi wakiusalama yani watanzania wapo tayari kuuza nchi yao ili rais wao auwawe. Kiukweli kabisa tuna hali mbaya sana kama taif nakama tusipo kitokomeza kizazi hiki cha wasio wazalendo usalama wetu upo ktk hatari. Mtu amekuwa na nafasi kubwa ya kitaifa anavujisha siri za taifa kwa kisingizio cha upinzani bado yupo mjini anavuta hewa nakupata kahawa hapana we need to act now. Inatisha ndugu zangu
Endeleeni kutumia risasi kama kwa lissu ndy njia pekee ya kuwafanya watu wawe wazalendo.
Tofauti ya ivo mayalla utapiga kelele sana.
Watendeeni watu iliyo haki yao, watakuwa tu wazalendo.
 
Ongeza mahaba ndugu ipo cku nawe utaonekana tu
Unaju ni hivi..ukweli kabisa kuna tabia za waTanzania wenyewe ambazo ni mbaya sana,mala kadhaa utamsikia mTanzania akisifia vya nje na kuponda vya ndani ya nchi yake,nadhani hua ni kama ujinga tu wa wengi,unaweza sikia mtu akimsifia mtu ilihali yupo huko nje ya mipaka awezavyo tu na hata huyo mtu hamjui wala hajawahi kumsogelea, hapa nchini watu wako tayali kuchafua uongozi ilihali huko huko nje wanakua wanajua wazi Tanzania ina uongozi imara..ni ka tabia tu fulani hivi ka kishenzi,maana ukweli ni kwamba ukitazama viongozi wa hapa Africa ni nani utamlinganisha na JPM? Yamkini wale wa zamani kama kina Nkwame Nkuruma,Patrik Lumumba na mtu kama Ghadafi,na waTanzania hawa hawa wanaona wazi lakini wakikaa tu na watu wa huko nje waponda nchi yao utadhani kuna kitu watalipwa au watabadilika kua watu wa nje, ukiiponda nchi yako nje ya mipaka ni sawa na unajitukana tu wewe mwenyewe, tukiachana na hayo bado ziko tabia nyingi tu..unaweza kua kijiweni unakunywa hata kahawa likapita gari tu kwa mfano zuri zuri hivi na watu wawe wanalijua hilo gari ni la tajiri fulani utaona maneno yanavyosemwa..wataanza kumsema huyo mtu utadhani wanalala nae chumbani kua wanamjua sana,anaweza akapita msichana ukasikia wati wanasema huyo dada kaungua na HIV kitambo,hawajawahi kumpima wala hawamjui,juzi hapa swala la Covid-19 mtu ana idadi ya vifo kwenye kijiwe cha kahawa ilihali hajafiwa na ndugu jamaa wala jirani,ukimbana na maswali anakua mkali anakwambia weww ni CCM. Yani Tanzania MUNGU aiponye tu lakini watu hawa ni tatizo kubwa sana sana. Sielewi tafisiri ya kiswahili vzr kua watu wa hivyo ndiyo wapumbavu,wajinga au wanatakiwa kuitwaje sijui kwa kweli.
 
Wanabodi,

Makala za Kwa Maslahi ya Taifa na Pascal Mayalla.
Naendelea na Makala zangu ziitwazo Kwa Maslahi ya Taifa, ambazo huchapishwa kwenye gazeti la Raia Mwema toleo la kila siku za Jumatatu. Hizi Makala zitafuatiwa na Kipindi cha TV chenye jina hilo hilo ambacho kitaanza kutoka kwenye vituo kadhaa vya TV hivi karibuni baada ya taratibu za udhamini kukamilika, vikiangazia hoja mbalimbali muhimu kwa maslahi ya taifa letu la Tanzania.

Hoja ya Udikiteta Tanzania.
Kwa wiki kadhaa sasa nimekuwa nikijadili hoja ya Udikiteta Tanzania. mada ya leo ni kuhusu uzalendo wa ajabu wa Watanzania kuunyamazia uongo unaoenezwa kimataifa kuhusu huu udikiteta Tanzania. Jee Sisi Watanzania, Tuna Uzalendo Gani Kunyamazia Huu Uongo Unaonezwa Kimataifa Kuwa Rais wa Tanzania ni Dikiteta na Tunatawaliwa Kidikiteta?. Au Kwa Kunyamaza Huku Ndio Kukubali Kwenyewe Kuwa ni Kweli Taifa Letu Tanzania Tuko Kwenye Udikiteta?.

Kama ni Kweli Tanzania Tuna Udikiteta na Sisi Wenyewe Tumeukubali, Kwa Nini Watuingilie?.
Kama ni kweli rais wetu Magufuli anatenda kinyume cha katiba na sheria, na taratibu za kumshughulikia zipo lakini sisi Watanzania wenyewe tumeridhika naye na utendaji wake huo huo, hivyo hivyo anavyotenda iwe kwa kuvunja katiba au kinyume cha sheria, Watanzania wenyewe tumeridhika na kukubali, who the hell is jirani yasiyomhusu, anayekuja kutusemea kwenye media yao kuwa rais wetu amekosea?. Kama wenyewe tumekubali na tumeridhika, huyu jirani anamsemea nani?!. Kwa nini Watanzania tunanyamasia uongo huu?.

Wiki ijayo, nitakuja na set ya maswali kuhusu hoja za udikiteta ambayo nitayaelekeza kwa Waziri wa Sheria na Katiba. Prof. Palamagamba Kabudi.

Jumamosi Njema.

Paskali
Update
Nitauapdate uzi huu kwa michango michache objective.
Hata hiki kinachoendelea sasa kuhusu alipo rais Magufuli na uvumi kuhusu afya yake, sio kitu cha kunyamazia!. Where is responsible journalism?, where is our media?. Kwanini tunanyamaza?.

Paskali
 
Hata hiki kinachoendelea sasa kuhusu alipo rais Magufuli na uvumi kuhusu afya yake, sio kitu cha kunyamazia!. Where is responsible journalism?, where is our media?. Kwanini tunanyamaza?.

Paskali
Wakati tulipoamua kujiimarisha kwenye utamaduni wa ki communist , hukuelewa athari zake Pascal Mayalla ?!. Magazeti, redio na TV vilivyojaribu kuwa fair kwa wananzengo unaviona hewani ?!. Na kama vipo hewani ni kwa fine kubwa. Unakumbuka kisa cha RIP Dr Mengi na dogo Spencer Lameck kupigwa mawe pale Lumumba siku ya kukabidhiwa cheti cha ushindi ?! Ikishakuwa vile ni mwandishi gani, atathubutu kusogeza pua ?!

Wewe mwenyewe ulijaribu kuuliza swali zuri kabisa . Lakini kilichofuata ni tafsiri ya jina lako na kuitwa Dodoma. U communist ni laana duniani . Kwenye u communist tunakuwa na zaidi ya wafalme.
 
Hata hiki kinachoendelea sasa kuhusu alipo rais Magufuli na uvumi kuhusu afya yake, sio kitu cha kunyamazia!. Where is responsible journalism?, where is our media?. Kwanini tunanyamaza?.

Paskali
Paskali, media zinaogopa kufungiwa kwa kuuliza tu wapo alipo mpendwa rais wetu, Mhe.Dr. John Pombe Joseph Magufuli. Imekuwa ni taboo kwa yeyote atakayeuliza ataadhibiwa kwa kuuliza tu. Sisi wananchi wa nchi hii tunataka kujua yupo wapi ili to clear the rumours about his whereabout, it is our core duties and responsibility as responsible citizens of this country to know where is our president and how is faring? Please i am going to start hashtag #Where is our president-TZ.
Tunataka kujua maana tunasikia uvumi kuwa anaumwa, lakini pia kuumwa si kosa la jinai, na siyo taboo, tunataka kujua anaendeleaje? Hiyo siyo privacy...Huyo ni kiongozi wa umma na sisi watanzania wote ni waajiri wake. Tunataka kujua yupo wapi...ni haki yetu, waziri mkuu Majaliwa umekosea, rais ni mwajiriwa wetu ikiwa pamoja na wewe kwani hujui mheshiwa premier kuwa mnalipwa kwa kodi zetu.
#Where is our president-TZ.
 
Nyie mnaokula vizuri na kutembea na magari mazuri ndo kazi yenu hyo!!

Mbona sisi huku mmoja anapigwa marisasi na wengine hawamtetei na ukitaka kufanya hvyo unapigwa burn na polis huo moyo wa kulitetea taifa utatoka wapi!!?

Kama viongozi wetu wanachafuliwa wachafuliwe tuu wataenda kuoga. Sie wavimba macho hatuna hata time nao😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Au nasema uongo ndugu zangu!!?
 
Nyie mnaokula vizuri na kutembea na magari mazuri ndo kazi yenu hyo!!

Mbona sisi huku mmoja anapigwa marisasi na wengine hawamtetei na ukitaka kufanya hvyo unapigwa burn na polis huo moyo wa kulitetea taifa utatoka wapi!!?

Kama viongozi wetu wanachafuliwa wachafuliwe tuu wataenda kuoga. Sie wavimba macho hatuna hata time nao😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂

Au nasema uongo ndugu zangu!!?
Husemi uongo kaka kula tano
 
Yan mtu anadhulumu uchaguzi wa nchi nzima,watu wameuza Mali zao wagombee,wakapiga kampeni, watu wakadamka asubuhi kwenda kupanga mstari kutwa nzima wapo juani ili kupiga kura,halaf mtu mmoja tu akaamue wadhulumiwe haki zao. Leo huyo mtu apatwe na majanga ya dunia watu wafurahi na kumtukana mimi nijitokeze kumkingia kifua kweli!? Uzalendo huo wa kinafiki sina..
 
Mayalla! Sote tunafahamu kilichojiri kwa miaka 6 sasa...

Wewe ni shahidi wa namna ambavyo hadi kampuni yako ilivyopunguza wafanyakazi..

Ni nyakati za viongozi kushuka na kujenga ule mshikamano halisi wa kitanzania...

Ni katika awamu hii unashuhudia kiongozi anasema ubebe msalaba wako umepatwa na janga asili kama tetemeko la ardhi unaambiwa serikali haina shamba na hakuna chakula cha msaada kitaletwa , pia walau kujengewa nyumba zingine..

Ukweli unafahamika haina haja ya kufanya sugar coating kweli ukweli usiopingika chuki hii ilifugwa muda mrefu na isipotafutiwa ufumbuzi itaendelea hata miaka kenda...leo hii tunaombeana kifo ujue tumefika hatua mbaya kama taifa..
 
Back
Top Bottom