Wakuu kifo cha huyo mwanafunzi kimeniuma sana japo hata simfahamu sababu hilo tatizo limeshanikuta.
kilichonifanya niumie zaidi ni maumivu aliyoyapata sababu nayajua nilishayapitia.
Baada ya operation kulazwa siku tano na kuruhusiwa nikasoma discharge form imeandikwa......
A patient suffered from "intestinal obstruction secondary to sigmoid volvulus'' He is doing better, passing slool and He is discharged.
Yaani tatizo langu ilikuwa ni zaidi ya intestinal obstruction(utumbo kujikunja) iyo secondary to sigmoid volvulus (yaani baada ya kujikunja na kuziba, tatizo lika develope utumbo ukavimba mvimbo mkubwa sana)
Madaktari walishangaa wanashangaa imekuwaje nikaweza kuishi na hilo tatizo mpaka lika develope kiasi hicho kumbe bana kilichokuwa kinanisaidia kila siku alfajiri nilikuwa nakimbia cross-country ndo chakula kitapita kwa tabu kwenye iyo brokadge, ndo maana ilikuwa kukata gogo ni mpaka nitoke running.
Siku ya kuugua kila kitu nachokula kina rudi chochote hata maji natapika, nasikia mpwito nikienda toi sikati gogo narudi ndani tumbo linauma kinyama siwezi kutembea wima nimenyooka, urefu wangu ni futi 6 na nchi 3 takini nilikuwa natembea kimo cha futi 3 kupunguza maumivu.
kufupisha nilienda hospitali usiku saa nane, kelele nilizokuwa napiga yaani kila mtu ile hospitali alijua hapo tatizo bado halijajulikana nimepigwa drip tu nasikia maumivu kinyama.
pakakucha maumivu ni makali nikaambia nesi maumivu nayosikia ni makali sana, hee nesi anasema dirisha la dawa bado kufunguliwa nisubili wafungue (hapo nilikuwa na bima ya NHIF) ikabidi dawa ya maumivu ikanunuliwe mtaani ikaletwa nesi akanichoma sindano.
ile sindano sikuisikia wakati anachoma, nikamiuliza tayari ushachoma akasema eeeh maajabu ile sindano ya kutuliza maumivu haikusaidia chochote maumivu ndo yakaongezeka mpaka saa tatu ndo kupelekwa utra sound ndo tatizo kujulikama hapo napiga mwano kinyama.
kule utra sound aliyekuwa ananifanyia examination kwa sababu nimelala sioni kwenye monitor nikamuuliza shida ni nini? akawa anajidai hii mashine mbovu yaani hata haionyeshi vizuri, nikamuambia nilisoma psychology chuo najua unachokifanya wewe nambie tu shida nini mimi naweza ku handle taarifa yoyote lakini hakunambia.
nikarudi wodini nikaambiwa natakiwa nifanyiwe emergency operation, nesi akaja kuniandaa nisaini operation ifanyike, sikuwa na weza ku saini alisaini girlfriend wangu, huyu ndo alienipeleka hospitali baada ya kuona hali yangu sio nzuri kulala geto mwenyewe nilimpigia simu jana yake nilikuwa nae gheto.
nikaandaliwa ule mpira wa mkojo unapitishwa kwenye mashine na nesi mrembo(ila hamfikii shemeji yenu) nmejikaza muda huo sipigi kelele naambiwa pole utapona, kamaliza anasukuma kitanda kwenda theater kuna ka umbali nikashindwa kuvumilia maumivu nilipiga kelele nazani hakuna mtu kwenye ile hospitali aliyewahi kupiga kelele kubwa vile yaani wanaojifungua walikiwa wananiulizia hizo kelele zinatoka wapi?
kule theater nikawekwa kwenye kitanda, nikaunganishwa nyaya nyaya zile, akapachika sindano kwenye kile kidude cha drip nilikiwa nacho mkononi nikalazwa chali pozi nimetanua mikono.
nikamuambia yule jamaa hilo pozi naumia nigeuke akaniruhusu, hapo bado wawengine wanavaa Sergio anasubiriwa, maama ilikuwa emergency halafu ilikuwa jumatano sio siku ya operation maama ile hospitali ni ya wilaya na tu, Operations zote huwa wana zi schedule juma nne na alhamis.
Eeh wana chelewa kuja maumivu makali hapo kile ki sindano sijui cha nini kipo kwenye mkono, yule mwamba alokiweka na yeye yupo. kichwa nikafikiria hiki ki sindano ni cha kunizima nikapata wazo nikipushi nizime maana maumivu ni makali sana, yaani muda huo nilikuwa natamani hata nife,
ite natala kupush dawa yule mwamba aliniona alifoka UNATAKA KUFANYA NINI UTAKUFA halafu akaniweka lile pozi chali bila kujali maumivu ya lile pozi sikujua kilichoendelea tena baada ya masaa mawili na nusu ndo natoka theater.
yale maumivu ya usiku niliongea na maza girlfriend akawa anampa updates, kipindi naenda theater maza akafunga safari kutoka mkoa mwingine maama mimi niko kikazi mkoa mwingine. natoka theater akapewa updates.
nimekuja kushtuka usiku bi mkubwa kashafika, wafanya kazi wenzangu ofisini wapo hawaamini maana jana yake siku niliyoanza kuumwa nilikwepo kazini.
Keshoyake Dr anapita swali ya kwanza kuulizwa "umejampa" nikamwambia ndio akanamia safi hiyo ni hatua nzuri ndo kujua kumbe kujampa ni suala la msingi sana, akanambia unaweza kutembea nikamuambia ndio bas nika natembea mule room napita kwenye korido ila natembea kizombi kuna mtu pembeni yuko standby kunidaka.
Dr alikuja kutoa lile bandage hee kuona mshono mrefu na hivi mimi ni mrefu yaani tumbo lote vertical umeshonwa nyuzi 27, nikawa naogopa kutembea nahisi mshono utafumoka utumbo umwagike kumbe ni kutu ambacho hakiwezekani.
kuruhusiwa nikaenda geto kuuguza mshono hapo, hapo huduma zote kupikiwa chakula, kupelekwa haja ndogo na kubwa, kusafishwa, kubadilishwa nguo kila kitu anafanya yule girlfriend wangu, maza hana kazi alivoona naendelea vizuri na huduma zote napata akanambia hata akiondoka nikamuambia poa akasepa kuendelea na majukumu yake.
Kabla hajaondoka maza alinambia huyu mwanamke wako usimuache nikamuuliza kwa nini hata hakunambia chochote, bas bana niliuguzwa huku nikiwa comfortable nakiri sidhani kama ningekuwa comfortable kama ningeuguzwa na mtu yoyoye mwingine, vuta picha unataka kwenda kukata gogo upekekwe ushikiliwe kwenye kukaa huko chooni umalize umwagiwe maji kujisafisha ufutwe majimaji uvalishwe urudishwe ndani.
Hizo kazi ni mara 100 azifanye mwanamke wako utakiwa comfortable kuliko azifanye mama yako. huwa nawashangaa kataa ndoa hawafikirii siku wakiugua,
Girlfriend wangu kabla ya mimi kuugua nilikuwa nimesha mpaga assignment kibao(bila yeye kujua) za kuwa mke alikuwaga amesha pass hizo assignment sema bado nilikuwa sijatangaza kumuoa. akanipa bonus ambayo sikumuambia maana aliachq kazi alikokuwa anafanya ili aniuguze saivi ni mke wangu halali na tuna watoto.
Kuhusu kutuliza mshono, nilikuwaga sielewi maana yake nilikuwa najua ni msemo tu wa kumwambia mtu atulie, nikajua baada ya kuupata mshono yaani inatakiwa uutulize tena usiwe na haraka utembee kizombi hashwaaa maana ukiutikisa mshono ni hatari,
kuna siku naenda hospita waangalie maendeleo wa mshono, chombo nimepanda dereva akapita kwenye vile vituta vidogovidogo kwa speed grrrriiiiii ebanae ndo nikaelewa maana ya kutuliza mshono.
Samahani kwa hili bandiko refu nimejikuta tu naandika nimemuhurumia sana huyo kijana maumivu aloyapata sababu I felt the same pain.