DOKEZO Uzembe wa Hospitali Kuu ya Mkoa Morogoro umesababisha kifo cha Mwanafunzi wa SUA

DOKEZO Uzembe wa Hospitali Kuu ya Mkoa Morogoro umesababisha kifo cha Mwanafunzi wa SUA

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Wakuu kifo cha huyo mwanafunzi kimeniuma sana japo hata simfahamu sababu hilo tatizo limeshanikuta.

kilichonifanya niumie zaidi ni maumivu aliyoyapata sababu nayajua nilishayapitia.

Baada ya operation kulazwa siku tano na kuruhusiwa nikasoma discharge form imeandikwa......
A patient suffered from "intestinal obstruction secondary to sigmoid volvulus'' He is doing better, passing slool and He is discharged.

Yaani tatizo langu ilikuwa ni zaidi ya intestinal obstruction(utumbo kujikunja) iyo secondary to sigmoid volvulus (yaani baada ya kujikunja na kuziba, tatizo lika develope utumbo ukavimba mvimbo mkubwa sana)

Madaktari walishangaa wanashangaa imekuwaje nikaweza kuishi na hilo tatizo mpaka lika develope kiasi hicho kumbe bana kilichokuwa kinanisaidia kila siku alfajiri nilikuwa nakimbia cross-country ndo chakula kitapita kwa tabu kwenye iyo brokadge, ndo maana ilikuwa kukata gogo ni mpaka nitoke running.

Siku ya kuugua kila kitu nachokula kina rudi chochote hata maji natapika, nasikia mpwito nikienda toi sikati gogo narudi ndani tumbo linauma kinyama siwezi kutembea wima nimenyooka, urefu wangu ni futi 6 na nchi 3 takini nilikuwa natembea kimo cha futi 3 kupunguza maumivu.


kufupisha nilienda hospitali usiku saa nane, kelele nilizokuwa napiga yaani kila mtu ile hospitali alijua hapo tatizo bado halijajulikana nimepigwa drip tu nasikia maumivu kinyama.

pakakucha maumivu ni makali nikaambia nesi maumivu nayosikia ni makali sana, hee nesi anasema dirisha la dawa bado kufunguliwa nisubili wafungue (hapo nilikuwa na bima ya NHIF) ikabidi dawa ya maumivu ikanunuliwe mtaani ikaletwa nesi akanichoma sindano.

ile sindano sikuisikia wakati anachoma, nikamiuliza tayari ushachoma akasema eeeh maajabu ile sindano ya kutuliza maumivu haikusaidia chochote maumivu ndo yakaongezeka mpaka saa tatu ndo kupelekwa utra sound ndo tatizo kujulikama hapo napiga mwano kinyama.

kule utra sound aliyekuwa ananifanyia examination kwa sababu nimelala sioni kwenye monitor nikamuuliza shida ni nini? akawa anajidai hii mashine mbovu yaani hata haionyeshi vizuri, nikamuambia nilisoma psychology chuo najua unachokifanya wewe nambie tu shida nini mimi naweza ku handle taarifa yoyote lakini hakunambia.

nikarudi wodini nikaambiwa natakiwa nifanyiwe emergency operation, nesi akaja kuniandaa nisaini operation ifanyike, sikuwa na weza ku saini alisaini girlfriend wangu, huyu ndo alienipeleka hospitali baada ya kuona hali yangu sio nzuri kulala geto mwenyewe nilimpigia simu jana yake nilikuwa nae gheto.

nikaandaliwa ule mpira wa mkojo unapitishwa kwenye m ashine na nesi mrembo(ila hamfikii shemeji yenu) nmejikaza muda huo sipigi kelele naambiwa pole utapona, kamaliza anasukuma kitanda kwenda theater kuna ka umbali nikashindwa kuvumilia maumivu nilipiga kelele nazani hakuna mtu kwenye ile hospitali aliyewahi kupiga kelele kubwa vile yaani wanaojifungua walikiwa wananiulizia hizo kelele zinatoka wapi?

kule theater nikawekwa kwenye kitanda, nikaunganishwa nyaya nyaya zile, akapachika sindano kwenye kile kidude cha drip nilikiwa nacho mkononi nikalazwa chali pozi nimetanua mikono.

nikamuambia yule jamaa hilo pozi naumia nigeuke akaniruhusu, hapo bado wawengine wanavaa Sergio anasubiriwa, maama ilikuwa emergency halafu ilikuwa jumatano sio siku ya operation maama ile hospitali ni ya wilaya na tu, Operations zote huwa wana zi schedule juma nne na alhamis.

Eeh wana chelewa kuja maumivu makali hapo kile ki sindano sijui cha nini kipo kwenye mkono, yule mwamba alokiweka na yeye yupo. kichwa nikafikiria hiki ki sindano ni cha kunizima nikapata wazo nikipushi nizime maana maumivu ni makali sana, yaani muda huo nilikuwa natamani hata nife,

ite natala kupush dawa yule mwamba aliniona alifoka UNATAKA KUFANYA NINI UTAKUFA halafu akaniweka lile pozi chali bila kujali maumivu ya lile pozi sikujua kilichoendelea tena baada ya masaa mawili na nusu ndo natoka theater.

yale maumivu ya usiku niliongea na maza girlfriend akawa anampa updates, kipindi naenda theater maza akafunga safari kutoka mkoa mwingine maama mimi niko kikazi mkoa mwingine. natoka theater akapewa updates.

nimekuja kushtuka usiku bi mkubwa kashafika, wafanya kazi wenzangu ofisini wapo hawaamini maana jana yake siku niliyoanza kuumwa nilikwepo kazini.

Keshoyake Dr anapita swali ya kwanza kuulizwa "umejampa" nikamwambia ndio akanamia safi hiyo ni hatua nzuri ndo kujua kumbe kujampa ni suala la msingi sana, akanambia unaweza kutembea nikamuambia ndio bas nika natembea mule room napita kwenye korido ila natembea kizombi kuna mtu pembeni yuko standby kunidaka.

Dr alikuja kutoa lile bandage hee kuona mshono mrefu na hivi mimi ni mrefu yaani tumbo lote vertical umeshonwa nyuzi 27, nikawa naogopa kutembea nahisi mshono utafumoka utumbo umwagike kumbe ni kutu ambacho hakiwezekani.

kuruhusiwa nikaenda geto kuuguza mshono hapo, hapo huduma zote kupikiwa chakula, kupelekwa haja ndogo na kubwa, kusafishwa, kubadilishwa nguo kila kitu anafanya yule girlfriend wangu, maza hana kazi alivoona naendelea vizuri na huduma zote napata akanambia hata akiondoka nikamuambia poa akasepa kuendelea na majukumu yake.

Kabla hajaondoka maza alinambia huyu mwanamke wako usimuache nikamuuliza kwa nini hata hakunambia chochote, bas bana niliuguzwa huku nikiwa comfortable nakiri sidhani kama ningekuwa comfortable kama ningeuguzwa na mtu yoyoye mwingine, vuta picha unataka kwenda kukata gogo upekekwe ushikiliwe kwenye kukaa huko chooni umalize umwagiwe maji kujisafisha ufutwe majimaji uvalishwe urudishwe ndani.

Hizo kazi ni mara 100 azifanye mwanamke wako utakiwa comfortable kuliko azifanye mama yako. huwa nawashangaa kataa ndoa hawafikirii siku wakiugua,

Girlfriend wangu kabla ya mimi kuugua nilikuwa nimesha mpaga assignment kibao(bila yeye kujua) za kuwa mke alikuwaga amesha pass hizo assignment sema bado nilikuwa sijatangaza kumuoa. akanipa bonus ambayo sikumuambia maana aliachq kazi alikokuwa anafanya ili aniuguze saivi ni mke wangu halali na tuna watoto.

Kuhusu kutuliza mshono, nilikuwaga sielewi maana yake nilikuwa najua ni msemo tu wa kumwambia mtu atulie, nikajua baada ya kuupata mshono yaani inatakiwa uutulize tena usiwe na haraka utembee kizombi hashwaaa maana ukiutikisa mshono ni hatari,

kuna siku naenda hospita waangalie maendeleo wa mshono, chombo nimepanda dereva akapita kwenye vile vituta vidogovidogo kwa speed grrrriiiiii ebanae ndo nikaelewa maana ya kutuliza mshono.

Samahani kwa hili bandiko refu nimejikuta tu naandika nimemuhurumia sana huyo kijana maumivu aloyapata sababu I felt the same pain.
@kogoshima soma hapa utaelewa kwa lugha ya ki tomaso itakufaa
 
Sijui kwanini wanafunzi pale SUA wanafariki kutokana na hili tatizo kwa wingi haswa third year ambao wanakaribia kumaliza
Kuchunguzwe tatizo nn naongea hivi kwakua ni mhitimu wa hicho chuo na zishatokea izo case wakati nasoma
 
Juzi usiku tulimpeleka hospitali ya Nanguji mwanachuo mwenzetu ambae alizidiwa, wakamfanyia vipimo na kusema utumbo umejikunja hivyo anapaswa kufanyiwa upasuaji kwa haraka, kwa pale gharama zilikuwa ni laki 8 hivyo tukaombwa kupelekwa hospitali ya mkoa kwasababu ya unafuu wa matibabu, tukapewa ambulance ikatupeleka hadi Hospitali Kuu ya mkoa Morogoro, pia tukawasiliana na mama wa mwenzetu nae akaanza safari ya kuja.

Baada ya kufika pale na jinsi situation ilivyokuwa ya dharura lakini tuliambiwa Daktari wa upasuaji hayupo available kwa muda huo kwasababu anahudumia wagonjwa wengine, tulisubiri pale mpaka asubuhi ilipofika na mama wa mwenzetu pia akawa ameshafika, still situation ya kumkosa Daktari ikaendelea, uzuri mama wa mtoto alikua ni Daktari pia hivyo baada ya kuangalia vipimo alivyokuja navyo mwanae kutoka hospitali ya Nanguji vilikuwa very clear kwamba hii ni emergency situation inayopaswa ishughulikiwe kwa haraka zaidi, wao wakazidi kusema Daktari wa upasuaji hayupo available.

Mama wa mwenzetu akaomba apewe room afanye upasuaji mwenyewe, niliondoka nilipoona wanampa vifaa kweli, na hiyo ilikuwa inaelekea jioni sasa, usiku nikampigia yule mama akasema hawakumruhusu na wamemwahidi kesho yake ndio atafanyiwa upasuaji.

Basi nikalala kwa amani nikijua asubuhi mwenzetu atapata huduma, lakini asubuhi nikapokea simu kwamba ndugu yetu, rafiki yetu ameaga dunia.

Kwakweli jambo hili limeniliza sana na nimeshindwa nikalia kimya.

Amefariki tarehe 4/Jul/ 2024 yaan leo.

Siku mbili zote mwenzetu anaishi kwa mateso mpaka umauti wake unamkuta, alikuwa bado wiki moja afanye final exams katika chuo cha SUA na alikuwa mwaka wake wa mwisho, kwakweli imeniuma naomba mpige sauti juu ya hili.

So laki 8 tu ndio mliona nyingi? Umaskiani huu, sativa ame clear juzi bili ya 32mill
 
Kabla ya kulaumu inawezekana madactari wa upasuaji ni wachache sana ...
 
Pole sana kwa msiba.

Sababu za utumbo kujikunja huwa ni nin?
Sio njaa??
 
Ni kweli mkuu lakini kwa issue ya emergency, labda ithibitike kulikuwa na wagonjwa wenye serious case kumzidi.
Nachojiuliza hospital ya mkoa morogoro Nina Imani ina department mbali mbali upande wa tiba Sina uhakika daktar anaefanya upasuaji kwa mama mjamzito (obstetrician) ndio atatakiwa afanye na majukum ya idara ya upasuaji wa mfumo wa chakula (surgical gastroenterology)
Na Sina uhakika na siku mbili mgonjwa asihudimiwe
Pia najiuliza mama yake ambae daktar anakuwaje na fikra za kufanya kazi kwenye taasisi ambayo hayuko authorized
Nina mashaka na taarifa hii japokuwa naumia kwa kumpoteza kijana mwenzangu poleni kwa wafiwa na SUA kwa ujumla
 
So sad,Dunia hii basi tu,binadamu sisi ni tatizo asa nchi zinazoendelea huduma za afya ni tatizo.Huduma zetu za afya bado kabusa Kuna siku mdogo wangu alifanyiwa operation akajifungua salama badae akaanza vimba uso nesi aliyekuwepo hakujali kumwita Dr,Hadi aliponipigia simu kuwa hayupo vizuri na baada ya kwenda kufika na kuanza kufatilia kwa jaziba Kali na maneno juu Ndo akafanyiwa maana nilianzia ofisi za wakubwa zao kwa jaziba Kali Ndo akauduniwa haraka sana.Watoa huduma wetu wabadilike Dunia ni mapito watende wema.Pole sana wafiwa ndugu jamaa na marafiki.RIP
 
Wakuu, Umasikini ni laana kabisa imagine watu wameshindwa kutoa 800k mtu afanyiwe upasuaji Private, Apumzike kwa Amani
 
Wakuu, Umasikini ni laana kabisa imagine watu wameshindwa kutoa 800k mtu afanyiwe upasuaji Private, Apumzike kwa Amani
Na huyo et n mtoto wa daktar na mwanafunzi wa chuo anakuwa na bima kuna vitu nashindwa kuvielewa kwa kweli nahisi mtoa taarifa kuna mahali anatupanga
 
Juzi usiku tulimpeleka hospitali ya Nanguji mwanachuo mwenzetu ambae alizidiwa, wakamfanyia vipimo na kusema utumbo umejikunja hivyo anapaswa kufanyiwa upasuaji kwa haraka, kwa pale gharama zilikuwa ni laki 8 hivyo tukaombwa kupelekwa hospitali ya mkoa kwasababu ya unafuu wa matibabu, tukapewa ambulance ikatupeleka hadi Hospitali Kuu ya mkoa Morogoro, pia tukawasiliana na mama wa mwenzetu nae akaanza safari ya kuja.

Baada ya kufika pale na jinsi situation ilivyokuwa ya dharura lakini tuliambiwa Daktari wa upasuaji hayupo available kwa muda huo kwasababu anahudumia wagonjwa wengine, tulisubiri pale mpaka asubuhi ilipofika na mama wa mwenzetu pia akawa ameshafika, still situation ya kumkosa Daktari ikaendelea, uzuri mama wa mtoto alikua ni Daktari pia hivyo baada ya kuangalia vipimo alivyokuja navyo mwanae kutoka hospitali ya Nanguji vilikuwa very clear kwamba hii ni emergency situation inayopaswa ishughulikiwe kwa haraka zaidi, wao wakazidi kusema Daktari wa upasuaji hayupo available.

Mama wa mwenzetu akaomba apewe room afanye upasuaji mwenyewe, niliondoka nilipoona wanampa vifaa kweli, na hiyo ilikuwa inaelekea jioni sasa, usiku nikampigia yule mama akasema hawakumruhusu na wamemwahidi kesho yake ndio atafanyiwa upasuaji.

Basi nikalala kwa amani nikijua asubuhi mwenzetu atapata huduma, lakini asubuhi nikapokea simu kwamba ndugu yetu, rafiki yetu ameaga dunia.

Kwakweli jambo hili limeniliza sana na nimeshindwa nikalia kimya.

Amefariki tarehe 4/Jul/ 2024 yaan leo.

Siku mbili zote mwenzetu anaishi kwa mateso mpaka umauti wake unamkuta, alikuwa bado wiki moja afanye final exams katika chuo cha SUA na alikuwa mwaka wake wa mwisho, kwakweli imeniuma naomba mpige sauti juu ya hili.

CCM CCM na hapo Chuoni utakuta kutwa nzima mnakimbizana na tshirt za CCM, hakuna tatizo jingine zaidi ya CCM na endeleenu kuwa wajinga hapo chuoni na kujipendekeza kwao.
 
So sad,Dunia hii basi tu,binadamu sisi ni tatizo asa nchi zinazoendelea huduma za afya ni tatizo.Huduma zetu za afya bado kabusa Kuna siku mdogo wangu alifanyiwa operation akajifungua salama badae akaanza vimba uso nesi aliyekuwepo hakujali kumwita Dr,Hadi aliponipigia simu kuwa hayupo vizuri na baada ya kwenda kufika na kuanza kufatilia kwa jaziba Kali na maneno juu Ndo akafanyiwa maana nilianzia ofisi za wakubwa zao kwa jaziba Kali Ndo akauduniwa haraka sana.Watoa huduma wetu wabadilike Dunia ni mapito watende wema.Pole sana wafiwa ndugu jamaa na marafiki.RIP
Sio nchi zinazo endelea sema CCM, shida ni CCM na tuendele kuwaabudu tu
 
Wakuu, Umasikini ni laana kabisa imagine watu wameshindwa kutoa 800k mtu afanyiwe upasuaji Private, Apumzike kwa Amani
Hio ni Hospitali ya Umma wanapaswa kumtibu mgonjwa then gharama baadse. Nyie ni Ma.ta.ko sana, huduma za mzingi na za haki mnataka zipigiwe magoti? Hio hispitali inaendeshwa kwa pesa za CCM au kodi zetu? Wewe ni moja ya wajinga wa hili taifa katika asilimia 90 ya wajinga na weww umo.

Nyie ndio wale mnao nunua haki zenu za msingi.
 
Na huyo et n mtoto wa daktar na mwanafunzi wa chuo anakuwa na bima kuna vitu nashindwa kuvielewa kwa kweli nahisi mtoa taarifa kuna mahali anatupanga
Haijalishi, kwani hio hospitali ni ya Private? si inaendeshwa kwa kodi za raia? Wewe naye ni mpumbavu sana, hio ni haki ya msingi, Hispitali inaendeshwa kwa kodi zetu.Matibabu ni haki ya msingi, walipaswa jutibu mgonjwa wakati anapata nafuu waulize gharama.

Mawazo kama yako watawala wakiyasoma wanafurahi sana kuona ni kiwango gani wanaongoza Mapimbi
 
Wakuu, Umasikini ni laana kabisa imagine watu wameshindwa kutoa 800k mtu afanyiwe upasuaji Private, Apumzike kwa Amani
Coment yako watawala wakiisoma wanagonga glass za wine kwa kufurahia ni kiwango gani wanatawala watu wajinga sana katika nchi hii.
 
Hivi ni kweli kwamba mlikosa laki nane wanachuo wote kuchangishana tu mlishindwa jamani
 
Juzi usiku tulimpeleka hospitali ya Nanguji mwanachuo mwenzetu ambae alizidiwa, wakamfanyia vipimo na kusema utumbo umejikunja hivyo anapaswa kufanyiwa upasuaji kwa haraka, kwa pale gharama zilikuwa ni laki 8 hivyo tukaombwa kupelekwa hospitali ya mkoa kwasababu ya unafuu wa matibabu, tukapewa ambulance ikatupeleka hadi Hospitali Kuu ya mkoa Morogoro, pia tukawasiliana na mama wa mwenzetu nae akaanza safari ya kuja.

Baada ya kufika pale na jinsi situation ilivyokuwa ya dharura lakini tuliambiwa Daktari wa upasuaji hayupo available kwa muda huo kwasababu anahudumia wagonjwa wengine, tulisubiri pale mpaka asubuhi ilipofika na mama wa mwenzetu pia akawa ameshafika, still situation ya kumkosa Daktari ikaendelea, uzuri mama wa mtoto alikua ni Daktari pia hivyo baada ya kuangalia vipimo alivyokuja navyo mwanae kutoka hospitali ya Nanguji vilikuwa very clear kwamba hii ni emergency situation inayopaswa ishughulikiwe kwa haraka zaidi, wao wakazidi kusema Daktari wa upasuaji hayupo available.

Mama wa mwenzetu akaomba apewe room afanye upasuaji mwenyewe, niliondoka nilipoona wanampa vifaa kweli, na hiyo ilikuwa inaelekea jioni sasa, usiku nikampigia yule mama akasema hawakumruhusu na wamemwahidi kesho yake ndio atafanyiwa upasuaji.

Basi nikalala kwa amani nikijua asubuhi mwenzetu atapata huduma, lakini asubuhi nikapokea simu kwamba ndugu yetu, rafiki yetu ameaga dunia.

Kwakweli jambo hili limeniliza sana na nimeshindwa nikalia kimya.

Amefariki tarehe 4/Jul/ 2024 yaan leo.

Siku mbili zote mwenzetu anaishi kwa mateso mpaka umauti wake unamkuta, alikuwa bado wiki moja afanye final exams katika chuo cha SUA na alikuwa mwaka wake wa mwisho, kwakweli imeniuma naomba mpige sauti juu ya hili.


So sad,Mungu ampumzishe mahala pema peponi.Amina!
 
Haijalishi, kwani hio hospitali ni ya Private? si inaendeshwa kwa kodi za raia? Wewe naye ni mpumbavu sana, hio ni haki ya msingi, Hispitali inaendeshwa kwa kodi zetu.Matibabu ni haki ya msingi, walipaswa jutibu mgonjwa wakati anapata nafuu waulize gharama.

Mawazo kama yako watawala wakiyasoma wanafurahi sana kuona ni kiwango gani wanaongoza Mapimbi
Elewa nilichoandika acha kutumia mihemko mzee rudia tena kusoma
Nb. D mbili muhim
 
Back
Top Bottom