Uzi maalum kwa wale wanaomuamini Mungu muumba

Uzi maalum kwa wale wanaomuamini Mungu muumba

Je, huoni Ulimwengu huu Mkubwa na yaliyomo katika mbingu na ardhi?!

-Je, umefikiria hata siku moja kuhusu Uumbaji wa mbingu na yaliyomo katika sayari?!

-Je, hukuwahi kuwa na mazingatio katika ardhi ile na vilivyomo ndani yake katika mito, bahari, mabonde na milima?!

-Je, uratibu huu uliopangwa vizuri kwa ubunifu na ufanisi wa hali ya juu haujakufurahisha?.

-Je, ni nani aliyeumba Ulimwengu huu na ukawa katika hali hii ya ubunifu wa hali ya juu iliyopangiliwa kwa mpangilio wa juu kabisa na kupambwa katika umbile hili lenye muujiza kiasi cha kuwa ni alama na ishara ya ukamilifu, na katika isiyokuwa na mfano uliotangulia?!

-Je, ameiumba nafsi yake?! Au katika Ulimwengu huu kuna Muumba mwenye uwezo? Allah amesema: “Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili, Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa mbingu na ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabu ya Moto.” (3:190-191).
 
Mtoa mada hongera sana kwa uchambuzi wako mzuri sana.....huu uchambuzi kibinadamu umeweza kukupa uelekeo wa uwepo wa Mungu je ukiingia kiroho itakuwaje?
"Nyani Ngabu,
Nimesoma comment yako naomba nikusaidie ufahamu kidogo kuhusu huyu Mungu anaetajwa na tunaemwamini kwa ajili ya utukufu wake,
Nilichoona kwako unamtaka Mungu katika flesh yani kama unavyomuona Nyani Ngabu ndivyo unataka umuone Mungu hakika kwa aina hiyo hutamuona Mungu kwa sababu Mungu ni roho, tokea msingi wa kuumbwa kwa ulimwengu huu roho ya Mungu na neno ndiyo iliyoyafanya haya tuyaonayo na kuyabeza.....soma Mwanzo 1:2 nanukuu "Nayo nchi ilikuwa ukiwa tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.3 Mungu akasema iwe nuru ikawa nuru" ukiendelea utaona vile uumbaji ulivyoendelea hapa nilitaka kukuonyesha tu kwamba Mungu ni roho.

Ili umwelewe Mungu na matendo yake unahitaji kumtafuta kwa roho...Soma Yohana 4:24 Mungu ni roho nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli, kweli ambayo ni neno lake.

Mapungufu uliyosema ya Mungu sijayaona ila mapungufu ni yakwetu sisi wanadamu kwa kuliacha pendo lake na kuasi. Utaniuliza kwa nini sasa Mungu aumbe mwanadamu ambaye atamuasi. Kwanza ufahamu kwamba Mungu hakuanza kuwepo baada ya kuumbwa kwa dunia la hasha... Mungu alikuwepo kabla hata dunia haijaumbwa, ukisoma Mwanzo Hiyo hiyo Mwanzo 1:26 Inasema Natumfanye mtu kwa Mfano wetu......naomba uchukue neno wetu alafu ujiulize kwanini wetu na si wangu? Neno la pili ni Mfano linamaana gani kwa nini si kama mimi? Hii inadhihirisha sisi ni kama kopi ya Mungu na neno wetu inadhihirisha kwamba mbinguni walikuwepo zaidi ya maelfu ya malaika wake ambao ndio alisaidiana nao katika uumbaji. Kama ningetumia tafsiri nyingine ningesema Mungu ndo alikuwa Engineer mkuu na maelfu au mabilioni ya malaika wake walikuwa kama wasaidizi. Inaonyesha ni kiasi gani Mungu ana uwezo na nguvu kusimamia mradi mkubwa namna hii design na kumpliment project kubwa hivi si kazi ndogo ilikuwa ni day and night mpk siku ya saba ndipo alipopumzika ebu kuweni na adabu kidogo mumheshimu na mumpe sifa zake Mungu mimi nitakupa sifa zote kwa ukuu wako mana hata Nyani Ngabu ni kazi yako iliyonjema sana. Uumbaji wa Mungu si sawa na hivi Viproject vyetu ambavyo hata wakati mwingine tunashindwa kudeliver matokeo mazuri. Hii mada ni pana sana natamani kushare nanyie kwa kadri Mungu atakavyonijalia sema sijui kufungua uzi niwe mkweli najua nijamaliza kujibu maswali yako naomba niendelee kukujibu kidogo kidogo ili nisiharibu uzi wa mwenzangu barikiwa sana.
 
Bujibuji hata kwenye ndoto ulinikimbia ulivyoona indian shape flat screen yangu
Mi mwenzako naogopa TV za chogo, mambo yangu mi flat screen. Ila kibabu cha Tegeta Masaiti kilinizidi spidi, halafu siku hizi JOHN WALKER zake kinanywea kwenye uvungu wa Kabati la chumbani kwenu. Asprin nakuangalia kwa jicho kali, weee poa tu
 
MUNGU yupo ,Aliyekuumba bila ww kutaka,ila kumrudia ni Hiyari yako au kinyume chake.
Matatizo wanayulalamika Mengi tumeyatengeneza ss Wanadamu

Ukitoka nje ya mstari unakutana na Adhabu.
Mungu yupo na shetani yupo wote tumeona kazi zao

MUNGU yupo,yupo,yupo ,yu Hai.Alitenda na anatenda mpaka milele.Hana mwanzo wala mwisho pia na matendo yake vivyo hivyo.
 
Mi mwenzako naogopa TV za chogo, mambo yangu mi flat screen. Ila kibabu cha Tegeta Masaiti kilinizidi spidi, halafu siku hizi JOHN WALKER zake kinanywea kwenye uvungu wa Kabati la chumbani kwenu. Asprin nakuangalia kwa jicho kali, weee poa tu
We dawa yako ni kukuchukulia mchepuko wako tu...

Ntaanza na Halima wa Family Bar... jana niligundua hajafunga ramadhani
 
Bujibuji hata kwenye ndoto ulinikimbia ulivyoona indian shape flat screen yangu
Huu wivu sijui niufanyeje...

dbsf.jpg
 
Mungu muweza wa yote, mwenye mapenzi kemkem, aliyepo mahali kote kwa wakati wote, na tararira zingine kama hizo, mpaka hivi sasa mungu huyo hakuna ushahidi wa uwepo wake.

Hilo mkubali mkatae, ndo ukweli wenyewe huo.

Huyo mungu mnayedai yupo anafeli mitihani midogo na myepesi sana ya maswali ya kawaida kabisa.

Jana/ leo imeletwa habari humu kuwa kuna mchungaji huko Ethiopia kauliwa na mamba ziwani alikokuwa anawabatiza sijui waumini wake wale.

Huyo mchungaji alikuwepo hapo ziwani akifanya kazi ya ki-mungu. Na nadhani ni haki nikimuita huyo mchungaji kuwa ni 'wakala' wa mungu.

Sasa huyo mungu alikuwa wapi kumnusuru kifo huyo 'wakala' wake? Iweje huyo mungu akampa akili na uwezo huyo mamba wa kumshambulia huyo 'wakala' wake huko ziwani hadi kumuua?

Sijawahi hata kuparuriwa na paka lakini nadhani kung'atwa na mamba hadi ufe kunauma kweli kweli.

Huyo mungu alishindwa nini kumnusuru huyo 'wakala' wake kuepuka hayo maumivu?

Ukweli ni kwamba mpaka hivi sasa hakuna ushahidi wa huyo mungu. Kilichopo ni mambo ya kufikirika tu, au waweza kuyaita 'imani'.

Kwa hiyo, kwangu mimi, mpaka hivi sasa huyo mungu ni kiumbe msasili [mythical figure].

Hakuna ushahidi unaothibitisha, unaotosha, na unaohitimisha kuhusu uwepo wake.
Kama huamini uwepo WAKE si mahali pako hapa.
 
Back
Top Bottom