Uzi maalum kwa wale wanaopinga uwepo wa Mungu

Uzi maalum kwa wale wanaopinga uwepo wa Mungu

Uyo Mungu, yupo kwenye imagination zetu tu, lakin hayupo... Na kama mnasema yupo, ni Mungu gani uyo ambae yupo, Mungu wa waislam, yaweh, Zeus Mungu wa wagiriki au Warumbe na mkisi Mungu wa Waganda, au yule wa wahindu. Miungu wapo wengi Sana Dunia hii, unatuaminishaje kwamba wako ndo sahihi?
 
Safi kabisa, Dunia inazunguka jua Kwa kasi ya karibu km 1000 Kwa saa ! Ni maajabu hayo MUNGU YUPO
Hii inaitwa Logical non sequitur.

Unaunganisha vitu viwili tofauti visivyo na uhusiano wowote ule kuunda hitimisho potofu.

Hujathibitisha Mungu huyo yupo, Unarukia kusema kuzunguka kwa Jua ni maajabu ya Mungu.

Huyo Mungu ni nini? Thibitisha kwanza uwepo wake.

Jua lipo na linathibitishika lipo.
 
Pia haijalishi ni wangapi wanaamini uwepo wa huyo Mungu, Bado Mungu huyo hayupo na wala hajawahi kuwepo kujidhihirisha mwenyewe kwamba yupo.

Mnahangaika sana kumwelezea na kumuongelea huyo Mungu kwa vile Hayupo, hajawahi kuwepo na hatawahi kuwepo kujiongelea, kujidhihirisha na kujitetea mwenyewe.
Sawa mkuu
 
Kama Mungu angekuwepo, kusengukuwepo Shetani, Mungu muweza wa yote na mjuvi wa vyote alimuumba vipi Shetani? Utagundua concept ya Shetani ilikopiwa na wakristo kutoka katika dini za dualism ambapo huwa Kuna miungu wawili, mmoja wa wema mwingine wa mabaya... Hii ilifanyika baada ya watu kuwa wanjiulza kama Mungu yupo kwanini Kuna mema na mabaya, ndo ukristo ukaanzisha iyo concept ya Shetani baadae, na ndo maana kwenye agano la kale hakuna sehemu Shetani ametajwa, alikuja kutajwa kwenye agano jipya kwenye biblia
 
Uwepo wa vita, magonjwa umaskini vinathibitisha kuwa uyo Mungu muwezo wa yote na mwenye upendo hayupo, kama aliweza kuumba ulimwengu kwa kutamka... Anashindwa nn kutamka na vta, magonjwa na umaskini vikaisha
Hawa watu waamini Mungu ukiwauliza maswali kama haya wanajifanya kama vile hawayaoni.

Wanapita na ku view Kimya Kimya.
 
Mi nachoweza tu kusema ni kua kwa tulipofikia, binadamu hana limit tena ya ufikiriaji. Ni eidha tu labda kitokee kitu ambacho hakijawai kuonekana kabisa ndo watu wanaweza shindwa kukielewa ila baada ya muda kitachunguzwa na majibu yatapatikana.
vitu ni vingi mno ambavyo sio vipya ni vya zamani na havielezeki kisayansi

miaka na miaka watakwambia "this is a subject of ongoing research"

mfano kitu cha kawaida tu kwa maelfu ya miaka wanajiuliza namna ya kuzuia binadamu asizeeke

lakini bado akili hijafikia hapo

labda kuna kuna kipindi watafanikiwa

ila ni vitu vingi ambavyo sio vipya na vinakosa majibu ya kisayansi kwa miaka na miaka
 
Kuna Mungu wa aina mbili kwa watu wanaoamini dini, Mungu wa kwanza, uyu ni yule ambae haonekani, huwez kumskia Wala kumshika, na watu wa dini wanakuwa wanjanja baada ya hapo, Wana Mungu wa aina ya pili, uyu tunamjua vizuri sana kupita maelezo, Ni Mungu mwenye hasira, tunajua anapenda tufanye nn na tusifanye nn, tuvae nn na tule nn na tusinywe nn. Sasa jiulize ni Mungu gani mnaesema yupo? Huyu ambae hatumjui? Au yule ambae tunajua kila ktu kuhusu yy. Mwisho wa siku kiuhalisia Mungu hayupo na hajawah kuwepo
 
Hii inaitwa Logical non sequitur.

Unaunganisha vitu viwili tofauti visivyo na uhusiano wowote ule kuunda hitimisho potofu.

Hujathibitisha Mungu huyo yupo, Unarukia kusema kuzunguka kwa Jua ni maajabu ya Mungu.

Huyo Mungu ni nini? Thibitisha kwanza uwepo wake.

Jua lipo na linathibitishika lipo.
Sitaki kujidai kwamba namjua saana MUNGU, wewe unamjua MUNGU kuliko hata Mimi, lakini ninachojua nikwamba MUNGU ANATHIBITISHWA KWA MATENDO YAKE MAKUU, UKIFUNUA TU BIBLIA UNAKUTANA NA MWANZO 1:1 INasema "HAPO MWANZO MUNGU ALIZIUMBA MBINGU NA NCHI......" Mimi najua yupo.....
 
Ukipinga uwepo wa Mungu au shetani inabidi usiamini katika dhana ya ubaya wa jambo lolote au uzuri wa jambo lolote kwa sababu kama uwepo wa Mungu na shetani ni myth basi kudhani jambo fulani ni baya au zuri ni myth, kudhani kwamba ukiua mtu ni jambo baya hiyo ni upotofu maana sababu inayotufanya tusiuane na kama nikileta sababu zangu za kuua inabidi zikubaliwe na ukipinga hizo ni shida zako sio zangu kwa kuwa siamini kama kuua ni jambo baya regardless sababu au bila sababu
Hii hoja yako yaweza kua debated na hoja kutoka kwenye Society formation.

Mojawapo ni kwamba jamii kuundwa ilitokea makubaliano ambayo jamii inasurrender haki zao zote isipokua ya kuishi. In return authority itaoffer protection kwa jamii.

Kisha authority itatengeneza taratibu na sheria ambazo zitakua ndiyo miongozo.

Hivyo basi, watu hatuui kwa sababu authority ishaonyesha ukiua na wewe utauawa. Zikaundwa mpaka mahakama kufanya huu uamuzi.

Hivyo kabla kabisa binadamu hajaletewa dini alikua na authority.
 
Uwepo wa vita, magonjwa umaskini vinathibitisha kuwa uyo Mungu muwezo wa yote na mwenye upendo hayupo, kama aliweza kuumba ulimwengu kwa kutamka... Anashindwa nn kutamka na vta, magonjwa na umaskini vikaisha
ulitaka afanye kama unavowaza weww kwamba hivyo vitu visiwepo ndo ijue yupo,

hayo ni matarajio yako tu,
kwamba kwasababu kuna magonjwa vita na umasikini ndo hayupo ?

hivi ni vitu unavyoviona vipo vinakutisha kwasababu ndo top ya vitu vibaya uvijuavyo

je kama kuna namna nyingine kubwa zaidi ameviepusha na ndo maana tupo humu kila siku kwa ma milioni ya miaka ?

hivyo vitu vimewai kuimaliza dunia ikaisha

ndo maana kwenye bandiko ni kua akili ya binadamu inategemea sana experience vitu ulivyoona na kusikia

umesikia njaa, mafuriko vita magonjwa, umeona ndo vikubwa kuliko vyote

hatuna experience na vikubwa ambavyo vikitokea labda tunaisha wote

ndo maana unasema kwanini magonjwa yapo.

swali: magonjwa yapo na hivyo vitu vyote tangu zamani lakini mbona tuna survive, na dunia imekwepo kwa miaka mingi sana ?
 
ulitaka afanye kama unavowaza weww kwamba hivyo vitu visiwepo ndo ijue yupo,

hayo ni matarajio yako tu,
kwamba kwasababu kuna magonjwa vita na umasikini ndo hayupo ?

hivi ni vitu unavyoviona vipo vinakutisha kwasababu ndo top ya vitu vibaya uvijuavyo

je kama kuna namna nyingine kubwa zaidi ameviepusha na ndo maana tupo humu kila siku kwa ma milioni ya miaka ?

hivyo vitu vimewai kuimaliza dunia ikaisha

ndo maana kwenye bandiko ni kua akili ya binadamu inategemea sana experience vitu ulivyoona na kusikia

umesikia njaa, mafuriko vita magonjwa, umeona ndo vikubwa kuliko vyote

hatuna experience na vikubwa ambavyo vikitokea labda tunaisha wote

ndo maana unasema kwanini magonjwa yapo.

swali: magonjwa yapo na hivyo vitu vyote tangu zamani lakini mbona tuna survive, na dunia imekwepo kwa miaka mingi sana ?
Kusurvive kwetu hakuhusiani na Mungu, kwenye magonjwa sayansi ya tiba ndo imesaidia kudhibiti magonjwa na sio Mungu. Na ndio maana hata ww ukiugua huendi kanisan Wala msikitini, utaenda hospital kutibiwa..
 
Sitaki kujidai kwamba namjua saana MUNGU, wewe unamjua MUNGU kuliko hata Mimi, lakini ninachojua nikwamba MUNGU ANATHIBITISHWA KWA MATENDO YAKE MAKUU, UKIFUNUA TU BIBLIA UNAKUTANA NA MWANZO 1:1 INasema "HAPO MWANZO MUNGU ALIZIUMBA MBINGU NA NCHI......" Mimi najua yupo.....
Hujui Mungu yupo bali una amini tu yupo kwa vile umekuta na umeaminishwa Mungu yupo.

Ungekuwa unajua Mungu yupo ungeweza kumthibitisha yupo na wala usinge hitaji imani ya kujua kwamba Mungu yupo.

Biblia kusema Mungu yupo ni hadithi za kutungwa sawa na hadithi za uwepo wa Dragons 🐉 watemao moto midomoni mwao ambapo kiuhalisia sio kweli.
 
Imagination ndo sifa kubwa iliyoweza kututofautisha na viumbe wengne, na kutufanya tuitawale Dunia, na tuwe na uwezo wa kuingamiza pia. Mwanadamu pekee kati ya wanyama wote duniani ndio anaweza kuwa na Imagination kali.. mwanadamu anaweza kutengeneza story ambayo sio ya kweli na akaiamini... Hii imesaidia kutufanya tuwe wamoja.. lakini kiuhalisia, hakuna Mungu huko juu Wala hakuna shetani, ni imagination zetu tu. That's why hutaweza kuthibitisha hata siku Moja sababu Mungu, Shetani, malaika, wachawi hawapo.
 
N
Sitatumia maandiko ya Dini Quran wala Bible, labda wataelewa kidogo, maana humu JF nimegundua wapo wengi, unaweza ukajikuta una chati hata na shetani directly, anapotosha

Tuanzie kwenye Civilization na Level ya akili na kufikiri viumbe mbalimbali wapo kwenye level tofauti za civilization na akili. Inaweza kuonekana kupitia namna yao ya maisha.

Mfano Simba wana territory yao wanaweka alama kabisa iwe kuacha kinyesi n.k ila wana mipaka ya utawala na kuna utawala wa simba dume eneo hilo ambapo akiingiliwa na Simba mwingine ambae hakua hapo lazima wapigane vibaya sana hadi moja akubali show.

Tembo pia vilevile kiasi kwamba mwenzao akifa wanahizunika na kuonyesha kuomboleza...

Mchwa pia, wapo wana utawala wao, wana malkia, kuna walinzi kuna wajenzi, na wanajenga haswa, kichuguu kimejengwa kwa ustadi haswa inaonyesha kabisa wana mawasiliano mazuri sana na wanajua wanachokifanya.

Nyuki pia vile vile, wana jenga nyumba yao, sehemu ya kuwekea asali, kuna malkia, kuna wanaolinda eneo, nknk.

Yaani hadi wanavyotengeneza asali kumlinda malkia na kulinda eneo lao, lina onyesha wazi level yao ya kujielewa na level ya mawasiliano ni kubwa kabisa.

wanyama ni wengi ambao tunaweza kuwa tumia kama reference, Sokwe etc.

Hawa viumbe wote, kila mmoja kwa nafasi yake mfano tuchukulie nyuki, wanajiona wana akili(ni kweli wanayo),
wanajiona wanajua mambo mengi na kufikiri logically kwamba huyu ametuchokoza kwaiyo tuji-oganize kushambulia na kujilinda, wanajua kujenga, wanamuheshimu malkia na kumlinda...

ila pia kuna mambo hawajui na hawajui kama hawajui na hawawezi kukuelewa hata ukijaribu kuwaelewesha,
na hautakua hata na intrest ya kuwaelewesha...

Mfano: Je binadamu anaweza kua na interest ya kutaka kumuonyesha nyuki ni jinsi gani binadamu wameendelea kiteknolojia?

Nyuki anaweza kuelewa kwamba binadamu anaweza kuongea na mtu wa marekani kupitia iternet kwamba binadamu anaweza kuwasiliana hivi Jamii Forums kwa id fulani na hawajawai kuonana wala kua na namba ya simu wala kukutana?

Nyuki anaweza kuelewa kwamba hilo bomba linalotoa maji au hiyo taa inayowaka usiku barabarani au nyumbani imetengenezwa na binadamu na sio kwamba ipo tuu... inakazi na bili zinalipwa?

Hayo ni baadhi ya maendeleo ya binadamu na kujaribi kulinganisha uwezo wa akili wa nyuki na binadamu,

Ni dhahiri kwamba hai make sense kwa nyuki, na hatuna interest ya kutaka kumuelewesha

Tumetofautiana kiakili na nyuki kiasi cha kua sisi tunaweza kumuelewa nyuki ila yeye hawezi kutuelewa

Nyuki nae usipo mlinganisha na binadamu, ana akili kubwa tuu na huenda anajiona vilevile binadamu anavyojiona kiakili, na anakiamini kile akili yake inachowaza kumbe ndo akili yake ilipoishia.

Vile vile kwa binadamu anajiona yupo advanced kiakili ambayo ni kweli pia kwa nafasi yake lakini pia na yeye ana limit ambayo akili yake inaishia.

Tunaona tu dunia, jua mwezi, maporomoko na vingine, ni kama tuu nyuki akikutana na taa, bomba la maji, kweli anaona taa inatoa mwanga, bomba linatoa maji...

Ila hajui hasa lile bomba imekuaje lipo pale, au taa imekuaje ipo pale, imewekwa na nani?

Anachojua inatoa mwanga, mechanism nyuma yake je inakuaje inawaka usiku mchana haiwaki? Inakazi gani haswa? Hajui na hana uwezo wa kufatilia kujua.

probably akiona gari anajua ni mojawapo ya viumbe wengine, hajui kama binadamu ndo yupo ndani anaendesha. au anaweza kua analichukulia kwa namna tofauti kabisa. au hata haelewi chochote.

Hiyo ni relation tu ya kuonyesha jinsi akili ya viumbe mbalimbali ina limit yake

Binadamu pia limit ya akili yetu ina limit inapoishia

Mfano ndo unakutana na Mtu anayesema "Mungu Hayupo kwasababu Huwezi kumuona wala kumgusa wala kusikia sauti yake"

Hiyo ni moja wapo ya limit ya akili yetu, ina depend moja kwa moja na milango ya fahamu, masikio macho, pua, ulimi, ngozi...

Anakwambia "jua lili kwepo tuu, na dunia ilikwepo tuu, kwamba kama jua au dunia haiwezekani kuwepo tuu, basi na Mungu hawezekani kuwepo"

Inaonyesha ni jinsi gani akili yetu inafikia limit, kuyaelewa mambo mengine..

Mambo ambayo hatuyajui bado ni mengi ni infinity ♾️, na ningumu hata kuingia akilini haya make sense kwasababu yapo beyond uwezo wa akili.

Kama vilevile tulivyoona kwa mfano wa nyuki, kwamba kumuelezea ha
Sitatumia maandiko ya Dini Quran wala Bible, labda wataelewa kidogo, maana humu JF nimegundua wapo wengi, unaweza ukajikuta una chati hata na shetani directly, anapotosha

Tuanzie kwenye Civilization na Level ya akili na kufikiri viumbe mbalimbali wapo kwenye level tofauti za civilization na akili. Inaweza kuonekana kupitia namna yao ya maisha.

Mfano Simba wana territory yao wanaweka alama kabisa iwe kuacha kinyesi n.k ila wana mipaka ya utawala na kuna utawala wa simba dume eneo hilo ambapo akiingiliwa na Simba mwingine ambae hakua hapo lazima wapigane vibaya sana hadi moja akubali show.

Tembo pia vilevile kiasi kwamba mwenzao akifa wanahizunika na kuonyesha kuomboleza...

Mchwa pia, wapo wana utawala wao, wana malkia, kuna walinzi kuna wajenzi, na wanajenga haswa, kichuguu kimejengwa kwa ustadi haswa inaonyesha kabisa wana mawasiliano mazuri sana na wanajua wanachokifanya.

Nyuki pia vile vile, wana jenga nyumba yao, sehemu ya kuwekea asali, kuna malkia, kuna wanaolinda eneo, nknk.

Yaani hadi wanavyotengeneza asali kumlinda malkia na kulinda eneo lao, lina onyesha wazi level yao ya kujielewa na level ya mawasiliano ni kubwa kabisa.

wanyama ni wengi ambao tunaweza kuwa tumia kama reference, Sokwe etc.

Hawa viumbe wote, kila mmoja kwa nafasi yake mfano tuchukulie nyuki, wanajiona wana akili(ni kweli wanayo),
wanajiona wanajua mambo mengi na kufikiri logically kwamba huyu ametuchokoza kwaiyo tuji-oganize kushambulia na kujilinda, wanajua kujenga, wanamuheshimu malkia na kumlinda...

ila pia kuna mambo hawajui na hawajui kama hawajui na hawawezi kukuelewa hata ukijaribu kuwaelewesha,
na hautakua hata na intrest ya kuwaelewesha...

Mfano: Je binadamu anaweza kua na interest ya kutaka kumuonyesha nyuki ni jinsi gani binadamu wameendelea kiteknolojia?

Nyuki anaweza kuelewa kwamba binadamu anaweza kuongea na mtu wa marekani kupitia iternet kwamba binadamu anaweza kuwasiliana hivi Jamii Forums kwa id fulani na hawajawai kuonana wala kua na namba ya simu wala kukutana?

Nyuki anaweza kuelewa kwamba hilo bomba linalotoa maji au hiyo taa inayowaka usiku barabarani au nyumbani imetengenezwa na binadamu na sio kwamba ipo tuu... inakazi na bili zinalipwa?

Hayo ni baadhi ya maendeleo ya binadamu na kujaribi kulinganisha uwezo wa akili wa nyuki na binadamu,

Ni dhahiri kwamba hai make sense kwa nyuki, na hatuna interest ya kutaka kumuelewesha

Tumetofautiana kiakili na nyuki kiasi cha kua sisi tunaweza kumuelewa nyuki ila yeye hawezi kutuelewa

Nyuki nae usipo mlinganisha na binadamu, ana akili kubwa tuu na huenda anajiona vilevile binadamu anavyojiona kiakili, na anakiamini kile akili yake inachowaza kumbe ndo akili yake ilipoishia.

Vile vile kwa binadamu anajiona yupo advanced kiakili ambayo ni kweli pia kwa nafasi yake lakini pia na yeye ana limit ambayo akili yake inaishia.

Tunaona tu dunia, jua mwezi, maporomoko na vingine, ni kama tuu nyuki akikutana na taa, bomba la maji, kweli anaona taa inatoa mwanga, bomba linatoa maji...

Ila hajui hasa lile bomba imekuaje lipo pale, au taa imekuaje ipo pale, imewekwa na nani?

Anachojua inatoa mwanga, mechanism nyuma yake je inakuaje inawaka usiku mchana haiwaki? Inakazi gani haswa? Hajui na hana uwezo wa kufatilia kujua.

probably akiona gari anajua ni mojawapo ya viumbe wengine, hajui kama binadamu ndo yupo ndani anaendesha. au anaweza kua analichukulia kwa namna tofauti kabisa. au hata haelewi chochote.

Hiyo ni relation tu ya kuonyesha jinsi akili ya viumbe mbalimbali ina limit yake

Binadamu pia limit ya akili yetu ina limit inapoishia

Mfano ndo unakutana na Mtu anayesema "Mungu Hayupo kwasababu Huwezi kumuona wala kumgusa wala kusikia sauti yake"

Hiyo ni moja wapo ya limit ya akili yetu, ina depend moja kwa moja na milango ya fahamu, masikio macho, pua, ulimi, ngozi...

Anakwambia "jua lili kwepo tuu, na dunia ilikwepo tuu, kwamba kama jua au dunia haiwezekani kuwepo tuu, basi na Mungu hawezekani kuwepo"

Inaonyesha ni jinsi gani akili yetu inafikia limit, kuyaelewa mambo mengine..

Mambo ambayo hatuyajui bado ni mengi ni infinity ♾️, na ningumu hata kuingia akilini haya make sense kwasababu yapo beyond uwezo wa akili.

Kama vilevile tulivyoona kwa mfano wa nyuki, kwamba kumuelezea hata teknolojia yetu hai make sense, kwaajili ya limit yao ya akili.
Nyuki anaweza kuelewa kuwa taa imetengenezwa na binadamu na umeme ulipiwa na binadamu sio kweli ELIMIKA USIPOTESHE
ta teknolojia yetu hai make sense, kwaajili ya limit yao ya akili.Nyu
 
Kusurvive kwetu hakuhusiani na Mungu, kwenye magonjwa sayansi ya tiba ndo imesaidia kudhibiti magonjwa na sio Mungu. Na ndio maana hata ww ukiugua huendi kanisan Wala msikitini, utaenda hospital kutibiwa..
usitoe mifano ya magonjwa, ni minor sana na Mungu ametupa uwezo wa kuyashughulikia,

ongelea mambo ambayo binadamu hajawai ku experience na hawezi kuyashughulikia

mimi nakuoa mfano ukaufatilie mwenyewe

mwaka 2019 kuna asteroid ilikua inakaribia kabisa kui gonga Dunia, na inge gongana na dunua, dunia ingepasuliwa haswa iwe nyang'any'anya, iwe rojorojo

astonoers wa hapa duniani ambao unaamini research zao na kuona wamekua advanced na wanajua vingi

wali detect hatari ya kugongana siku chache kabla na pia hawakua na namna ya kuzuia

waki calculate speed yake na position ya Dunia ikaonekana inagongana na Dunia July 25 2019

ila siku chache baadae haikuendelea na hiyo direction ila ilipishana na dunia kwa kilometers chache sana

ikawa imepita

hiyo ni moja wapo ambayo tutasema pia tume experience hatari yake,
wew unaongelea, njaa, vita magonjwa kwamba yapo kwasababu Mungu hayupo ?

kuna vitu vingine vya hatari kuliko hata Collision pia probably vinaepushwa ni kwamba tuu hatujui
 
Sure kaka, Mungu yupo.
Sometimes ukifikiria sana at the end unafika point unakubali yupo aliyeumba huu ulimwengu.
Kuna wakati huwa na imagine tupo na zaidi ya mabilioni ya sayari lakini mwamba akachagua Earth for humans, huwezi sema tu eti from no where binadam tu tukawa kwenye hii sayari.
 
usitoe mifano ya magonjwa, ni minor sana na Mungu ametupa uwezo wa kuyashughulikia,

ongelea mambo ambayo binadamu hajawai ku experience na hawezi kuyashughulikia

mimi nakuoa mfano ukaufatilie mwenyewe

mwaka 2019 kuna asteroid ilikua inakaribia kabisa kui gonga Dunia, na inge gongana na dunua, dunia ingepasuliwa haswa iwe nyang'any'anya, iwe rojorojo

astonoers wa hapa duniani ambao unaamini research zao na kuona wamekua advanced na wanajua vingi

wali detect hatari ya kugongana siku chache kabla na pia hawakua na namna ya kuzuia

waki calculate speed yake na position ya Dunia ikaonekana inagongana na Dunia July 25 2019

ila siku chache baadae haikuendelea na hiyo direction ila ilipishana na dunia kwa kilometers chache sana

ikawa imepita

hiyo ni moja wapo ambayo tutasema pia tume experience hatari yake,
wew unaongelea, njaa, vita magonjwa kwamba yapo kwasababu Mungu hayupo ?

kuna vitu vingine vya hatari kuliko hata Collision pia probably vinaepushwa ni kwamba tuu hatujui
Sasa iyo asteroid kutokugonga Dunia kunathibitsha vipi uwepo wa Mungu, maana kama Mungu angekuwepo hata izo asteroids za hatari asingeziumba, afu baadae aje azikwepeshe tena...
 
Back
Top Bottom