Uzi maalumu: Tabia zinazokera katika jamii

Uzi maalumu: Tabia zinazokera katika jamii

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Naandika uzi huu kwa kumuunga mkono mtangazaji mkongwe (mstaafu) ndugu Leonard Mambo Mbotela aliyekuwa akitangazia Voice of Kenya (VoK) na baadaye Kenya Broadcasting Corporation (KBC) katika kipindi maarufu kilichovuma wakati huo kwa jina la “Je huu ni uungwana?” Katika kipindi hicho, Leonard alikuwa akiangazia tabia mbaya katika jamii na kuwaasa wanajamii kuachana nazo.

Sitaki kuwachosha na maneno mengi; ngoja niingie kwenye mada moja kwa moja. Kuna baadhi ya tabia za watu zinakera na kusikitisha. Juzi nilikuwa nasafiri kwenye basi la abiria kutoka Kawe kwenda Mbagala. Ndani ya basi hilo pia alipanda kijana barobaro mwenye umri wa makamo. Tulipofika Magomeni yule kijana akaanza kuongea na mpenzi wake kwenye simu kwa sauti kubwa bila aibu akimjulisha kuwa amepanda basi lakini kuna traffic jam hivyo anaweza kuchelewa kufika. “Nisubiri nakuja mpenzi wangu, hata mimi nina hamu sana, nipo kwenye foleni”. Alisikika akiongea kimahaba kijana wa watu. Kitendo hiki kiliwashangaza abiria wakamgeukia kumtazama na baadhi walisikika wakisonya hapa na pale. Kisha akakata simu na kukaa kimya.

Tulipofika mbele kidogo akampigia simu tena huyo mpenzi wake. Safari hii akiuliza: “Umechukua chumba namba ngapi? Yaani hapa nina genye balaa, nikifika tu kazi inaanza. Kabla hajamaliza kuongea, abiria wote wakaguna: “Aaaaa! “Maneno gani haya unaongea kwenye basi la abiria?” Alisikika akilalamika abiria mmoja aliyefurwa kwa hasira. Kuanzia hapo abiria wote wakaanza kumsakama kwa maneno makali. Walimsema mpaka akili zikamrudia. Hadi anashuka kituo cha Keko, jamaa yupo kimya kama amemwagiwa maji ya barafu. Na hata baada ya jamaa kushuka bado waliendelea kumsema hadi niliposhuka kituo cha Mtongani nikawaacha wakiendelea kumjadili.

Kwa kweli kuna baadhi ya watu hawana kaba ya ulimi na wala hawachagui mahali pa kuongelea mambo yao. Wanajiropokea tu kama wehu! Hili la kuropoka kwenye vyombo vya usafiri linashuhudiwa na watu wengi ila tu watu hawapendi kuingilia ujinga wa awatu wengine hadi pale tabia hii inapokuwa imevuka mipaka (kama ilivyotekea kwa huyu kijana).

Tabia nyingine inayokera ni pale mtu anapoenda dukani kununua sigara kisha anaiwasha na kuanza kuivuta na kupuliza moshi pale pale bila kujali kama watu waliomzunguka ni wavutaji wenzake au la. Na kibaya zaidi kuna baadhi huwatuma watoto kuwanunulia sigara na kuwaagiza waiwashe kabisa. Hii sio akili bali ni matope.

1668365295736.png

Kuvuta sigara hadharani ni moja ya tabia zinazokera(Chanzo:Mtandao)

Nawe ndugu mwanaJF kuna baadhi ya tabia ambazo hupendezwi nazo. Nimefungua huu uzi maalumu ili kila mtu atupie tabia ambayo anaona haifai katika jamii ingawa inatendwa na watu kila kukicha. Kwa kufanya hivi, bila shaka wahusika wataacha tabia hizi chafu na kuanza kusihi maisha yanayoipendeza jamii.

Karibuni.
 
Nimemkumbuka Wambura Mtani wa Redio free Afrika.

Naongeza yangu

Hii mambo ya kuongea na simu katikati ya watu tena simu ndefu tunakusikiliza wewe tu. Yani tuko kwe daladala au foleni unapokea au kupiga simu unaongea wew tu. Ustaarabu ni kupokea kama simu unaona ni ndefu unamwambia sorry nitakupigia baadaye
 
Nimemkumbuka Wambura Mtani wa Redio free Afrika.

Naongeza yangu

Hii mambo ya kuongea na simu katikati ya watu tena simu ndefu tunakusikiliza wewe tu. Yani tuko kwe daladala au foleni unapokea au kupiga simu unaongea wew tu. Ustaarabu ni kupokea kama simu unaona ni ndefu unamwambia sorry nitakupigia baadaye
Kweli kabisa mkuu. Na unakuta mwingine anaongea upuuzi tu na kuwa kero kwa wengine. Ustaarabu wa kijamii na jambo la muhimu sana.
 
Kuna wale wanaotafuna tafuna vitu kwenye dala dalaaaaa.....
 
Kuna wale wanaotafuna tafuna vitu kwenye dala dalaaaaa.....
Au wale wanachomeka kijiti cha toothpick mdomoni hadi usipokuwa makini wanaweza kukutoboa macho. Na wengine huenda mbali zaidi hadi kuchomeka njiti hizi kwenye nywele za kichwani.
 
kuna wale wa kupenda kujisifia na mara nyingi akiona unamtisha au umemshitukia aanza kukuuliza " UNANIJUA MIMI NANI"
Wale wa kujimbwambafai au? Wale jamaa wana mikwara wee acha tu aisee!!!
 
Au wale wanachomeka kijiti cha toothpick mdomoni hadi usipokuwa makini wanaweza kukutoboa macho. Na wengine huenda mbali zaidi hadi kuchomeka njiti hizi kwenye nywele za kichwani.
Eeeeh... kuna wale ambao akikuonaa kwa mbali atakuitaaa jina laki weeeeeeeee tpaul weeeeeeeeee..
Yan mm siitiki.. Na nikikuona nakwambia kwamba sitaki uniite njiani ukiniona popote pale
 
Wale wa kujimbwambafai au? Wale jamaa wana mikwara wee acha tu aisee!!!
eeeh sasa kuna moja alikuwa anajifanya usalama mtaani kuna siku . katika harakati za kumwagia moyo nikamkuta kwenya bar moja akinengua.

tukakutana mtaani nikataka kumpaka akasema nikaushe ile yeye ndo kazj yake inampa ugari hapa mjini yeye sio hata usalama wa taifa
 
Eeeeh... kuna wale ambao akikuonaa kwa mbali atakuitaaa jina laki weeeeeeeee tpaul weeeeeeeeee..
Yan mm siitiki.. Na nikikuona nakwambia kwamba sitaki uniite njiani ukiniona popote pale
Na wengine hadi wanataja cheo chako na kuanza kukutangaza kwa watu wakati wewe hujawahi kuwaambia. Wanaudhi wee acha tu!! Unakuta umekaa mahali unapiga stori na jamaa zako hata hawajui unafanya kazi gani.......wengine wanahisi wewe ni mtu wa Usalama wa Tiafa........halafu anakuja mpuuzi mmoja kuropoka cheo chako hadharani 😀 😀 😀 😀 😀
 
eeeh sasa kuna moja alikuwa anajifanya usalama mtaani kuna siku . katika harakati za kumwagia moyo nikamkuta kwenya bar moja akinengua.

tukakutana mtaani nikataka kumpaka akasema nikaushe ile yeye ndo kazj yake inampa ugari hapa mjini yeye sio hata usalama wa taifa
Hahaha! Umenifanya nicheke kwa sauti mkuu.....mjini mipango😀😀😀😀😀
 
Hahaha! Umenifanya nicheke kwa sauti mkuu.....mjini mipango😀😀😀😀😀
😁😁🤣🤣 nchi hii ina vichwa vibovu ving sana usipokuwa makini vitakutisha na nchi utaiona ngumu hii utataman ukimbilie somalia au congo
 
Hata kula mnataka kutukataza???🙄🙄
Kula ni jambo la heshima. Kama una njaa, kaa mahali ule umalize uendelee na safari. Sio lazima ulie chakula kwenye basi ya abiria. Unakuta mtu anakula vipande vya nyama wakati mtu aliyeketi naye siti moja hali nyama. Huoni kwamba anageuka kuwa kero kwa mwenzake?

Au utakuta mtu anakula karanga anamenya maganda na kuyapuliza yanapepea kwenye basi zima yanawachafua wenzake. Hii ni shida!
 
Wanawake vaeni Kwa heshima tafadhalini sana, mkumbukeni mke wa Lutu.
Kweli kabisa hawa viumbe wanakera sana kwenye upande wa mavazi. Utakuta mtu kavaa nguo ya kulalia hadi mapindo ya chupi yanaonekana lakini anapuyanga tu mtaani kana kwamba hakuna tatizo lolote.
 
Tabia Ya Unakuja Dukani Kwangu Unataka Kitu Cha Elf 20 Wakat Mfukon Una Elf 10 Halaf Waanza Kujilalamisha Kile Kitu Nikuuzie Kwa Elf 10 Wakat me Nimenunua Elf 15,
N.B Kama Huna Pesa Ya Kutosha Kaa Nyumbani Usije Kutusumbua Huku Sokoni Tunatafuta Fweza Hatugawi Misaada.
 
Back
Top Bottom