Uzi maalumu wa kufarijiana kwa wale wote wanaopita kwenye hali ngumu za kimaisha

Uzi maalumu wa kufarijiana kwa wale wote wanaopita kwenye hali ngumu za kimaisha

Kwa maoni yangu maisha magumu ni sehemu ya maisha ya kawaida. Watu wengi wanamaisha magumu kuliko maisha mazuri.

Ukijua hivyo hautasikitika na kutisikisa sana Hali ngumu inapokuja.

Wangapi wanaumwa, wako jela, wanauguza, wamefiwa, wanaumwa, hawana kazi, elimu, afya nzuri, pia wote tutakufa. nk

Binadamu wenye maisha mazuri bila matatizo hakuna hata mmoja. Wote lazima tupitie hali ngumu. Makosa ni kufikiria ni kitu cha ajabu, siyo cha kawaida.

Mtazamo wangu hali zote ni sehemu ya maisha. Maisha ni kupambana na Hali zote.
 
Miaka 2 Sasa Sina Kazi Wala Kibarua Kila Mchakato Unabuma Daaah Maisha Magumu Jamani, Meseji Ikiingia Kwenye Simu Ujue Ni Kampuni Ya Simu Na Promosheni Zao Hakuna Cha Bebi Wala Honey Wala I Miss U ... Jamaniiiii
Yana mwisho hayo
 
Maisha yana mitihani mingi mno muhimu chukulia kama changamoto na kusonga mbele...
 
Miaka 2 Sasa Sina Kazi Wala Kibarua Kila Mchakato Unabuma Daaah Maisha Magumu Jamani, Meseji Ikiingia Kwenye Simu Ujue Ni Kampuni Ya Simu Na Promosheni Zao Hakuna Cha Bebi Wala Honey Wala I Miss U ... Jamaniiiii
Dah! Pole sana
 
Kwa maoni yangu maisha magumu ni sehemu ya maisha ya kawaida. Watu wengi wanamaisha magumu kuliko maisha mazuri.

Ukijua hivyo hautasikitika na kutisikisa sana Hali ngumu inapokuja.

Wangapi wanaumwa, wako jela, wanauguza, wamefiwa, wanaumwa, hawana kazi, elimu, afya nzuri, pia wote tutakufa. nk

Binadamu wenye maisha mazuri bila matatizo hakuna hata mmoja. Wote lazima tupitie hali ngumu. Makosa ni kufikiria ni kitu cha ajabu, siyo cha kawaida.

Mtazamo wangu hali zote ni sehemu ya maisha. Maisha ni kupambana na Hali zote.
Mkuu nisawa but usiwe na madeni, ukiwa na madeni na hayalipiki hii dunia utaiona chungu mara 200
 
Kifarijiana ni neno negative mno kimaendeleo, wanafarajiana waliofiwa, kwa maana ya kuwa aliyeondoka hana turning back!
Ila wa Wapambanaji wanatiana Moyo.
Fact[emoji123]
 
Nimepiga moyo konde hadi nimechoka, nimepambana hadi najihurumia, nimetiwa moyo na kufarijiwa hadi basi.. ila ugumu wa mambo kama vile ninauchochea,,, kwasasa ninaangalia kitakachotokea tu..
Mungu ninayemuamini ndio ameruhusu haya yatokee na ninajua anao uwezo wa kubadilisha hii hali
Pole sana mkuu,ni changamoto za maisha,one day yes...tupambane mkuu.
 
Miaka 2 Sasa Sina Kazi Wala Kibarua Kila Mchakato Unabuma Daaah Maisha Magumu Jamani, Meseji Ikiingia Kwenye Simu Ujue Ni Kampuni Ya Simu Na Promosheni Zao Hakuna Cha Bebi Wala Honey Wala I Miss U ... Jamaniiiii
Mungu ni mwema,yatakwisha mkuu
 
Pole sana mkuu,ni changamoto za maisha,one day yes...tupambane mkuu.
Asante sana mkuu, kupambana ni jambo la muhimu ila kama mapambano hayaonyeshi dalili yoyote ya mafanikio basi hata nguvu ya mapambano inapungua.
Miujiza ya Mungu ndio pekee iliyobaki kuweza kunitoa hapa nilipo..
 
Asante sana mkuu, kupambana ni jambo la muhimu ila kama mapambano hayaonyeshi dalili yoyote ya mafanikio basi hata nguvu ya mapambano inapungua.
Miujiza ya Mungu ndio pekee iliyobaki kuweza kunitoa hapa nilipo..
Shida nyingine hiyo miujiza uwe na imani, wakati mwingine nawaza hizi shida zina toka kwa shetani au kwa Mungu?
 
Nimepiga moyo konde hadi nimechoka, nimepambana hadi najihurumia, nimetiwa moyo na kufarijiwa hadi basi.. ila ugumu wa mambo kama vile ninauchochea,,, kwasasa ninaangalia kitakachotokea tu..
Mungu ninayemuamini ndio ameruhusu haya yatokee na ninajua anao uwezo wa kubadilisha hii hali

Ameni!
 
Shida nyingine hiyo miujiza uwe na imani, wakati mwingine nawaza hizi shida zina toka kwa shetani au kwa Mungu?
Imani inapungua sana wakati wa shida na unafiki unaongezeka, hatupaswi kumuomba Mungu wakati wa shida pekee ila wakati wote.
Hizi shida aidha ziwe zinatoka kwa Shetani au kwa Mungu ila lazima zipate kibali kutoka kwa Mungu, kama hajaamua upitie magumu basi Shetani hana uwezo wa kubadili maamuzi ya Mungu.
 
Imani inapungua sana wakati wa shida na unafiki unaongezeka, hatupaswi kumuomba Mungu wakati wa shida pekee ila wakati wote.
Hizi shida aidha ziwe zinatoka kwa Shetani au kwa Mungu ila lazima zipate kibali kutoka kwa Mungu, kama hajaamua upitie magumu basi Shetani hana uwezo wa kubadili maamuzi ya Mungu.
Mkuu hongera sana umeiva kwenye haya mambo safi sana. Kwahiyo kila kitu ni mpango wa Mungu?
 
Mara nyingi sana, unapopata shida ni Mungu amekuacha uipate ili ujifunze. Wewe usilalamike. Badala yake mwombe Mungu halafu MWAMINI KABISA kwamba atakutoa kwenye hiyo shida yako. Watu wengi sana walio matajiri sasa walipata matatizo na katika kuyatatua ndipo wakapata upenyo wa kutokea. Wagunduzi wakubwa wa vifaa tunavyotumia sasa walijaribu tena na tena na tena mpaka mwishowe wakafaulu. Aliyetengeneza balbu ya umeme alijaribu karibu mara elfu tatu kabla haijawaka. USIKATE TAMAA UNAPOPATA SHIDA

Ukimtegemea Mungu kwenye shida yako huwezi kupata taabu moyoni. KAMWE usiwe unafikiria shida uliyonayo. Badala yake fikiria NAMNA YA KUJIKWAMUA huku ukimwamini na kumwomba Mungu akusaidie. Hebu jiulize:- Mahali kama kwenye jiji la Dar ni watu wangapi hawana ajira? Ni maelfu (au hata malaki) ya watu. Lakini hawafi njaa, Mungu anajua namna anavyowapa msaada wanaendelea kuishi.

NO RETREAT, NO SURRENDER
 
Mara nyingi sana, unapopata shida ni Mungu amekuacha uipate ili ujifunze. Wewe usilalamike. Badala yake mwombe Mungu halafu MWAMINI KABISA kwamba atakutoa kwenye hiyo shida yako. Watu wengi sana walio matajiri sasa walipata matatizo na katika kuyatatua ndipo wakapata upenyo wa kutokea. Wagunduzi wakubwa wa vifaa tunavyotumia sasa walijaribu tena na tena na tena mpaka mwishowe wakafaulu. Aliyetengeneza balbu ya umeme alijaribu karibu mara elfu tatu kabla haijawaka. USIKATE TAMAA UNAPOPATA SHIDA

Ukimtegemea Mungu kwenye shida yako huwezi kupata taabu moyoni. KAMWE usiwe unafikiria shida uliyonayo. Badala yake fikiria NAMNA YA KUJIKWAMUA huku ukimwamini na kumwomba Mungu akusaidie. Hebu jiulize:- Mahali kama kwenye jiji la Dar ni watu wangapi hawana ajira? Ni maelfu ( au hata malaki) ya watu, lakini hawafi njaa kwa vile Mungu anajua namna anavyowapa msaada wanaendelea kuishi.

Kwa hivyo, unapopata shida:- NO RETREAT, NO SURRENDER
 
Back
Top Bottom