Uzi maalumu wa kuweka tetesi na Taarifa za usajili Ligi Kuu ya NBC kwa msimu ujao 2022/2023

Uzi maalumu wa kuweka tetesi na Taarifa za usajili Ligi Kuu ya NBC kwa msimu ujao 2022/2023

Midala kucheunye to Dar young Africans - Diel done
IMG-20220615-WA0036.jpg
 
Usajili huu mbona wakawaida sana!
Kwa wachezaji wazawa, hao ndio mastaa wetu. Kumbuka kuna nafasi 12 tu za wageni na kati ya hao, ni wachezaji 8 tu wanaruhusiwa kuhusika katika mchezo mmoja wa Ligi ya Bara. Maana yake ni kwamba wachezaji wazawa wanatakiwa wawe wengi maana kuna nafasi zaidi ya 18 katika usajili wa wazawa na katika mchezo mmoja wa Bara unaweza ukawahusisha wachezaji kuanzia 1 hadi 18. Sasa hapo ndio uone umuhimu wa kusajili wachezaji wazawa, na wazawa wenyewe walio na unafuu ndio hawa hawa akina Kiombo na Kibu. Ndio maana usishangae pia kuona timu inasajili akina Nkane na Ngushi
 
Jamaa halafu ni pancha sana akiguswa kidogo huwa anakaa benchi sana.
 
Akiweza kuhimili presha ya timu kubwa kama Simba atafanya vizuri vinginevyo atapotea ndani ya muda mfupi tu na itakuwa hasara nyingine kwa Simba. Lakini kwa akili yangu ya kawaida tu nafikiri Lusajo wa Namungo ni bora sana kumzidi huyu Kyombo. Lusajo amecheza ligi muda mrefu kwa kiwango kizuri tu hivyo tayari yupo "matured". Na haihitaji kuzoea presha ya timu kubwa kwani hali hiyo aliishaipita siku nyingi wakati akichezea Yanga enzi hizo anaanza kucheza ligi kuu. Na Lusajo namuona ndio angekuwa mbadala wa Boko kwa muda mrefu ujao. Na kiufundi zaidi mshambuliaji ambaye alianzia kucheza kama kiungo kama alivyo kwa Lusajo anakupa kitu cha ziada kwenye eneo la ushambulaiji.

Mwisho wa siku ngoja tuwaache viongozi wa Simba ndio wenye dhamana ya timu yao. Ikifanya vizuri watasifiwa na mashabiki wao na ikifanya vibaya wajiandae na dhahama kwani sidhani kama itakuwa rahisi kwa wananchama na mashabiki wao kukubaliana na hali kumaliza msimu mwingine bila hata kombe moja. Kikubwa tu viongozi wa Simba wajue na wakumbuke wao wana "overhaul" timu nzima kwa sababu walichelewa ku "repair" timu yao kwa wakati. Hivyo wawe makini sana maana doto wake wa Kariakoo yeye msimu huu ana "repair" tu sehemu kidogo zenye mapungufu. Ukikosea kwenye " repair" ni balaa na unatoa tu sehemu ndogo iliyokosewa na kuirekebisha lakini ukikosea kwenye "overhaul" ni dhahama maana itabidi ufumue kila kitu uanze tena mwanzo upya kabisa na wakati huo unakuta muda umeshakuacha.
 
Unasajili vp bila kocha?

Bongo bhana, hata huko Ulaya Kocha akitimuliwa yule anayeletwa huwa anakuja kunusuru timu, na hatua ya kwanza ni kuwajengea wachezaji imani tu wapambane na sio mbinu zake.

Mbinu huendana na aina ya Wachezaji, mfano Kibu Denis kwa namna anavyocheza, kujiposition unaina kabisa kwa Nabi hawezi cheza kabisa, pia ukija kwa Pablo ukimchukua Kiungo kama Aucho au Chama kwa kocha kama Pablo hawezi kitoboa maana Pablo anapenda viungo wenye kuwa na speed na nguvu nk.

Hivyo Simba wangeanza na Kocha kisha kocha, aingalie Simba katika angle zote, yaan ile Simba ambayo inafungwa kizembe, na ile ambayo inapambana kwa jasho na damu, kupitia hapo kocha atajua ni wachezaji gani wanabaki katika kiwango chao, iwe wamefungwa au kushinda. Hapo ndipo maboresho ya kikosi hutokea.

Kwa usajili huu ni wazi sasa Simba inarudi ilipotoka Yanga ambapo walikuwa wanasajili kwa mihemko, msimu unaoisha huu Yanga imesajili wachezaji ambao sio tu kocha alijaribu kuwaona bali alipendekeza kutoka ukanda wetu huu huu wa Afrika Mashariki.

Simba wasisajili kama Ndondo Cup, watulie, natamani sana kuona Simba na Yanga zote zikifika hatua ya Makundi this time na ikiwezekana Nusu Fainali ya CCL. Ila mikurupuko hii naona kabisa Jwaneng wanakuja kutufumua hapa hapa tena.
 
1655794410767.png


Imeelezwa Ki Aziz ataingia nchini mapema ndani ya wiki hii kwa ajili ya kumalizana kila kitu na Yanga.

Baada ya kumalizana katika masuala ya kusaini mikataba, atangazwa ndani ya mwezi huu, yaani hadi kufikia Juni 29, kila kitu kitakuwa wazi juu ya usajili wake.

Mtoa taarifa huyo alisema, mara baada ya Aziz Ki kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Ivory Coast msimu huu akiwa na ASEC hivi karibuni, ataingia nchini kwa ajili ya maandalizi hayo ya kutambulishwa ikiwemo kutengenezewa video pamoja na kupigwa picha kama ilivyotokea kwa Lazarous Kambole.

“Unajua Aziz Ki mkataba wake unamalizika Juni 28, mwaka huu, hivyo Yanga kwa sasa haiwezi kumtambuisha kama ni mchezaji wao halali.

“Ambacho kitafanyika wiki inayoanzia Jumatatu, Azizi Ki atatua nchini kisha atamalizana na Yanga na mambo ya picha pamoja na video za utambulisho zitafanyika, baada ya hapo watasubiri mpaka ipite tarehe 28 kisha watamtangaza kuanzia tarehe 29. Utambulisho wake utakuwa wa kipekee, kama mfalme.

“Lakini pia inawezekana pia wakamtangaza kabla ya tarehe hizo kama tu Yanga watakuwa wamezungumza vizuri na viongozi wa ASEC na kupewa ruhusa ya kufanya hivyo
 
Viungo wa kati.!
-Kelvin Nashon
-Azeez Andambwile
-Baraka Majogoro
--Hassan Nassoro
-Gustapha Simon

Mchezaji gan ungetamani timu yako imsajili
 
Viungo wa kati.!
-Kelvin Nashon
-Azeez Andambwile
-Baraka Majogoro
--Hassan Nassoro
-Gustapha Simon

Mchezaji gan ungetamani timu yako imsajili
Mchukue huyo kelvin Nashon halafu utakuja kunishukuru baadae

Huyo ndo kile kizazi cha akina Job, kibwana, Mshery,Kibabage, kabwili........kiungo mkabaji wao alikuwa Kelvin Nashon ile U-17 ya coach Kim Poulsen
 
Back
Top Bottom