Uzi maalumu wa Mimea Tiba inayotuzunguka majumbani

Uzi maalumu wa Mimea Tiba inayotuzunguka majumbani

Leo tunaendelea na majina ya namba zilizobaki tuone zikiwa kwenye mahusiano zinakuwaje. Majina ya watu Yana nguvu kubwa Sana katika mahusiano ya mtu na mtu, hivyo yanaweza yakapelekea watu wakawa kwenye mahusiano ya aina Fulani kulingana na namba za majina yao. Tunaangalia namba za majina kwa kutumia alfabeti za kiingereza A mpaka Z.

A, j na s Ni namba 1
B, k na t Ni namba 2
C, l na u Ni namba 3
D, m na v Ni namba 4
E, n na w Ni namba 5
F, o na x Ni namba 6
G, p na y Ni namba 7
H, q na z Ni namba 8
I na R ni namba 9

Mfano tunachukua jina la John na Fatuma tuone wakiwa kwenye mahusiano wataishi maisha gani.

J. O. H. N
1 +6 +8 +5=20
20=2+0=2
Jina la John Lina namba 2.

F. A. T. U. M. A
6+1+2+3+4 +1=17
17=1+7=8
Jina la Fatuma Lina namba 8.

Baada ya kupata namba za majina ya John na Fatuma, tunajumlisha namba zao 2+8=10, 10=1+0=1. Hivyo basi, mahusiano ya John na Fatuma yatakuwa Chini ya namba 1.

Sifa ya namba 1 Ni kujiongoza yenyewe, namba 1 Ni namba yenye ubinafsi. Hivyo basi, mahusiano ya John na Fatuma yatakuwa na ubinafsi ndani yake, kila mmoja atakuwa anaangalia upande wake. Lakini pia, kutakuwa na mabishano katika mahusiano yao, kwa sababu kila mmoja hatopenda kupelekeshwa na mwenzake. Mahusiano yao yatakuwa na majivunia ndani yake, kila mmoja atajiona Bora kwa mwenzake.

Ingekuwa namba 4, mahusiano yao yangekuwa kwenye wakati mgumu Sana. Namba 4 Ni namba ya upinzani. Hivyo kila mmoja angekuwa mpinzani kwa mwenzake, vurugu na kupigana ingekuwa Ni Jambo la kawaida. Lakini pia, katika mahusiano yao wangekuwa Wana panda na kushuka kwenye kipato chao.

Ingekuwa namba 5, mahusiano yao yangekuwa rahisi kuachana na kutengana. Mahusiano ya namba 5 yanaenda kwa kutumia akili nyingi. Jambo la kuachana na kurudiana Ni Jambo la kawaida kwenye mahusiano ya namba tano. Namba 5 inataka tuishi nao kwa akili, sio kuangalia hisia ya mtu. Uzuri wa namba 5 upo kwenye mahusiano ya kibiashara, Ni rahisi kufanikiwa, kwa sababu namba 5 Ni namba ya biashara.

Ingekuwa namba 7, mahusiano yao yangekuwa ya Siri au mmoja wapo angekuwa msiri kwa mwenzake. Siri zipo nyingi, inawezekana ikawa mmoja wapo anamficha mwenzake Kama ana biashara, nyumba, pesa au ana mwanamke au mwanaume wa pembeni. Angalizo, usije ukamuhesabia mume wa mtu au mke wa mtu alafu ikaja namba 7, utajiingiza kwenye matatizo, maana Cha mtu sumu.

Ingekuwa namba 8, John au Fatuma, mmoja wapo angechelewa kumpenda mwenzake. Hapa ingechukuwa muda mrefu mmoja wapo kumkubalia mwenzake kuingia kwenye mahusiano. Ila mahusiano yakianza kunakuwa na heshima kubwa Sana kwenye mahusiano, kila mmoja anamuheshimu mwenzake.

Namba zingine nilishazielezea huko nyuma, hivyo leo nilikuwa namalizia namba 1, 4, 5, 7 na namba 8. Watu wengi wametaka nizielezee namba zote, Nami nikaona Ni Bora nizimalizie.
By magical powerView attachment 2898420
Je ukihesabu ukapata 11 tafsiri yake inakuaje au unazijumlisha tena..?!
 
  • Thanks
Reactions: KJ4
SULUHISHO LA CHOO KIGUMU/KUTOPATA CHOO:

Ikiwa una matatizo ya kupata CHOO, na umeenda hospitali bila suluhisho basi soma hapa.
1. Maji-hakikisha unakunywa maji ya kutosha kuanzia asubuhi ili kuruhusu mmeng'enyo wa chakula tumboni.

2. Viazi vitamu - wote tunavifahamu, na hapa nazungumzia vipikwe kwa kuchemsha. Kula hadi ushibe. Narudia tena, ''kula mpaka ushibe''.

3. Nanasi - menya nanasi na kula hadi utosheke, na siyo kutengeneza sharobati.

4. Maembe ya kuiva - osha , kata na kula kadri utakavo jaaliwa. Usitengeneze juisi.

MAJIBU: Utapata matokeo kuanzia siku ya kwanza.. Kwa majibu mazuri zaidi, tumia kwa wingi vyakula hivyo kwa siku 3 na kuendelea. Hutosumbuka tena.

NB: 1. Epuka kula limao na ndimu, chipsi kavu au vyakula vya sampuli hiyo.
2. Nenda toilet ukiwa na maji ya kutosha.
3. Usipopata majibu muone tabibu wako.

''NADHANI DAWA HII TAMU''
 
ELIMU YA BURE..VYAKULA (TIBA).. TOA ADHABU..wabaya wataanza kukukwepa.

Hivi ni baadhi ya vyakula muhimu sana katika tiba asili. Wakati maisha yakiendelea kama kawaida, utumiapo vyakula hivi utajikuta UKIJITIBU mwenyewe bila kufahamu ama KUJIKINGA na majanga ya kishetani na kichawi automatically.

Kama si hivo basi UTAWAHANGAISHA walozi wako na KUWAADHIBU VIKALI masheitwan walioko mwilini mwako au katika makazi yako kwani hutumia makazi na mwili wako kama
makao yao huku ukiwahifadhi, kuwatunza, kuwalinda na kuwatumikia bila ya wewe kufahamu, wakati huo huo wakikuharibia kila kitu japo utaona kana kwamba unajiharibia mwenyewe (self destruction) huku wakikulia timing ya kukuteketeza mazima (total destruction) .. Sasa kabla ya total destruction JIFAHAMU VEMA.

1. Chumvi ya mawe, wakati mwingine pikia chumvi mawe katika mapishi yako ya kila siku. Pia ukiona kitu usichokielewa, mimina au nyunyiza chumvi mawe kwenye hicho kitu.. Alafu chukua hatua.

2. Pilau, Mara moja moja pika pilau kwako. Faida ya kitiba IPO katika vile viungo vyake bila kusahau kitunguu saumu.

3. Pika mbaazi, choroko, kunde nk bila kusahau ufuta, ubuyu na ukwaju.

4. Pendelea kutumia vyakula vya baharini. Hata kama si mpenzi wa vyakula hivyo basi Mara moja moja jiongeze tu kula vyakula hivyo.

5. Pika na tumia chai ya viungo asili kama mdalasini, iliki, karafuu, mchaichai nk. Usichukulie poa ati vinauzwa kwa Tsh mia.

6. Kivumbasi.. Mwinura mkubwa .. Kashwagara. Tumia mmea huo kupikia chai pia . mikoa mingine kiungo kikuu cha chai ni mwinura mkubwa. Wengine hutumia kivumbasi kupikia kahawa za kutafunwa. Faida sana.

7. Epuka uzinzi na ulevi, mashetani hupitia sana hapa, ukiachana na VISASI vya wanadamu vitokanavyo na stress za mapenzi.

8. Mara moja moja tumia maji bahari kujikogesha mwili wako. Usijisingizie ati bahari iko mbali nawe, usafiri upo sehemu zote.

9. Nenda katika ibada yako kanisani au msikitini kulingana na imani yako.. Hats kama ni nyumbani kwako, usimsahau Mungu.

10. Usimnyenyekee shetani hata siku moja ati ''yaani nimehangaika kote ila sijapata tiba..nimeamua kuacha'' .. Unajipa madhambi ya bure wewe.

11. Kachungulie, usiache muda mrefu ukapita bila kwenda KUNAKO ili '' kujifuatilia mwenyewe'' utafahamu mengi yaliyokuzunguka.

12. Tumia mboga za majani aina nyingi uwezavyo. Utakuta jamii moja wanatumia, nyingine hawatumii. Ukiwa umenisoma hapa basi jitahidi ule, mfano katika jamii moja ni mboga, kwingine ni chakula cha sungura. Nakwambia we kula mboga hizo.

Hayo ni baadhi tu, ikiwa mwilini mwako una uchawi, unaweza ukauondoa japo unaweza usitambue hilo. Pia kama kuna jini mchafu mwilini mwako utamuadhibu na kumuhangaisha. Uwezekano ni mkubwa sana akaukimbia mwili wako.

Cha msingi na sekondari, fuatilia ili usafishe mwili wako kuondoauchawi, masheitwani, kunusi na nuksi, ufungue liziki zako na vifungo vingine na kung'arisha nyota na update kazi ili maisha yaendelee. Kumbuka maisha haya ni yako binafsi (mwili, roho na nafsi) ni vyako na havina mbadala (spea). Jihangaikie mwenyewe. ULIZA CHOCHOTE, NITAKUJIBU.
 
Assalam alleykumu swalamaaaa

♥ FAIDA ZA KUTUMIA MARASHI ROSE ♥




🎤Naam na leo tena kwenye jukwaa letu la kupeana faida kede kede juu ya tiba asili/visomo/kisunna n.k

🎤Leo bhana nakuja na faida hii juu ya MARASHI ROSE na miujiza yake kwenye fani yetu ya tiba asili

🎤Nazani kila mtu anayajua/ameyaona/ameyasiki au kashawahi kuyatumia basi leo ngoja nikupe faida na maajabu yake kwa uchache zaidi

✏RANGI YA MARASHI ROSR

🖎Marashi rose yana rangi kama ya maji safi yaliyo tulia na ung'aa na muonekano kama mazito mazito kiasi

✏MAGONJWA YANAYO TIBIWA KWA KUTUMIA5 MARASHI ROSE

🖎Marashi Rose ni Bingwa kwenye na ni Mazuri sana kwenye tiba za asili/kisuna n.k kwa kuwa nguvu yake ni kubwa sana ambayo haina kifani

Marashi Rose ni mwamba wa miamba kwenye kutibu Matatizo ya kiroho (kichawi) Na matatizo ya kimwili (kisayans) kama ifuatavyo 👇👇

●MARADHI YA KIROHO (KICHAWI)

-Kutibu nuksi/mikosi na mabalaa

Haya ndo yenyewe kwenye izi shida na wengi tunajua hilo sasa kama unasumbuliwa na matatizo hayo basi chukua

*Marashi rose vichupa 3
*Maji ya zamzami
*Maji ya bahari
*Marashi mrujuani
*Maji ya waridi
*Mashari maji
*Unga wa hiriki
*Chumvi ya mawe

Changa vitu ivyo kwa pamoja kisha tia kwenye ndoo ya maji safi na utaongeza maji yajae mpaka juu kisha hifadhi mahara pasafi na utakuwa ukichota kidogo kidogo kisha unaoga kutwa x2 kwa siku 7 tu

Akikisha unaogea uwanjani na mahara pasafi na uvae nguo au kitambaa cheupe

Baada a siku 7 kitambaa kikatupwe bahari/ziwani au kwenye mtu wenyemaji mengi yanayotembea kwa kasi

-Mvuto wa kupenwa na na kukubalika na watu

Ukitakuwa na mvuto mujaribat wa kupendwa na kuvutiwa na watu basi chukuwa marashi rose yasomee yasini mubini 7 (kila ukimaliza mubini 7 tia nia yako kisha choma ubani zuhura kwenye chetezo na umswalie mtume muhammad s.w kwa ktumia swati fatihi x11 kisha ndo uwendee kusoma)

Baada ya hapo marashi haya uyatumie kujipaka kama mafuta au umwagie mwagie kwenye nguo zako n.k

●MARADHI YA KIMWILI (KISAYANSI)

-Naam mimi (Mujuu Wa Babu) nimeshudia nguvu ya ajabu juu ya Marashi rose zidi ya kutibu maradhi ya kimwili kama vidonda sugu ambavyo havisikii dawa uwezi amini nililetewa mtoto wa miaka 6 ambae alipatwa na kidonda kwenye nyayo kilikuwa kinaenea mguuni mimi nilitumia tu marashi rose kumtibu

Kwa mtu mwenye kidonda sugu kisicho pona chukua kichupa k kimoja cha marashi rose kisha tumia kuosha eneo ambalo lina kidonda fanya ivyo kutwa x3 majibu ni baada ya siku 8 tu ila usiache kutumia mpaka upone hii utanishukuru hatakama ulioza na ukataka kukatwa mguu basi tumia hii njia kisha lete malejesho hapa 💪💪

-Kutibu homa za matumbo tumia kuchanganya na maji kisha kunywa

Hii hata kwa wale wenye mchafuko wa damu inawafaa sana hii wadumu nayo tu

✏FAIDA ZA MARASHI ROSE

🖎Marashi Rose yanafaida kemkem kwenye mambo ya tiba za asili/kisuna n.k marashi haya yamekuwa amaarufu na tegemezi kwa wataalam wa tiba mbadala n.k

✏HASARA ZA MARASHI ROSE

🖎Marashi Rose hayana madhara yeyote kwa mtumiaji sio kwa kunywa wala kwa kuoga hakuna madhara zaidi ya kuwa na radha za sukari nyingi ila kama utaweka kwenye maji ya kunywa basi weka kiasi tu ili uweze kuyanywa

✏NGUVU ZA MARASHI ROSE

🖎Marashi rose nguvu zake ni thabiti na yananguvu aswa wala si utani na ni mujarabu sahihi

🎤Na haya ndiyo maajabu na faida za MARASHI ROSE kwa uchache zaidi

🙏Leo naishia hapa muwe na siku njema👏👏

🇹🇿


🔥By Dr magical power .
 
Mti hii kwauku kwetu twauita kitodzo unakifanyaje,Aya mapenz haya hapa, Najina lengine mashona nguo au gusa unase au kiboko yamahabba wewe mwenye mumeo au mkeo unataka atulie asisikilize yoyote bila Rai yako au asimfikirie yoyote mwenza wako Zaid yako wewe chafunya chukua hivyo vimimba vinavyokamata nguo hivyo vikaange au viponde Kisha uo unga wake changanya na asali mbichi kidogo bakaaa kwenye dhakar wakat watendo lkn paka kwaumakini asikuone tumia mbinu zako mwenyewe nawewe dada nawe utapakaa kwenye uke wako vizur bc hiyo ndokiboko yalimbwata mkishafanya ilo tendo akili zake kuanzia siku hiyo atakuwa nakuwazatu wwe Nakama nimsichana au Unatabia zakutembea nawake zawatu usitumie hiyo dawa au watembea namwanaume zawatu usitumie kabisaa dawa hiyo nakuomba Sana ndugu yang nihatar Sanaa maana Kama mtu anamkewe atamuacha kwajili yako nakama mtu anamumewe nawewe umemfanyia hivyo ataachika,Chukua changanya na Asali mbichi kidogo pakaa kwandani kwenye uke wako Aya ingia kwenye tendo,Maana kunawatu wanaachika kilasiku limbwata Hilo hapo misinaga maficho sifichi kitu.
By magical power.
Screenshot_20240211-205051.jpg
 
Wakuuu naomnbeni msaada .

Dawa / Tiba ya kupunguza matiti, manyonyoau wengie huita maziwa.
 
Wataalamu ninaomba formula au dawa ya mtu kuacha pombe .Nia yangu nikijua niitengeneze niwasaidie vijana wanaoumiza sana familia zao kwa ulevi.naambiwa ipo mitishamba ambayo mtu anaacha kabisa pombe.Tatizo hawa vijana ni hohe hahe hawana hela za kuona waganga wakubwa wapone .
Tafuta majani yanaitwa Murda yakaushe kisha yaweke kwenye karatasi fanya Kama unavuta sigara Moshi wake hii usaidia wavutaji wa aina zote na walevi
 
Kama kuna mtu ana afya ya kusuasua, mwili uliokondeana, chukua matunda ya muegeya yakaushe kisha saga na tumie kama lishe kila siku kijiko kimoja cha chakula kwenye uji halafu njoo na majibu yetu hapa mkuu.
Shukran sana mkuu. Na vipi kama umenenepa sana na unataka kupunguza mwili....
 
Kama kuna mtu ana afya ya kusuasua, mwili uliokondeana, chukua matunda ya muegeya yakaushe kisha saga na tumie kama lishe kila siku kijiko kimoja cha chakula kwenye uji halafu njoo na majibu yetu hapa mkuu.
Ni kweli kabisa.Matunda ya mmea huu yana uwezo mkubwa sana wa kuongeza kinga ya mwili,ina maana automatically ni lazima uimarishe afya ya mtu aliyenyong'onyea.
Matunda haya yanatumika sana katika kuongeza wingi wa damu mwilini.Tena ukipata yale mabichi kabisa ambayo hayajakaushwa inakuwa ni the best sana.Ukitaka kujitibi kwa weledi zaidi unachuma mabichi unakatakata na kuchanganya na nanasi iliyoiva bila kuitoa maganda halafu unachemsha kwa pamoja unachuja na unakunywa mchanganyo huo asubuhi,mchana na jioni.Watu wengi wa kijijino ndiyo formula yao namba moja ya kuongeza damu mwilini.
 
Mti hii kwauku kwetu twauita kitodzo unakifanyaje,Aya mapenz haya hapa, Najina lengine mashona nguo au gusa unase au kiboko yamahabba wewe mwenye mumeo au mkeo unataka atulie asisikilize yoyote bila Rai yako au asimfikirie yoyote mwenza wako Zaid yako wewe chafunya chukua hivyo vimimba vinavyokamata nguo hivyo vikaange au viponde Kisha uo unga wake changanya na asali mbichi kidogo bakaaa kwenye dhakar wakat watendo lkn paka kwaumakini asikuone tumia mbinu zako mwenyewe nawewe dada nawe utapakaa kwenye uke wako vizur bc hiyo ndokiboko yalimbwata mkishafanya ilo tendo akili zake kuanzia siku hiyo atakuwa nakuwazatu wwe Nakama nimsichana au Unatabia zakutembea nawake zawatu usitumie hiyo dawa au watembea namwanaume zawatu usitumie kabisaa dawa hiyo nakuomba Sana ndugu yang nihatar Sanaa maana Kama mtu anamkewe atamuacha kwajili yako nakama mtu anamumewe nawewe umemfanyia hivyo ataachika,Chukua changanya na Asali mbichi kidogo pakaa kwandani kwenye uke wako Aya ingia kwenye tendo,Maana kunawatu wanaachika kilasiku limbwata Hilo hapo misinaga maficho sifichi kitu.
By magical power.View attachment 2901031
Na kuhusu marijuana maelezo yake kidogo
 
Tatizo la maumivu chini ya mgongo.
Tiba yake tafadhali.
 
Na dozi ikoje avute mara ngap
dawa ya kuacha pombe,sigara na madawaKwa wale wanaotumia sigara,bangi na madawa ya kulevya na wanahitaji KUACHA hii ndyo dawa mujarabu kwa

⚡wanywaji wa pombe
⚡Bhangi, sigara
⚡Mirungi , ugoro
⚡Na madawa mengine ya kulevya ukitaka KUACHA

🌹 Chukua dawa inayoitwa MURDA , chukua majani yake uyaanike yakauke


🌹Kisha chukua majani hayo na uyasokote kama sigara kisha vuta msokoto huo nusu asubui na nusu yake jioni , yaani kutwa mara mbili

🌹Dawa hiyo utayumia kwa siku tano tuu. Hakika hutotamani walakutimia tena vilevi vyako

🌹 Na dawa hii ilivyo mujarabu ukivuta mara ya kwanza tu hapo hapo jaribu kuvuta bhangi au sigara au kunywa Hakika utaona inakukera sanaa na ni mbaya
 
dawa ya kuacha pombe,sigara na madawaKwa wale wanaotumia sigara,bangi na madawa ya kulevya na wanahitaji KUACHA hii ndyo dawa mujarabu kwa

⚡wanywaji wa pombe
⚡Bhangi, sigara
⚡Mirungi , ugoro
⚡Na madawa mengine ya kulevya ukitaka KUACHA

🌹 Chukua dawa inayoitwa MURDA , chukua majani yake uyaanike yakauke


🌹Kisha chukua majani hayo na uyasokote kama sigara kisha vuta msokoto huo nusu asubui na nusu yake jioni , yaani kutwa mara mbili

🌹Dawa hiyo utayumia kwa siku tano tuu. Hakika hutotamani walakutimia tena vilevi vyako

🌹 Na dawa hii ilivyo mujarabu ukivuta mara ya kwanza tu hapo hapo jaribu kuvuta bhangi au sigara au kunywa Hakika utaona inakukera sanaa na ni mbaya
Hapa umefafanua vizuri umesaidia wengi.tunaomba umalizie na picha ya mmea huo
 
Back
Top Bottom