Culture Me
JF-Expert Member
- May 24, 2017
- 10,490
- 21,398
Huyo Paka itakua owner wake alikua pale msikitini, alienda kumsubiri ndio maana akawa hataki kuondoka, kuhusu kutoogopa jiwe ni sababu Paka wanaofugwa hua sio waoga kama Paka wa porini, alipoona hatari inamjia akaamua kuwafukuza na ndio maana mliporudi mkamkuta pale pale.Na ramadhani moja hivi wallah sitakaa nikaisahau, zilikua zile ramadhan za mwisho mwisho watu hulala msikitini nikamwambia mama leo naenda lala msikitini nikajibebea daku langu mdogo mdogo baada ya swala ya tarawehe kuisha
Nikampitia mtoto wa bibi yangu tukaongozana kwenda masjid nakumbuka siku hiyo nilikunywa sana juice ikawa naenda haja ndogo vibaya sana, tulipofika msikitini nikamwambia mwenzangu kabla hatujajiweka sawa kulala nisindikize msalani, choo kilikuwepo ndani ya maeneo ya msikiti, tukatoka kuelekea huko
Kabla hatujafika tukakuta paka kati kati ya njia ya kuelekea msalani, nikamwmabia mwenzangu tutapitaje pale tumfukuze paka ndio twende bas tukawa tunamfukuza yule paka lakini hajigusi kabisa hata kusogea hana habari nikamrushia kijiwe ndio kwanza akiangalia kilipomgonga nikamwambia mwenzangu mama yangu alinambia paka hua anafukuzwa mara tatu asipoondoka si paka wa kawaida bas tukamrushia jiwe kwa mara ya mwisho kinyume chake yule paka akatutimua mbio nilizipanda ngaz za kuingia mskitini bila kupenda wenzetu wengine wakatuuliza kuna nn tukawambia kuna paka ametukimbiza hawakutuamini wakatoka wathibitishe tulikua kundi kubwa tu tukamkuta kajisogeza pembeni kidogo napale alipokua mwanzo tukarusha jiwe akatutoa mbio tulikimbia tena kuingia ndan ya msikiti nilichokifanya nikarudi nyumbani nikamwelezea mama bas had leo najiuliza maajabu ya yule paka kutukimbiza
So relax hakuna mauza uza yoyote.