Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uholanzi na JamiiForums kinazindua Mradi wa Kuimarisha Ushiriki wa Vijana katika Michakato ya Kisiasa na Chaguzi.
Bernadetha Kafuko, Mkurugenzi Mtendaji TCD
Vijana wetu ni nguzo yetu, tuna wajibu wa kuwaandaa. Kipaji lazima kipaliliwe ili kuzaa matunda mazuri
Tunataka Vijana wajue mchakato mzima wa Uchaguzi
Vijana wengi wanatumia muda mwingi Mitandaoni. Tunataka Vijana wajue kutumia Mitandao ya Kijamii wakiwa na ajenda maalum na zenye tija
Tunawashukuru JamiiForums kwa utayari wao wa kushirikiana na Kituo cha Demokrasia Tanzania
ijana wetu wa kwenye Vyama, niwaambie Kiongozi mahiri ni yule mwenye Taarifa sahihi. Ili kupata Taarifa sahihi tunatakiwa kusoma. Ukitaka kuwa Kiongozi mwenye kutoa hoja, soma!
Niwaombe Vijana msome Katiba, ili muwe na maoni wakati Mchakato huu utakapoanza na mtuoneshe jinsi gani mnataka mabadiliko
Wiebe de Boer, Balozi wa Uholanzi - Tanzania
Napenda kuwashukuru TCD na Uongozi wake kwa Uzinduzi wa Mradi huu wa kuimarisha Ushiriki wa Vijana katika Michakato ya Siasa na Chaguzi
Kuimarisha Kituo cha Demokrasia Nchini ilikuwa hatua ya muhimu baada ya Uchaguzi wa Mwaka 2020
Serikali ya Uholanzi itaendelea kuunga mkono jitihada za kuimarisha Ushiriki wa Vijana katika masuala ya Siasa
Tuna jukumu kubwa la kuwafikia Maelfu ya Vijana kote Nchini Tanzania na kuimarisha ushiriki wao katika masuala ya kisiasa pamoja na michakato ya Chaguzi
Didier Chassot, Balozi wa Uswisi - Tanzania
Nimefurahi kuwa hapa leo na kuongea na Vijana kuhusu masuala ya Siasa na Chaguzi.
Takwimu zinaonesha TTanzania ina kasi kubwa ya ongezeko la Vijana
Tunapongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua zake za kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Vijana
Uswisi imejikita kuimarisha mazingira ya Nafasi za Kiraia (Civic Space) ikiwemo masuala yanayohusu Vijana ili sauti zao zisikike
Nahimiza Vijana kutumia fursa kama hii ya Kituo cha Demokrasia (TCD) na nyingine zilizopo mbele yao ili kuhakikisha sauti zenu zinasikika. Vijana ndio Taifa la Leo
Kadele Mabumba, Hans Seidel Foundation
Tunaona suala la ushiriki wa Vijana katika Siasa ni ajenda ya Kimataifa
Si vibaya kujiuliza katika Platforms ambazo Vijana wanazo, wanapewa nafasi ya kutoa maoni yao?
Vijana ndio walengwa wa Mafunzo yatakayotolewa katika Mradi huu
Ni vizuri Vijana tutakaopata nafasi ya kushiriki mradi huu tuwashirikishe Vijana wengine waliopo katika Vyama vyenu
Maxence Melo, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums
Niwashukuru kwa fursa ya kufanya kazi na TCD
Sisi ni Asasi ya Kiraia na Waendeshaji wa Mtandao wa Where We Dare To Talk Openly wenye ushiriki mkubwa wa kisiasa. Siasa zetu zilipofika, zipo "shaped" na digitali
Hatuamini mnafanya vibaya kwenye Mitandao, tunaamini mnafanya vizuri lakini tunaona inaweza kufanyika vizuri zaidi
Sisi tutawajengea uwezo ili muweze kufanya kazi yenu ya Siasa vizuri kwenye Ulimwengu huu wa Digitali
Prof. Ibrahim Lipumba, Makamu Mwenyekiti wa TCD
Tanzania ni Nchi ya Vijana, matatizo yanayotukabili kama Taifa (Maji safi, Ajira, Huduma Bora nk) ni matatizo yanayowakabili Vijana
Ufumbuzi wa matatizo haya lazima utegemee ushiriki wa Vijana
Vijana lazima muelewe kuwa Demokrasia ni nyenzo ya Maendeleo. Utawala wa Kiimla unaweza kuwa na gharama kubwa
Kiongozi mmoja anapoamua kufanya lolote lile, matokeo yake yanaweza kuwa makubwa
Demokrasia ya kweli inawapa Watu fursa ya kuchagua Viongozi makini wa kusimamia maendeleo yao
Uchaguzi Huru na wa Haki pekee haitoshi, lazima kuwepo na Serikali ambayo inawajibika
Nchi hii hakuna mwenye Hatimiliki, ni yetu sote!
Wananchi wanapenda misingi ya Demokrasia iheshimiwe
Kate Kamba (CCM)
Nimepewa kazi ya kutoa neno la shukrani kwa Mgeni Rasmi (Prof. Ibrahim Lipumba). Niwashukuru wote walioandaa Warsha hii
Vijana lazima mjue Historia, ukishaijua hutakosea. Historia lazima tuijue ili kujijenga. Hapa tulipofika, tumetoka mbali
Tujaribu kufikiria jinsi ya kujenga Nchi yetu kwa kutumia Vyama
Vijana mdai Haki ya Kugombea katika Vyama vyenu. Demokrasia lazima iwe na Usawa wa Kijinsia, na itoe fursa za kugombea Uongozi
Vijana msiogope kugombea! Matatizo yatatatuliwa na Vijana
Twende kwenye Siasa za Kujenga Nchi, na sio zile za "Maji Taka" ambazo hazitatusaidia. Watu hawawezi kuishi kwa maneno tu, Wanahitaji Afya, Elimu nk.
Tukienda hivi Watu wetu hawatapata shida kwani tutakuwa tunajenga Nyumba moja
Jussa Ismail (ACT - Wazalendo)
Tume zetu za Uchaguzi zinateuliwa na Rais, hapati Mapendekezo kutoka kwa yeyote. Matokeo yake tunakuwa na kina 'Jecha'
Jecha aligombea uongozi CCM akaangushwa, akawa M/Kiti wa ZEC; akafanya yake
Mwishoni, alichukua fomu kugombea Urais kupitia CCM
Sheria ya Vyama vya Siasa ilikuwa na Mapungufu yake tangu mwaka 1992. Marekebisho ya Mwaka 2019 yaliweka maoni yote ya Vyama vya Siasa kapuni
Tunaamini Sheria hii inapaswa kuandikwa upya. Msajili wa Vyama vya Siasa awe Msajili, na sio Mdhibiti
Bernadetha Kafuko, Mkurugenzi Mtendaji TCD
Vijana wetu ni nguzo yetu, tuna wajibu wa kuwaandaa. Kipaji lazima kipaliliwe ili kuzaa matunda mazuri
Tunataka Vijana wajue mchakato mzima wa Uchaguzi
Vijana wengi wanatumia muda mwingi Mitandaoni. Tunataka Vijana wajue kutumia Mitandao ya Kijamii wakiwa na ajenda maalum na zenye tija
Tunawashukuru JamiiForums kwa utayari wao wa kushirikiana na Kituo cha Demokrasia Tanzania
ijana wetu wa kwenye Vyama, niwaambie Kiongozi mahiri ni yule mwenye Taarifa sahihi. Ili kupata Taarifa sahihi tunatakiwa kusoma. Ukitaka kuwa Kiongozi mwenye kutoa hoja, soma!
Niwaombe Vijana msome Katiba, ili muwe na maoni wakati Mchakato huu utakapoanza na mtuoneshe jinsi gani mnataka mabadiliko
Wiebe de Boer, Balozi wa Uholanzi - Tanzania
Napenda kuwashukuru TCD na Uongozi wake kwa Uzinduzi wa Mradi huu wa kuimarisha Ushiriki wa Vijana katika Michakato ya Siasa na Chaguzi
Kuimarisha Kituo cha Demokrasia Nchini ilikuwa hatua ya muhimu baada ya Uchaguzi wa Mwaka 2020
Serikali ya Uholanzi itaendelea kuunga mkono jitihada za kuimarisha Ushiriki wa Vijana katika masuala ya Siasa
Tuna jukumu kubwa la kuwafikia Maelfu ya Vijana kote Nchini Tanzania na kuimarisha ushiriki wao katika masuala ya kisiasa pamoja na michakato ya Chaguzi
Didier Chassot, Balozi wa Uswisi - Tanzania
Nimefurahi kuwa hapa leo na kuongea na Vijana kuhusu masuala ya Siasa na Chaguzi.
Takwimu zinaonesha TTanzania ina kasi kubwa ya ongezeko la Vijana
Tunapongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua zake za kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Vijana
Uswisi imejikita kuimarisha mazingira ya Nafasi za Kiraia (Civic Space) ikiwemo masuala yanayohusu Vijana ili sauti zao zisikike
Nahimiza Vijana kutumia fursa kama hii ya Kituo cha Demokrasia (TCD) na nyingine zilizopo mbele yao ili kuhakikisha sauti zenu zinasikika. Vijana ndio Taifa la Leo
Kadele Mabumba, Hans Seidel Foundation
Tunaona suala la ushiriki wa Vijana katika Siasa ni ajenda ya Kimataifa
Si vibaya kujiuliza katika Platforms ambazo Vijana wanazo, wanapewa nafasi ya kutoa maoni yao?
Vijana ndio walengwa wa Mafunzo yatakayotolewa katika Mradi huu
Ni vizuri Vijana tutakaopata nafasi ya kushiriki mradi huu tuwashirikishe Vijana wengine waliopo katika Vyama vyenu
Maxence Melo, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums
Niwashukuru kwa fursa ya kufanya kazi na TCD
Sisi ni Asasi ya Kiraia na Waendeshaji wa Mtandao wa Where We Dare To Talk Openly wenye ushiriki mkubwa wa kisiasa. Siasa zetu zilipofika, zipo "shaped" na digitali
Hatuamini mnafanya vibaya kwenye Mitandao, tunaamini mnafanya vizuri lakini tunaona inaweza kufanyika vizuri zaidi
Sisi tutawajengea uwezo ili muweze kufanya kazi yenu ya Siasa vizuri kwenye Ulimwengu huu wa Digitali
Prof. Ibrahim Lipumba, Makamu Mwenyekiti wa TCD
Tanzania ni Nchi ya Vijana, matatizo yanayotukabili kama Taifa (Maji safi, Ajira, Huduma Bora nk) ni matatizo yanayowakabili Vijana
Ufumbuzi wa matatizo haya lazima utegemee ushiriki wa Vijana
Vijana lazima muelewe kuwa Demokrasia ni nyenzo ya Maendeleo. Utawala wa Kiimla unaweza kuwa na gharama kubwa
Kiongozi mmoja anapoamua kufanya lolote lile, matokeo yake yanaweza kuwa makubwa
Demokrasia ya kweli inawapa Watu fursa ya kuchagua Viongozi makini wa kusimamia maendeleo yao
Uchaguzi Huru na wa Haki pekee haitoshi, lazima kuwepo na Serikali ambayo inawajibika
Nchi hii hakuna mwenye Hatimiliki, ni yetu sote!
Wananchi wanapenda misingi ya Demokrasia iheshimiwe
Kate Kamba (CCM)
Nimepewa kazi ya kutoa neno la shukrani kwa Mgeni Rasmi (Prof. Ibrahim Lipumba). Niwashukuru wote walioandaa Warsha hii
Vijana lazima mjue Historia, ukishaijua hutakosea. Historia lazima tuijue ili kujijenga. Hapa tulipofika, tumetoka mbali
Tujaribu kufikiria jinsi ya kujenga Nchi yetu kwa kutumia Vyama
Vijana mdai Haki ya Kugombea katika Vyama vyenu. Demokrasia lazima iwe na Usawa wa Kijinsia, na itoe fursa za kugombea Uongozi
Vijana msiogope kugombea! Matatizo yatatatuliwa na Vijana
Twende kwenye Siasa za Kujenga Nchi, na sio zile za "Maji Taka" ambazo hazitatusaidia. Watu hawawezi kuishi kwa maneno tu, Wanahitaji Afya, Elimu nk.
Tukienda hivi Watu wetu hawatapata shida kwani tutakuwa tunajenga Nyumba moja
Jussa Ismail (ACT - Wazalendo)
Tume zetu za Uchaguzi zinateuliwa na Rais, hapati Mapendekezo kutoka kwa yeyote. Matokeo yake tunakuwa na kina 'Jecha'
Jecha aligombea uongozi CCM akaangushwa, akawa M/Kiti wa ZEC; akafanya yake
Mwishoni, alichukua fomu kugombea Urais kupitia CCM
Sheria ya Vyama vya Siasa ilikuwa na Mapungufu yake tangu mwaka 1992. Marekebisho ya Mwaka 2019 yaliweka maoni yote ya Vyama vya Siasa kapuni
Tunaamini Sheria hii inapaswa kuandikwa upya. Msajili wa Vyama vya Siasa awe Msajili, na sio Mdhibiti