Uzoefu wangu wa kwenda kwa Waganga kwa Mwaka mmoja

Uzoefu wangu wa kwenda kwa Waganga kwa Mwaka mmoja

Mimi nilikwenda kwa mganga enzi za ujana na nikaliwa milioni 4 ndani ya miezi miwili kwa ishu ya kuachwa na mpenzi akaolewa na mwingine,aisee popote ulipo Gladys sitokusahau nilikupenda Sana na binti yangu nikampa jina lako,ulinifanya nikaliwe milioni 4 na mganga kwamba utarudi kwangu,nakutakia ndoa njema popote ulipo,pesa zikaliwa na ukurudi kwangu, ukiambiwa na mganga leta pesa aisee lazima utaipata tu na utapeleka iwe kwa kukopa au kuuza chochote, baada ya kushindwa kurudi kwa Glady wangu ikiwemo kuvunja Sana nazi njiapanda aisee Mimi na mganga au mambo ya waganga ni maji na mafuta, ni life experience aisee KILA mtu analo lakupitia.
Alikuwa ni soulmate kwangu aisee ilikuwa ni ngumu kumuacha sababu nafsi zilikuwa zishaungana ni miaka 13 imepita but still umuota mara moja moja.
 
Mimi nilikwenda kwa mganga enzi za ujana na nikaliwa milioni 4 ndani ya miezi miwili kwa ishu ya kuachwa na mpenzi akaolewa na mwingine,aisee popote ulipo Gladys sitokusahau nilikupenda Sana na binti yangu nikampa jina lako,ulinifanya nikaliwe milioni 4 na mganga kwamba utarudi kwangu,nakutakia ndoa njema popote ulipo,pesa zikaliwa na ukurudi kwangu, ukiambiwa na mganga leta pesa aisee lazima utaipata tu na utapeleka iwe kwa kukopa au kuuza chochote, baada ya kushindwa kurudi kwa Glady wangu ikiwemo kuvunja Sana nazi njiapanda aisee Mimi na mganga au mambo ya waganga ni maji na mafuta, ni life experience aisee KILA mtu analo lakupitia.
Alikuwa ni soulmate kwangu aisee ilikuwa ni ngumu kumuacha sababu nafsi zilikuwa zishaungana ni miaka 13 imepita but still umuota mara moja moja.
Angekuwa soulmate angekuacha? Wewe ndio ulimpenda sio yeye ndio maana akakuacha!

Soulmate sio ya upande mmoja, ni wote wawili mnapenda na kuelewana katika SHIDA na raha!
 
Salam,

Katika maisha kuna wakati unapitia mambo magumu sana mpaka unataka kukata tamaa, na ukiwa katika hali hiyo washauri wanakuwa wengi lakini huwezi kukosa mtu mmoja atakaye kwambia "Jaribu kuangalia upande wa pili", "Nenda kwa mtaalam, sio bure wewe umerogwa."

Hali hiyo nimeipitia kipindi cha nyuma, mambo yangu yalikuwa hayaendi kabisa nimebanwa hasa. Mshauri akaja akaniambia atanipeleka Kibaha kwa mganga, kweli nilienda kwa mganga. Hiyo ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza katika maisha, niliogopa sana siku hiyo lakini nikasema haina jinsi.

Mganga yule ni mmama maarufu sana pale Kibaha, baada ya kufika nikapanga foleni maana kulikuwa na watu wengi kidogo. Hatimaye zamu yangu ilifika ya kumuona mtaalamu, nilipofika akasema utaniambia shida yako au nikwambie mimi?

Nikaomba aniambie, akapandisha majini pale akaanza kufunguka aliniambia vitu vingi ambavyo vyote ni vya kweli. Nikasema hapa ndio penyewe sasa, akaniambia tatizo lako ndani ya wiki moja litakuwa limeisha. Akanipa dawa za kuoga, nyingine nilioga pale pale na nyingine nilienda kuoga nyumbani.

Ikaisha wiki hamna kitu, wiki mbili mpaka mwezi tatizo bado. Ukipiga simu kuuliza akasema watu wanatofautiana, wengine dawa hufanya kazi haraka na wengine huchelewa kwa hiyo uwe mvumilivu. Mara kadhaa pia nilikuwa naenda pale kwa ajili ya kuongezewa dozi.

Baada ya miezi miwili nikaona labda tatizo langu kashindwa na hapo ka roho kwa kupenda waganga kaliniingia, nikaanza kuzunguka sehemu mbali pamoja na kuuliza watu waganga nitawapata wapi. Nilipata waganga maeneo mbalimbali; Manzese, Magomeni, Bagamoyo, Morogoro, Tanga, Iringa na Musoma.

Nilichogundua waganga wengi sana wanakwambia mambo ya kila siku ambayo hata wewe unaweza kumwambia mtu mwingine. Mganga anasema; hapa naona pesa kwako haikai (wakati hilo ni swala la kawaida kabisa) au unapishana pishana na mke wako/mume wako, huko kazini kuna watu wanakuchukia nk.

Mganga alikuwa akiniambia hayo mambo ya kawaida nilikuwa naachana nae namwambia ntarudi kupata tiba.

Kwa kipindi chote cha mwaka na kitu, sehemu zote nilizoenda ambaye aliweza kunipa taarifa sensitive ambazo najua hizi hazijui mtu ni sehemu moja tu hapo Kibaha lakini naye hakuweza kutatua matatizo yangu.

Hivyo, binafsi naona waganga hawana uwezo wa kutatua shida za watu bali wamejawa na uongo na utapeli. Huo ndio uzoefu wangu mimi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwenda kwa waganga, kama una uzoefu tofauti share na wewe.
The unpaid Seller Utingo Mshana Jr Soma Tena Mzee Wa Kazi Chafu mjingamimi bagamoyo
 
Mambo yamehamia kwa manabii na mitume sasa wewee . ...huko ni kupiga hela tu
 
Salam,

Katika maisha kuna wakati unapitia mambo magumu sana mpaka unataka kukata tamaa, na ukiwa katika hali hiyo washauri wanakuwa wengi lakini huwezi kukosa mtu mmoja atakaye kwambia "Jaribu kuangalia upande wa pili", "Nenda kwa mtaalam, sio bure wewe umerogwa."

Hali hiyo nimeipitia kipindi cha nyuma, mambo yangu yalikuwa hayaendi kabisa nimebanwa hasa. Mshauri akaja akaniambia atanipeleka Kibaha kwa mganga, kweli nilienda kwa mganga. Hiyo ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza katika maisha, niliogopa sana siku hiyo lakini nikasema haina jinsi.

Mganga yule ni mmama maarufu sana pale Kibaha, baada ya kufika nikapanga foleni maana kulikuwa na watu wengi kidogo. Hatimaye zamu yangu ilifika ya kumuona mtaalamu, nilipofika akasema utaniambia shida yako au nikwambie mimi?

Nikaomba aniambie, akapandisha majini pale akaanza kufunguka aliniambia vitu vingi ambavyo vyote ni vya kweli. Nikasema hapa ndio penyewe sasa, akaniambia tatizo lako ndani ya wiki moja litakuwa limeisha. Akanipa dawa za kuoga, nyingine nilioga pale pale na nyingine nilienda kuoga nyumbani.

Ikaisha wiki hamna kitu, wiki mbili mpaka mwezi tatizo bado. Ukipiga simu kuuliza akasema watu wanatofautiana, wengine dawa hufanya kazi haraka na wengine huchelewa kwa hiyo uwe mvumilivu. Mara kadhaa pia nilikuwa naenda pale kwa ajili ya kuongezewa dozi.

Baada ya miezi miwili nikaona labda tatizo langu kashindwa na hapo ka roho kwa kupenda waganga kaliniingia, nikaanza kuzunguka sehemu mbali pamoja na kuuliza watu waganga nitawapata wapi. Nilipata waganga maeneo mbalimbali; Manzese, Magomeni, Bagamoyo, Morogoro, Tanga, Iringa na Musoma.

Nilichogundua waganga wengi sana wanakwambia mambo ya kila siku ambayo hata wewe unaweza kumwambia mtu mwingine. Mganga anasema; hapa naona pesa kwako haikai (wakati hilo ni swala la kawaida kabisa) au unapishana pishana na mke wako/mume wako, huko kazini kuna watu wanakuchukia nk.

Mganga alikuwa akiniambia hayo mambo ya kawaida nilikuwa naachana nae namwambia ntarudi kupata tiba.

Kwa kipindi chote cha mwaka na kitu, sehemu zote nilizoenda ambaye aliweza kunipa taarifa sensitive ambazo najua hizi hazijui mtu ni sehemu moja tu hapo Kibaha lakini naye hakuweza kutatua matatizo yangu.

Hivyo, binafsi naona waganga hawana uwezo wa kutatua shida za watu bali wamejawa na uongo na utapeli. Huo ndio uzoefu wangu mimi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwenda kwa waganga, kama una uzoefu tofauti share na wewe.
Pesa ililiwa kimasihara😂
 
Jamaa; Mganga naomba nisaidie kuangalia mwanangu wamemfanya nini,sana anaumwa maradhi ya ajabu ajabu tukienda hospital hatuoni ugonjwa wowote na sawa hazimsaidii..usiku halali
Msaidie kijana wangu


Mganga: mzee,mizimu inaonesha kijana wako amelala na mke wa mtu mwenye mke kamroga.

Jamaa: heee!!mwanangu Ni mtoto mchanga wa mwaka mmoja..

Mganga:...........
 
Jamaa; Mganga naomba nisaidie kuangalia mwanangu wamemfanya nini,sana anaumwa maradhi ya ajabu ajabu tukienda hospital hatuoni ugonjwa wowote na sawa hazimsaidii..usiku halali
Msaidie kijana wangu


Mganga: mzee,mizimu inaonesha kijana wako amelala na mke wa mtu mwenye mke kamroga.

Jamaa: heee!!mwanangu Ni mtoto mchanga wa mwaka mmoja..

Mganga:...........
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi nilikwenda kwa mganga enzi za ujana na nikaliwa milioni 4 ndani ya miezi miwili kwa ishu ya kuachwa na mpenzi akaolewa na mwingine,aisee popote ulipo Gladys sitokusahau nilikupenda Sana na binti yangu nikampa jina lako,ulinifanya nikaliwe milioni 4 na mganga kwamba utarudi kwangu,nakutakia ndoa njema popote ulipo,pesa zikaliwa na ukurudi kwangu, ukiambiwa na mganga leta pesa aisee lazima utaipata tu na utapeleka iwe kwa kukopa au kuuza chochote, baada ya kushindwa kurudi kwa Glady wangu ikiwemo kuvunja Sana nazi njiapanda aisee Mimi na mganga au mambo ya waganga ni maji na mafuta, ni life experience aisee KILA mtu analo lakupitia.
Alikuwa ni soulmate kwangu aisee ilikuwa ni ngumu kumuacha sababu nafsi zilikuwa zishaungana ni miaka 13 imepita but still umuota mara moja moja.
Pole sana aseee...mjifunze kuwa na mwanamke zaidi ya mmoja..hayo ndio madhara ya kuwa na mwanamke mmoja tu anayempenda zaidi ya unavyojipenda.

Kuhusu waganga hapa ndio naona ulipoanza chukia nao baaada ya kuingia mkenge..ila waganga wa kweli wapo na wanapiga kazi vzr tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Waganga na wapandisha mashetani na majini wengi wana uwezo tu wa kukwambia kilichokwisha kukutokea lakini si kijacho ama suluhu yake..
Na hicho kilichokwiahatokea kiroho tunaita ni tendo mfu lilishakamilika na linajulikana hivyo halina madhara tena

Hawa matatibu wanachofanya sio kutibu mzizi wa tatizo bali ni kutafuta tu kukupa unafuu ama kubahatisha

Tiba halisi za kichawi ni kutumia furmula ileile iliyotumika kukuroga ili upate codes na tracking mpaka tatizo lilipoanzia. Tofauti na hapo ni story tuu..

Kama kucha ama nywele zako zilifungwa na kufukiwa mahali ni mpaka mtaalam avipate hivyo vitu avifukue avifubaze .. Akishindwa kufanya hivyo hakuna tiba hapo

Shida inayowakumba wengi ni kupata ile formula na mahali kitu kilipowekwa.. Kwakuwa kama kuna kitu kiko complicated kwenye ushirikina ni njia iliyotumika kukuroga
Mshana Jr .
Mie ndugu yangu inaonekana ametupiwa Vipande vya majini Ni zaidi ya miaka 10 sasa.
Anasikia makelele kwenye masikio, maumivu sehem ya mwili.nk tiba yake inawezekana je mkuu.


Naona tuna waganga zaidi ya watatu lakini wameshindwa.
 
Imani zetu tulizonazo ziwe positive au negative zina nguvu kubwa ya ajabu kuliko tunavyofikiri. Chochote unachoiaminisha akili yako kitajenga imani inayoongoza maisha yako, katika kufanikiwa au kuanguka. Ni imani yako tu, lakini ina nguvu sana. Hata wale waliofanikiwa wakiamini ni kupitia mganga au aina yoyote ya ushirikina, hawakufanikiwa kwasababu hiyo ya uganga, bali walifanikiwa kwasababu mganga au ushirikina uliwapa nguvu ya imani kwamba wanaweza na watafanikiwa au hawawezi na hawatafanikiwa. Ukiibeba imani na ikawa yako na kuendelea kuamini unachoamini ndivyo itakavyokuwa. Ni dhana ngumu kidogo kuielewa.

Imani tulizonazo zinatokana na akili zetu, kwamba unacholisha kwenye akili yako, ndicho kinageuka na kuwa imani yako, hivyo akili yako ukiilisha ujinga, utakuwa na imani nyingi za kijinga na maisha yako yatajaa ujinga,........ na ukiilisha akili yako mambo mema ya maana, utakuwa na imani ya maana na kupelekea kuwa na maisha ya mema na ya maana. Hapa inategemea tafsiri yako ya 'maisha ya maana au kijinga ' ni nini kwako.

Ukiamini kwa moyo wako wote kwamba una uwezo wa kufanya jambo fulani, na hata kama kuna vikwazo na changamoto mbalimbali, bado haibadilishi imani yako kwamba utafanikiwa unachokitaka. Vivyo hivyo ukiamini kwa moyo wako wote, kwamba huna uwezo, umekata tamaa na kwamba hutafanikiwa unachotaka, basi ni kweli kwamba hutafanikiwa.

Hebu jiulize mambo mangapi ulidhani ni magumu?, lakini uliamini kwamba unaweza na utafanikiwa, na kweli ulifanikiwa. Hapo hapo hebu rudi nyuma utafakari mchakato wake, na jinsi ulivyojenga fikra zilizokusukuma na kukujengea imani kwamba utafanikiwa.

Imani hizi haziishii kwa waganga tu, zinakwenda hata kwenye imani za kidini, kimahusiano, makazini, na zinaongoza maisha yetu ya kila siku.

Kama unataka kubadili maisha yako ili yawe bora zaidi, acha kuilisha akili yako mambo ya hovyo, na anza kuilisha akili yako mambo mazuri ya maana na hatimaye utajenga imani yenye kupelekea maisha bora uyatakayo. Hakikisha imani yako kwamba utafanikiwa - haitetereki

Mwana falsafa mmoja aliwahi kusema haya:
Beliefs have the power to create and the power to destroy. One person with a belief is equal to ninety nine who have only interests.
Kabisa mkuu ubongo kama tumbo kuna mda una njaa

ukiamua kulisha tumbo lako ovyo ndivyo pia na matokeo ya afya yako yatakavyobadilika

Ile nafasi ya ubongo yenye njaa ukaamua kulisha hapo upuuzi na kauupuzi katakaa hapo kwenye ubongo na matokeo yakulisha ujinga kwa ubongo wako yanafahamika

Sent from my SM-G950F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom