Uzoefu wangu wa kwenda kwa Waganga kwa Mwaka mmoja

Uzoefu wangu wa kwenda kwa Waganga kwa Mwaka mmoja

Duh umenikumbusha Jambo man. Siku moja maza anasema alipelekwa kwa mganga na ***** ( Bibi yangu) hivyo basi walipofika ,mwenye shida (mamayangu) akaitwa ndani kusema shida. Basi akaambiwa unafeli wapi wewe? Yule uliyekuja nae yaani Bibi yangu ndo humroga!
Cha ajabu Yule Bibi yangu alipata ugonjwa wa presha kisa tatizo la mwanae. Iweje amroge?
Basi maza anasema alipotoka ndani akaulizwa umeambiwaje mwanangu ? Akamjibu nimepewa dawa nitumie nitapona.
Bibi alifariki miaka 21 iliopita. Maza Yuko Hadi leo . Hutumia stories hii kutukumbusha fitna za waganga na wachawi

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Duh umenikumbusha Jambo man. Siku moja maza anasema alipelekwa kwa mganga na mama yake( Bibi yangu) hivyo basi walipofika ,mwenye shida (mamayangu) akaitwa ndani kusema shida. Basi akaambiwa unafeli wapi wewe? Yule uliyekuja nae yaani Bibi yangu ndo humroga!
Cha ajabu Yule Bibi yangu alipata ugonjwa wa presha kisa tatizo la mwanae. Iweje amroge?
Basi maza anasema alipotoka ndani akaulizwa umeambiwaje mwanangu ? Akamjibu nimepewa dawa nitumie nitapona.
Bibi alifariki miaka 21 iliopita. Maza Yuko Hadi leo . Hutumia stories hii kutukumbusha fitna za waganga na wachawi

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Jamaa; Mganga naomba nisaidie kuangalia mwanangu wamemfanya nini,sana anaumwa maradhi ya ajabu ajabu tukienda hospital hatuoni ugonjwa wowote na sawa hazimsaidii..usiku halali
Msaidie kijana wangu


Mganga: mzee,mizimu inaonesha kijana wako amelala na mke wa mtu mwenye mke kamroga.

Jamaa: heee!!mwanangu Ni mtoto mchanga wa mwaka mmoja..

Mganga:...........
Ha ha ha.ikawaje sasa mkuu?
 
Huko ni uhuni tu. Me nilipewa dawa ya mpenzi nikaambiwa demu mwenyewe atanitafuta tena walikuwa mademu wawili.

Wiki ya tatu hii bado nasikilizia ila sioni dalili.

Nahesabu nimepigwa
Kijana wanawake wanavutwa kwa pesa na chakula kitamu tu mitishamba haitasidia kama huna pesa
 
Salam,

Katika maisha kuna wakati unapitia mambo magumu sana mpaka unataka kukata tamaa, na ukiwa katika hali hiyo washauri wanakuwa wengi lakini huwezi kukosa mtu mmoja atakaye kwambia "Jaribu kuangalia upande wa pili", "Nenda kwa mtaalam, sio bure wewe umerogwa."

Hali hiyo nimeipitia kipindi cha nyuma, mambo yangu yalikuwa hayaendi kabisa nimebanwa hasa. Mshauri akaja akaniambia atanipeleka Kibaha kwa mganga, kweli nilienda kwa mganga. Hiyo ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza katika maisha, niliogopa sana siku hiyo lakini nikasema haina jinsi.

Mganga yule ni mmama maarufu sana pale Kibaha, baada ya kufika nikapanga foleni maana kulikuwa na watu wengi kidogo. Hatimaye zamu yangu ilifika ya kumuona mtaalamu, nilipofika akasema utaniambia shida yako au nikwambie mimi?

Nikaomba aniambie, akapandisha majini pale akaanza kufunguka aliniambia vitu vingi ambavyo vyote ni vya kweli. Nikasema hapa ndio penyewe sasa, akaniambia tatizo lako ndani ya wiki moja litakuwa limeisha. Akanipa dawa za kuoga, nyingine nilioga pale pale na nyingine nilienda kuoga nyumbani.

Ikaisha wiki hamna kitu, wiki mbili mpaka mwezi tatizo bado. Ukipiga simu kuuliza akasema watu wanatofautiana, wengine dawa hufanya kazi haraka na wengine huchelewa kwa hiyo uwe mvumilivu. Mara kadhaa pia nilikuwa naenda pale kwa ajili ya kuongezewa dozi.

Baada ya miezi miwili nikaona labda tatizo langu kashindwa na hapo ka roho kwa kupenda waganga kaliniingia, nikaanza kuzunguka sehemu mbali pamoja na kuuliza watu waganga nitawapata wapi. Nilipata waganga maeneo mbalimbali; Manzese, Magomeni, Bagamoyo, Morogoro, Tanga, Iringa na Musoma.

Nilichogundua waganga wengi sana wanakwambia mambo ya kila siku ambayo hata wewe unaweza kumwambia mtu mwingine. Mganga anasema; hapa naona pesa kwako haikai (wakati hilo ni swala la kawaida kabisa) au unapishana pishana na mke wako/mume wako, huko kazini kuna watu wanakuchukia nk.

Mganga alikuwa akiniambia hayo mambo ya kawaida nilikuwa naachana nae namwambia ntarudi kupata tiba.

Kwa kipindi chote cha mwaka na kitu, sehemu zote nilizoenda ambaye aliweza kunipa taarifa sensitive ambazo najua hizi hazijui mtu ni sehemu moja tu hapo Kibaha lakini naye hakuweza kutatua matatizo yangu.

Hivyo, binafsi naona waganga hawana uwezo wa kutatua shida za watu bali wamejawa na uongo na utapeli. Huo ndio uzoefu wangu mimi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwenda kwa waganga, kama una uzoefu tofauti share na wewe.
Ndugu yangu
Njoo kwa Yesu atakusamehe dhambi zako na kukutatulia shida zako zote.


Anafanya bure. Unachotakiwa kuwa nacho ni Imani pekee
 
Salam,

Katika maisha kuna wakati unapitia mambo magumu sana mpaka unataka kukata tamaa, na ukiwa katika hali hiyo washauri wanakuwa wengi lakini huwezi kukosa mtu mmoja atakaye kwambia "Jaribu kuangalia upande wa pili", "Nenda kwa mtaalam, sio bure wewe umerogwa."

Hali hiyo nimeipitia kipindi cha nyuma, mambo yangu yalikuwa hayaendi kabisa nimebanwa hasa. Mshauri akaja akaniambia atanipeleka Kibaha kwa mganga, kweli nilienda kwa mganga. Hiyo ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza katika maisha, niliogopa sana siku hiyo lakini nikasema haina jinsi.

Mganga yule ni mmama maarufu sana pale Kibaha, baada ya kufika nikapanga foleni maana kulikuwa na watu wengi kidogo. Hatimaye zamu yangu ilifika ya kumuona mtaalamu, nilipofika akasema utaniambia shida yako au nikwambie mimi?

Nikaomba aniambie, akapandisha majini pale akaanza kufunguka aliniambia vitu vingi ambavyo vyote ni vya kweli. Nikasema hapa ndio penyewe sasa, akaniambia tatizo lako ndani ya wiki moja litakuwa limeisha. Akanipa dawa za kuoga, nyingine nilioga pale pale na nyingine nilienda kuoga nyumbani.

Ikaisha wiki hamna kitu, wiki mbili mpaka mwezi tatizo bado. Ukipiga simu kuuliza akasema watu wanatofautiana, wengine dawa hufanya kazi haraka na wengine huchelewa kwa hiyo uwe mvumilivu. Mara kadhaa pia nilikuwa naenda pale kwa ajili ya kuongezewa dozi.

Baada ya miezi miwili nikaona labda tatizo langu kashindwa na hapo ka roho kwa kupenda waganga kaliniingia, nikaanza kuzunguka sehemu mbali pamoja na kuuliza watu waganga nitawapata wapi. Nilipata waganga maeneo mbalimbali; Manzese, Magomeni, Bagamoyo, Morogoro, Tanga, Iringa na Musoma.

Nilichogundua waganga wengi sana wanakwambia mambo ya kila siku ambayo hata wewe unaweza kumwambia mtu mwingine. Mganga anasema; hapa naona pesa kwako haikai (wakati hilo ni swala la kawaida kabisa) au unapishana pishana na mke wako/mume wako, huko kazini kuna watu wanakuchukia nk.

Mganga alikuwa akiniambia hayo mambo ya kawaida nilikuwa naachana nae namwambia ntarudi kupata tiba.

Kwa kipindi chote cha mwaka na kitu, sehemu zote nilizoenda ambaye aliweza kunipa taarifa sensitive ambazo najua hizi hazijui mtu ni sehemu moja tu hapo Kibaha lakini naye hakuweza kutatua matatizo yangu.

Hivyo, binafsi naona waganga hawana uwezo wa kutatua shida za watu bali wamejawa na uongo na utapeli. Huo ndio uzoefu wangu mimi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwenda kwa waganga, kama una uzoefu tofauti share na wewe.
Ni mwezi umepita napiga gambe, asbh nina stress nakutana na mganga..tukakubaliana akajinadi paleee nikasema sawa subiri nitamtafuta, akaja sema nimtumie elfu 5 aanze kazi nikatuma..

Akanitafuta, kwenda home kwake pa kawaida mno..nikanote.

Akaanza story, za ww pesa inaingia mkono wa kupokelea na zinatoka yaani haikai, ila anaona magari, nyumba na mali nyingi kwangu, nikasema sawa eeh tufanyaje?

Akapiga story zake, mara sijui koo nne zipo kwa baba na mama, ila mama hawanaga shida ila ni koo nne za baba tuziangalie..nikasema sawa, eeeh

Piga sana porojo pale, nilikua sina kitu nimeamka na elfu 9 nikanywa chai ya buku ikabaki elfu nane...

Sasa anasema tununue kuku wadogo wawili, tuanze kazi na dawa nioge...eeeh sawa ila mm sina kitu leo, hapo napigia hesabu elfu nane yangu inisogeze kwenye kula.

Nikakaza, kwenye stori nikajichanganya nina elfu 8 imebakia ya kula, eeeeh akaanza itaka ile elfu nane tununue kuku mmoja nianze dawa pesa ntapata au ntaenda kula kwake mpaka yakae sawa, ndio nikamuona hamna mganga hapa ni kichaa tu bora mm.

Nikakaza siwezi kumpa hiyo pesa, nikaaga akagoma kunisindikiza na tulienda wote kwake..hahaha

Nikarudi home, nikajiuliza sijawahi kwenda kwa mganga mbna kazi nilikua napata mwanzo, kwaiyo akili imechoka nianze kumtegemea binadamu mwenzangu,kweli??

Sitokaa nirudi maisha yangu, ila kama mtu haujui vitu vingi na uingiliani na watu..wanakuchota akili wajinga kabisa..kumtegemea binadamu kama ww..hamna
 
Waganga wa kweli wapo
tena wanao jua hasa

alafu sasa wanafahamiana, mfano kilinge kikichafuliwa ama likitokea tatizo kubwa maruhani/majadi huelekeza nani ana uwezo kama wao wa kutatua shida iyo

haya majini huzidiana nguvu tena sana, nimewahi shuhudia mke wa jamaa alipandisha majini/maruhani akawa anamwambia mmewe mambo ya ofisini akamtaja mwamba mmoja kwamba hawezekani kurogwa ni chuma mnooooo

jamaa katika udadisi akawa anamuuliza anatumia dawa/mganga gani yule mke wa jamaa anasema haoni kitu zaidi ya kuona jamaa ni nondo na hawezekani
 
Waganga na wapandisha mashetani na majini wengi wana uwezo tu wa kukwambia kilichokwisha kukutokea lakini si kijacho ama suluhu yake..
Na hicho kilichokwiahatokea kiroho tunaita ni tendo mfu lilishakamilika na linajulikana hivyo halina madhara tena

Hawa matatibu wanachofanya sio kutibu mzizi wa tatizo bali ni kutafuta tu kukupa unafuu ama kubahatisha

Tiba halisi za kichawi ni kutumia formula ileile iliyotumika kukuroga ili upate codes na tracking mpaka tatizo lilipoanzia. Tofauti na hapo ni story tuu..

Kama kucha ama nywele zako zilifungwa na kufukiwa mahali ni mpaka mtaalam avipate hivyo vitu avifukue avifubaze .. Akishindwa kufanya hivyo hakuna tiba hapo

Shida inayowakumba wengi ni kupata ile formula na mahali kitu kilipowekwa.. Kwakuwa kama kuna kitu kiko complicated kwenye ushirikina ni njia iliyotumika kukuroga
mkuu kuna waganga wanajua na wanajua tena na tena ila ni wachache na wanafahamiana

kuna waganga unaenda anakwambia tiba yako inaweza chukua hata mwaka mzima sasa chagua azime moto (akufungie mambo yako haraka haraka ) ama aanze mdg mdg kuchimbua tatizo

cha kuchosha kwenye kuchimbua tatizo anaibua mengi mnoo na kuna wakati unaanza kudhoofika wakati anakutibu

na wale wabaya wako wakifahamu umeanza shughulikiwa wanakupa roho ya kukataa kuendelea na tiba (mara nyingi mganga wa kweli hakubembelezi anakuacha uende ) wewe hapa utasema alikutapeli (huwa hawachukui hela)

waganga wakweli mara nyingi hawapendi kutibu ila hulazimishwa na maruhani wao/majini na mara nyingi hutibu watu wa familia/koo zao na marafiki wachache

kuhusu kutibu kutokana na ulivyo rogwa ndivyo tiba huwa, huwa wanawavuta wale walio kuloga na kuwaagiza walete kama ni kucha, kutambaa ama kitu kilichofukiwa sehemu. inakuwa(ga) kimbembe kuleta vile vitu maana kuna baadhi ya washiriki kukuloga wanakuwa hawataki kuvitoa ila wanalazimishwa na wanatoa ndio mambo yako yanatengenezwa

tutabishana sana ila kuna waganga wapo wanajua na wanajua tena
 
...Mtume muhammad (s.a.w) anasema"atakeyekwenda kwa mganga au kuhani na akamuamini basi amekufuru na kujivua uislam wake,
na atakayekwenda na asimuamini basi swala zake za siku arubaini hazikubaliki..na atakayemshirikisha mwenyezi mungu basi motoni milele....akifa hvyo.
Dini ya kiislam imekemea vikali sana sana vitendo vya kishirikina
 
Salam,

Katika maisha kuna wakati unapitia mambo magumu sana mpaka unataka kukata tamaa, na ukiwa katika hali hiyo washauri wanakuwa wengi lakini huwezi kukosa mtu mmoja atakaye kwambia "Jaribu kuangalia upande wa pili", "Nenda kwa mtaalam, sio bure wewe umerogwa."

Hali hiyo nimeipitia kipindi cha nyuma, mambo yangu yalikuwa hayaendi kabisa nimebanwa hasa. Mshauri akaja akaniambia atanipeleka Kibaha kwa mganga, kweli nilienda kwa mganga. Hiyo ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza katika maisha, niliogopa sana siku hiyo lakini nikasema haina jinsi.

Mganga yule ni mmama maarufu sana pale Kibaha, baada ya kufika nikapanga foleni maana kulikuwa na watu wengi kidogo. Hatimaye zamu yangu ilifika ya kumuona mtaalamu, nilipofika akasema utaniambia shida yako au nikwambie mimi?

Nikaomba aniambie, akapandisha majini pale akaanza kufunguka aliniambia vitu vingi ambavyo vyote ni vya kweli. Nikasema hapa ndio penyewe sasa, akaniambia tatizo lako ndani ya wiki moja litakuwa limeisha. Akanipa dawa za kuoga, nyingine nilioga pale pale na nyingine nilienda kuoga nyumbani.

Ikaisha wiki hamna kitu, wiki mbili mpaka mwezi tatizo bado. Ukipiga simu kuuliza akasema watu wanatofautiana, wengine dawa hufanya kazi haraka na wengine huchelewa kwa hiyo uwe mvumilivu. Mara kadhaa pia nilikuwa naenda pale kwa ajili ya kuongezewa dozi.

Baada ya miezi miwili nikaona labda tatizo langu kashindwa na hapo ka roho kwa kupenda waganga kaliniingia, nikaanza kuzunguka sehemu mbali pamoja na kuuliza watu waganga nitawapata wapi. Nilipata waganga maeneo mbalimbali; Manzese, Magomeni, Bagamoyo, Morogoro, Tanga, Iringa na Musoma.

Nilichogundua waganga wengi sana wanakwambia mambo ya kila siku ambayo hata wewe unaweza kumwambia mtu mwingine. Mganga anasema; hapa naona pesa kwako haikai (wakati hilo ni swala la kawaida kabisa) au unapishana pishana na mke wako/mume wako, huko kazini kuna watu wanakuchukia nk.

Mganga alikuwa akiniambia hayo mambo ya kawaida nilikuwa naachana nae namwambia ntarudi kupata tiba.

Kwa kipindi chote cha mwaka na kitu, sehemu zote nilizoenda ambaye aliweza kunipa taarifa sensitive ambazo najua hizi hazijui mtu ni sehemu moja tu hapo Kibaha lakini naye hakuweza kutatua matatizo yangu.

Hivyo, binafsi naona waganga hawana uwezo wa kutatua shida za watu bali wamejawa na uongo na utapeli. Huo ndio uzoefu wangu mimi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwenda kwa waganga, kama una uzoefu tofauti share na wewe.
Duh
 
Mimi nilijua uganga ni uwongo mtupu long time ago, uncle wetu aliwahi kujifanya mganga kumbe ilikuwa ni njaa zake tuu, basi mother akamwambia najua unachofanya na ushetani wako na usipoacha ill expose you, uncle alikuwa akisema mimi natengeneza pesa tuu sister nikimaliza shida zangu nitaacha na wakati mwingine alikuwa anaongea wazi wazi kuhusu kula pesa za wajinga huku sisi tukicheka, hakuishia hapo alipoacha uganga akaingia kwenye uhubiri wa kusali usiku kucha kwa akili yake ya kutafuta umaarufu na kupiga mademu, alikuwa vituko kweli kweli lakini naona siku hizi yuko normal na ana familia nzuri tuu
 
mkuu kuna waganga wanajua na wanajua tena na tena ila ni wachache na wanafahamiana

kuna waganga unaenda anakwambia tiba yako inaweza chukua hata mwaka mzima sasa chagua azime moto (akufungie mambo yako haraka haraka ) ama aanze mdg mdg kuchimbua tatizo

cha kuchosha kwenye kuchimbua tatizo anaibua mengi mnoo na kuna wakati unaanza kudhoofika wakati anakutibu

na wale wabaya wako wakifahamu umeanza shughulikiwa wanakupa roho ya kukataa kuendelea na tiba (mara nyingi mganga wa kweli hakubembelezi anakuacha uende ) wewe hapa utasema alikutapeli (huwa hawachukui hela)

waganga wakweli mara nyingi hawapendi kutibu ila hulazimishwa na maruhani wao/majini na mara nyingi hutibu watu wa familia/koo zao na marafiki wachache

kuhusu kutibu kutokana na ulivyo rogwa ndivyo tiba huwa, huwa wanawavuta wale walio kuloga na kuwaagiza walete kama ni kucha, kutambaa ama kitu kilichofukiwa sehemu. inakuwa(ga) kimbembe kuleta vile vitu maana kuna baadhi ya washiriki kukuloga wanakuwa hawataki kuvitoa ila wanalazimishwa na wanatoa ndio mambo yako yanatengenezwa

tutabishana sana ila kuna waganga wapo wanajua na wanajua tena
Tuwekee na walipo asa mwanza apa😁
 
Tuwekee na walipo asa mwanza apa😁
hapa natoa ushuhuda tu wa ninayo fahamu

kuhusu kumpeleka mtu, siwezi mpeleka mtu yoyote wa humu maana moja ya sharti la huko

ukimpeleka mtu akaharibu basi adhabu huwa hadi kwako kwa uliye mpeleka. pia unaweza kuwa na haraka ya tiba ukaona ni uongo maana muhusika ana haraka ya kutibu
 
hapa natoa ushuhuda tu wa ninayo fahamu

kuhusu kumpeleka mtu, siwezi mpeleka mtu yoyote wa humu maana moja ya sharti la huko

ukimpeleka mtu akaharibu basi adhabu huwa hadi kwako kwa uliye mpeleka. pia unaweza kuwa na haraka ya tiba ukaona ni uongo maana muhusika ana haraka ya kutibu
Duuh ata kuelekeza tu ni kuvunja masharti kaz kweli kweli
 
...Mtume muhammad (s.a.w) anasema"atakeyekwenda kwa mganga au kuhani na akamuamini basi amekufuru na kujivua uislam wake,
na atakayekwenda na asimuamini basi swala zake za siku arubaini hazikubaliki..na atakayemshirikisha mwenyezi mungu basi motoni milele....akifa hvyo.
Dini ya kiislam imekemea vikali sana sana vitendo vya kishirikina
Sasa unakwendaje kwa mganga halafu usimuamini?
 
Back
Top Bottom