VAT itaua makampuni mengi ya mikoani, TRA angalieni hili

Mimi ndio maana nasema serikali inakosa mapato mengi sana kutoka kwenye informal business, zina mzunguko mkubwa sana wa pesa lakini haziliingizii pesa taifa,
Nadhani kama kuna kazi kubwa wizarw ya viwanda na biashara wanatakiwa kuifanyia kwa nguvu tena urgently ni kurasimisha biashara...output ya MKURABITA nadhani ilitakiwa iwe hivi ...hii itaongeza tax base then hata VAT inaweza shushwa kidogo kwa sababu base itakua kubwa ..
 
Too bad.
 
Tangu huyo mzungu aseme Hadi Leo no kweli tz haijapiga hatua!?.. FDI ni Hasi au chanya!?..akiongea mzungu unaona la maana!!
Actually huyo mzungu aliongelea kua income tax Tanzania ni kubwa which is fact, income tax Tz ni 30% which makes it hard to build capital ...so basically Bado hatujapiga hatua kwenye Hilo ..sorry
 
Actually huyo mzungu aliongelea kua income tax Tanzania ni kubwa which is fact, income tax Tz ni 30% which makes it hard to build capital ...so basically Bado hatujapiga hatua kwenye Hilo ..sorry
nimekuuliza tangu huyo mzungu aongee huo upuuzi FDI imepungua au imeongezeka!?..sijauliza income tax Mimi,kwao income tax ni kiasi gani!?
 
Huyo mzungu hakuongelea fdi,
Unajua FDI ni nini!?.. foreign direct investment,huyo mpuuzi wako kadai makampuni hayatokuja,ndo nakuuliza tangu aseme FDI imeshuka au imepanda!?
 
VAT ilikuja 1997,tukapiga kelele wee Ila ipo na siku zinaenda,Kodi hamtaki,tozo hamtaki,kukopa hamtaki,pesa za miradi na kuendesha nchi zitatoka wapi enyi mbuzi!?

Mbuzi na nguchiro ni wewe usiejua biashara, nani umeona kakataa kulipa kodi, umeelewa alichoclaim mtoa maada au unakurupuka tu
 
Mbuzi na nguchiro ni wewe usiejua biashara, nani umeona kakataa kulipa kodi, umeelewa alichoclaim mtoa maada au unakurupuka tu
Ku-claim!?...hakuna la maana hapo zaidi ya kutaka Kodi zisiwepo/zipingue
 
Njoo tulime kama ID yako sisi wakulima hatujui VAT ni mdudu gani
 
kwa case yako lazima uziweke bidhaa zile unanunua kwa vat utachaji na mboga mboga unazonunua bila vat huzichaji wakati wa utoaji wa risiti, ninakushauri haya kwa uzoefu wa kuendesha biashara yenye kujumuisha bidhaa zinazonunuliwa na risiti na nyingine bila risiti ila ni lazima uwe smart na usikubali kuyumbishwa vinginevyo utaifunga biashara bila kupenda.
 
Unajua FDI ni nini!?.. foreign direct investment,huyo mpuuzi wako kadai makampuni hayatokuja,ndo nakuuliza tangu aseme FDI imeshuka au imepanda!?
Najua maana ya fdi, hii ni discussion tu tumia lugha yenye staha...huyo jamaa Aliyemquote mzungu alikosea ndio maana nikamrekebisha ... kwenye hiyo video hakuna sehemu imezungumzwa fdi , imezungumzwa income tax na impact yake kwenye ku build capital...
 
Alisema hakuna investment itakuja so hatutoendelea
 
Ni senator wa Marekani ,tena alitolea mfano specific Tanzania , hahaaa ili uone hali ilivyo mbaya , hiyo video ninayo ,akiongelea hili suala la VAT Tanzania pia
 
Hoja yangu umeielewa? Nimependekeza nini na kwa sababu gani? Au unasoma heading tu na kukimbilia kucomment?
 
Huwa nashangaa sana. Tanzania mfanyabiashara anachukuliwa kama mhalifu na mamlaka za serikali.

Hakuna juhudi ya kumfanya mfanyabiashara astawi zaidi ya kutengeneza mazingira adidimie na afilisike.

Hao wafanyakazi wanao tunatuna maofisini hawajui kwamba bila wafanyabiashara wao hawaoati mishahara?
 
Hoja yangu umeielewa? Nimependekeza nini na kwa sababu gani? Au unasoma heading tu na kukimbilia kucomment?
Kwakweli nimeelea nusu kwa sababu umeandika so generic na kuambatanisha kodi tofauti katika jedwali moja ukitaka ziunganishwe katika ulipaji.

Either way kwenye VAT hakuna kulipa mara mbili, na wala aitakiwi kuwa na athari kwa mfanyabiashara kwa sababu ni kodi ya mlaji.

Kitu ambacho ukipi maanani katika pendekezo lako ni tafsiri yenyewe ya VAT (‘value added tax) au kodi ya ongezeko la thamani. Sina shaka unaelewa hizo definition ila sidhani una apply katika mapendekezo.

Bidhaa (finished goods) inapanda thamani at each stage of the supply chain. Mfano Manufacture atauza kwa retailer gross 1180, katika hiyo net ambayo ya biashara tsh 1000 + 18% Vat (tsh 180),retailer nae atauza gross tsh 1416, net yake tsh 1200 + 18% Vat (tsh 216) at each stage of the supply VAT inaongezeka.

Sasa TRA na kwengine kote duniani wao wanataka thamani ya juu kabisa ya VAT katika hiyo safari ya bidhaa hadi kufikia kwa mlaji. Manufacture alie charge VAT tsh 180 kwa retailer na kuwapa TRA, retailer hiyo hela ataenda idai na kurudishiwa. Na retailer atapeleka tsh 216 ambayo mlaji awezi idai. Ndio maana ikaitwa kodi ya ongezeko la thamani.

Kurahisisha hizo hesabu za VAT watu wanafanya booking, better still kuna software applications.

Utakiwi kupiga hesabu za revenue kupata VAT ya kulipa. Kwa sababu kama ni duka unaweza kuwa unauza na bidhaa ambazo VAT zake tofauti sio kila kitu VAT ni 18% zingine ni lower.

If you done booking kwenye ledgers unatenga gross ya kila bidhaa ‘net’ pekee yake na ‘vat’ pekee. Kwa mifano yetu 1200 net, VAT 216. Baada ya hapo all the nets zinaenda kwenye trial balance, income statement; wakati VAT zinaenda kwengine kwenye return account.

Mie sielewi kwanini hii concept ya VAT kwa baadhi ya watu ni shida kuilewa tena unakuta ana biashara wakati huku kijijini kwetu ni accounting miezi ya mwanzo tu mwaka wa kwanza utasoma hayo mambo miezi michache tu maana ni straigt forward., Na kufanya kazi ya booking uitaji ata qualification ya accounting huku kijijini kwetu zaidi ya kujua kutumia computer tu na simple arithmetic.

Mziki wa accounting nchi za wenzetu upo kwenye income/corporate tax mbinu za kuipunguza hiyo kodi, kuonyesha biashara ipo vizuri kwa watu watakaosoma hiyo statement kuvutia shareholders, kupata mikopo kirahisi, kumchanganya auditor vitabu vyako safi na unafuata IFRS policies na mambo mengine serious ya kuipamba biashara na kupunguza unavyoweza kama Donald Trump.

Ila napata shida sana kuona watu wanapo struggle na hiii concept ya VAT Tanzania. Yaani ata mtu akimuajili accountant nchi za wenzetu ni kwa sababu ya income tax huko ndio kuna kichefu kichefu lakini sio VAT.
 
Umerudia nilichokiandika, halafu in the end hoja yangu hujaigusa kabisa. Napendekeza kodi zote zitokanazo na biashara za bidhaa (sio huduma) , yaani (VAT , income Tax, service levy etc) zilipwe zote na kwa mara moja kama kodi moja tu, pale pale bandarini au kiwandani, hata kama ni 80% ya thamani ya bidhaa, potelea mbali, lakini ilipwe yote infull. Kwanini? Nimeshaeleza tayari.., sasa jadili hoja badala ya kudodosa dodosa aimlessly kile ambacho nimeshakieleza kwenye preamble.
 
Sasa utawezaje kucharge income tax bila ya kuitoa VAT kwanza.

Hesabu zipo hivi
  1. VAT inatoka kwanza
  2. Net ya mauzo inatengeneza revenue
  3. Unaruhusiwa kutoa costs of sales (ambazo ni gharama za purchase ya hizo bidhaa less VAT if finished good for trade).
  4. Unpata gross profit
  5. Less admin expenses, salaries, bad debt, insurance, OC, insurance na kila aina ya gharama ambayo unadhani imetumika kwenye biashara mpaka mafuta ya gari. charges za kuleta mizigo na kila unachofikiri ni expense.
  6. Unapata income before tax
  7. Unaruhusiwa kutoa qualified charitable donations kabla ya tax
  8. Unaruhusiwa kutoa ‘capital allowances’ mashine ulizonunua kama zina qualify/au depreciation value as an expense
  9. Kilichobaki ndio income tax.
Sasa utawezaje kukata hizo kodi zote kwa pamoja wakati VAT na income/corporate tax hesabu zake tofauti.

Isitoshe kuna maslahi kwenye kulipa kodi sina uhakika Tanzania, ila huku kijiji kwetu kwa mfanya biashara mdogo unapewa miezi tisa baada ya mwaka kodi kuisha ndio umalize deni, biashara kubwa unamiezi zaidi na unalipa on instalment za quarterly.

Kuna tax rebates ukipata hasara kwenye biashara ambayo unaweza dai ufidiwe kupitia kodi ulizolipa nyuma au kudai mbeleni.

Sasa nani mwenye akili timamu atataka hizo kodi zichanganywe. Sio kwamba stages za hesabu zake tofauti kwenye accounting process bali ata maslahi pia. Hakuna mfanyabiashara atakae kuboli hilo.

PS hakuna kodi inayoitwa service levy; hiyo ni income kwa biashara au taasisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…