VAT itaua makampuni mengi ya mikoani, TRA angalieni hili

VAT itaua makampuni mengi ya mikoani, TRA angalieni hili

Sasa utawekaje utawezaje kucharge income tax bila ya kuitoa VAT kwanza.

Hesabu zipo hivi
  1. VAT inatoka kwanza
  2. Net ya mauzo inatengeneza revenue
  3. Unaruhusiwa kutoa costs of sales (ambazo ni gharama za purchase less VAT if finished good for trade).
  4. Unpata gross profit
  5. Less admin expenses, salaries, bad debt, insurance, OC, insurance na kila aina ya gharama ambayo unadhani imetumika kwenye biashara mpaka mafuta ya gari. charges za uzalishaji.
  6. Unapata income before tax
  7. Unaruhusiwa kutoa qualified charitable donations kabla ya tax
  8. Unaruhusiwa kutoa ‘capital allowances’ mashine ulizonunua kama zina qualify/au depreciation value as costs.
  9. Kilichobaki ndio income tax.
Sasa kama utawezaje kukata hizo kodi zote kwa pamoja VAT na income/corporate tax kwa wakati mmoja.

Isitoshe kuna maslahi kwenye kulipa kodi sina uhakika Tanzania, ila huku kijiji kwetu kwa mfanya biashara mdogo unapewa miezi tisa baada ya mwaka kodi kuisha ndio umalize deni, biashara kubwa unamiezi zaidi na unalipa on instalment za quarterly.

Sasa nani mwenye akili timamu atataka hizo kodi zichanganywe. Sio kwamba stages za hesabu zake tofauti kwenye accounting process bali ata maslahi pia. Hakuna mfanyabiashara atakae kuboli hilo.

PS hakuna kodi inayoitwa service levy; hiyo ni income kwa biashara au taasisi.
Wewe unaeleza utaratibu ulivyo, mimi nakueleza ninachopendekeza iwe, na nimeshatoa sababu kwanini iwe hivyo. Sheria tumetunga sisi, hivyo tunaweza kuzibadolisha, au ni msaafu huo? Inshort tunapendekeza kodi moja tu. Hata ikiwa 300% ya thamani ya bidhaa, potelea mbali, na sio lazima iitwe jina tulilozoea, inaweza itwa ‘Total tax’
 
Wewe unaeleza utaratibu ulivyo, mimi nakueleza ninachopendekeza iwe, na nimeshatoa sababu kwanini iwe hivyo. Sheria tumetunga sisi, hivyo tunaweza kuzibadolisha, au ni msaafu huo?
Unachopendekeza akiwezekani sio kwasabu sheria ni tatizo, its impractical kwa accounting steps kuanzia kwenye day book hadi kutengeneza, trial balance, income statement and statement of financial position.

Hizo kodi zipo kwenye stages tofauti, are even an account mbona unapwaya hivyo.
 
Unachopendekeza akiwezekani sio kwasabu sheria ni tatizo, its impractical kwa accounting steps kuanzia kwenye day book hadi kutengeneza, trial balance, income statement and statement of financial position.

Hizo kodi zipo kwenye stages tofauti, are even an account mbona unapwaya hivyo.
Kodi hii haitahitaji chochote kuhusu trial balance wala statement (na ndio lengo kuu, kuondoa complexity na cost za kuikusanya), unaagiza / kuzalisha mzigo wa thsmani x , unslipa kodi 10x bandarini au kiwandani, na habari ineishia hapo. Acha kufikiria ndani ya hilo box ndugu.
 
Kodi hii haitahitaji chochote kuhusu trial balance wala statement (na ndio lengo kuu, kuondoa complexity na cost za kuikusanya), unaagiza mzigo wa thsmani x , unslipa kodi 10x bandarini au kiwandani, na habari ineishia hapo.
Unazungumzia kama mfanyabiasha au individual tu umeagiza au kununua kitu kiwandani kwa matumizi binafsi?

Tuanze hapo ili tuwe kwenye page moja.

Kwasababu income tax ni process ndio maana nikakueleza hiyo ndio sababu kubwa watu wanatumia accountants not because of VAT.
 
Unazungumzia kama mfanyabiasha au individual tu umeagiza au kununua kitu kiwandani?

Tuanze hapo ili tuwe kwenye page moja.

Kwasababu income tax ni process ndio maana nikakueleza hiyo ndio sababu kubwa watu wanatumia accountants not because of VAT.
Nasema hivi, hata kama huo mzigo umeagizwa au kuzalishwa na shetani au jini, achilia mbali kampuni au individual, au hata kama huo mzigo umejiagiza wenyewe, unalamwa ‘Total tax’ ya 500% na habari imeishia hapo..., huku ndani watu wauze kadri watakavyo, hakuna cha Vat, income tax wala chochote!! Maelfu ya vijana wa TRA wapewe majembe wakalime, wanakula tu mishahara ya bure
 
Haya ndio mambo yalio nifanya niseme sinto kaa niwe mfanya biashara nchi hii maana najua sina uwezo wa kukwepo kodi zao na mwisho wakija kunizingua naweza nikajikuta naingia kwenye matatizo bure.
Bora niendelee kua mfugaji na mkulima, huku nikiwakopesha watumishi pesa za mimba mdogo mdogo
Hautopona tataribu za kusajili wafugazi zipo njiani.... Utalipwa tu Kodi
 
Nasema hivi, hata kama huo mzigo umeagizwa au kuzalishwa na shetani au jini, achilia mbali kampuni au individual, au hata kama huo mzigo umejiagiza wenyewe, unalamwa ‘Total tax’ ya 500% na habari imeishia hapo..., huku ndani watu wauze kadri watakavyo, hakuna cha Vat, income tax wala chochote!!
Hii sasa umeamua kuandika tu it’s illogical.

Haya umenunua mzigo wa million 100, margin ya faida million 20. Mpaka hapo VAT unadaiwa million 21.6 kwa sababu umeamua kuilipa mwenyewe badala ya mlaji.

Faida yako million 20 income tax 30% unatakiwa ulipe 6 million.

Stamement yako ya bank itakwambia baada ya hiyo biashara kichaa umetoa milllion 100 umerudisha (120-21.6-6=92.4) hapo bado ujaongeza gharama zako za wafanyakazi, umeme, usafirishaji etc.

Hiyo sera wakuwekee wewe tu hakuna mfanyabiashara mwingine atakubali.

👋
 
Hii sasa umeamua kuandika tu it’s illogical.

Haya umenunua mzigo wa million 100, margin ya faida million 20. Mpaka hapo VAT unadaiwa million 21.6 kwa sababu umeamua kuilipa mwenyewe badala ya mlaji.

Faida yako million 20 income tax 30% unatakiwa ulipe 6 million.

Stamement yako ya bank itakwambia baada ya hiyo biashara kichaa umetoa milllion 100 umerudisha (120-21.6-6=92.4) hapo bado ujaongeza gharama zako za wafanyakazi, umeme, usafirishaji etc.

Hiyo sera wakuwekee wewe tu hakuna mfanyabiashara mwingine atakubali.

👋
Ndugu, hii kodi si Vat, si income tax wala si kodi yoyote specific, ni kodi moja, tunaweza kuita ‘Total tax’, hata wakiamua iwe 500% potelea mbali, mlaji wa mwisho ndio atailipa; ila ilipwe yote mara moja infull pale pale kiwandani au bandarini.., huku mtaani biashara ifanyike freely kabisa bila kodi yeyote.., maana kodi imeshalipwa ‘In totality’ at the source au point of entry. Sahau kuhusu VAT for once na uelewe hoja, break out of that box ndugu
 
Wana JF,

Ujumbe huu uende kwa Rais Samia pamoja na TRA.

Huu mfumo mpya ambao TRA imeuanzisha katika kukusanya VAT umeleta matatizo makubwa sana hasa kwa kampuni za wilayani na mikoani.

Kawaida VAT huwa hivi. Mfanyabiashara unaauza bidhaa yako au huduma yako na kuongeza VAT juu ambayo mlaji huibeba. VAT haitakiwi kuwa mzigo kwa muuzaji bali mnunuzi wa huduma.

Sasa kinachotokea TZ hasa kwa kampuni kubwa zilizoko wilayani ni kwamba
1. Ukiwa VAT registered unaweza kuwa na ushindani na makampuni mengine ambayo sio VAT registered. Kwahiyo ukiongeza VAT kwenye bidhaa yako, inakula kwako kwasababu huduma yako itakuwa aghali zaidi. Hili linatokea sana kwa biashara kubwa huko wilayani. Kwahiyo hawaongezi VAT kwenye mauzo yao na badala yake wanatoa VAT kwenye faida zao. Mfano mauzo ya milioni 50 kwa mwezi, VAT yake ni milioni 9.

2. Inatakiwa utoe VAT ya manunuzi yote unayofanya katika kutengeneza mauzo yako. Bahati mbaya wilayani wafanyabiashara ambao ni VAT registered ni wachache sana. Kwahiyo unajikuta huna receipts kabisa za manunuzi yenye VAT. Kwenye expenses zako VAT ni zero

Huko nyuma mfanyabiashara alikuwa anaruhusiwa kuingiza VAT ya baadhi ya matumizi yake. Lakini sasa wamebana, kama huna receipt imekula kwako. Maana yake katika hayo mauzo ya milioni 50 ni kama wewe hujaweka matumizi yoyote. Yaani umezalisha milioni 50 bila ku invest hata senti tano.

Kwahiyo ikifika tarehe 20 mwezi unaofuata inabidi ulipe hiyo milioni 9 ya VAT. Na of course utakuwa hauna maana huenda hata fida tu ya biashara yako haifiki hiyo figure.

3. Unaweza kuta hao uliowauzia huduma yako hawalipi ontime. Kama sisi wengine hata sasa tunadai madeni ya October 2022. Sasa TRA wanataka VAT yao hapo hapo. Kwahiyo unatakiwa kulipa hiyo milioni 9 ambayo hujapokea malipo yake.

Matokeo ya hizo points tatu ni kufilisika. Yaakiendelea hayo mimi mimi miezi mitatu inayokuja huenda ikabidi kufunga biashara na kuondoa wafanyakazi kama 30. Kwasasa ni stress tu na kutoa pesa zangu zingine ili kulipa hizo VAT. Mwisho wa siku kila mwezi ni hasara tu.

Kwa mfano huko nyuma nilikuwa nalipa wastani wa VAT milioni moja kwa mwezi. Miezi miwili ya mwaka huu nimelipa average kwa mwezi milioni 9.

Wanavyofanya nchi zingine, mfanyabiashara anachagua kulipa VAT flat rate kwa mfano katika VAT uliyokusanya unalipa 25% na hakuna mambo ya kudai VAT ya matumizi au unadai VAT ya matumizi. Mfanyabiashara anachagua njia ambayo ni nafuu kwake.

Kwa TZ huu mfumo mpya wa kulazimisha unaenda kuua biashara zetu. Hivi hata kwa akili ndogo kweli kwenye biashara ya kama hoteli, unaweza kuzalisha mauzo ya milioni 50 bila kuwa na matumizi yoyote ya maana? Ina maana watu wanafanya manunuzi ila ni kwenye maduka ambayo sio VAT registered. Biashara kama ya hoteli faida haizidi asilimia 20. Sasa VAT pekee ikichukua asilimia 18, kuna biashara tena hapo?

Ukiwa Dar au miji mikubwa ni rahisi kununua kila kitu kutoka maduka ambayo ni VAT registered. Lakini wilaya kama kule Ngara huna luxury hiyo.

Wahusika chukueni hatua.
Good observation ila washinda ofisini hawaelewi hii kitu. Ni mara nyingi tumeongea kuhusu hili, VAT kwa Tanzania ndio inaua taasisi nyingi Tanzania. Hakuna VAT relief kwenye biashara nyingi TZ
 
Labda hujasoma andiko vizuri. Bishara ya hoteli huko wilayani hizo receipts zenye VAT utazitoa wapi? Utaenda Dar kununua nyama? Kununua mchele? Kununua mboga? Kununua mafuta?

Hiyo kwasasa ni issue kubwa sana kwa wafanyabiashara wakubwa walioko huko wilayani kwa mfano Ngara.

Utalazimika tu kununua vitu kwa wasio na receipts za VAT. Ukiwa mikoani au Dar unaweza kununua at least nusu ya matumizi kwenye maduka yenye receipts lakini sio huko wilayani.
Na vitu vyote ulivyovitaja havitoi unafuu wa VAT kwa kuwa ni vyakula vya shambani ambayo viko exempted from VAT.
 
Mapitio ya VAT lazima yafanyike na kuboreshwa ikiwezekana ibakie single digit, haiwezekani dunia ya ushindani VAT iwe two digit tena kwenye nchi ambayo bado biashara nyingi watu wanajikongoja taratibu kukua lakini serikali hiyo hiyo inawarudisha nyuma
Kumbuka tuna wachumi wenye PhD ambazo hazikununuliwa pia sio za kujadili uganga wa kienyeji Bali Ni za kujadili masuala makini Kama haya Ila zimekaa tu zimejaa ego aka kibri na kujiona kuwa zina uwezo wa kujua kesho.

Kumbuka hizo PhD hazijavumbua jipya zaidi ya kukariri yaliyovumbuliwa na wengine Kama kasuku baadaye zikayarudisha kwenye karatasi zikakubalika kuwa zinaweza kukariri so zipo juu ya binadamu wengine wote.


Usomi wa mwafrika Ni wa kukariri kuwa wa kwanza Basi ndio unajiona u Bora. Na mtu anasoma ulaya akiwashinda wazungu kukariri zinajitapa Ila akili kubwa za kuwaza na kuvumbua Kama za akina Elon musk huwa zinaonekana vilaza darasani.
 
TRA hawawezi kukuelewa. Na hii shida ipo kwa maelfu ya watu wenye biashara kubwa huko mawilayani. Hasa kama input kwenye mauzo yake ni local.

Lengo la VAT halikuwa hilo kwamba mzigo ubebwe na kampuni bali mlaji mmoja mmoja. Kibaya hata hiyo VAT sio kwamba umeongeza kwenye mauzo bali unatoa kwenye faida. Biashara yangu ningelikuwa Dar ingelikuwa ndogo na wala kusingelikuwa na attention kubwa lakini huko wilayani shida.

Mimi ningetegemea huko wilayani ndiko at least kungelikuwa na incentives za kusaidia makampuni. Hivi kila mtu akiwekeza Dar tu, nchi yetu itakuwa na hali gani?
Wekeza mjini tu mkuu huko vijijini wewe ndio unakuwa chanzo cha mapato cha kila taasisi ya serikali na utaitwa sana kushiriki uchangiaji wa maendeleo ya kijiji
 
Hata inapo tokea mfanya biashara anafunga, ahakikishe anapo peleka barua pale tra pia lazima ajiandikishe kwenye kitabu cha wageni ili ikija kutokea siku wanamdai kodi aseme nilisha kuja kuleta barua ya kusimamisha biashara na nilijiandikisha kwenye kitabu ya wageni (hua wanatabia ya kuficha barua)
Kiofisi barua zinapelekwa mbili, moja ya ofisi husika, nyingine inapigwa muhuri "RECEIVED" unaondoka nayo. Wakijisahaulisha utatoa hii nakala yako. Mpokeaji anapaswa kusign kwenye barua yako kwamba amepokea.
 
Una mashine ya kutengeneza Chakula cha mifugo, ukiuza unatoa risiti yenye VAT.
Malighafi unanunua kwa wakulima ie uduvi, dagaa, soya, mahindi ila hayana risiti, je hapa unafanyaje TRA wasikuumize?
Ntakushauri unofficially, at your own risk jifunze kuuza bila kutoa risiti na bila kukamatwa, maana ukikamatwa hapo utalia na kusaga meno, pia jifunze kujinasua ukikamatwa.

Officially, wewe umenunua raw material haina VAT, umeiprocess kupata bidhaa nyingine, VAT inaanzia kwako. Yaani kwenye bei yako ya kuuza, ongeza na VAT kabisa. Hapa ndo ugumu unakuja, kama bei ni 2000 kwa kilo wewe yakwako inatakiwa iwe 2000 + (18% of 2000), which is 2360. Sijui kama utapata wateja maana kila mtu anajua kua sehemu nyingine ni elf 2.

Serikali yenyewe kabla haijanunua inapiganisha bei then inamfata mwenyewe bei rahisi.
 
Hata inapo tokea mfanya biashara anafunga, ahakikishe anapo peleka barua pale tra pia lazima ajiandikishe kwenye kitabu cha wageni ili ikija kutokea siku wanamdai kodi aseme nilisha kuja kuleta barua ya kusimamisha biashara na nilijiandikisha kwenye kitabu ya wageni (hua wanatabia ya kuficha barua)
Hii kweli nakumbuka tulifunga. Duka letu dodoma mwaka 2012 .na barua ilienda TRA kuusu taarifa za kufunga
Lkn 2022 tumefungua biashara mpy tumekuta deni 5m
Kwaiyo kama unafunga biashara yako its better baki na signed copy kutika TRA husika
 
Hata inapo tokea mfanya biashara anafunga, ahakikishe anapo peleka barua pale tra pia lazima ajiandikishe kwenye kitabu cha wageni ili ikija kutokea siku wanamdai kodi aseme nilisha kuja kuleta barua ya kusimamisha biashara na nilijiandikisha kwenye kitabu ya wageni (hua wanatabia ya kuficha barua)
Unaenda na dispatch book yangu wanasaini na kuweka muhuri
 
Back
Top Bottom