Mwacheni Rais Samia aongoze kwa maono yake na si vivuli au viatu vya wengine
Kumtaka afuate nyayo ni kumkwaza. Samia ana personality yake tofauti na ya mwendazake
Hawezi kutumia personality yake kufanya ya Marehemu, JK, Hayati Mkapa, Mwinyi au Hayati Nyerere!
kila zama na kitabu chake , ni wakati wake kuandika zama hizi kwa kitabu chake
Katika mambo aliyoandika
Mzee Mwanakijiji moja ni sisi kuwa Taifa lililogawanyika.
Kazi ngumu mbele ya mama Samia ni kuliunganisha Taifa lilivyovurugwa na Marehemu
Marehemu aliligawa Taifa kwa namna zozote unazofikiri, iwe jinsia, ukabila, udini , hata rangi
Marehemu hakujali Utu alijali Vitu, Mama Samia arudishe hadhi , heshima na utu wa mwananchi
Kiongozi anaongoza watu si madaraja au miti, hivyo kutojali uhai na maisha ya watu si kiatu cha kuvaa
Hivi mnataka Rais Samia avae viatu vya kukataa sayansi na kuhubiri madogori na mapambio kwa gharama kubwa sana za maelefu ya maisha ya wananchi! kiatu hicho mama asikijaribu wala kukifikiri!
Rais Samia halazimiki kufuta kila kilichoachwa na Marehemu lakini analazimika kufuta mabaya aliyoacha na yaliyoliacha Taifa hili na makovu makubwa sana.
Kiongozi hapimwi kwa Vitu bali Utu. Mwendazake anapimwa kwayo ndiyo maana kipimo cha utu wake kipo mgongoni kama si kushoto. Hukumu yake imesimama katika utu licha ya vitu alivyotengeneza
Mwacheni Rais Samia aongoze kwa zama zake na aandike legacy yake kwa maono yake