Video Clip: Jerry Silaa adai kuna Jaji anamlinda tapeli wa viwanja

Video Clip: Jerry Silaa adai kuna Jaji anamlinda tapeli wa viwanja

Majaji nani anawateua? Wanateuliwa kwa vigezo gani? Kusikia haya madudu kunatia unajisi mahakama
Majaji wengi walikua mahakimu vilaza jpm na bi tozo wamewateua na kuharibu sifa za majaji wetu....majaji wenye uweledi wamebaki wachache
 
Anachofanya Silaa ni kujaribu kuingilia muhimili wa mahakama, Jambo ambalo siyo Sawa na haileti picha nzuri, aache watu waende mahakamani kujitetea au kujibu mashtaka waliyoshtakiwa nayo, atakayeibuka mshindi basi ndio ameshinda
Uhuru wa mahakama unahalalisha jaji kuwaita watulishi wa ardhi mlango wa uani,uhuru wa mahakama wa nchi kama kweli ungekua unafuatwa viongozi wengi wangekuwepo jela
 
Anayedhani kuwa hajapata hukumu ya haki tokana na sababu anazoeleza huyu waziri Jerry Silaa utaratibu wa kisheria si unamtaka apinge hiyo hukumu kwa kukata rufaa mahakama ya juu?
a taratibu na sheria..
Ungekuwa mjane ,yatima,umedhulumiwa ardhi usingeandika haya .Yakikukuta urudi tena kutuandikia kwa mbwembwe kabisa
 
Ungekuwa mjane ,yatima,umedhulumiwa ardhi usingeandika haya .Yakikukuta urudi tena kutuandikia kwa mbwembwe kabisa

Hujui na huelewi..

Na kwa taarifa yako mimi pia ni yatima sina baba wala mama, wote walishafariki..

Lakini hoja wala siyo hii ama hayo mawazo yako butu na yenye kutu..

Hoja ni hii, kwamba, kwanini wewe usielewe kuwa ktk nchi yetu tuna mfumo wa utoaji haki kwa ajili ya watu wote wakiwemo yatima, wajane na yeyote aliyedhulumiwa chochote ikiwemo ardhi kama unavyodai?

Nimesema toka awali kuwa, kila mtu anajua kuwa mfumo wetu huu wa utoaji haki kupitia mahakama zetu uko compromised na serikali (executive) kiasi cha kuathiri HAKI ZA WATU kama hivyo unavyoona wewe..

Lakini walioiharibu mahakama na mfumo mzima wa utoaji HAKI si ni hawahawa kina Jerry Silaa na serikali yao kupitia chama chao cha CCM kilichoshika hatamu serikalini..?? Au hujui hili..?

Na cha ajabu ni kuwa, eti wao haohao tena wanatoka na kuanza kuilaumu mahakama na Majaji/mahakimu kuwa hawatoi haki sawasawa..!

Na ina maana wewe Lukub hulioni tatizo hili kweli au umedhulumiwa kiasi cha ufahamu na akili zako kuvurugikiwa kabisa?

Na kweli kabisa unadhani na kuamini kuwa Waziri Jerry Silaa au Rais mwenyewe anaweza kuingilia na kutengua hukumu ya kisheria ya mahakama iliyokwisha kutolewa pasipo kufuata utaratibu huohuo wa kimahakama kuitangua?

Mimi nakuambia haiwezekani hata kama hukumu hiyo imetolewa Jaji mwenye maslahi binafsi na kwa kuonea upande mmoja bila kujali mtu huyo ni yatima, mjane, mfiwa au yeyote..!!

TIBA YA HIKI ANACHOKILALAMIKIA Waziri Jerry Silaa sio cheap statement kama hii ya kwako ya kujificha nyuma ya u-yatima au u-jane au u-fiwa na mengine yanayofanana na hayo. Bali tiba ya kweli na ya kudumu ni;

1. Kuwaambia CCM na serikali yao kuwa wao ndio wameiharibu mahakama kwa kuwapa maelekezo mahakimu na majaji kuamua mashauri kinyume cha sheria na haki. Hilo limejengeka na kuwa utamadauni. Sasa utamaduni huo unaanza kumtafuna na kumwathiri kila mtu wakiwemo hao yatima na wajane wako. Hivyo tuwaambie waache unafiki na warudi kwenye mstari..!

2. Wao kina Jerry Silaa na CCM na serikali yao ndio wanaoteua majaji ambao wengine ni makada wa CCM na wako kule kuwalinda wao na kuharibu mtiririko mzima wa utoaji haki kwa kulea rushwa na upendeleo. Sasa wanamlalamikia nani. Mfano huyo Jaji anaemlalamikia si kawekwa pale na Rais na mwenyekiti wake wa CCM? Alikuwa hajui status yake?

3. NI LAZIMA SASA NA NI WAKATI wa kujenga mfumo mpya wa kikatiba, kisheria na kiutawala utakajenga mfumo huru wa utoaji haki (judicial system) na kuzifanya mahakama zetu kuwa huru bila kuingiliwa na mhimili wa utendaji - setikali (executive). Hii inawezekana tu kwa kuirekebisha katiba yetu ya mwaka 1977 inayompa madaraka mtu mmoja aitwaye Rais kuteua kila Jaji au kuifuta kabisa hiyo na kuandika nyingine mpya..

HIYO NDIYO SULUHU. Na kamwe suluhu sio hiyo ya unafiki wa wana CCM akiwemo waziri Jerry Silaa au wewe Lukub unayeficha udhaifu wa mfumo wa utoaji haki kwenye status ya u - yatima au u-jane..!
 
Hujui na huelewi..

Na kwa taarifa yako mimi pia ni yatima sina baba wala mama, wote walishafariki..

Lakini hoja wala siyo haya mawazo yako butu na yenye kutu..

Hoja ni hii, kwamba, kwanini wewe usielewe kuwa ktk nchi yetu tuna mfumo wa utoaji haki kwa ajili ya watu wote wakiwemo yatima, wajane, waliodhulumiwa chochote sio ardhi tu?

Nimesema toka awali kuwa, kila mtu anajua kuwa mfumo wetu huu wa utoaji haki kupitia mahakama zetu uko compromised na serikali (executive) kiasi cha kuathiri HAKI ZA WATU..

Lakini walioiharibu mahakama na mfumo mzima wa utoaji HAKI ni hawahawa kina Jerry Silaa na serukali yao kupitia chama chao CCM kilichoshika hatamu serikalini..

Na cha ajabu ni wao haohao tena wanatoka na kuanza kuilaumu mahakama na Majaji/mahakimu kuwa hawatoi haki sawasawa..!

Ina wewe Lukub hulioni tatizo kweli?

Na kweli kabisa unadhani Waziri Jerry Silaa au Rais mwenyewe anaweza kuingilia na kutengua hukumu ya kisheria ya mahakama pasipo kufuata utaratibu huohuo wa kimahakama?

Mimi nakuambia haiwezekani hata kama hukumu hiyo imetolewa kwa kuonea upande mmoja. Na hata kama aliyeonewa ni yatima, mjane, mfiwa au yeyote..!!

TIBA YA HIKI ANACHOKILALAMIKIA Waziri Jerry Silaa sio cheap statement kama hii ya kwako ya kujificha nyuma ya u-yatima au u-jane au u-fiwa na mengine yanayofanana na hayo. Bali tiba ya kweli na ya kudumu ni;

1. Kuwaambia CCM na serikali yao kuwa wao ndio wameiharibu mahakama kwa kuwapa maelekezo mahakimu na majaji kuamua mashauri kinyume cha sheria na haki. Hilo limejengeka na kuwa utamadauni. Sasa utamaduni huo unaanza kumtafuna na kumwathiri kila mtu wakiwemo hao yatima na wajane wako. Hivyo tuwaambie waache unafiki na warudi kwenye mstari..!

2. Wao kina Jerry Silaa na CCM na serikali yao ndio wanaoteua majaji ambao wengine ni makada wa CCM na wako kule kuwalinda wao na kuharibu mtiririko mzima wa utoaji haki kwa kulea rushwa na upendeleo. Sasa wanamlalamikia nani. Mfano huyo Jaji anaemlalamikia si kawekwa pale na Rais na mwenyekiti wake wa CCM? Alikuwa hajui status yake?

3. NI LAZIMA SASA NA NI WAKATI wa kujenga mfumo mpya wa kikatiba, kisheria na kiutawala utakajenga mfumo huru wa utoaji haki (judicial system) na kuzifanya mahakama zetu kuwa huru bila kuingiliwa na mhimili wa utendaji - setikali (executive). Hii inawezekana tu kwa kuirekebisha katiba yetu ya mwaka 1977 inayompa madaraka mtu mmoja aitwaye Rais kuteua kila Jaji au kuifuta kabisa hiyo na kuandika nyingine mpya..

HIYO NDIYO SULUHU. Na kamwe suluhu sio hiyo ya unafiki wa wana CCM akiwemo waziri Jerry Silaa au wewe Lukub unayeficha udhaifu wa mfumo wa utoaji haki kwenye status ya u - yatima au u-jane..!
Nakupa mfano kuna bibi wa kijiji cha Olumotonyi Arumeru kadhurumiwa Ardhi na mahakama imekwisha toa hukumu arudishiwe ardhi yake lakini anatishiwa mpaka na polisi asije kukanyaga kwenye hiyo ardhi na walinzi wapo na ukuta na nyumba ,huyu anapata haki yake wapi ?Neno moja la RC juzi limetosha kuwafurusha majangiri ,wamekimbia wenyewe wanajua mzee baba acheki na kima.
 
Nakupa mfano kuna bibi wa kijiji cha Olumotonyi Arumeru kadhurumiwa Ardhi na mahakama imekwisha toa hukumu arudishiwe ardhi yake lakini anatishiwa mpaka na polisi asije kukanyaga kwenye hiyo ardhi na walinzi wapo na ukuta na nyumba ,huyu anapata haki yake wapi ?Neno moja la RC juzi limetosha kuwafurusha majangiri ,wamekimbia wenyewe wanajua mzee baba acheki na kima.

Hili ni tatizo jingine tofauti kabisa..

Na ni tofauti na anacholalamikia waziri Jerry Silaa. Huyu Waziri anai - criticise mahakama na Jaji kuwa ametoa hukumu ya upendeleo na kutaka waziri wa sheria aingilie kati nje ya utaratibu wa kimahakama..

======================================

Lakini kwa ishu hii hapo Arusha, vyombo vya utendaji serikalini akiwemo waziri mwenyewe au polisi wanaweza kuingilia kuhakikisha aliyekwisha kupewa haki na mahakama anapata haki yake..

Hata hivyo kwa scenario hii uliyoielezea ktk mgogoro huu wa huyu mama, ni wazi kuwa liko tatizo jingine nyuma ya mgogoro huo..

Mfano iweje polisi wazuie utekelezaji wa hukumu ya mahakama iliyokwisha kutolewa badala ya wao kusimamia utekelezaji wake ambayo ndio kazi yao?

Nafikiri, kama polisi wanazuia, basi kuna uwezekano upande ulioshindwa nao walisha object hiyo hukumu kisheria na hivyo polisi kupata uhalali wa kuzuia utekelezaji wa hukumu ya awali..

Fuatilia vizuri na utaelewa. Usifanyie kazi maneno ya kusikia mitaani..
 
Lakini Waziri kasema kuna forgery iliyofanywa na Bwana Matunda,na ilithibitishwa na forensic ya police! Hili limekaaje!!??
Ndiyo maana hata ukimsikia Matunda kwenye clip ya YouTube iliyopo humu anasema kuwa aliambiwa aende Mahakamani kushtaki na hukuenda. Pia hakuhudhuria mirathi wakati ni mdau wa uwekezaji. Anakijuwa alichokifanya
 
Anachofanya Silaa ni kujaribu kuingilia muhimili wa mahakama, Jambo ambalo siyo Sawa na haileti picha nzuri, aache watu waende mahakamani kujitetea au kujibu mashtaka waliyoshtakiwa nayo, atakayeibuka mshindi basi ndio ameshinda
Mahakama zimeshafeli ndio maana watu wamedhulumiwa haki zao
 
Slaa kilichomuondoa Ardhi ni Lile tukio la kuamuru yule mwananch kule Morogoro polisi wamchukue kama vile muhalifu.
 
Uongozi sio Elimu.

Kiongozi ni Ama Azaliwe, au Atengenezwe kupitia Elimu.

Sasa Makonda ni wa kuzaliwa ndio maana wajinga wachache kama wewe mnaojiona mmesoma ndio hammpendi.

Lkn kwakua Makonda ni Kiongozi wa kuzaliwa, ndio maana Kila Ziara zake anaambata na watu wa Sheria, na kada zote, hiii tunaita DHANA YA USHIRIKISHAJI
Kwa kweli Makonda ana kipawa na nyota ya kusikilizwa mahali popote.
Ana uwezo mkubwa wa kujua aongee nini kwa wakati gani,kuchanganua hoja kwa haraka na kujua nani ni muongo na nani ni mkweli na nani ni mbabaishaji ndani ya sekunde chache kitu ambacho watendaji au viongozi wengine inawachukua mwaka mzima kujadili kesi moja na kuujua ukweli ni upi.
 
Lakini naona kwenye 'conflict of interest' hapa haifiti vizuri kwa sababu mtu ambaye zamani nilipokuwa wakili alileta documents zake nimgongee mhuri hakuwezi kunifunga kwa baadaye nikiwa jaji kuamua kesi dhidi yake au kwa upande wake. Conflict of interest inatokea kama uhusiano wa huyo jaji na mtu aliyemgongea mhuri kwenye documents zake unaweza au utaathiri uamuzi wake (yaani kwamba hataweza kuwa fair kwa sababu hiyo).
Kwani ukiwa wakili unaruhusiwa kugonga mihuri kwenye nyaraka feki?Na kama hairuhusiwi basi huyo jaji aliogopa kwamba ataulizwa kama huyu jamaa ameshindwa kesi kwa kigezo cha nyaraka feki kwa nini ulivyokuwa wakili ulicertify hizo nyaraka kuwa ni valid so ikabidi ampe ushindi tapeli ili kufupisha mambo lakini Mungu si Atumani kaja waziri wa ardhi anayechimbua na kufukua makaburi hapo ndio imeleta kizaazaa na Jaji kuumbuka.
 
Hili liinchi ndo maana haliendelei. Kila penye upuuzi ambapo tulitakiwa kushirikiana kuukataa hutokea wajinga kama wewe
Na hiyo ndio utofauti wa nchi ya Kenya na Tanzania kwenye kudai haki tumeachwa mbali sana.
Kenya akijitokeza mpigania haki akajieleza sababu zake zikiwa na mashiko wananchi wote wanaelewa chapchap na wanamsapoti lakini ukija Tanzania anajitokeza mtu kupigania haki za wananchi inajitokeza mijitu mijinga kama mizezeta inaanza kupinga jambo la manufaa kwa ajili ya wananchi wote
 
Kama hao maafisa ardhi wamelala atafanyaje,inabidi aingilie kuwanusuru raia wenye matatizo
Mkuu wa idara unapokuwa hujui nini cha kufanya watendaji wa chini wakikosa uwajibikaji ufanisi
Alafu unaenda kufanya wewe badala ya wao
Basi nafasi iliyopo siyo size yako
 
Mkuu wa idara unapokuwa hujui nini cha kufanya watendaji wa chini wakikosa uwajibikaji ufanisi
Alafu unaenda kufanya wewe badala ya wao
Basi nafasi iliyopo siyo size yako
Kama umekabidhiwa idara yote imeoza na imezungukwa na vibaka watupu huwezi ukakaa ofisini utegemee kuletewa ripoti zilizo sahihi itakulazimu uingie mstari wa mbele kwenye field/Saiti wakati huo una plan B ya kuwachuja mmojammoja maana huwezi ukawafukuza wote kwa mara moja.
 
Back
Top Bottom