Video: Je, hiki ndio kimesababisha Kemikimba, Katibu Mkuu Wizara ya Maji kutenguliwa?

Video: Je, hiki ndio kimesababisha Kemikimba, Katibu Mkuu Wizara ya Maji kutenguliwa?

Mimi ni mwanaume lakini huwa napata tabu sana ya kuwaelewa wanaume wenzangu kuhusu mwanamke akifanya kosa kwenye nyadhifa yake.Wengi wa wanaume wana nasibisha kosa hilo na jinsia lakini kosa akifanya mwanaume hakuna anaye nasibisha na jinsia yake.
Ni mfumo dume au inferiority complex kwa baadhi ya wanaume?

Nashukuru sana umeliona hili, ni inferiority complex inawasumbua wanaume wengi pindi wamuonapo mwanamke kwenye uongozi, ndio maana mwanamke akikosea anasemwa kwa jinsia yake ila mwanaume akikosea anaonekana kateleza tu.
 
Huyu mama kazingua sana unadhani aliyeandika hicho kimemo amejisikiaje?! Huenda kimemo kilikuwa na ujumbe mzuri wa kujenga, pia wa kukumbushia jambo sema tu viongozi walio wengi hawapendi kufundishwa, au kuelekezwa wanahofia kuwa nafasi zao zitachukuliwa na aliye na uwezo mkubwa. Anasahau kwamba kiongozi anatakiwa ajifunze kuwa mnyenyekevu na msikivu.
 
Ni kweli Viongozi wengi hupelekewa vikaratasi vyenye jumbe mbalimbali lakini Nafikiri Huyo Mama Alipelekewa kikaratasi chenye Ujumbe wa Dharau ambao hakuweza Kuvumilia, Ndio Maana Akakitupa. Huyo aliye andika huweenda aliwaambia na wenzie, So Kibinadamu mtu akikuonesha Dharau mbele za Watu hutakiwi kuwa Mnyonge katika Process ya Ku react na Kujipa Confidence unatakiwa kumonesha Dharau Mara mbili ya Ile Aliyo kuonesha, Tumeona Kipindi Cha Magufuli alikuwa Hakubali mambo Ya Kijinga anamaliza pale Pale.

Je kuna mwenyewe anajua Nini Kiliandikwa kwenye Hicho Kimemo? Kosa Kubwa Ingekuwa kama Amepelekewa Kimemo hajakisoma na Kamlipua mpelekaji lakini kakisoma kaona kwa Level yake na Level ya Mtu aliyempeleka ni Kudharirishwa.

Haina Tofauti na Alicho Kifanya RC CHALAMILA KULE SOKONI [emoji120]
Kumbe hata ww hujakiona lkn unaongea as if umekiona.

Yote kwa yote huyo maza anaonesha ni kiburi na jeuri kilichompata anastahili
 
Iko hivi; kwenye Itifaki kiongozi kabla ya kuongea lazima akaribishwe na mwenye shughuli..kwenye huo mkutano ni watumishi wa Wizara ya Maji/DAWASA ambapo mgeni rasmi alikuwa Mhe. Waziri wa Maji na huyo KM alikuwa anaongea ili amkaribishe Waziri.
Sasa iko hivi; kama unaongea kabla ya muongeaji Mkuu/Mgeni Rasmi hutakiwwi kuwa mzungumzaji sana maana unaweza kuongea yale yote ambayo muongeaji Mkuu anakwenda kuzungumza na kwa kufanya hivyo inakuwa hakuna maana ya Mgeni Rasmi kuongea.
Kwa maelezo hayo hapo juu kwa nilichokiona hapo kinafanana na maelezo yangu na ndiyo maana hao watu wa HR ambao kiutaratibu ndio wasimamizi wa Itifaki walikuwa wanamkumbusha Bosi/KM kwamba imetosha amkaribishe Mhe. Waziri ambae ndiye alikuwa muongeaji Mkuu.
Alichoharibu zaidi ni kushindwa kuficha hisia zake na kumkaribisha Waziri kihuni.
Yote kwa yote alijiona yuko sahihi lakini kimsingi waliokuwa wanampelekea kimemo walikuwa wanamsaidia na wakati mwingine asichokijua inawezekana vimemo hivyo alipelekewa kwa maelekezo halali ya Waziri.
Nawaza tu kwa sauti..huyu Dada kule Arusha kwenye semina elekezi sijui alienda kutalii tu.
Wasalam.
Itakuwa ww ndie mpeleka kinote, lkn ukweli haufichiki yule mama hafai kuwa kiongozi
 
Kama alikuwa ni mtumishi atarejeshwa katika nafasi ya juu ya muundo wa kada yake. Anakuwa Afisa Mkuu Daraja la I. Anaendelea kutumwa na kuagizwa kazi na mkuu wake wa idara au kitengo.
Before alikuwa Mkurugenzi wa mojawapo ya kurugenzi pale Wizarani, kisha alipanda kuwa Naibu KM, then KM
 
Aina hii ya viongozi wapo wengi sana ni vile tu haijatokea matendo yao yakawa captured live on camera.

Hawajiamini, wana uwezo mdogo na wameegesha mambo hivyo ukiwaingilia kidogo tu unawavuruga.

Hawafai kuwa viongozi. Kuna namna nyingi sana za kudeal na insubordination (if that was truly the case) ila sio kuleta taharuki mbele ya watu namna ile.
 
Nimewaangalia Kiumakini hao akina Biden, Trump na Obama kama walishawahi nao kupewa Vikaratasi wakiwa Wanahutubia katika Podiums zao sijaona ila kama una Video ya Ushahidi wa ulichokisema tafadhali niwekee / tuwekee hapa ili tukuamini.

Nijuavyo ( kama GENTAMYCINE ) kwa Kiongozi kuletewa Kikaratasi ukiwa Unahutubia katika Podium ni uthibitisho tosha kuwa huaminiki, msahaulifu, mbabaishaji, hujui Kitu, utakosea mbele ya Safari kwa Kubwabwaja Kwako kwingi Jukwaani na huna Akili ( Popoma ), ila basi tu upo upo.

Mkuu Gentamycine:

Umeangalia President Bush alipoletewa habari ya September 11 alipokuwa Sarasota Florida? Haikuwa note...alinong'onezwa sikioni akiwa darasa la chekechea.....Hakupanick hata kidogo kukatisha darasa, alivuta subira alitulia...akaongeza kama dk moja....Hata waliomchukia Bush wanakiri alionyesha utilivu wa hali ya juu......nikipata muda nitaiweka clip/video yake Mkuu.
 
Mkuu Gentamycine:

Umeangalia President Bush alipoletewa habari ya September 11 alipokuwa Sarasota Florida? Haikuwa note...alinong'onezwa sikioni akiwa darasa la chekechea.....Hakupanick hata kidogo kukatisha darasa, alivuta subira alitulia...akaongeza kama dk moja....Hata waliomchukia Bush wanakiri alionyesha utilivu wa hali ya juu......nikipata muda nitaiweka clip/video yake Mkuu.

View: https://youtu.be/enLdoTg9HBI
 
Tutegemee nini kwa mtu anaeitwa mikimba?

Kaiachia mikimba.

As a woman she is super stupid. Kazi haziendeshwi kwa "emotions". She's not composed at all.

Kama ndiyo sababu ya kutumbuliwa, anastahiki.
Ndugu yangu ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜† umenichekesha japo umetukosea. Kemikimba majina ya kwetu Kagera. Huyu dada ndugu yako katika imani ni mtu wa kwetu Kagera. Kwao washika dini swalat hamsa mnasema sio!?

Kwa hili anastahili kutolewa hapo. Anaonekana ana jazba na dharau sana. Hafai uongozi.
 
Ndugu yangu ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜† umenichekesha japo umetukosea. Kemikimba majina ya kwetu Kagera. Huyu dada ndugu yako katika imani ni mtu wa kwetu Kagera. Kwao washika dini swalat hamsa mnasema sio!?

Kwa hili anastahili kutolewa hapo. Anaonekana ana jazba na dharau sana. Hafai uongozi.
Majina yanaakisi vitendo.
 
Aina hii ya viongozi wapo wengi sana ni vile tu haijatokea matendo yao yakawa captured live on camera.

Hawajiamini, wana uwezo mdogo na wameegesha mambo hivyo ukiwaingilia kidogo tu unawavuruga.

Hawafai kuwa viongozi. Kuna namna nyingi sana za kudeal na insubordination (if that was truly the case) ila sio kuleta taharuki mbele ya watu namna ile.
Kikwetu, kama mtoto kakosea na ukawa umeshashika kiboko kwa ajili ya kumchapa, mgeni akibisha hodi, huyo mtoto anaweza kulimika au adhabu ikaahirishwa kwa muda. Ukimwadhibu mbele ya mgeni utakuwa umemdharau huyo mgeni. Waziri pale alienda kama mgeni. Alichokifanya KM ni sawa na kumwadhibu mtoto mbele ya mgeni.

Kikwetu, kugombana mbele ya wakubwa zako ni dharau. Waziri ndiye aliyekuwa mkubwa kuliko wote kwenye hilo kusanyiko. Asingepaswa kureact kiasi kile mbele ya mkubwa wake. Alichokifanya ni sawa na kumwonesha dharau mkubwa wake.
 
Huyu hastahili kuwa kiongozi. Mbona kuletewa ki note wakati unazungumza ni jambo la kawaida sana? Wanaletewa vi note hati kina Bidden, Trump na Obama? sembuse yeye? Yeye nani?
Kwahiyo Boss wake naye hastahili??
Kwani aliyeanzisha hiii staili ni Nani? Kwenye Mei Mosi 2022 she did the same.
Akiwa Kwenye Mikutano hataki Mabango wala walioonewa wamweleze jambo? So awe mpole anapoona wateule wake wanafanya kama yeye.
 
Back
Top Bottom