Zanzibar 2020 VIDEO - KAMPENI ZANZIBAR: Tundu Lissu awapa somo muhimu Wazanzibar na Watanganyika juu ya Muungano. Je, Magufuli - CCM anaijua historia hii kweli?

Zanzibar 2020 VIDEO - KAMPENI ZANZIBAR: Tundu Lissu awapa somo muhimu Wazanzibar na Watanganyika juu ya Muungano. Je, Magufuli - CCM anaijua historia hii kweli?

Sasa muungano wa nini? Unatusaidiaje?
 
Lissu anataka kuuboresha muungano kwa kuleta serikali tatu

Kuendelea na muungano wa aina hii usio na ridhaa ya Wazanzibari ipo siku wataingia mitaani kushinikiza viongozi wao wauvunje na Mtakuwa hamna jinsi ya kuwazuia maana hakuna jeshi la kuufanya muungano uwepo kama Wazaznzibar kwa umoja wao wataingia mtaani kuukataa!

Mwenye akili ni yule anayewasikiliza wazanzibar wanataka nini leo. Ukiwalazimishia aina ya muungano huu ambao unategemea tuwapandikizie wazanzibari vibaraka, kisha tuwashindishe kwa figisu kwenye sanduku la kura, kisha tuwalinde kwa kutumia majeshi huu muungano hautofika popote siku wazanzibar wakiamua kuingia mtaani kuukataa!

Lissu ndiye mzalendo wa kweli anayetaka tuunusuru Muungano kwa kutengeneza muungano uliofair, Nje ya hapo it is a matter of time kabla Wazanzibar hawajarevolt!
 
Sababu inataka kuimeza Zanzibar na kuifanya Unguja wilaya na pemba wilaya na kuweka sikali moja tu,na kuwatimuwa wanyapara na vibaraka wake, ikifikia huko itakuwa hawa vikaragosi hawana thamani tena.
 
Hakuna aliyeyejaribu kuvunja muungano au kuungana na wavunja muungano huu uliopo kama ulivyo sasa aliyefaniiwa kushika uraisi iwe wa muungano au wa Zanzibar awe wa CCM au upinzani

Aboud Jumbe na Seif shariff Hamad walikwama kwa sababu hiyo. AKINA warioba, Lowasa waligombea wakashindwa kwa hivyo kipengele sababu alienda kuungana kwenye UKAWA na Maalim Seif mtaka kuvunja muungano huu wa serikali mbili uliopo

Lisu kajiingiza mwenyewe kwenye mdomo wa mamba biashara imeisha .Hapewi uraisi

Muungano uliopo ni eneo sensitive ambalo mwanssiasa yeyote anayeutaka uraisi hatakiwi kuligusa negatively kuwa anavunja huu muungano wa serikali mbili uliopo
 
Sijui kama mgombea Urais wa CCM mwaka huu ndg John Pombe Magufuli anaijua historian na kuielezea mbele ya kadamnasi kama hii kwa ufasaha kama afanyavyo huyu msomi wa viwango vya juu kabisa, Mh. Rais Tundu Lissu..
Huyu ada yake ameeitendea haki
 
Nina hakika wengi wanao comment hapa hawajaisikiliza hiyo clip hapo wamesoma heading tu basi.

Kwa kweli mhe Tundu Lissu huku anakokwenda sasa kunazidi kuwajengea watu fikira fulani hasi dhidi yake.
Kabisa.
 
Ninashangaa mods kuunganisha thread yangi na ya Kituturu. Yeye amemponda Magufuli mimi nimeonesha uhaini wa Lissu. Wapi wapi mambo haya mawili?
 
Huyu kweli anastahili kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
Kwa kauli hizi, si ni wazi ameonesha kuwa atavunja Muungano?...
Uwongo mkubwa sera ya Chadema kuhusu Muungano iko wazi, hawataki kuuvunja Muungano ila watu wataulizwa wanataka mfumo gani wa Muungano kama ilivyokuwa kwa tume ya jaji Warioba. Muungano umekuwa unalalamikiwa sana hivyo lazima muafaka upatikane.
 
Bara na visiwani tumeshakuwa ndugu. Tuna muingiliano wa damu na kijamii.

Muungano nao ni muhimu sana kwa usalama wa pande zote. Lissu analeta mentality za kikoloni kwani anataka turudi kwenye kifungo cha mipaka ya kikoloni kwasababu za kisiasa...
Mkuu sio wewe tu hata mimi nimeshangaa sana, tatizo kubwa ninalo liona hapa ni kwamba Mhe. Tundu Lissu anataka kutumia hoja yoyote ambayo anaamini inaweza kumpa point dhidi ya ccm bila kujali wala kupima matokeo ya anachokihubiri.

Okay, labda ni propaganda tu Ila akishafika Ikulu kama atashinda huo urais ataachana na hilo wazo.
 
Uwongo mkubwa sera ya Chadema kuhusu Muungano iko wazi, hawataki kuuvunja Muungano ila watu wataulizwa wanataka mfumo gani wa Muungano kama ilivyokuwa kwa tume ya jaji Warioba. Muungano umekuwa unalalamikiwa sana hivyo lazima muafaka upatikane.
Uongo upi? Umeiangalia na kuisikiliza hiyo tweet ya Ngurumo niloyoituma?
 
Ninashangaa mods kuunganisha thread yangi na ya Kituturu. Yeye amemponda Magufuli mimi nimeonesha uhaini wa Lissu. Wapi wapi mambo haya mawili?
Kuna kitu fulani hujakijua humu JF mkuu naamini ukishakijua huto shangaa tena.
 
Hata ningekuwa wa Lesotho, nimeuliza swali muhimu Sana kwa mustakabali wa Tanzania. Huyo mgombea wenu anatakiwa aungane na wanaharakati wenzie. Amethibitisha kuwa hana sifa hata robo za kuwa mkui wa nchi
Tatizo la Mgombea WAO anaongea vitu ambavyo hakupaswa kuongea..Wazanzibar hawatakiwi kujua Historia yao. Wanatakiwa kuwepo kama walivyo sasa. Tuwaamulie nani anawafaa kuwatawala na sio wao wenyewe..Tatizo la TL anaharibu kabisaa yaani Sio vyema kwa kweli..🙁🙁
 
Mimi Ni CCM kindaki daki, Ila kwenye hili niwe muwazi. Nimeweka uchama pembeni, nikiwa Kama mtanzania nasema kwa dhati ya moyo wangu, Tundu Lissu hastahili kuwa Rais wetu
Si kwa sababu ya chuki binafsi tuu dhidi yake huna lolote. Uwezo wake mkubwa sana unajulikana ila ninyi na mabosi wenu mnamuogopa kama alivyosema
mzee Warioba kwamba [emoji116]..

Screenshot_20200908-011041.jpg
 
Back
Top Bottom