Zanzibar 2020 VIDEO - KAMPENI ZANZIBAR: Tundu Lissu awapa somo muhimu Wazanzibar na Watanganyika juu ya Muungano. Je, Magufuli - CCM anaijua historia hii kweli?

Wazanzibar wanaijua historia yao kwa kuiishi. TL amesoma hivyo asijifanye much know
 
Aisee waliompiga risasi za miguu Lissu walipoteza risasi zao tu,maana brain bado iko superbly/intact.
 
Hakuna aliyeyejaribu kuvunja muungano au kuungana na wavunja muungano huu uliopo kama ulivyo sasa aliyefaniiwa kushika uraisi iwe wa muungano au wa Zanzibar awe wa CCM au upinzani...
Kama Mwenge umewahi kuzuiwa kukimbizwa basi ya Muungano pia yanawezekana. By the way, nani ameongelea habari za kuuvunja Muungano?
 
Yehodaya, badala ya kutumia jukwaa kama alilolitumia yeye kumwaga sumu, mnaunguruma humu, sijui mnawasaidiaje waachane na huyo mtumwa wa historia.
 
Kana Mwenge umewahi kuzuiwa kukimbizwa basi ya Muungano pia yanawezekana. By the way, nani ameongelea habari za kuuvunja Muungano?
Hao wenye hisia za kihalifu watakujibu nani ameongelea kuvunja muungano. Ogopa maneno ya kweli, yanauma kuliko ncha ya sindano.
 
Yehodaya, badala ya kutumia jukwaa kama alilolitumia yeye kumwaga sumu, mnaunguruma humu, sijui mnawasaidiaje waachane na huyo mtumwa wa historia.
Niseme wazi mimi ni mmoja ambaye Historia sekondari nikioata D na hadi Leo huwa nalalamika kuwa baraza la mitihani lilinipendelea ilitakiwa wanipe F, Historia mimi siipendi ni somo la kuongelea marehemu

Mwalimu akiingia darasani ni kuongelea marehemu tu utafikiri mko makaburini kwenye kusoma wasifu wa marehemu

Unakuta anaanza leo tutajifunza kuhusu marehemu Mkwawa kesho tutaongelea marehemu Karl Peters na marehemu chifu manangungo,keshokutwa tutaongelea marehemu nyerere,Marehemu Karume na Marehemu Aboud Jumbe na Marehemu Sultan wa Zanzibar!!! Yaani hadi nywele zilikuwa zinanisisimka najiona niko makaburini nikaacha kuhudhuria vipindi vya historia

Hilo somo lifundishwe kwa wafanyakazi wa mortuary au ma MC wa misibani

Somo limejaa marehemu tu loop
Lisu kabobea kwenye kueleza wasifu wa marehemu waliopita

Nchi kusonga mbele mtu hatakiwi kuwa mtumwa wa historia kikwete alisemq
 
Historia ya watu wa KLM/ Kanda ya kaskazini inajulikana? Unajua Base on history hakuna kitu kinaitwa Tanzania.

Well hii haiondoi ukweli kuwa Tl ana akili, akili nyingi...
Hivyo hivyo hata kama ccm itaendelea kuitawala Zanzibar haitabadili maisha yao na kuwaondolea shida na mahitaji yao, bali wimbo utaendelea kuwa ule ule tu.

Kwa maana hiyo wacha wazanzibar wachague wapi wanahitaji na maamuzi yao yaheshimiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muungano ni tatizo la KISIASA.

CCM-Zanzibar wamekuwa wakitumia vyombo vya dola toka Tanganyika kuwakandamiza waZanzibari wenzao.

Sisi wa-Tanganyika kama tunataka kuulinda muungano ni lazima tuhakikishe HAKI inatenda Zanzibar.

Maingiliano ya kiuchumi, kiulinzi, kibiashara, na kifamilia, yanaweza kudumishwa bila ya Watanganyika kujihusisha na dhambi ya kuunga mkono upande mmoja wa waZnz kudhulumu haki za kisiasa za upande mwingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…