Video: Ni kama masihara hivi lakini polepole Mikocheni na Masaki zinaenda kutawaliwa na Wachina

Rais analishugulikia alishatengeneza tume ya ku-curb influx ya "wageni" Kariakoo.
Sawa. sasa tatizo lipo wapi? Kuwa wanachukua maeneo prime u?

Nieleweshe tu mkuu.

Yani kama tatizo sio la kisera, je ni la kijamii? Na kwanini iwe mchina pekee na sio watu kutoka nchi zingine? Wahindi labda.
 

Sasa si ungeanzisha uzi wako wa rasilimali na bandari

Unahangaika na uzi wangu wa uchuuzi na mediocrity wa nini?

Sehemu gani nimeandika mambo ya rasilimali kwenye uzi wangu?

Nimechoka ulipo sema mwanzoni kuwa Wachina wapewa kuwa Adminiatrators wa bandari.

Sina neno kubwa zaidi ya kukwambia hujui unachokitetea.


Una absttact ideas nyingi sana. Wewe ni idealist.
 

Hakuna tatizo hata wakiamua kuinject 1 trillion dollars za uwekezaji TZ so long as sheria na taratibu zinafuatwa.

Hizo hela zitafungua fursa zingine kwa kila mtu- trickle down economy.

Rais anavutia wawekezaji kila siku nyie mpo hapa kupinga wageni. Bongo aliyewajaza uwoga wa kuogopa wageni, kuogopa kwenda nje na kuongea kingereza aliwajaza ujinga endelevu.
 
Sawa. sasa tatizo lipo wapi? Kuwa wanachukua maeneo prime u?

Nieleweshe tu mkuu.

Yani kama tatizo sio la kisera, je ni la kijamii? Na kwanini iwe mchina pekee na sio watu kutoka nchi zingine? Wahindi labda.

Hamna tatizo mkuu. Kikubwa kwa kuwa wana hela, Oysterbay, Mikocheni na Masaki yote iwe ya Wachina tu.

Waswahili wote wakae Goba, Tandale na Tegeta. Ila hayo maeneo prime wakae wao tu maana hela si wanazo.


Wakiamua kuanzisha magenge ya uhalifu, wizi na biashara za kikahaba kama walivyofanya huko London na Los Angeles ni sawa tu maana hata sisi Watanzania tukiwa China tunaruhusiwa kufanya hivyo.

Kwani tukiwa kwenye nchi ambayo real estate price kwenye the most expensive places in the country inaaamuliwa na wachina shida iko wapi?

Nashauri pia maduka yote ya Oysterbay na Masaki, restaurants na hospitali zote wapewe wachina. Yaani mchina akiwa ana hela apewe kila kitu.

Hakuna shida kabisa. Wachina kwa kuwa wana pesa wapewa rich neighborhood waswahilo kaeni uswekeni
 
wanalipa kodi au hawalipi? kama wanalipa, shida yako nini? wakati hata wasingekuja wewe au yule msingekuja kuishi masaki au mikocheni maisha yenu yote.
 

Sawa sawa. Nakuunga mkono.

Na ile tume ambayo aliunda Rais kwa ajili ya kudhibiti "wageni" Kariakoo pia nadhani aivunje haina umuhimu.

Kwa kuwa wachina ni rafiki zetu na wana hela, hata huko Kariakoo wenyewe ndo wapewe kipaumbele maana zita-"trikle down on the economy"

Kikubwa pesa mkuu. Maana si umeona hata kule Guangzhou Watanzania wanapewa kipaumbele kuliko Wachina.

Kikubwa ni pesa.
 
halafu mbona wabongo kwao wanaenda, unataka wachina nao watimue wabongo kwao, hiyo kariakoo si itakufa.
 
Jamii yetu imejaa au inajazwa hofu kila kukicha, tunalalamika wachina na wachina ndio wanamalizia ujenzi Ubungo pale stand ya zamani, miradi mikubea ya ujenzi yupo, bidhaa nyingi Kariakoo zinatoka kwake, bodaboda zote nchini ni yeye.

Sisi hakuna tunachozalisha, wala hakuna sheria za kumbana afungue viwanda nchini, bei za boda na bajaji ziko juu sio kwasababu ya mchina ila sisi wenyewe tunatesana na kodi, na bado tunamlalamikia mchina.
 

Umetoka nje ya mada.

Wapi nimeseme wasizalishe piki piki na kujenga madaraja?
 
Huwezi yajua sababu umechagua ujinga
"Simple mind discuss people.
Ordinary mind discuss events
Great mind discuss Idea."

Nafikiri ungeleta hoja yako tuipime tuone ni ipi ipo sahihi. Vinginevyo wewe ni mpumbavu.

Katka Dunia ya Leo huwezi kwepa economic migration hasa katka nchi zetu ambazo ni third world countries. Kulikataa hili ni ujinga.
 
Mkuu. Sikutaka nikupeleke huko, sasa cjui ni kwnn unakata tamaa bure tu.

Ni kamavile unanijengea na kunilisha maneno.

Basi swali liwe. WATANZANIA TUFANYE NINI? Tuwakatae wageni wote ama wachina tu peke yao?
 
Huko cha mtoto mbona fika Mkoa wa Pwani ujuonee halafu wanawazalisha mno dada zetu
 
Wachina tangu lini wakawa wawekezaji wa maana Tanzania. Wachina ni Madalali tu kama madalali wengine.


Nitajie investment yoyote ya wachina yenye Capital Kama Dangote Cement, Barick Tanzania, TBL, N.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…