Mimi niwapongeze Kwa KAZI mnayoifanya. Ila Watanzania wa Leo siyo wajinga. Narudia wapiga kura siyo wajinga. Akituambia Jimboni Kwakwe amefanya nini basi nitasubiri.
Nakubaliana na wewe kwamba watanzania wa leo sio wajinga. Ni kweli pia kwamba yake mema anayofanya mtu ndio yanayompaisha kisiasa.
Ni kweli pia kwamba Magufuli kafanya mengi na yanaonekana, na ni mazuri.
Lakini yapo maswali kadhaa. Swali la kwanza, je Magufuli mwenyewe anajua ukweli huu? Napata mashaka, jinsi anavyotumia nguvu nyingi kuwabana wapinzani wake. Ni kama vile hajui kwamba kafanya mengi ambayo yatampa ushindi. Nguvu za kibabe za dola, rushwa kuwaghilibu wapinzani "waunge mkono juhudi", na wizi na uporaji wa moja kwa moja katika chaguzi za marudio na uchaguzi wa serekali za mitaa, hali hii inatia shaka kama kweli Magufuli "anajitambua", au pengine anajua fika kwamba kuna mabaya mengi kayafanya ambayo yanamtia hofu.
Kumbuka watanzania siyo wajinga.
Magufulinomics imeondoa fedha kwenye mzunguko, na kufanya maisha yawe magumu sana. Kudharau kilimo imesababisha watanzania walio wengi kuendelea kusota katika lindi la ufukara.
Kutowaamini wakandarasi wazawa na wafanyabiashara, imesababisha kazi nyingi kurundikwa kwa wageni.
Mkakati wa Magu wa kudharau rasilimali watu imesababisha maafa katika sekta nzima ya utumishi wa umma, kufeli kwa jitihada zake katika sekta nyingi.
Mfano katika sekta ya afya, badala ya kuanza na uboreshaji kwa watoa huduma, yeye kaanza na majengo na vifaa, kiasi. Katika sekta ya elimu, alijikita kwenye madawati na majengo, wakati maslahi ya walimu, ajira mpya, zikikwama.
Mimi naamini Magufuli anayajua haya yote, na anajua kwamba akiacha yajadiliwe hadharani na kwa uhuru, ataadhibiwa kwenye sanduku la kura. Siamini kama Magufuli yupo tayari kwa uchaguzi huru na wa haki