Video: Tundu Lissu alisema ukweli mchungu sana kuhusu muungano wa Tanganyika na Zanzibar. CCM walimshambulia vibaya, lakini waliufyata kwa hoja zake

Video: Tundu Lissu alisema ukweli mchungu sana kuhusu muungano wa Tanganyika na Zanzibar. CCM walimshambulia vibaya, lakini waliufyata kwa hoja zake

Naked truth
20220213_134754.jpg
 
Sidhani kama upande wa wenzetu ccm wanauwezo wa kujibu hoja za Lissu. Kwa hili walikuwa waungwana wakaufayta.
 
Huyu ndugu, ni mtu anayetafuta maarifa popote pale yanapopatikana....

Watu wa namna hawadandanyiki kwa sababu wanakuwa wanajua yote kama siyo kila kitu...!
Kwakweli Tunamhitaji awe Rais. Anajua kila kitu. Ana exposure ya kitaifa na kimataifa. Sio Mshamba wa mambo.

Zaidi anapenda Haki amani na utu.
 
Du! Huyu jamaa hoja imekaa kiushahidi.
Intact Muungano kwa nyakati za Mwl alikuwa na logic kwa mfumo aliouweka,ila sio kwa sasa
Tundu Lissu hajawahi kuniangusha. He has been always at highest level of intergrity.
 
Huko Lumumba fc haya ndio maisha yao[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Umenikumbusha tukio la majuzi hapa mkuu waziri wa maliasiri na utalii ambaye ni mwanasheria anasema " ardhi ni Mali ya rais'" wabunge wa CCM wanagonga meza mara spika akatoa ufafanuzi "Ardhi ni Mali ya umma" wanagonga meza.sasa unajiuliza hawa watu ni mazwazwa kiasi gani?
 
Umenikumbusha tukio la majuzi hapa mkuu waziri wa maliasiri na utalii ambaye ni mwanasheria anasema " ardhi ni Mali ya rais'" wabunge wa CCM wanagonga meza mara spika akatoa ufafanuzi "Ardhi ni Mali ya umma" wanagonga meza.sasa unajiuliza hawa watu ni mazwazwa kiasi gani?
Wa kusikitikiwa zaidi ni sisi tuliokubali kuongozwa na watu wa aina hiyo
 
Mi napenda sana uwezo wake wa kupambanua mambo as if hakusoma shule za hapa kwetu!Mungu akipenda ampe kibari Lissu siku moja aje awe Raisi wa nchi hii,may be tunaweza faidi uwezo alionao KWA upana zaidi
 
Duniani kote hakuna muungano wa aina hii..hizi zilikua njama za kiwiziwizi tu...eti nchi moja serikali mbili..ila moja ni kupe/chawa ambayo haichangii chochote...huku ikiwa na kauli ya changu changu..chako chetu..mfano mzuri umiliki wa ardhi.

Kingine mgawo unaoendelea huu wa fedha za mikopo..hauna ratio yoyote mbaya zaidi ni mzigo kwa serikali ya Tanganyika iliyovikwa koti la JMT..serikali iliyoshindwa kulipa deni la umeme wa Tanesco hadi kupewa msamaha inawezaje kulipia mabilioni ya pesa inayopewa kama mgao kupitia mikopo.

Kimsingi huu muungano hauna maslahi kwa taifa..ila kwa wachache wezi wenye maslahi yao binafsi.

Muungano uwekee upya..iwe nchi moja yenye serikali moja..au ziwe serikali tatu.

#MaendeleoHayanaChama
Kwa nini machogo bado mnang'ang'ania kubaki Zanzibar? Muungano mpya anautaka nani? Siyo Wazanzibari. Nyie machogo kama mnataka muungano mpya ongeeni na Kagame au Kenyatta au Museveni mpate muungano mpya.

#FreeZanzibar
 
Umenikumbusha tukio la majuzi hapa mkuu waziri wa maliasiri na utalii ambaye ni mwanasheria anasema " ardhi ni Mali ya rais'" wabunge wa CCM wanagonga meza mara spika akatoa ufafanuzi "Ardhi ni Mali ya umma" wanagonga meza.sasa unajiuliza hawa watu ni mazwazwa kiasi gani?
🤣🤣🤣🤣🤣hamna kitu wale
 
Mi napenda sana uwezo wake wa kupambanua mambo as if hakusoma shule za hapa kwetu!Mungu akipenda ampe kibari Lissu siku moja aje awe Raisi wa nchi hii,may be tunaweza faidi uwezo alionao KWA upana zaidi
Nimejaribu angalau kuwa kama Lissu kuwa na akili nyingi na umakini. He is my role model so far.

Tunahutaji Rais mwenye uwezo mkubwa.

Amerika na Ulaya huchagua watu wenye uwezo mkubwa kwa akili na hekima.

Hapa Tunaye Ni Tundu Lissu.

Mungu aliyemponye alimwandalia jambo.
 
Lissu ni mtu mwenye upeo mkubwa, mpenda haki sana na mtu mwenye ujasiri usio na mfano.
Tupende au tusipende Tz inahitaji mtu kama Lissu kuwa rais wa hii nchi, na kwa wale tunaoweza kuona mbali tunahisi hakuna namna unaweza kuzuia Lissu kuja kuwa rais wa hii nchi. Ni suala la muda tu.

Mimi binafsi kwa mara ya kwanza nilimsikia Lissu miaka kama 20 iliyopita, haikuwa kwenye majukwaa ya kisiasa, lakini papo hapo nikagundua uwezo uliokuwa nao Lissu haikuwa wa kawaida na kitu hicho hicho wenzangu wengine niliokuwa nao walikiona vile vile.
 
Isitoshe anaefaidika kwenye huu muungano ni Zanzibar(Tanzania visiwani) kwasababu wao wanunua ardhi nyingi sana nakujenga huku bara pia bado wanaleta ujinga. Mtu wa bara huku akitoka kwenda kule inakaa tu kama ndege jonihata kama una uwezo kama Mo huwezi miliki ardhi tena nadhani Mo hana pia na wengine hili tu kwanza ni tatizo kama vipi liangaliwe hili swala. Kitu gani Tanzania bara inafaidi kuliko Tanzania visiwani?

Hata mtupe Tanganyika yote hamwezi kulipia hata roho ya mtu mmoja ya mliowauwa 1964 na mnaoendelea kuuwa kila siku za uchafuzi / uchaguzi zinapofika, yaani tufaidi kwa kuuliwa ndugu zetu na kunajisiwa mama zetu na dada zetu huku mali zetu zikiporwa ? UNA AKILI KIJANA WEWE
 
View attachment 2118569
Hii ni kutoka katika maktaba ya mjadala na michango ya wajumbe mbalimbali wa bunge la kupata katiba mpya mwaka 2012/2013 huko Dodoma. Bahati mbaya CCM walivuruga mchakato huo na hivyo kukwama na taifa kupata hasara mabilioni ya fedha zilizopotea bure bila kuleta matokeo...

Katika bunge hilo la mchakato wa kupata katiba mpya, wajumbe wengi walitoa michango iliyotia fora sana na kuwa kumbukumbu nzuri...

Ila baadhi wachache walikuwa na michango na mawazo bora zaidi ya wengine..

Mmoja wa mchango wa kukumbukwa sana ulikuwa wa ndugu Tundu Lissu mbunge wa bunge la katiba (CHADEMA) na mbunge wa bunge la JMT kutoka Jimbo la Singida Mashariki wakati huo....

Mnakumbuka, kabla ya hii, ilitanguliwa na hotuba yake kali sana ya kuukosoa muungano wenyewe na kumkosoa vikali pioneer wa muungano huo na mwasisi wa taifa hili Mzee Julius K. Nyerere...

Baadhi ya wana CCM walikwazika sana kiasi cha kumjengea hoja kuwa "kamtukana" baba wa taifa lao yaani Mwl. Julius K. Nyerere. Wakamshambulia sana ndani na nje ya bunge hilo...

Siku chache baada ya negative reaction ya hotuba yake hiyo toka kwa baadhi ya wana CCM, sasa kwa dakika kama 10 hivi, mtazame na sikiliza akijibu viroja vya wana CCM hao ktk video hiyo hapo juu...

NB:
Samahanini sana kwa ubora duni wa picha wa video hiyo. Hata hivyo, sauti ndiyo muhimu zaidi na inasikika kwa uzuri sana...

Pia background, unaweza kuisikia sauti ya Mama Samia Suluhu Hassan [Sasa ni Rais wa JMT] lakini wakati huo akiwa mmoja wa wenyeviti wa bunge hilo la katiba ya wananchi..
Huyu mwamba huyu
 
Back
Top Bottom