VIDEO: Tundu Lissu, aliyepigwa risasi akipinga ukabila na u-Mobutu, na yeye aiga kuongea vilugha majukwaani

VIDEO: Tundu Lissu, aliyepigwa risasi akipinga ukabila na u-Mobutu, na yeye aiga kuongea vilugha majukwaani

Tindikali

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2010
Posts
2,086
Reaction score
2,823
Jambo nyeti la mwisho alilofanya Tundu Lissu kabla ya kupigwa risasi, na ambalo wachunguzi wengi wa kisiasa wamesema lilichangia kupangwa mashambulizi ya kigaidi dhidi yake, ni kutoa hotuba ile ya "Mtoto wa Dada," ambamo alishutumu vikali na kulaani kwa nguvu ukabila na undugu uliokuwa unaota mizizi ghafla kuanzia utawala wa awamu ya tano.

Alisema Rais huyu anafanya mambo yaliyokataliwa na waasisi wa nchi hii ya kujali kabila lake kwanza.

Na tumeshuhudia Rais huyu wa sasa akipanda majukwaani na kuweka mbele Kisukuma bila kuzingatia misingi ya kuendeleza Utaifa mmoja, unaoongea lugha ya Taifa moja, lugha ya Kiswahili.

Tundu Lissu, kati ya watu wote, na yeye eti ameangukia mtego huo wa kuongea cha kwao majukwaani. Anatuangusha.

Mwalimu Nyerere anaviringika kaburini.



 
Kama unataka ufanye jambo zuri lolote hapa Tanzania basi jua huwezi kuwa wewe wa kwanza lazima alianza Magufuli na yeye ndio atamalizia ukweli ni kwamba siku zinavyo zidi kwenda Tundulisu ataendelea kutoka kwenye Ramani mdogo mdogo
 
Jambo nyeti la mwisho alilofanya Tundu Antipas Lissu kabla ya kupigwa risasi, na ambalo wachunguzi wengi wa kisiasa wamesema lilichangia kupangwa mashambulizi ya kigaidi dhidi yake, ni kutoa hotuba ile ya "Mtoto wa Dada," ambamo alishutumu vikali na kulaani kwa nguvu ukabila na undugu uliokuwa unaota mizizi ghafla kuanzia utawala wa awamu ya tano. Alisema Rais huyu anafanya mambo yaliyokataliwa na waasisi wa nchi hii ya kujali kabila lake kwanza...
Mleta mada hapo Tundu Lissu yupo jukwaani? Alafu umewai fika vijijini singida? Unadhani wanajua kiswahili? Basi umepotea sana!!!

Hapo Tundu Lissu watu wanamsalimia kwa kilugha chao unataka awajibu kiingereza? Unataka awajibu kiswahili?

CCM mmekosa hoja kabisa. Magufuli hasemwi tu kuongea kisukuma bali kwa nepotism yake anayoionesha wazi tena mchana kweupe kwa kuwapendelea watu wake!!!

Kama Tundu Lissu angekuwa Singida Mjini alafu anaongea kinyaturu hapo ungekuwa na hoja ila kwa huko vijijini hapo huna hoja yeyote!!

Lissu kuongea kilugha kijijini tena kwao hilo sio tatizo lolote ndugu!!
 
Hapa ndio umeonesha vizuri nani aliehusika kumshambulia Tundu Lissu, hukumu yake ipo, na Mungu ndie hakimu wa kweli.
Tunazidi kukusanya ushahidi nani anahisika kumpiga risasi Lissu. Hadi watafikia kutajana majina kabisa mwaka huu.

Chezea spana za Lissu nini??😄
 
Kumbuka juzi tu hapa kasema tz kuna corona watu wengi wanapoza maisha kimyakimya,chakushangaza alikua anakumbatiana na watu bila woga hawa watu hawa zakuambia changanya na za kwako.
Mtakimbilia sana kwenye Corona mwaka huu. Ila kihoja hamtamzidi mwaka huu. Huyo ndo Lissu😃
 
Jambo nyeti la mwisho alilofanya Tundu Antipas Lissu kabla ya kupigwa risasi, na ambalo wachunguzi wengi wa kisiasa wamesema lilichangia kupangwa mashambulizi ya kigaidi dhidi yake, ni kutoa hotuba ile ya "Mtoto wa Dada," ambamo alishutumu vikali na kulaani kwa nguvu ukabila na undugu uliokuwa unaota mizizi ghafla kuanzia utawala wa awamu ya tano. Alisema Rais huyu anafanya mambo yaliyokataliwa na waasisi wa nchi hii ya kujali kabila lake kwanza...
Umemtaja aliyemshambulia Mh. Lissu kama hizo ndiyo miongoni mwa sababu za shambulio like la kigaidi basi msiwasingizie watu wasiojulikana.Bebeni lawama zenu wenyewe.

Ikungi kuna Wazee wa Kinyaturu, wengine hawafahamu kiswahili,je unamlinganishaje na Ukabila wa Jiwe? Hawana ulinganifu wowote. Acha Rais Mtarajiwa asalimie Wazazi wake apendavyo, tunamfahamu kuwa hana tabia za Ukabila.Ukienda Kijijini kwenu unaongea English/ Kiswahili?
 
Mleta mada hapo Tundu Lissu yupo jukwaani? Alafu umewai fika vijijini singida? Unadhani wanajua kiswahili? Basi umepotea sana!!!

Hapo Tundu Lissu watu wanamsalimia kwa kilugha chao unataka awajibu kiingereza??? Unataka awajibu kiswahili?...
Unaji contradict.

Kama Singida hawajui Kiswahili angeongea hotuba nzima ki-Singida.

Tundu Lissu anatuangusha, anaanza kulainika, anamuiga JPM kuongea vilugha majukwaani. Ni ajabu iliyoje.
 
Chagua moja, usiji contradict.

Singida hawajui Kiswahili au alikuwa tu anasalimia Kilugha?

Maana kama hawajui Kiswahili angeongea hotuba nzima ki-Singida.

Tundu Lissu anatuangusha, anaanza kulainika, anamuiga JPM kuongea vilugha majukwaani. Ni ajabu iliyoje.
Hujasikia wakimsalimia kwa kilugha? Hoja yako ni nini hasa?

Nimekwambia hapo ni Singida tena kijijini. Lugha kuu ya mawasiliano hapo ni native language. Lissu akiongea hiyo lugha kwenye mazingira hayo kuna shida?

Kwani magufuli anaongeaga kisukuma kijijini tu?

Juzi uliona mwakyembe kwenye kura za maoni? Kilichomuangusha ni usemi wa kinyakyusa tu Allie kako!!!

CCM kusema ukweli hamna hoja ya kumshinda Lissu!! No wonder mliishia kumpiga risasi tu!!
 
Jambo nyeti la mwisho alilofanya Tundu Antipas Lissu kabla ya kupigwa risasi, na ambalo wachunguzi wengi wa kisiasa wamesema lilichangia kupangwa mashambulizi ya kigaidi dhidi yake, ni kutoa hotuba ile ya "Mtoto wa Dada," ambamo alishutumu vikali na kulaani kwa nguvu ukabila na undugu uliokuwa unaota mizizi ghafla kuanzia utawala wa awamu ya tano...
Acha kujaza mashudu kwenye server za JF.
 
Hii nchi haijawahi kupata rais mbaya.
Kibaya na kinacholigharimu taifa hili ambacho pia ni kigumu kupambana nacho ni Chama cha mapinduzi.

Ili nchi hii iwe bora sana na juhudi za watawala ziwe na manufaa makubwa na kila MTU awe huru kwenye nchi yake ni lazima CCM ifikie mwisho wa kujiona kuwa ni chama cha kimungu kisicho na mwisho kama alivyo Mungu muumba.

Ni lazima CCM ijitafakari kuwa nacho ni chama cha siasa tu kama vingine na sio imani au dini kuwa kikifa basi ndio mwisho wa Tanzania. Hata had vyo tumeona wajumbe wake wengi ni wazee wa miaka zaidi ya 70 ambao kiukweli wanakibeba chama kwa nguvu zote mpaka za kiroho.

Tundu Lisu na Membe wasikurupuke na kuwa na Tamaa kwa kujiona kila mmoja anakubalika zaidi. Wajiulize,Je, hiyo kukubalika zaidi kwa mmoja mmoja inatotosha kuiangusha CCM iliyojibinafsishia twasisi zote za umma na majeshi yote kuwa idara za chama badala ya umma?

Tulipokua tunashauri kuwa Chadema ya mbowe ijikite vijijini na kuwaunganisha wanachama nchi nzima ili waanzishe kazi ya kujijengea Ofisi kuanzia kwenye mashina au msingi walikuja na hoja kuwa hawana muda wa kujenga majengo wao wanajenga fikra.
Walisahau kuwa ujenzi wa pamoja unawaunganisha sana watu na kujiona kuwa ni sehemu ya Chama au taasisi hiyo na ni rahisi kujua nani yupo tayari na nini ni mpita njia.

Kwa tunaojua historia za dini tunakumbuka ujenzi wa mnara wa Babeli ulivyowatanya watu wote kukusanyika sehemu moja tuu huku wakigoma kutawanyika na kusambaa dunia nzima. Ujenzi uliposhindikana ndipo wakatawanyika kama ilivyo Leo kwa Chadema ya Mlevi Mbowe ilivyotawanyika baada ya kukosa hata Ofisi ya makao makuu.

Sasa leo hii ukiwauliza mpaka sasa mnauhakika wa kupata kura ngapi za wanachama hai; watakosa jibu kabisa kwa kutegemea kura za huruma badala ya mikakati na Sera mpya tofauti na zile kongwe za CCM zilizoandaliwa tangu mkoloni ,ni mwendelezo tuu!!
 
Mleta mada hapo Tundu Lissu yupo jukwaani???
Ndio yuko jukwaani.

Hili sio jukwaa?





Dakika ya 1:50 anaomba msamaha kwa kuongea Kinyaturu, anajua anachemsha!

Hapo hayuko na Wanyaturu tu! Na ni mgombea wa kiti cha Kitaifa, anaongea na Taifa pia.

Hatutaki vilugha, hatutaki ukabila, hatutaki tabia za JPM, tunataka lugha ya Taifa.
 
Mleta mada hapo Tundu Lissu yupo jukwaani??? Alafu umewai fika vijijini singida? Unadhani wanajua kiswahili??? Basi umepotea sana!!
Sio kweli kuwa hawajui kiswahili,Jana Tundu Lissu alikuwa anapokelewa na ndugu zake,baada ya jaribio la washenzi kushindikana!
Ulitegemea waongee Kisukuma!
Aliyepanga like jaribio na wanaunga mkono watakufa meno yakiwa nje!
Huu Ni Mipango wa Mungu!
Zaburi 35!
 
Unaji contradict.

Kama Singida hawajui Kiswahili angeongea hotuba nzima ki-Singida.

Tundu Lissu anatuangusha, anaanza kulainika, anamuiga JPM kuongea vilugha majukwaani. Ni ajabu iliyoje.
We kiaz wa lumumba tuliza msambwanda wako
 
Kumbe ndio nyie mliomfanyia unyama ule!? Basi sawa!

kwa hiyo kifupi ni kwamba huna utetezi dhidi ya blunder kama lile, kuongea vilugha majukwaani kama vile JPM

Tundu hajarudi yule yule, amelainika, anamuiga mpaka Magu tabia za kikabila
 
Ndio yuko jukwaani.

Hili sio jukwaa?





Dakika ya 1:50 anaomba msamaha kwa kuongea Kinyaturu, anajua anachemsha!

Hapo hayuko na Wanyaturu tu! Na ni mgombea wa kiti cha Kitaifa, anaongea na Taifa pia.

Hatutaki vilugha, hatutaki ukabila, hatutaki tabia za JPM, tunataka lugha ya Taifa.
Kweli mkuu, nimekusoma, Mimi pia nakerwa mno na hili Jambo la kiongozi kuongea kilugha huku akijua Tanzania yote inamsikiliza

Lakini kwa Tundu Lissu naweza kumpa benefit of doubt kidogo

Kuongea kwake kilugha kaongea tu kidogo Kama kuwaambia watu nimerudi nyumbani baada ya miaka mingi nje, Tena alikuwa akijishtujia Kama ulivyosema ikimaanisha anajua Ni wrong na kaifanya tu one time

Hii Ni tofauti na Ile ya Magufuli kipindi Cha kampeni ambapo alikuwa akihutubia almost kisukuma tupu baadhi ya mikutano yake Huko Kanda ya ziwa

Nilidhani baada ya uchaguzi ataacha lakini akaendelea na hata alifikia kuwaambia maafisa wake Wasibomoe nyumba za watu Huko Mwanza kwa Sababu Ni watu wa kwao na walimpa kura

Pia amekuwa akichochea ukabila wa wazi kwa wateule wake, Kuna kipindi yupo Ziarani, akawaambia wananchi nipo na mtu wenu nilimemchagua kuwa Waziri, kisha akamtoa yule Waziri na kumwambia aongee na wananchi kilugha,

Akiwa Dodoma pia alimwambia Ndugai azungumze Kigogo na wananchi

Pia Mara nyingi akiwa Ikulu anaapisha anataja makabila ya watu aliowateua na kusema najua kabila lako mpo hivi au vile,
Huu Ni ujinga wa kuchochea watu wawe loyal kwa makabila yao badala ya nchi

Au Wamuunge mtu mkono Sababu Ni wa kabila lao na sio sifa zake


Msikilize Lissu hapa yupo nyumbani kwao kabisa Ila hajaongea kilugha kabisa

 
Back
Top Bottom