VIDEO: Tundu Lissu, aliyepigwa risasi akipinga ukabila na u-Mobutu, na yeye aiga kuongea vilugha majukwaani

VIDEO: Tundu Lissu, aliyepigwa risasi akipinga ukabila na u-Mobutu, na yeye aiga kuongea vilugha majukwaani

..kweli.

..pamoja na kuchombeza kilugha, TL alitakiwa atafsiri ktk lugha yetu adhimu ya Kiswahili.

..nayasema hayo kwa kuzingatia kwamba wako watu[wageni wake] waliomsindikiza kama Salum Mwalimu, Susan Kiwanga, etc ambao hawazungumzi Kinyaturu.

..pia tukio zima lilikuwa linafuatiliwa kila pembe za Tanzania hivyo ni vizuri wafuatiliaje waelewe kila lililozungumzwa.
Ni kiongozi wa kitaifa, anafuatiliwa kila pembe ya nchi. Sawa kabisa.

Tundu Lissu sio Chifu wa Wanyaturu.

Wakati Rais Magufuli anaongea kuhusu Corona akiwa kanisani kwake Chato mbona hatukusema aaah bwana eeh, yuko kwao huko, anaongea Wasukuma wenzie! Tulimsikiliza.

Kwa sababu alikuwa anaongea na Taifa, ni kiongozi wa Kitaifa.

Jumamosi, akiwa nyumbani kwake Bedminster, New Jersey, Donald Trump amesaini amri kupitisha mambo ya dharura ya Corona mbali na Washington. Nchi nzima ilimsikiliza. Ni kiongozi wa Kitaifa.

Hatutegemei Tundu Lissu, kati ya watu wote duniani, awe na vitabia tabia vinavyotaka kufanana fanana na Magufuli.

Lissu ni mgombea Urais. Tunategemea awe na hulka, silka na mwenendo wa Urais. Rais wa Tanzania moja.

Julius Nyerere hakuwahi kumsalimia mama yake Kizanaki kama kuna Mnyakyusa mmoja kasimama pembeni.
 
Hawa jamaa wa kijani wakiishiwa hoja wanaenda kukoki bullets ndo upeo wao hapo ujue umeishia
Hujasikia wakimsalimia kwa kilugha? Hoja yako ni nini hasa?

Nimekwambia hapo ni Singida tena kijijini. Lugha kuu ya mawasiliano hapo ni native language. Lissu akiongea hiyo lugha kwenye mazingira hayo kuna shida?

Kwani magufuli anaongeaga kisukuma kijijini tu?

Juzi uliona mwakyembe kwenye kura za maoni? Kilichomuangusha ni usemi wa kinyakyusa tu Allie kako!!!

CCM kusema ukweli hamna hoja ya kumshinda Lissu!! No wonder mliishia kumpiga risasi tu!!
 
Jambo nyeti la mwisho alilofanya Tundu Lissu kabla ya kupigwa risasi, na ambalo wachunguzi wengi wa kisiasa wamesema lilichangia kupangwa mashambulizi ya kigaidi dhidi yake, ni kutoa hotuba ile ya "Mtoto wa Dada," ambamo alishutumu vikali na kulaani kwa nguvu ukabila na undugu uliokuwa unaota mizizi ghafla kuanzia utawala wa awamu ya tano.

Alisema Rais huyu anafanya mambo yaliyokataliwa na waasisi wa nchi hii ya kujali kabila lake kwanza.

Na tumeshuhudia Rais huyu wa sasa akipanda majukwaani na kuweka mbele Kisukuma bila kuzingatia misingi ya kuendeleza Utaifa mmoja, unaoongea lugha ya Taifa moja, lugha ya Kiswahili.

Tundu Lissu, kati ya watu wote, na yeye eti ameangukia mtego huo wa kuongea cha kwao majukwaani. Anatuangusha.

Mwalimu Nyerere anaviringika kaburini.




Hata Nyerere alizungumza kizanaki kijijini kwake Butiama. Na kwenye hotuba zake kuna moja alisema "wote maniganyanza!" lakini pia alitoa tafsiri ya kiswahili.
Hii siyo hotuba kwa taifa, ni mazungumzo na wanakijiji wenzake. Haijalengwa kwa taifa zima, bado huu siyo mkutano wa kampeni.
Tatizo liko pale mtu mwenye mamlaka na vyombo vya umma vya habari vinavyorusha hotuba yake kwa taifa zima anapoamua kutumia kilugha chake huku akijua audience ni taifa zima kupitia media za taifa zilizoko pale.
 
Sio kweli kuwa hawajui kiswahili,Jana Tundu Lissu alikuwa anapokelewa na ndugu zake,baada ya jaribio la washenzi kushindikana!
Ulitegemea waongee Kisukuma!
Aliyepanga like jaribio na wanaunga mkono watakufa meno yakiwa nje!
Huu Ni Mipango wa Mungu!
Zaburi 35!
Tv zenyewe za kuonyesha hazipo zimewekwa mifukoni sibora wanaangalia humu jf
 
Tatizo liko pale mtu mwenye mamlaka na vyombo vya umma vya habari vinavyorusha hotuba yake kwa taifa zima anapoamua kutumia kilugha chake huku akijua audience ni taifa zima kupitia media za taifa zilizoko pale.
hapo unamshusha mgombea wa chama kikubwa cha upinzani, Tundu Lissu, kwamba yeye akiongea Singida hasikilizwi na Taifa zima, unamfanya ni Diwani wa Singida Vijijini!

vyombo vilivyorusha hotuba ya Lissu sio "media za taifa" ?

audience iliyomfuatilia Lissu haikuwa ni audience ya taifa zima?

Lissu anagombea Urais, ajifunze kuenenda kitaifa, na asiige ya JPM.

Vichwa vya habari havipendezi....

 
Mn
Jambo nyeti la mwisho alilofanya Tundu Lissu kabla ya kupigwa risasi, na ambalo wachunguzi wengi wa kisiasa wamesema lilichangia kupangwa mashambulizi ya kigaidi dhidi yake, ni kutoa hotuba ile ya "Mtoto wa Dada," ambamo alishutumu vikali na kulaani kwa nguvu ukabila na undugu uliokuwa unaota mizizi ghafla kuanzia utawala wa awamu ya tano.

Alisema Rais huyu anafanya mambo yaliyokataliwa na waasisi wa nchi hii ya kujali kabila lake kwanza.

Na tumeshuhudia Rais huyu wa sasa akipanda majukwaani na kuweka mbele Kisukuma bila kuzingatia misingi ya kuendeleza Utaifa mmoja, unaoongea lugha ya Taifa moja, lugha ya Kiswahili.

Tundu Lissu, kati ya watu wote, na yeye eti ameangukia mtego huo wa kuongea cha kwao majukwaani. Anatuangusha.

Mwalimu Nyerere anaviringika kaburini.




Mnajitahidi sana sana kuokoteza maneno ya kijingakijinga.....
 
hapo unamshusha mgombea wa chama kikubwa cha upinzani, Tundu Lissu, kwamba yeye akiongea Singida hasikilizwi na Taifa zima, unamfanya ni Diwani wa Singida Vijijini!

vyombo vilivyorusha hotuba ya Lissu sio "media za taifa" ?

audience iliyomfuatilia Lissu haikuwa ni audience ya taifa zima?

Lissu anagombea Urais, ajifunze kuenenda kitaifa, na asiige ya JPM.

Vichwa vya habari havipendezi....


Anaongea kijijini kwake na wanakijiji wenzake, hata Nyerere alifanya hivyo. Haongei na taifa, hayuko kwenye kampeni, na wala siyo rais ndiyo useme kauli yake ni kauli ya serikali. Chombo kilichurusha hiyo clip siyo cha taifa, siyo TBC hiyo.
Kuna mahali pa kuenenda kitaifa, kinyumbani na kifamilia. Tofautisha hayo.
 
Hapa ndio umeonesha vizuri nani aliehusika kumshambulia Tundu Lissu, hukumu yake ipo, na Mungu ndie hakimu wa kweli.
Lilikuwa tukio la kusikitisha sana.
 
Mleta mada hapo Tundu Lissu yupo jukwaani? Alafu umewai fika vijijini singida? Unadhani wanajua kiswahili? Basi umepotea sana!!!

Hapo Tundu Lissu watu wanamsalimia kwa kilugha chao unataka awajibu kiingereza? Unataka awajibu kiswahili?

CCM mmekosa hoja kabisa. Magufuli hasemwi tu kuongea kisukuma bali kwa nepotism yake anayoionesha wazi tena mchana kweupe kwa kuwapendelea watu wake!!!

Kama Tundu Lissu angekuwa Singida Mjini alafu anaongea kinyaturu hapo ungekuwa na hoja ila kwa huko vijijini hapo huna hoja yeyote!!

Lissu kuongea kilugha kijijini tena kwao hilo sio tatizo lolote ndugu!!
Zilikuwa zama ngumu
 
Zilikuwa zama ngumu
Wanamuomba awape tumehuru. Hivi historia ya wazazi wake nani anaijua? Mwenyekiti yeye katuonyesha Dad wake wamevaa 3-piece suit utotoni, Tundu je? Hata picha hakuna?
 
Back
Top Bottom