Video: Ubishani ni Zanzibar ni nchi au siyo? Wenzenu upande wa Zanzibar ni Wazanzibari au Watanzania? Wasira, Rais Samia vs Tundu Lissu: Nani mkweli?

Wana Rais,wimbo wa Taifa,bendera,bunge,baraza la mawaziri,mipaka,ni vile tu hawana kiti UN ila ni nchi kamili
Hata ukiwa na kila kitu, bila sovereignty, wewe sio nchi!. Zanzibar haina dola, haina sovereignty hivyo sio nchi!.
P
 
Wakiamka asubuhi moja wakapiga kura kujitoa Kwenye muungano wanasonga,tukubali kama nchi kuna tatizo la muundo au katiba,wakina Lissu wanatumia hizo loop holes kupiga kwenye mshono
Mkuu mdukuzi , hilo haliwezekani aslaan!. Unakijua kilichomkuta Abdul Jumbe?. Nani atathubutu kufanya ujinga huo?. Tanzania ni nchi moja ya JMT, kitendo cha kujitoa muungano ni sawa na uhaini kwa JMT!, no one can dare do that!. Mwisho wa uwezo wao ni kwa vitimbakwiri kupiga tuu kelele!, there's nothing they can do!. Huu
Muungano wetu adimu na adhimu tutaulinda kwa gharama yoyote!.
P
 
Hawa watoto wa 2000 wakiingia madarakani muungano kwa heri,
 
🤣🤣🤣🤣.......nimekupata vizuri mkubwa. Autonomy Zanzibar ndo inayofanya wabara watake autonomy ya Tanganyika.
 
Dawa ni kuwepo Serikali ya Tanganyika! Kila serikali ijiamlie mambo yake kasoro Ulinzi,Uhamiaji,mambo ya nje na ndani yawe ya Muungano kama ilivyo sasa!
Tanganyika na Zanzibar zisiwe nchi bali mataifa mawili ndani ya nchi moja ya Tanzania.
 
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa JMT. Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT.
2. Wananchi wa Zanzibar ni Watanzania ila pia ni wakaazi wa Zanzibar. Ukaazi sio uraia.
P
Mkuu kuna taifa la Tanzania linaloundwa na nchi mbili; Tanganyika na Zanzibar. Kumbuka wajumbe wa UN ni mataifa sio nchi! Tanzania haikuwahi kuwa nchi!
 
Mkuu kuna taifa la Tanzania linaloundwa na nchi mbili; Tanganyika na Zanzibar. Kumbuka wajumbe wa UN ni mataifa sio nchi! Tanzania haikuwahi kuwa nchi!
wewe ni raia wa wapi?
 
Dawa ni kuwepo Serikali ya Tanganyika! Kila serikali ijiamlie mambo yake kasoro Ulinzi,Uhamiaji,mambo ya nje na ndani yawe ya Muungano kama ilivyo sasa!
Tanganyika na Zanzibar zisiwe nchi bali mataifa mawili ndani ya nchi moja ya Tanzania.
Mkuu serikali iliyopo ni ya Tanganyika ila ililzimisha kibabe iwe serikali ya Tanzania.

Maana hakuna utaratibu uliofanyika wa kuunda muungano isipokuwa Nyerere (Tanganyika) aliamka asubuhi na decree ya kubinafsisha Tanganyika kuwa Tanzania!

Hatujawahi kuwa na serikali ya Muungano!
Mkuu are sure huu mfano uliotumia unaakisi the reality uliyo taka kupresent au unakimbia hoja kwa mfano mwepesi???
 
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa JMT. Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT.
2. Wananchi wa Zanzibar ni Watanzania ila pia ni wakaazi wa Zanzibar. Ukaazi sio uraia.
P
Mkuu Pascal Mayalla
Mwanahabari Nguli na Wakili Msomi nakusalimu!

Ulifanikuwa Kusoma Katiba Ya zanzibar ya mwaka 1984 yenye marekebisho ya 2010?
Vipi kuhusu Sheria namba 5 ya mwaka 1985 au Sheria ya Mzanzibari ya Mwaka 1985?

Jaribu Kuipitia Itapata Majibu Maana Inajenga Msingi wa Katiba Ibara ya 6 ya zanzibar kuhusu Uraia wa Mzanzibar na Mtanzania..

Pia Soma Katiba Ya JMT ibara ya 1 na ya 2 kisha turudi kwenye Mjadala wa Kisheria
 
Mkuu Pascal Shida ni aina ya Muungano Tanzania Iliyoingia..
Kama unakumbuka Kitabu cha mwalimu Nyerere Aliwahi kusema Alianzisha Muungano ambao Sio yeye tu ambaye alikuwa Mgeni nao hata Dunia nzima..
Ila anaelezea Kuhsu aina za Muungani Serikali moja, Shririkisho..
Ila hakufanya Hivyo...

Unahisi Tunahitaji aina gani ya Muungano??
 
Lakini Unajua Kuwa Katiba ya zanzibar ina Nguvu kisheria Pia??
 
🤣🤣🤣🤣
 
Tanzania ni nchi inayotambulikana kimataifa. kama huijui basi ni wewe peke yako

Mkuu uhaini ni nini, uhaini ni kutaka kupata madaraka bila kufuata utaratibu. Je serikali ya Tanganyika ili fuata utaratibu wa kujigeuza kuwa serikali ya Muungano???

Haikufanya uhaini kujinyonga bila idhini ya wananchi wake ili iwe serikali ya Muungano???

Mkuu wakati wa muungano ni nchi gani ilikuwa jike na ipi ilikuwa dume???

Na kama zote zilikuwa majike ilikuwaje nchi moja ikawa dume baada ya Muungano???
 
Vipi kama Akitokea Mpinzani akachukua Urais Zanzibar vipi bado unahisi hawawezi kufanya Hivyo?

Kumbuka katika katiba ya zanzibar Rais Anafanya maamuzi Mwenyewe Bila kufata Ushauri wa mtu yoyote..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…