It's true katiba ya Zanzibar imefanya uhaini kujiinua na kujiita nchi na kutaja mipaka yake, ila katiba ya JMT haiitambui katiba ya Zanzibar!, kwasababu haituhusu!. Huwezi kufanya uhaini kwa sehemu ambayo sio nchi!. Katiba ya Zanzibar kujiita nchi ni kujifurahisha tuu, mwisho Chumbe!. Nchi ni moja tuu, JMT!.
Hata wewe na mkeo, anabeba pochi lake au mkoba wake, wewe huwa unachunguza anabeba nini kwenye mkoba wake?. Kwa nini huchunguzi?, ni kwasababu, hayakuhusu!.
Zanzibar ina utawala wake wa ndani, ni mambo yasiyotuhusu, hata akijiita nchi ya Zanzibar, taifa la Zanzibar, ufalme wa Zanzibar. etc, as long as kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, mambo ya Zanzibar ni yao, hayatuhusu, kuna tatizo gani?.
Tanzania ni nchi moja, yenye uraia mmoja tuu wa JMT, Zanzibar sio nchi, bali ni sehemu ya JMT, huwezi kufanya uhaini kwa eneo ambalo sio nchi!.
P