Video: Ubishani ni Zanzibar ni nchi au siyo? Wenzenu upande wa Zanzibar ni Wazanzibari au Watanzania? Wasira, Rais Samia vs Tundu Lissu: Nani mkweli?

Video: Ubishani ni Zanzibar ni nchi au siyo? Wenzenu upande wa Zanzibar ni Wazanzibari au Watanzania? Wasira, Rais Samia vs Tundu Lissu: Nani mkweli?

Naunga mkono hoja. Nimezaliwa mwaka 1960 na Muungano umenikuta nina mika 4. Nimesoma kwenye nchi ya Tanzania hadi shahada ya uzamili ndani ya Tanzania.

Leo hii nitakuwa kichaaa kudai Tanganyika. Tanganyika ili cease 1964 na sijawahi kupungukiwa kitu kwa kutokuwapo kwa Tanganyika.

Wengi wa wanaochangia huu mjadala wanafurahishwa na uropokaji wa Lissu tu lakini ukiwauliza Ta ganyika itakupa nini ambacho leo huna ndani ya Tanzania wanabaki hawana jibu.

Kwa mfano ardhi huko Tanzania bara tuna 945,000 Square kilometres na mapori kibao. Mtu hajashika hata ekari moja kwenye mapori ya Kisarawe, ila anatamani apate ardhi ZNZ yenye 2,045 Square kilometres, its absurd and weird

..umetoka hoja nzuri sana zenye data.

..sasa kama Tanganyika ni 945,000 sq km, na Zanzibar ni 2,045 sq km, sisi Watanganyika tumekosa nini mpaka tu-sacrifice utaifa na utambulisho wetu ili tuungane na kanchi kadogo hivyo?

..Sisi Watanganyika tumepungukiwa nini, mpaka tuhitaji kuungana na Zanzibar, na kuwaruhusu watutawale, na kutuingilia ktk maamuzi ya nchi yetu? Muungano unatuongezea nini?
 
Sio ubatili, hakuna raia wa Zanzibar kwasababu Zanzibar sio nchi, haina raia, nchi ni Tanzania na uraia ni mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Ila Zanzibar ni eneo halali lenye utawala wake wa ndani na eneo hilo lina wakaazi, hivyo kile kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar ni kitambulisho cha ukaazi wa eneo la Zanzibar na sio kitambulisho cha uraia wa Zanzibar, hakuna raia wa Zanzibar, raia wote ni raia wa Tanzania na wana haki zote za uraia sawa sawa ikiwemo kumiliki ardhi na ajira ndani ya JMT!.
P

..Zanzibar ni nchi.

..tena wana Katiba yao inayosema " Zanzibar ni nchi ... "
 
Sasa huoni kuwa hapo Wazanzibari hawautaki? Ni Watanganyika ndio wanaolazimisha chini ya mwamvuli wa muungano ?

..wanaolazimisha ni CCM.

..Na humo wamo baadhi ya Watanganyika, na baadhi ya Wazanzibari.

..Tanganyika ikirejeshwa, italazimisha kuandikwa upya kwa Katiba, na Sheria zetu, kitu ambacho kitakwenda kupunguza madaraka ambayo CCM wanayo.
 
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa JMT. Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT.
2. Wananchi wa Zanzibar ni Watanzania ila pia ni wakaazi wa Zanzibar. Ukaazi sio uraia.
P
Hapa unakosea, Zanzibar ina Rais, ina bendera yake, ina katiba yake na ina raia wake wanaitwa Wazanzibari, unasemaje Zanzibar siyo nchi, eti ni sehemu ya JMT? Tanzania ilitoka wapi? Zanzibar ipo Tanganyika haipo, ili tuwe sawa Zanzibar ipotee.
 
..Zanzibar ni nchi.
..tena wana Katiba yao inayosema " Zanzibar ni nchi ... "
Mkuu JK JokaKuu , ndio maana nimewashauri humu, elimu ya uraia kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu inahitajika hata kwa watu kama wawe.

1. Tanzania ni nchi moja ya JMT, yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar, Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

2. Maneno ya Zanzibar ni nchi, kwenye katiba ya Zanzibar ni mambo ya ndani ya Zanzibar, katiba ya JMT haiitambui katiba ya Zanzibar, kiukweli nchi ni moja tuu ya JMT na uraia ni mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

P
 
Wewe umfundishe nani uraia bana acha unafiki wa kupindisha uhalisia kwani nyie waramba asali mkoje..wewe hauna haki ya kutusemea ukweli tunao ujua bana... Tanganyika is Tanganyika and Zanzibar Will remain to be Zanzibar
Mkuu JK JokaKuu , ndio maana nimewashauri humu, elimu ya uraia kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu inahitajika hata kwa watu kama wawe.

1. Tanzania ni nchi moja ya JMT, yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar, Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

2. Maneno ya Zanzibar ni nchi, kwenye katiba ya Zanzibar ni mambo ya ndani ya Zanzibar, katiba ya JMT haiitambui katiba ya Zanzibar, kiukweli nchi ni moja tuu ya JMT na uraia ni mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

P
 
..umetoka hoja nzuri sana zenye data.

..sasa kama Tanganyika ni 945,000 sq km, na Zanzibar ni 2,045 sq km, sisi Watanganyika tumekosa nini mpaka tu-sacrifice utaifa na utambulisho wetu ili tuungane na kanchi kadogo hivyo?

..Sisi Watanganyika tumepungukiwa nini, mpaka tuhitaji kuungana na Zanzibar, na kuwaruhusu watutawale, na kutuingilia ktk maamuzi ya nchi yetu? Muungano unatuongezea nini?
Security transcends all reasons
 
..wanaolazimisha ni CCM.

..Na humo wamo baadhi ya Watanganyika, na baadhi ya Wazanzibari.

..Tanganyika ikirejeshwa, italazimisha kuandikwa upya kwa Katiba, na Sheria zetu, kitu ambacho kitakwenda kupunguza madaraka ambayo CCM wanayo.
Tuungane kwenye EAC unatosha. Kila mtu aende kivyake yaishe maneno na kuuliwa Wazanzibari.
 
Kwa Zanzibar inawezekana kwasababu Zanzibar ina autonomy yake ya mambo yake ya ndani, wakati mambo ya Tanzania ni ya wote wakiwemo Wanzanzibari.

Elimu kuhusu katiba, sheria na haki ni muhimu ili watu wajue kuhusu autonomy ya Zanzibar na kuacha hizi kelele za ubaguzi, kutaka kuwabagua, tena afadhali ya sasa, mimi nimeingia Zanzibar kwa passport enzi hizo!.

P
Tanganyika ina autonomy ya mambo yake ya ndani?.
 
Security transcends all reasons

..sio kweli kwamba Znz ni tishio la usalama wa Tanganyika, au majirani zake wengine.

..Na kama ni tishio tungeweza kuwasaidia kujilinda kama tulivyosaidia Comoro na Shelisheli, na sio kusalimu amri kwao, na kuua utaifa wetu.
 
..sio kweli kwamba Znz ni tishio la usalama wa Tanganyika, au majirani zake wengine.

..Na kama ni tishio tungeweza kuwasaidia kujilinda kama tulivyosaidia Comoro na Shelisheli, na sio kusalimu amri kwao, na kuua utaifa wetu.
Tumesalimu kwao kivipi? Wakati marais wote tunawapangia huku Bara?
 
Kwani ili nchi iitwe nchi ni vigezo gani vinaangaliwa.mkitupa hivi vigezo tutakuwa pamoja.
 
Sasa umeeleweka juu ya zanzibar kiukweli chuki imekujaa juu ya zanzibar na hutamani hata uwepo wa zanzibar lakini ishatokezea tu na huna uwezo wa kuifuta hata nyerere alisema kama angekuwa na uwezo angevitupa mbali sana na tanganyika
Huu ndio ukweli wa mambo, tena sio wanahisi tumewaoa, bali huyo mwanamke ndie alijitongozesha, akajibebisha, Mzee Tanganyika akachukua ngoma, akaoa, akatia ndani, analisha, anatunza, anagharimia kila kitu, mke kazi kupendeza tuu, kila kitu bure!.

Niliwahi kuuliza humu Tangu lini Mke Ndani Ya Ndoa Akaomba Uhuru ili Kutoka Nje Ya Ndoa? Aruhusiwe?

Tanzania itakuwa na wanaume wa ajabu wanao ona wivu na wake zao kwa kutamani wawe sawa kwa sawa!.
Mwacheni mkeo apendeze. Mpe kila anachokitaka!.

P
w
 
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa JMT. Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT.
2. Wananchi wa Zanzibar ni Watanzania ila pia ni wakaazi wa Zanzibar. Ukaazi sio uraia.
P
Watu wanakatiba yao bado mnazungumzia ukazi naserikali yao ya mseto ,JMT kuna mseto wa serikali?
 
Kwa hiyo shida ya "kutojitambua" iko upande wetu wa pili yaani Tanganyika..

Tanganyika na Watanganyika wako wapi?

Jina halisi la nchi hii kumbe linapaswa kuwa ni

"Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar"

na siyo


"Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"

Hili jina la "Tanzania" ilitoka wapi? Shida iko kweye jina hili. Uchawi uko humu ndani ya jina hili. Inawezekana vipi kiongozi mmoja anayeitwa "Julius Kambarage Nyerere" abadili jina la nchi na uraia wetu bila ya ridhaa ya wananchi wenyewe??

Huu ni wakati wa kuhoji maamuzi ya huyu aitwaye baba wa taifa hili Mwl Julius K. Nyerere..

Kuna maamuzi yake mengine mengi yalikuwa very fatal na ya hovyo sana na yanahitaji kurekebishwa sasa au kuachana nayo kabisa maana ni mitego ya mauti na kikwazo cha ustawi wetu kama taifa na nchi..

Ndio maana sisi vijana wa buku mbili tunamtambua pombe kama Baba wa Taifa
 
Ubaya hawapendi tuongelee muungano

Ila ukweli ni kwamba dhoruba ndio usalama wa samaki kutovuliwa
 
Kwa Zanzibar inawezekana kwasababu Zanzibar ina autonomy yake ya mambo yake ya ndani, wakati mambo ya Tanzania ni ya wote wakiwemo Wanzanzibari.

Elimu kuhusu katiba, sheria na haki ni muhimu ili watu wajue kuhusu autonomy ya Zanzibar na kuacha hizi kelele za ubaguzi, kutaka kuwabagua, tena afadhali ya sasa, mimi nimeingia Zanzibar kwa passport enzi hizo!.

P
Mkuu una shida sana wewe,bora ungebaki Mzilankende kuliko kusumbua Watanganyika wasio na hatia.Mnatukosea sana kwa elimu hizi za kudidimiza haki za upande mmoja wa Muungano na kuinua haki za upande mwingine kisa tu wanazungukwa na bahari.
 
Back
Top Bottom