Video: Wakili Boniface Mwambukusi akifafanua kisheria na kikatiba ni kwanini uteuzi wa Naibu Waziri Mkuu ni uvunjaji wa katiba ya JMT ya 1977

Video: Wakili Boniface Mwambukusi akifafanua kisheria na kikatiba ni kwanini uteuzi wa Naibu Waziri Mkuu ni uvunjaji wa katiba ya JMT ya 1977

Haya sasa n huyu Wa Sasa hivi kapewa kwa sababu gani unawez kuniambia 🤔🤔🤔🤔 maana mmmh Doubtfull
Sababu anazo mwenyewe. Ila naweza nikabuni. Nafikiri Biteko amejipambanua kama mchapakazi na mfuatiliaji sana. Kwa hiyo kwenye kipindi hiki anahitaji mtu anayeweza kumtuma popote.

Kwa upande wa kisiasa anatafuta turufu ya Sukuma Gang na kanda ya ziwa ambayo ni muhimu kwa kura za 2025
 
Sikubaliani na point #2. Ukifanya ammendment ya kisheria itabidi iwe ya kudumu. Kwa hiyo hata akija Rais mwingine itabidi amuweke Naibu WM.

Hawa manaibu wanawekwa kukidhi mambo fulani tu. Kwa mfano Salim Ahmed Salim alipewa unaibu mwaka 1985 ili kumtunzia hadhi kwa kuwa alikuwa na profile kubwa baada ya kuwa mtarajiwa wa Urais wa Tanzania Nyerere alipokuwa anatoka.

Mrema alipewa kama shukrani tu kwa namna alivyo kuwa anashughukikia masuala ya ufisadi wa akina Chavda, wizi wa dhahabu etc.

Mwabukusi ni boksi tupu halina kitu zaidi ya kelele na kufoka. Msimpe umaarufu asiokuwa nao
Umepatia 💯 Kwa ulio andika hapo juu.
 
Mkuu Uzima Tele I beg to differ with my learned senior Counsel. Naendelea na msimamo na maoni yangu kuwa Mhe. Rais yuko sahihi kikatiba kuanzisha na kumteua wa kushika Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu.

Nimeitaja ( na hata Wakili Mwabukusi ameitaja) ibara ya 36 (1). Inatoa mamlaka kwa Rais kuanzisha nafasi/ofisi za kimadaraka.

Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu haipo/haikutajwa kwenye Katiba. Jana ndiyo imeanzishwa. Majukumu yake yataainishwa kwenye Hati ya Kuanzishwa kwake.

Kuanzishwa kwa Ofisi hiyo hakumaanishi kuivunja, kuivuruga, kuiingilia au kuibadili Ofisi ya Waziri Mkuu. Ni Ofisi mpya inayojitegemea iliyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba (Ibara ya 36(1)).
Vipi kuhusu hoja hii ya Leaned Senior Counsel Boniface Mwabukusi; ofisi ya PM, DPP, AG, Bunge au CAG ni ofisi za umma zilizoundwa na kuwekewa utaratibu na masharti maalumu kikatiba kuanzia katika uteuzi, utendaji na uwajibikaji wa watu wanaoteuliwa na kushika ofisi hizi..."
 
Hoja nzuri ya kisheria ya wakili msomi Boniface Mwabukusi.

Pia naongezea pale katiba inapokuwa kimya haimaanishi basi unaweza kufanya lolote inatakiwa mfanya maamuzi ajiulize inakubalika kijamii na siyo ku abuse power uliyopewa kwa kuwa katiba ipo kimya.

Ni vizuri viongozi wakatambua katiba ni mali ya wananchi katika maandishi na ile ambayo haijaandikwa, mfano katiba haisemi viongozi wachaguliwe kutoka maeneo yote ya Tanzania lakini mawaziri wanapoteuliwa wananchi hutizama uteuzi huo kuona kama ni jumuishi kwa maana una wateuliwa kutoka pande kadhaa za jamhuri ya muungano wa Tanzania na kutoka makundi kadhaa ya kijamii.

Hivyo hili la Naibu Waziri Mkuu wananchi kuhoji linauzito wake na bahati nzuri hoja za wakili Mwabukusi zinakazia hoja kuwa uteuzi huu wa Naibu Waziri Mkuu siyo tu wananchi hawajaukubali bali hata katiba imesiginwa.

Hivyo ni muhimu viongozi kujiuliza kama wananchi wataafiki maamuzi wanayofanya viongozi hata kama katiba ipo kimya maana wananchi ndiyo mabosi wao.

The Tenth Amendment says that the Federal Government only has those powers delegated in the Constitution. If it isn’t listed, it belongs to the states or to the people. Source : The Bill of Rights: What Does it Say?


View: https://m.youtube.com/watch?v=wwEZOj5VKSg
 
Kumbukumbu zangu zinaniambia alikua Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Maana ubumge wenyewe kwa mara ya kwanza aliingia bungeni mwaka 1985
Kabla ya 1985 waziri wa sheria na mwanasheria mkuu wa serikali kuna kipindi nafasi hizo ziliunganishwa.

Bungeni aliingia hata kabla ya 1985 kwa nafasi yake ya AG.
 
HUYU MWABUKUSI ,MIMI KWA SASA NDIO MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI.

JAMAA ANA AKILI, ANA EXERCISE TAALUMA YAKE, HAWA WENGINE PANYA ROAD, WAMESOMA KWA KUKALILI 🤣🤣.


JAMAA ANAONGEA KWA UELEWA .



NAKUBALIANA NAYE 100%
 
Mkuu Uzima Tele I beg to differ with my learned senior Counsel. Naendelea na msimamo na maoni yangu kuwa Mhe. Rais yuko sahihi kikatiba kuanzisha na kumteua wa kushika Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu.

Nimeitaja ( na hata Wakili Mwabukusi ameitaja) ibara ya 36 (1). Inatoa mamlaka kwa Rais kuanzisha nafasi/ofisi za kimadaraka.

Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu haipo/haikutajwa kwenye Katiba. Jana ndiyo imeanzishwa. Majukumu yake yataainishwa kwenye Hati ya Kuanzishwa kwake.

Kuanzishwa kwa Ofisi hiyo hakumaanishi kuivunja, kuivuruga, kuiingilia au kuibadili Ofisi ya Waziri Mkuu. Ni Ofisi mpya inayojitegemea iliyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba (Ibara ya 36(1)).

Mkuu, Waziri Mkuu ni Ofisi.

Ofisi hii hupata kibali kupitia Bunge.


Huyu naibu anaenda kua naibu kwenye ofisi ya Waziri Mkuu.

Kibali chake anakipata wapi??.

Mimi sio MWANASHERIA.
 
Vipi kuhusu hoja hii ya Leaned Senior Counsel Boniface Mwabukusi; ofisi ya PM, DPP, AG, Bunge au CAG ni ofisi za umma zilizoundwa na kuwekewa utaratibu na masharti maalumu kikatiba kuanzia katika uteuzi, utendaji na uwajibikaji wa watu wanaoteuliwa na kushika ofisi hizi..."
Hapo Mwabukusi atakuwa ameteleza. Kwa nini iwe halali kwenye kuvunja wizara na kuunda mpya na iwe haramu kuanzisha ofisi ya Naibu Waziri Mkuu wakati hata ofisi za mawaziri nazo zimewekewa utaratibu wake wa uteuzi na majukumu yake? Naungana na Petro Mselewa kwenye hili.
 
NB: JF Moderators, naomba hii thread ijitegemee. Najua imeshajadiliwa lakini naona huyu wakili kaja kivingine. Tuwape watu nafasi wajadili hoja yake..

Back to the topic;

✍️Ni kweli Hayati Mwl Julius K. Nyerere aliwahi kuunda ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na kumteua Dr Salim A. Salimu kushika SER=221]JokaKuu[/USER] denooJ Mag3 na wengine mna maoni yoyote?
Naona kuna watu wanataka kupotosha. Haijawi tokea Nyerere akateua Naibu waziri mkuu. Na Salim Hamed Salim hajawahi kuwa naibu Waziri Mkuu.

Historia inachakachuliwa na watu wamenyamaza tu. Vijana wengi hawajui historia ya hii nchi. hata baadhi ya wanasiasa tulionao leo. Ni wachache tulioweza waona viongozi wote wa nchi hii, ambao tunaweza kutoa historia kidogo.

Mwaka 1984 baada ya Sokoinne kufa Mwalimu Nyerere alimteuwa Salim Hamed Salim kuwa Waziri Mkuu. Na wakati huo Waziri Mkuu alikuwa anakuwa pia Makamu wa pili wa Rais baada ya Rais wa Zanznibar.

Mwaka 1985 Nyerere aliachia madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na uchaguzi ulifanyika chini ya chama kimoja Mwinyi alie kuwa Mgombea pekee alishinda kwa kura za ndiyo na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwinyi alikuwa ni Rais na kule Zanzibar alikuwa Idrisa Abdul Wakil Mwinyi. Hivyo nafasi ya Waziri Mkuu ilibidi ateuliwe mtu kutoka bara ndipo Jaji Joseph sinde Warioba aliteuliwa na kushika hiyo nafasi huku akiwa pia makamu wa kwanza wa Rais.

Salim Hamed Salim aliteuliwa kuwa Waziri wa ulinzi na alifanya mabadiliko na maendeleo makubwa kwa jeshi letu kwa mara ya kwanza wakawa na uniform zaidi ya moja. Akaagiza magari mengi sana kwa ajiri ya jeshi.

Sasa mnao sema Nyerere alimteuwa Jaji Warioba sijui ilikuwa lini? Nyerere kaachia Urais Oct 1985. Tena nakumbuka Mwinyi alipo mteuwa Warioba, kuna uwanja wa Musoma ulikuwa unajengwa. Kulikuwa na tofali. Ule uwanja ulisimama kujengwa na tofali zote zikachukuliwa kupelekwa huko Nyamuswa- Ikizu kujenga nyumba ya Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais ndugu Joseph Sinde Warioba.

Wakati huo mimi nilikuwa mdogo tu, na chipukizi wa kudumu katika kupokea viongozi. Hivyo nilihoji kwa nini walichukua tofali za kujengea uwanja wa musoma na kuzipeleka zikajenge nyumba kwao waziri mkuu, tulijibiwa wameazima tofali hivyo watazirudisha kumalizia uwanja.

Walisema ni aibu waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais nyumbani kwao kutokuwa na nyumba ya maana hivyo wamefanya vile hili kumhifadhi waziri mkuu wetu.

Niseme tu hadi leo zile tofali hazijarudishwa na uwanja wa Musoma umebaki kama ulivyo. Ulitakiwa jukwaa zijengwe kwa kuzungushwa. Uwanja huu jukwaa kubwa na lile dogo zilijengwa mwaka 1984-1985 wakati wa kufanyika sherehe za kuzaliwa chama cha mapinduzi.

Tafadhali mzee Warioba mzee wetu rejesha tofali Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume Musoma umaliziwe kujengwa. Ahadi ni deni!

Nakumbuka sana kwani nilikuwa kamanda wa kikosi. (Pratoni kamanda) sherehe hizi zilifana sana kwani kwa mara ya kwanza vijana tulifundishwa mbinu za kivita. Jeshi ndo lilikuwa likitoa mafunzo pia tulikuwa na mwalimu wa Haraiki yeye alisomea China na Urusi ya zamani huyu mwalimu aliagizwa kutoka Comoro.
Na wakati wa mafunzo yalikuja magari ya maziwa na tulikunywa sana maziwa tukipumzika kabla ya kuendelea tena na mazoezi.

Kuna watu tumeonja raha za utawala wa Nyerere japo kuna wapinzani leo wanamtukana, nachojua hawamjui vema Nyerere na wazee wenzake akina Mkwawa. Walijitahidi kwa kiasi chao.

Viongozi wote wa Taifa walikuwepo kuanzia Rais Nyerere, Rais Mwinyi toka Zanzibar, Waziri Kiongozi wa Zanzibar Maalim Seif, waziri Mkuu Salim Hamed Salim, Mzee Mfaume Rashid Kawawa. Akina Bibi Titi Mohamed na wengineo wengi.

Sifa zilimwagika kwa ile haraiki, bila kumsahau mkaguzi alie kuwa anakuja kutuona tumeiva kiasi gani, Major General Mwita Marwa.

Baada ya sherehe hizi kuna baadhi vijana tuliteuliwa kwenda Urusi.

Baadae miaka ya 90 na ushee, wakati huo Mrema akiwa waziri wa mambo ya ndani. Kwa kazi alizokuwa anafanya. Mawaziri wenzake wakata mzingua asiwaingilie kwani Mrema aliwabana hadi mawaziri.

Ndipo Rais Mwinyi akamteuwa Mrema kuwa Naibu waziri Mkuu. Lakini uteuzi huu ulileta gumzo kiasi kwamba haukuwa unatambulika rasmi. Ulifanywa kisiasa zaidi. Ndo maana Mrema hakuwai kulipwa mafao, wala kutambulika rasmi kwani hata ofisi ya naibu wa rais hakuwa nayo.

Hivyo niseme tusipotoshe historia ya hii nchi. Kutaka kutetea mambo ambayo siyo. Warioba hakuwa waziri Mkuu wakati wa Nyerere bali Mwinyi na alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais pia.

Salim Hamed Salim hakuwai kuwa naibu Waziri Mkuu bali alikuwa Waziri Mkuu na Makamu wa pili wa Rais.


Nafasi ya Naibu Waziri Mkuu ilitolewa mara moja tu, nayo ilikuwa ya kisiasa zaidi. Ilikuwa kwa Mrema pekee. Ndo maana hata Mrema mwenyewe alikuwa akiongea atajitambulisha rasmi kama waziri wa mambo ya ndani mstaafu. Akisema naibu waziri mkuu alikuwa akicheka yeye mwenyewe kwani alijua cheo hiko hakikuwepo kikatiba.

Waziri mkuu ni anatakiwa athibitishwe na Bunge. Hivyo hata naibu wake maana yake anauwezo wa kutenda sawa na waziri Mkuu, na bahati mbaya Katiba haijatamka juu ya naibu waziri mkuu.
 
Hizi technicalities zinatutoa kwenye Uhalisia na Ufanisi.., Hata kama anaruhusiwa sio kwamba ndio afanye..., Binafsi sioni faida ya alichofanya hata kama kingekuwa kinaruhusiwa; Mimi kama mmoja wa walipa Kodi nachelea kusema haya ni matumizi mabaya ya vijisenti...
 
Mkuu Uzima Tele I beg to differ with my learned senior Counsel. Naendelea na msimamo na maoni yangu kuwa Mhe. Rais yuko sahihi kikatiba kuanzisha na kumteua wa kushika Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu.

Nimeitaja ( na hata Wakili Mwabukusi ameitaja) ibara ya 36 (1). Inatoa mamlaka kwa Rais kuanzisha nafasi/ofisi za kimadaraka.

Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu haipo/haikutajwa kwenye Katiba. Jana ndiyo imeanzishwa. Majukumu yake yataainishwa kwenye Hati ya Kuanzishwa kwake.

Kuanzishwa kwa Ofisi hiyo hakumaanishi kuivunja, kuivuruga, kuiingilia au kuibadili Ofisi ya Waziri Mkuu. Ni Ofisi mpya inayojitegemea iliyoanzishwa kwa mujibu wa Katiba (Ibara ya 36(1)).
Basi ipewe jina tofauti kama ndio hivyo
 
Uko sawa ndugu yangu denooJ

Kwa maelezo zaidi naomba usome post yangu #16 hapo juu nikijibu hoja ya wakili Petro E. Mselewa..

Lakini nikuulize tena swali hili;

kwamba, unadhani inawezekana Rais wa JMT akaamka kesho na kuanzisha ofisi na cheo cha Makamu wa pili wa Rais wa JMT na Kisha akateua Kwa sababu tu katiba inampa mamlaka ya kuanzisha ofisi na kumteua mtu kushika wadhifa wa ofisi hiyo?
Ndiyo inawezekana na pia ilikuwepo sikumbuki tu ni nani aliyeiondoa lakini iliwepo
 
NB: JF Moderators, naomba hii thread ijitegemee. Najua imeshajadiliwa lakini naona huyu wakili kaja kivingine. Tuwape watu nafasi wajadili hoja yake..

Back to the topic;

✍️Ni kweli Hayati Mwl Julius K. Nyerere aliwahi kuunda ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na kumteua Dr Salim A. Salimu kushika wadhifa huo kikatiba PM akiwa Jaji Joseph Sinde Warioba...

✍️Vivyo hivyo Rais ally Hassan Mwinyi aliwahi kufanya kosa la namna hii na nafasi hiyo kushikwa na Hayati Augustine L. Mrema wakati kikatiba PM akiwa John Malecela..

✍️Sasa Rais Samia Suluhu Hassan naye kafanya makosa hayahaya.

Je, makosa ya mwingine yanaweza kuhalalisha jambo?

✍️Msikilize Wakili Msomi Boniface Mwambukusi akitolea ufafanuzi wa kisheria na kikatiba wa makosa haya..👇👇👇👇
View attachment 2735582

Aliyoyasema kwa ufupi (quotes):

".....Ni kweli Rais kikatiba ana mamlaka na haki (right) ya ku - constitute na ku - abolish any office at anytime. Lakini haki na wajibu huu hau - extend kwenye office ambazo zimeanzishwa na katiba....."

".....Kwa mfano; ofisi ya PM, DPP, AG, Bunge au CAG ni ofisi za umma zilizoundwa na kuwekewa utaratibu na masharti maalumu kikatiba kuanzia katika uteuzi, utendaji na uwajibikaji wa watu wanaoteuliwa na kushika ofisi hizi..."

"....Mfano, Waziri Mkuu anapoteuliwa ni lazima athibitishwe na wananchi kupitia Bunge lao. Kwa maana hiyo, ni makosa na kwa kweli haiwezekani Rais atafute mtu mwingine kwa mlango wa nyuma (au wa uani) na amkasimishe majukumu ya kikatiba ya Waziri Mkuu. Hizo zitakuwa vurugu na ni kukiuka katiba.."


Ndugu Petro E. Mselewa, Pascal Mayalla JokaKuu denooJ Mag3 na wengine mna maoni yoyote?
Hili suala kwa mara kwanza linatakiwa lipelekwe mahakamani kutafuta tafsiri sahihi maana sheria zilizotungwa chini ya Chenge zina makengeza na vichaka vingi kujifichia wenyewe nia OVU na rasilimali za nchi
 
NB: JF Moderators, naomba hii thread ijitegemee. Najua imeshajadiliwa lakini naona huyu wakili kaja kivingine. Tuwape watu nafasi wajadili hoja yake..

Back to the topic;

✍️Ni kweli Hayati Mwl Julius K. Nyerere aliwahi kuunda ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na kumteua Dr Salim A. Salimu kushika wadhifa huo kikatiba PM akiwa Jaji Joseph Sinde Warioba...

✍️Vivyo hivyo Rais ally Hassan Mwinyi aliwahi kufanya kosa la namna hii na nafasi hiyo kushikwa na Hayati Augustine L. Mrema wakati kikatiba PM akiwa John Malecela..

✍️Sasa Rais Samia Suluhu Hassan naye kafanya makosa hayahaya.

Je, makosa ya mwingine yanaweza kuhalalisha jambo?

✍️Msikilize Wakili Msomi Boniface Mwambukusi akitolea ufafanuzi wa kisheria na kikatiba wa makosa haya..👇👇👇👇
View attachment 2735582

Aliyoyasema kwa ufupi (quotes):

".....Ni kweli Rais kikatiba ana mamlaka na haki (right) ya ku - constitute na ku - abolish any office at anytime. Lakini haki na wajibu huu hau - extend kwenye office ambazo zimeanzishwa na katiba....."

".....Kwa mfano; ofisi ya PM, DPP, AG, Bunge au CAG ni ofisi za umma zilizoundwa na kuwekewa utaratibu na masharti maalumu kikatiba kuanzia katika uteuzi, utendaji na uwajibikaji wa watu wanaoteuliwa na kushika ofisi hizi..."

"....Mfano, Waziri Mkuu anapoteuliwa ni lazima athibitishwe na wananchi kupitia Bunge lao. Kwa maana hiyo, ni makosa na kwa kweli haiwezekani Rais atafute mtu mwingine kwa mlango wa nyuma (au wa uani) na amkasimishe majukumu ya kikatiba ya Waziri Mkuu. Hizo zitakuwa vurugu na ni kukiuka katiba.."


Ndugu Petro E. Mselewa, Pascal Mayalla JokaKuu denooJ Mag3 na wengine mna maoni yoyote?
Kama kweli ni “mjuzi” wa sheria mbona kesi yake ilitupiliwa mbali?
 
Nasubiria wenye ujuzi wa Sheria waje....
Mkuu Mimi sijui Sheria kwasababu sikuisomea, lakini ABC za Katiba nazijua. Mwambukusi haijui Katiba au anapotosha kwa makusudi.
Halafu mtoa post kachemka. Dk. Salim aliteuliwa na Rais Mzee Mwinyi sio Mwl. Nyerere.
 
Back
Top Bottom