Video ya Rais wa Sudan Kusini akitokwa na haja ndogo yazua maswali kuhusu afya za viongozi

Video ya Rais wa Sudan Kusini akitokwa na haja ndogo yazua maswali kuhusu afya za viongozi

Katika tukio lisilo la kawaida, Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir mwenye miaka 71 ameonekana akitokwa na haja ndogo wakati wa hafla ya Kitaifa na wimbo wa Taifa ukipigwa. Kitendo hicho kinaibua maswali kuhusu hali za kiafya za viongozi wengi duniani kuendelea kukaa madarakani hata baada ya umri wao kuwa mkubwa na wengine wakiwa na afya zisizoridhisha.

Mwaka huu 2022, pia mgombea wa Urais nchini Nigeria Bola Ahmed Adekunle Tinubu mwenye miaka 70 alionekana akiwa na mfuko maalumu wa kuhifadhia mkojo wakati wa mchakato wa kuanza kampeni hali iliyopelekea wananchi kuhoji kuhusu afya yake na majukumu anayotaka kugombea.

KUWEKA HAPA UNA MOYO YAAN ...
NGOJA NKANUNUE JEZI YA FRANCE MIE NIJIANDAE...BABU KAKOMAA KAM HAKUNA TUKIO..KINGINE WALINZI MMOJA ALIKUWA ANACHEKA KMOYOMOYO HAHAHAAAAA ...

DJ NAOMBA WIMBO WA DUNIA TUNAPITAA EE KILAKITU KITABAKIAA..........
 
Kama katiba zinataka utimamu wa akili kwa nini zisitake utimamu wa afya? Hata kama kiongozi atapata ugonjwa utaokaochukua muda mrefu kutibiwa na kupona au kutokupona ni bora ajiuzulu. Maradhi ambayo yataathiri uimara wa afya ya kiongozi ni aibu kwa taifa bora aachie madaraka akashughulikie afya yake
 
Bado M7 anakomaa.
Ukute kwenye ile miguo yake oversize kuna adult diaper.
Siku hizi safari zake zote anatembea na gari lenye choo.

1671010935423.png
 
Huyo ana afadhali maana kutozuia mkojo kunaweza kusiathiri akili na ufanyaji wa maamuzi. Kuna huyu Bola Asiwaji Tinubu (BAT) mgombea wa chama tawala cha APC pale Nigeria, huyu mzee hana sifa yoyote ya kuwa Rais hata angekuwa na miaka 50. Ukitazama speech zake bila teleprompter hawezi kabisa kuongea, anatetemeka mwili, anatembea kwa shida, uwezo wake wa kufikiri ni mdogo kwa sababu akiulizwa hiki anajibu kile. Waliosoma nae wana miaka zaidi ya 80 ila yeye anasema ana 70 na ngapi sijui. Hii Afrika ina shida sanaView attachment 2446300
Mtu kama huyu ni dhahiri ni mroho, mbinafsi, mlafi anayelenga maslahi yake. Waafrika na shetani wana udugu.
 
Katika tukio lisilo la kawaida, Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir mwenye miaka 71 ameonekana akitokwa na haja ndogo wakati wa hafla ya Kitaifa na wimbo wa Taifa ukipigwa. Kitendo hicho kinaibua maswali kuhusu hali za kiafya za viongozi wengi duniani kuendelea kukaa madarakani hata baada ya umri wao kuwa mkubwa na wengine wakiwa na afya zisizoridhisha.

Mwaka huu 2022, pia mgombea wa Urais nchini Nigeria Bola Ahmed Adekunle Tinubu mwenye miaka 70 alionekana akiwa na mfuko maalumu wa kuhifadhia mkojo wakati wa mchakato wa kuanza kampeni hali iliyopelekea wananchi kuhoji kuhusu afya yake na majukumu anayotaka kugombea.

Na kweli sio tukio la kawaida hadi mwenyewe kajistukia.

Ila hio ni dharura ya kibinadamu , tunampa pole sana.
 
Angevaa suti ya rangi nyeusi, kidogo ingesaidia kuficha hiyo aibu.
Hiyo rangi ya suti aliyovaa, si rafiki kama wanajua kibofu kishafanya yake.
Viongozi wa kung'ang'ania madarakani, kila uchaguzi wapo. Utasema hakuna wengine wenye sifa za kuongoza nchi...
 
Back
Top Bottom