Vifo Katesh; Je, Tanzania kuna milima mingine kama mlima Hanang?. Serikali imechukua hadhari gani?

Vifo Katesh; Je, Tanzania kuna milima mingine kama mlima Hanang?. Serikali imechukua hadhari gani?

Yeah. Kulingana na kitabu cha Ufunuo, milima yote ina 'uwezo wa kuwaangukia na kuwafunika binadamu'.

Screenshot_20231205-125758.jpg

Screenshot_20231206-154105.jpg
 
Inaelekea wewe bado kijana mdogo! Landslide iliyotokea Makonde plateau huko Mtwara ilikuwa kubwa sana na iliangamiza vijiji na watu wengi sana. Majanga kama haya kuyazuia ni vigumu sana kwa sababu mbalimbali.

Kwa mfano ili kuzuia maporomoko ya mlima Hanang ilitakiwa kupunguza uwingi wa maji kwa kuzibua chem chem (springs) ili zitiririshe maji mengi. Kitendo cha kutiririsha maji mengi baada ya muda mrefu kungesababisha vijito kutoka mlimani kupungua maji. Kwa hiyo watu wangelalamika na kupelekea kumtuhumu huyo aliyetoa wazo hilo kama mhujumu uchumi!

Kitaalamu inawezekana kujenga vipima maji (piezometers) ili kupima uwingi wa maji kila wakati lakini inahitajika utashi wa kisiasa kuidhinisha matumizi ya fedha zinazotakiwa.
Hujajibu swali, je, waendelee kujenga na kuishi hapohapo na vilevile pamoja na wenzao wenye mazingira kama haya? haitatokea tena, itatokea baada ya muda gani tena?
 
Kwa kuongezea,

Ili nchi iendelee inahitaji vitu vifuatavyo; WATU, ARDHI, SIASA SAFI, NA UONGOZI BORA. Kwa sasa Tanzania imebaki vitu viwili tu...
Kuna visiwa vya kwenye bahari ya Pacific vinaelekea kuzama chini ya bahari kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na usawa wa bahari kupanda.

Kwa hiyo, vinapanga kuendelea kama nchi mtandaoni tu baada ya kuzama baharini.

Usije kushangaa visiwa hivi vikapata maendeleo kama nchi za mtandaoni, bila ya kuwa na ardhi, wakati sisi tuna ardhi lakini hatuna maendeleo.
 
Maendeleo hayaji kwa idadi kubwa ya watu, maendeleo yanakuja kutokana na kujua kutumia watu na kupanga uchumi vizuri kulingana na idadi ya watu.

Unaweza kuwa na watu wengi, lakini hujajipanga, unaongeza njaa tu.

Ingekuwa maendeleo yanatokana na wingi wa watu, India ingekuwa imeendelea kuliko Marekani na Nigeria ingekuwa imeendelea kuliko Italy.
Sio kweli, unampotosha mwenzako, watu wengi ndio uchumi wenyewe. Hakuna nchi ambayo haipendi masoko ya China na India kwa bidhaa zao kutokana na idadi yao kubwa ya watu (consumers). Nchi za magharibi zina uchumi mkubwa kwasabu ya dhambi inazozifanyia nchi nyingine kwenye masoko (WTO) lakini na uporaji kutoka nchi nyingine. Kwanini viwanda vingi vya Marekani viko Asia?
 
Hujajibu swali, je, waendelee kujenga na kuishi hapohapo na vilevile pamoja na wenzao wenye mazingira kama haya? haitatokea tena, itatokea baada ya muda gani tena?
Hapo waendelee kujenga tu kwa sababu baada ya maporomoko hayo ardhi haitakuwa na uwezo wa kuhifadhi maji tena. Sehemu ya ardhi iliyobaki itachuruzisha maji na kubaki kiasi cha kawaida na hivyo haitatokea tena.
 
Sio kweli, unampotosha mwenzako, watu wengi ndio uchumi wenyewe. Hakuna nchi ambayo haipendi masoko ya China na India kwa bidhaa zao kutokana na idadi yao kubwa ya watu (consumers). Nchi za magharibi zina uchumi mkubwa kwasabu ya dhambi inazozifanyia nchi nyingine kwenye masoko (WTO) lakini na uporaji kutoka nchi nyingine. Kwanini viwanda vingi vya Marekani viko Asia?
Sawa.

Endeleeni kuzaana bila mpango halafu muone kama kuzaana ndiyo utatuzi wa matatizo yenu.

Hawa watu ulionao unapata shida kuwalisha, kuwasomesha, etc.

Huna mipango mizuri ya kutumia nguvukazi. Watu hawa wachache hujui kuwatumia.

Halafu unasema, hapa tatizo langu ni watu wachache, ngoja niongeze watu wawe wengi.

Sasa kama hawa wachache hujui kuwatumia, hao wengi utawezaje kuwatumia?

Kwenye habari za mataifa ya magharibi na chumi zao, nimetoa mfano wa Japan. Japan si nchi ya magharibi.

Tujikite Africa kuondoa habari za magharibi.

Nchi zenye chumi tajiri kabisa kwa per capita income ni pamoja na Seychelles na Mauritius. Hizi nchi zina watu wachache lakini GDP per capita kubwa.

Ingekuwa wingi wa watu ndio unaoketa maendeleo, Nigeria ingezipita Mauritius na Seychelles kwa GDP per capita.

Tuangalie mifano kwa data.

Kwa hesabu za mwaka 2021:

Nigeria ina takriban watu milioni 215 na GDP per capita ya US $2066.

Seychelles ina watu 99,258 na GDP per capita ya US $14,653.

Kipato cha mtu mmoja wa Seychelles, kwa wastani, kwa hesabu za mwaka 2022, kilikuwa takriban mara saba ya kipato cha wastani cha mtu wa Nigeria kwa mwaka huo huo, licha ya Nigeria kuwa na watu mara 2166 zaidi ya Seychelles.

Sasa, mnaosisitiza kuwa wingi wa watu ndio uchumi bora, hamuoni kuwa Nigeria kuna watu wengi sana wanaogawana umasikini, wakati Seychelles kuna watu wachache wana uchumi mzuri tu, mara saba ya uchumi wa Nigeria kwa GDP per capita?
 
Mkuu umeongea vyema lkn nchi hii ina lack mipango ndio tatizo mama kwa kweli.
Kuna maeneo au mikoa ilitakiwa kusiwepo makazi kabisa maana kuna support kilimo almost mkoa mzima au wilaya nzima.
Yaani sisi kama nchi tuna Dhani maisha yatakuwa hivi milele wakati mabadiliko ni mengi sana.
Kizazi kijacho kitatumia ngivu nyingi sana kuweka mambo sawa.
Hata maeneo yanayofaa kilimo na ufugaji wanakwenda kupima viwanja vya makazi kana kwamba watu hawahitaji chakula wala nyama na maziwa tena na ardhi sehemu nyingine hakuna. Watu wanakwenda kujenga kwenye njia za maji bila kuwa na mipango ya kuzuia mvua kubwa zisinyeshe. Mipango mibovu.
 
Tunasubiri vifo ili turushe helkopta kuangalia kiwango cha uharibifu na idadi ya waliokufa badala ya kunusa mapema hatari na dalili vifo.

Kwa kilichotokea Hanang ni matokeo ya mipango mibaya ya watanzania wenzetu tunaowalipa kwa kazi ya kutulinda na majanga. Kuna idadi kubwa ya watanzania ambao wameruhusiwa kujenga chini na juu ya milima, mabondeni, kwenye njia za maji na wanyama. Watu hawa wamepewa vibali vyote ama vya kujenga, au kuingiza umeme na maji kwenye nyumba zao bila kupewa onyo la aina yoyote wala elimu ya namna ya kuishi kwenye maeneo hayo.

Maswali:,
1. Je, baada ya maafa ya Katesh, watu waendelee kujenga na kuishi kwenye maeneo yao yaleyale yaliyokubwa na janga au wahamie kwingine?
2. Je, Tanzania hakuna watanzania wanaoishi kwenye maeneo yanayofanana na maeneo ya Katesh?
3. Je, kuna mifumo gani ya kutaarifiana kama ving'ora kama likitokea janga?

Kinga ni bora kuliko kiba hii tunayoiona.
Sidhani kama unajua Hanang' wewe acha lawama zisizo na msingi...Hakuna kitu kama hicho
 
Tunasubiri vifo ili turushe helkopta kuangalia kiwango cha uharibifu na idadi ya waliokufa badala ya kunusa mapema hatari na dalili vifo.

Kwa kilichotokea Hanang ni matokeo ya mipango mibaya ya watanzania wenzetu tunaowalipa kwa kazi ya kutulinda na majanga. Kuna idadi kubwa ya watanzania ambao wameruhusiwa kujenga chini na juu ya milima, mabondeni, kwenye njia za maji na wanyama. Watu hawa wamepewa vibali vyote ama vya kujenga, au kuingiza umeme na maji kwenye nyumba zao bila kupewa onyo la aina yoyote wala elimu ya namna ya kuishi kwenye maeneo hayo.

Maswali:,
1. Je, baada ya maafa ya Katesh, watu waendelee kujenga na kuishi kwenye maeneo yao yaleyale yaliyokubwa na janga au wahamie kwingine?
2. Je, Tanzania hakuna watanzania wanaoishi kwenye maeneo yanayofanana na maeneo ya Katesh?
3. Je, kuna mifumo gani ya kutaarifiana kama ving'ora kama likitokea janga?

Kinga ni bora kuliko kiba hii tunayoiona.
Kuna mlima unaitwa Mkindu au Mguluwandege. Mwaka jana mwezi wa nne kuliporomoka majabali usiku fulani. Majabali hayo hayakufika chini na wananchi pale wanafahamu. Mlima upo Morogoro eneo la Mkindu.

Watu wanaendelea kujenga kuufuata mlima huo. Na umekaa kimtego haswaa
 
Hata maeneo yanayofaa kilimo na ufugaji wanakwenda kupima viwanja vya makazi kana kwamba watu hawahitaji chakula wala nyama na maziwa tena na ardhi sehemu nyingine hakuna. Watu wanakwenda kujenga kwenye njia za maji bila kuwa na mipango ya kuzuia mvua kubwa zisinyeshe. Mipango mibovu.
Tamaa za fedha na ujinga wa kutoiona kesho vinasababisha maafa siku za usoni
 
Kwa mujibu wa Samico Tanzania Mlima Hanang' una kitambi.

Sasa unashauri watu wa Moshi wahame?
Watu wanajisemesha tu bila kujali context. Kwa land scape ya Tanzania ni sehemu gani ambapo Kuna makazi hakuna milima, vijilima au milima mikubwa? Hizi natural disaster ni sehemu ya maisha yanapotokea tukubali kwamba it's because of nature. Katesh ni mji wa zamani sana na haijawahi tokea kitu kama hicho na watu wa Ile jamii wanajua kutunza mazingira Yao sana sana. Palipotokea tukio kulikuwa well conserved Kuna miti na uoto wa asili na nyumba zilijengwa strategically kufuata landscape...Tuache lawamazisizo na msingi
 
Kwa kiasi kikubwa nchi hai lack mipango. Tuna mipango mingi tu.

Nchi ina lack utekelezaji wa mipango.

Miaka ya 1980s wakati tulishaanza kuhamisha makao makuu kwenda Dodoma, Wa Nigeria walikuja kupata idea kama yetu. Walitaka kuhamisha mji mkuu kutoka Lagos kwenda Abuja.

Wakaja kujifunza kwetu, wakachukua makabrasha kuyafanyia kazi.

Wakaenda kuhamisha mji mkuu wao kutoka Lagos kwenda Abuja. Wakamaliza.

Sisi tuliowapa mipango tukawa bado hatujamaliza zoezi kwa miaka mingi, mpaka leo mabalozi karibu wote bado wako Dar. Wanaona hatujawa serious kwenye hili.

Tumepanga mipango miingi, utekelezaji mdogo sana.

Kuna jamaa mmoja alikuwa mwanaharakati wa elimu, jamaa alikuwa well connected kitaa anakijua, halafu kasoma mpaka Harvard mambo ya kimataifa yuko vizuri. Basi alikuwa anafanya activism sana mambo ya elimu.

JK akamuona. Akasema wewe nakitaka uje juwa mshauri wangu mambo ya elimu. Jamaa akasema naam, hapa sasa nimepata sikio la rais, mambo yataenda vizuri, tutabadili mengi.

Basi jamaa kila akimshauri JK, JK anamwambia hilo? Hilo tunalijua tangu miaka 10 nyuma, mtafute Katibu Mkuu wizara ya elimu atakupa makabrasha yote. Jamaa akimshauri JK kitu kingine, anaambiwa, hilo? Hilo tulishafanya utafiti Mzumbe, mtafute Mkuu wa Chuo atakupa makabrasha yote.

Yani jamaa alifikiri yeye anajua mambo mengi, serikali haijui tu, na akipata nafasi ya kushauti serikali, watabadili mengi.

Akaja kugundua kuwa, mambo mengi aliyotaka kushauri, serikali ilikuwa inayajua, tena zaidi ya alivyoyajua yeye.

Tatizo halikuwa kujua, tatizo lilikuwa utekelezaji.

Jamaa alijiuliza, sasa hapa nafanya nini? Ikabidi aache ile kazi, kwa sababu hakuna alichokuwa anafanya.

Makabrasha kibao yanapata vumbi, studies kibao watu wanefanya na kushauri.

Tatizo ni kwenye utekelezaji huko.
Mimi nimefanya utafiti mwingi sana kwenye maswala mbalimbali nchini, lakini nakwambia shida kubwa ya nchi yetu hii ni siasa za chama kushika hatamu na kiendelee kubaki madarakani kwa gharama yoyote ile. Kila maamuzi mtaalamu atayoishauri serikali lazima yahakikishe kuwa hayaigombanishi CCM na wapiga kura. Huu ndio mtaji mkuu wa CCM kuendelea kubaki madarakani. Ndio maana leo hii huwezi kupanga wala kusafisha miji, huwezi kuwaondoa watu mabondeni au chini ya milima hatarishi.

Wazo la kuhamishia makao yetu makuu kwenda Dodoma lilikuwa na maana na manufaa kwenye miaka ya 1970s, lakini liliendelea kupoteza maana baada ya maendeleo ya sekta ya habari na mawasiliano. leo hii njia za kupashana habari na kupata taarifa hazihitaji kwenda Dodoma tena kutoka Dar au Mtwara, gharama za kuhamia dodoma kwenye miaka hii 2020s zingeweza kuepukika kama tungejikita zaidi kwenye kukuza njia za habari na mawasiliano ili kila mtanzania apate huduma zote za wizara husika kwenye ngazi ya makao makuu ya wilaya yake. Unanda Dodoma kufanya nini?
 
Kuna mlima unaitwa Mkindu au Mguluwandege. Mwaka jana mwezi wa nne kuliporomoka majabali usiku fulani. Majabali hayo hayakufika chini na wananchi pale wanafahamu. Mlima upo Morogoro eneo la Mkindu.

Watu wanaendelea kujenga kuufuata mlima huo. Na umekaa kimtego haswaa
Ukishaishi kwa kuamini kudra za Mwenyezi Mungu utajenga popote pale.

After all, unaweza kuacha kujenga milimani ukajenga sehemu tambarare, lakini kwa kudra tu ukapigwa radi vilevile.

Hii mentality ya kuishi kwa kudra ndiyo inatugharimu.
 
Hapo waendelee kujenga tu kwa sababu baada ya maporomoko hayo ardhi haitakuwa na uwezo wa kuhifadhi maji tena. Sehemu ya ardhi iliyobaki itachuruzisha maji na kubaki kiasi cha kawaida na hivyo haitatokea tena.
Hiyo theory yako ni theory kama ya embe, kwamba ukila sehemu ya juu ndani utaakutana na kokwa. hakuna kitu kama hiko, leo utakutana na land slide kesho utakutana na lava ya moto kama ya nyiragongo, kesho utafunikwa na jivu na kesho kutakumbana na moshi mbaya tu. Huwezi kutoa majibu mepesi ya kiasi hicho mkuu. Nyumba moja baada ya kujengwa ukatokea mpasuko kwenye ukuta na msingi, mwenye nyumba akasema msiogope wapangaji hapo ndio mwisho wa mpasuko kwakuwa ardhi ilikuwa inajiweka sawa tu, imeshamaliza. Lakini ile nyumba ikawa ya kwanza kuanguka siku lilipotokea tetemeko dogo tu lililozibakisha nyumba nyingine.
 
Sawa.

Endeleeni kuzaana bila mpango halafu muone kama kuzaana ndiyo utatuzi wa matatizo yenu.

Hawa watu ulionao unapata shida kuwalisha, kuwasomesha, etc.

Huna mipango mizuri ya kutumia nguvukazi. Watu hawa wachache hujui kuwatumia.

Halafu unasema, hapa tatizo langu ni watu wachache, ngoja niongeze watu wawe wengi.

Sasa kama hawa wachache hujui kuwatumia, hao wengi utawezaje kuwatumia?

Kwenye habari za mataifa ya magharibi na chumi zao, nimetoa mfano wa Japan. Japan si nchi ya magharibi.

Tujikite Africa kuondoa habari za magharibi.

Nchi zenye chumi tajiri kabisa kwa per capita income ni pamoja na Seychelles na Mauritius. Hizi nchi zina watu wachache lakini GDP per capita kubwa.

Ingekuwa wingi wa watu ndio unaoketa maendeleo, Nigeria ingezipita Mauritius na Seychelles kwa GDP per capita.

Tuangalie mifano kwa data.

Kwa hesabu za mwaka 2021:

Nigeria ina takriban watu milioni 215 na GDP per capita ya US $2066.

Seychelles ina watu 99,258 na GDP per capita ya US $14,653.

Kipato cha mtu mmoja wa Seychelles, kwa wastani, kwa hesabu za mwaka 2022, kilikuwa takriban mara saba ya kipato cha wastani cha mtu wa Nigeria kwa mwaka huo huo, licha ya Nigeria kuwa na watu mara 2166 zaidi ya Seychelles.

Sasa, mnaosisitiza kuwa wingi wa watu ndio uchumi bora, hamuoni kuwa Nigeria kuna watu wengi sana wanaogawana umasikini, wakati Seychelles kuna watu wachache wana uchumi mzuri tu, mara saba ya uchumi wa Nigeria kwa GDP per capita?
Kule kwetu tulizaliwa wengi, watoto 20 kwa wanawake 3 wa baba, lakini wote tulikwenda shule kwakuwa watoto wote tulikuwa na kazi za kufanya kule shambani, kwenye mifugo, kwenye mizinga ya baba na dukani. Tulikuwa tunalima sana, kuchunga sana, kukamua sana, kulisha kuku sana, kulinda tumbili sana, kurina asali sana na kulisha kuku sana kiasi kwamba hatukuwa na shida ya chakula wala ada ya shule na chuo. Bro, ni sera tu mbovu.
 
Ulisha wahi lini kuona Tz tuko vizuri kwenye disaster preparedness and mitigation? Never ever! Sina maana mbaya.
 
Ukishaishi kwa kuamini kudra za Mwenyezi Mungu utajenga popote pale.

After all, unaweza kuacha kujenga milimani ukajenga sehemu tambarare, lakini kwa kudra tu ukapigwa radi vilevile.

Hii mentality ya kuishi kwa kudra ndiyo inatugharimu.
Umecompare na kuContas😅
 
Hiyo theory yako ni theory kama ya embe, kwamba ukila sehemu ya juu ndani utaakutana na kokwa. hakuna kitu kama hiko, leo utakutana na land slide kesho utakutana na lava ya moto kama ya nyiragongo, kesho utafunikwa na jivu na kesho kutakumbana na moshi mbaya tu. Huwezi kutoa majibu mepesi ya kiasi hicho mkuu. Nyumba moja baada ya kujengwa ukatokea mpasuko kwenye ukuta na msingi, mwenye nyumba akasema msiogope wapangaji hapo ndio mwisho wa mpasuko kwakuwa ardhi ilikuwa inajiweka sawa tu, imeshamaliza. Lakini ile nyumba ikawa ya kwanza kuanguka siku lilipotokea tetemeko dogo tu lililozibakisha nyumba nyingine.
Hiyo argument yako siyo ya kisayansi! Kuna uhusiano gani wa kisayansi kati ya landslide ya Hanang na lava ya moto au jivu na moshi mbaya? Kuna vitu umesimuliwa lakini huvielewi unaishia kujichanganya! Mlima Hanang ni wa volcano na kwa sasa imesinzia (extinct) kwa hiyo haihusiki na landslide iliyotokea.

Kilichosababisha landslide hapo Hanang ni aina ya mwamba au udongo uliopo ambao una uwezo wa kuhifadhi maji, mwinuko wa mlima na mvua za muda mrefu na nguvu ya gravity ambayo ndiyo hasa imesukuma hiyo miamba ikabomoka.
 
Watu wanajisemesha tu bila kujali context. Kwa land scape ya Tanzania ni sehemu gani ambapo Kuna makazi hakuna milima, vijilima au milima mikubwa? Hizi natural disaster ni sehemu ya maisha yanapotokea tukubali kwamba it's because of nature. Katesh ni mji wa zamani sana na haijawahi tokea kitu kama hicho na watu wa Ile jamii wanajua kutunza mazingira Yao sana sana. Palipotokea tukio kulikuwa well conserved Kuna miti na uoto wa asili na nyumba zilijengwa strategically kufuata landscape...Tuache lawamazisizo na msingi
Jidanganye tu aisei, hali ya hewa ya sasa na zamani ni tofauti sana, mazingira yamechafuliwa sana, huwezi kuongea kauli jumuishi kama hizo za kutoa false hope. Leo hii watu wa katesh wakiona wingu zito sana limetanda na kusikia mngurumo upande ulioko mlima hanang wanakurupuka kutoka kwenye nyumba zao. Unadhani kuna mtu anatamani kujenga upya nyumba palepale ilipozolewa ile ya kwanza?
 
Pia kwa kasi yetu ya kuzaana, wakati nchi haiongezeki, huko mbele watu watazidi kubanana tu.

Hivyo tunahitaji kupangilia vizuri sana both land use na family planning.

Enzi za kuzaana zaana ovyo tu na kuishi kwa kujua nchi kubwa tu hii zinaisha.
Tz kuja kufikia kubanana hy bado sana, hata tukiwa 150M bado ardhi ipo kubwa sana tuu labla useme kubanana kwenye majiji na sio Tz nzima
 
Back
Top Bottom