Vifo Katesh; Je, Tanzania kuna milima mingine kama mlima Hanang?. Serikali imechukua hadhari gani?

Vifo Katesh; Je, Tanzania kuna milima mingine kama mlima Hanang?. Serikali imechukua hadhari gani?

Usishonw koti 1 nchi nzima. Kila mahali pana upekee wake. Jinsi mlima Hanang ulivyoanza ni tofauti na meru nk. Jielimishe.

Sehemu ya Mji wa katesh upo kwenye mkondo wa maji haswa wale watu kwa kwanza. Ulipopanuka umeelekea srhemu za miinuko na mabonde. Miji mingi ipo hivyo.
mipango miji wapo kila wilaya lakini watu wanajenga kwenye mikondo ya maji kwanini? kura? rushwa? elimu yao ndogo? dharau? au?
 
Mkuu,

Kama hujui jinsi ya kutumia nguvukazi yako ya sasa, kuongeza watu ambao wataongeza utegemezi bila kuwa productive ni kuongeza tatizo.

Tunaweza kujua 10 si square root ya 2, hata kabla hatujajua square root ya 2 ni nini.

Tunaweza kujua jibu fulani si jibu sahihi hata kabla hatujajua jibu sahihi ni lipi.

Tunaweza kujua kwamba, jibu la kutaka kumaliza umasikini kwa kuongeza watu, bila ya kuwa na mipango sahihi ya kutumia nguvukazi zao, si jibu sahihi, hata kabla hatujajua jibu sahihi ni lipi.
unapotaka kujenga kiwanda cha mikate lazima ujue wangapi wanakula mikate kwenye eneo lako kwanza na nguvu yao ya manunuzi (purchasing power). Mchawi wetu mkuu wa ndani kaka ni uchaguzi na kura na mchawi wetu mkuu wa nje ni ukolonimamboleo (neocolonialism).
 
unapotaka kujenga kiwanda cha mikate lazima ujue wangapi wanakula mikate kwenye eneo lako kwanza na nguvu yao ya manunuzi (purchasing power). Mchawi wetu mkuu wa ndani kaka ni uchaguzi na kura na mchawi wetu mkuu wa nje ni ukolonimamboleo (neocolonialism).
Hoja ya kwamba suluhisho la umasikini wetu ni kuzaana zaidi ni sawa na hoja ya kwamba wewe jenga kiwanda cha mikate tu, hakikisha mnazaana sana ili kuwe na wateja.

Bila kujua hao wanaozaliwa watamudu kununua mkate ama la.
 
Hoja ya kwamba suluhisho la umasikini wetu ni kuzaana zaidi ni sawa na hoja ya kwamba wewe jenga kiwanda cha mikate tu, hakikisha mnazaana sana ili kuwe na wateja.

Bila kujua hao wanaozaliwa watamudu kununua mkate ama la.
Kim Jong Un anawalilia wanawake wazee, china imeondoa sheria ya kuzaa mtoto mmoja. Wewe hata hujui uhusiano wa uchumi na population. marekani inatafuta wahamiaji waende wakanunue hotdogs zao.

View: https://www.youtube.com/watch?v=-nolzvHl-UU
 
Mwenye akili timamu ni yule anaejiuliza mwenyewe maswali kuhusu "ni kwanini tuko hivi na kwa nini tumebaki hivi tulivyo kiuchumi, kielimu, kiafya, kiuzazi,.......?". Ataendelea kujiuliza mwenyewe "Ni kwanini Afrika yote inafanana fanana kimaendeleo na mambo Yao mengine yote?" Ataendelea kujiuliza "ni kwanini hata nchi zilizobadilisha vyama vyao tawala kama vile Zambia, Malawi, Kenya, Liberia, DR Congo, Uganda, nk hata wao bado hali Yao kiuchumi Iko vilevile TU?"

Ukishapata majibu ya maswali hayo ndiyo uje na majibu ya mjadala kati ya uhusiano kati ya idadi ya watu na maendeleo.
Sitaki kukujibu "kishabiki (kwa Tanzania), wala Kishamba/kipumbavu", kwa sababu umeuliza maswali mengi yanayohitaji mjadala makini (ambao huwezi kuupata humu JF).

Kwa nini nchi za Kiafrika, zinafananafanana, hata zile zilizobadili serikali; kama hiyo mifano uliyoiweka hapo juu!

Sijui kama hii ndiyo sababu unayotaka sote tuitumie kwa hapa Tanzania ili tuendelee na CCM, kwa vile kubadili vyama hakuna manufaa? (Naweka hiyo alama, sijui kama hiyo ndiyo unayolenga kwa andiko lako hili).

Sitaeleza nionavyo mimi, kuhusu hayo maswali uliyo uliza hapo. Lakini sikubaliani na hiyo dhana unayoilenga kuhusu kubadisha tawala na maendeleo ya nchi Tatizo siyo kubadili serikali/tawala na vyama; tatizo ni vyama kama hiyo CCM ilivyo sasa na kuendelea kubadilika ikitoka kwenye misingi yake na kuporomoka katika malengo yake.
 
Milima kama ya Hanang ina nguvu za asili, acha volcano tu, wazee wa kimila wanaweza kuelezea vizuri kuliko wasomi
 
Upo sahihi sana, kuwa na population inategemea watu hao wanauwezo gani kujikwamua kiuchumi ili kusaidia uchumi wa nchi kuinuka! Kwa mfano hata population kubwa iliyopo serikali ingewekeza kwenye uzalishaji wa malighafi nyingi zinazoagizwa nje, zikazalishwa Tanzania zikawa processed hapa hapa kwa sababu ya population kuwa zikatumika hapa hapa, na zinazozidi tuka export nje ya nchi kwa wingi uchumi wa nchi ungekuwa sana.

Wataalamu waangalie namna ya kupata malighafi, viwanda vijengwe kwa ajili ya processing,, tutumie vitu vyetu tunavyozalisha wenyewe tu, na tu export kwa wingi kama uchumi wetu haujakuwa maradufu.
Cheki hii: Sasa hivi lengo letu kubwa ni kwenda kuwatafuta nje watu wenye mihela ya kutosha waje wawekeze hapa, tusubiri wavune ili nasi tupate vibarua. Tukishashiba tu, tayari maendeleo yamepatikana!

Siyo mabaya(?), kwa maana kama uwekezaji huo ungekuwa na malengo ya kutuwezesha nasi kujijenga zaidi ili tuwe na uwezo wa kuzifanya kazi zote hizo na sisi wenyewe kuwa na uwezo wa kiteknologia ili tuweze kuwa wawekezaji wenyewe.
Lakini unapokwenda kutafuta wawekezaji wa kuchimbua madini yako yote, hata yale ya msingi kabisa na kuyapeleka huko nje yakatengeneze vifaa vya msingi zaidi, huku ikiachiwa mashimo na matakataka, na pesa inayotokana na uwekezaji huo hata huwezi kuonyesha mradi hata mmoja wa maana uliofanyika juu yake; huo ni uwekezaji wa kiuchaa!

Swali ni hivi kwa nini tunajina wenyewe kuwa watu duni sana tusioweza kufanya chochote kuleta maendeleo yetu? Hili ndilo swali wanalotakiwa kuwa wanalijibu hawa viongozi wanaokimbilia nje kila mara, hata katika mambo madogo tunayoweza kuyamudu wenyewe.

Kwa mfano wa hivi karibuni: Hao watu wa "Carbon Blue" wanaosemwa kupewa maeneo ya misitu yetu yenye ukubwa wa asili mia nane (8%) ya nchi yetu...; wanawekeza kiasi gani cha pesa katika muda wao wote wa miaka 30? Nchi hii haina uwezo wa kufanya kazi hiyo, na huku kila mwaka tunazalisha vijana wasiokuwa na kazi za kufanya?

Ku'manage' misitu na kupanda miti na kulima mazao kufufisha hewa ukaa, hatuna uwezo wa kazi hiyo?

Sijasema popote hiyo iwe miradi ya serikali, lakini serikali inao wajibu mkubwa kuwapamga wananchi wake wafaidike na miradi ya aina hii. Private sector siyo ile inayotoka nje tu. Tunayo tele hapa sisi wenyewe.
 
Nimeona hii video watu wanadai ni kitonga
 

Attachments

  • VID-20231207-WA0004.mp4
    6.4 MB
Enzi za kuzaana zaana ovyo tu na kuishi kwa kujua nchi kubwa tu hii zinaisha
Hii dunia bwana! Wakati wengine wanalia wimbi la ongezeko kubwa, wengine kina 'Kim Jon Un" wanalia na kuwaomba wanawake wao waongeze bidii ya kuzaa! 😄
 
Hii dunia bwana! Wakati wengine wanalia wimbi la ongezeko kubwa, wengine kina 'Kim Jon Un" wanalia na kuwaomba wanawake wao waongeze bidii ya kuzaa! 😄
Watawala sehemu nyingi watataka kuongeza watu, watalilia watu wazae.

Kwa sababu wanataka kuongeza wafuasi, watumwa, wanataka kuongeza walipa kodi, wanataka kuongeza watu watakaolipia NSSF.

Lakini maswali ya msingi yako pale pale, kuongeza watu ni jambo sahihi kwa mipango ya kiuchumi ya nchi hiyo?

Hao watu waliopo North Korea tu wanakimbia, wanatoroka kwenda China na South Korea.

North Korea ni kama gereza moja kubwa sana, ni kama vile wananchi wote wapo gerezani, nchi nzima ni kama gereza. Sasa naona raia wamestuka wanaona katika maisha haya ya nchi nzima kuwa gereza, kuzaa watoto ni kuwaleta kwenye gereza tu, wanagoma.

Mpaka mkuu Kim Jong Un analia.
 
Mwenye akili timamu ni yule anaejiuliza mwenyewe maswali kuhusu "ni kwanini tuko hivi na kwa nini tumebaki hivi tulivyo kiuchumi, kielimu, kiafya, kiuzazi,.......?". Ataendelea kujiuliza mwenyewe "Ni kwanini Afrika yote inafanana fanana kimaendeleo na mambo Yao mengine yote?" Ataendelea kujiuliza "ni kwanini hata nchi zilizobadilisha vyama vyao tawala kama vile Zambia, Malawi, Kenya, Liberia, DR Congo, Uganda, nk hata wao bado hali Yao kiuchumi Iko vilevile TU?"

Ukishapata majibu ya maswali hayo ndiyo uje na majibu ya mjadala kati ya uhusiano kati ya idadi ya watu na maendeleo.
Mkuu 'kavulata', mchango wako huu unazidi kuninyima utulivu wa mawazo. Nimekwisha andika juu yake na kuondoka; lakini bado akili imebaki tu kwenye haya uliyo andika hapa.

Mimi najibu kifupi tu kwa haraka. Tatizo ni UONGOZI.
Uongozi usiokuwa na maono, uliochanganyika na kujinufaisha wenyewe badala ya kunufaisha nchi zao.

Pili, kamwe hatuwezi kutotaja mazingira yanayotuzunguka. Kama mazao yetu na vyanzo vyetu vya mapato hatuna uwezo wa kuhakikisha vinaendelea kuzalisha ili tupate mitaji ya kujiendeleza, tutaanzia wapi. Kama uchumi wa dunia umeporomoka, wa kwetu unaporomoka zaidi.

Hapa Tanzania tulikuwa mashuhuri enzi zile katika uzalishaji wa mkonge na pamba. Mjapan kagundua nyuzi za 'nilon', soko letu likadoda. Brazil alipokuwa kinara wa uzalishaji wa kahawa, kahawa yetu ikadoda; n.k., .

Taifa linategemea utalii kama chanzo mashuhuri cha pato. Anapoingia COVID - 19; hapo utalaumu vipi kuvurugika kwa shughuli za pato la nchi hizi?

Sasa kosa lipo wapi? Linarudi palepale kwenye uongozi mbovu usiokuwa na maono; maono ya kujipanga vizuri ili kuhimili majanga haya yanapo tokea. Elimu yetu inakuwa mbovu, haitoi mazao yanayolenga kupambana, badala yake tunazalisha mazao yanayo jitambulisha kuwa "CHAWA" wa kunyonya uchafu toka kwa hao viongozi wabovu.

Tatu, ni vizuri pia kuvuta subira. Tazama nchi zingine duniani zilipitia wapi. Portugal ya miaka ya 60; 80; pamoja na kuwa na makoloni mbalimbali nje, lakini ilikuwa ni nchi maskini tu! Hivyo hivyo na Hispania na kwingineko. Nchi jirani zilipoanza kuinuka, na wao zikawainua.

Nchi za Asia, kulikuwa na Japan pekee akitamba maeneo hayo wakati Korea Kusini na wengineo wakiwa katika hali duni kabisa hadi kwenye miaka ya 60 hivi. China walikuwa wakihangaika tu, Vietnam vilevile; Thailand, Indonesia na kwingineko. Mazingira ya leo ni tofauti kwa nchi hizo.
Kwa hiyo, hata sisi tunakwenda hivyo hivyo, hasa kwenye nchi zitakazo bahatika kuwa na viongozi wenye uchungu na hali za maisha ya wanachi wao na kuweka sera zinazohakikisha mafanikio yanapatikana haraka.

Isingekuwa CCM wanavyoturudisha nyuma zaidi, Tanzania ingekuwa ni miongoni mwa nchi za kwanza kabisa katika Afrika kuondokana na uduni wa maisha ya wananchi wake; kwa sababu kila nyenzo muhimu za kutuwezesha kufanya hivyo tunazo; tunacho kikosa ni uongozi imara wa kutupeleka huko haraka.

Wingi wa watu siyo hoja muhimu, ingawaje sioni sababu kwa Tanzania sasa hivi kubana ongezeko la watu.
 
Pia kwa kasi yetu ya kuzaana, wakati nchi haiongezeki, huko mbele watu watazidi kubanana tu.

Hivyo tunahitaji kupangilia vizuri sana both land use na family planning.

Enzi za kuzaana zaana ovyo tu na kuishi kwa kujua nchi kubwa tu hii zinaisha.

Nchi bado kubwa watu wazaane tuu
 
Nchi bado kubwa watu wazaane tuu
Hii hoja imedadavuliwa zaidi kwenye uzi huu, endelea kufuatilia majibizano kama una point za nyongeza za kimantiki zilete.

Tumedadavua dhana nzima ya "nchi kubwa" ilivyo pana kuzidi ukubwa wa eneo tu.
 
Hii hoja imedadavuliwa zaidi kwenye uzi huu, endelea kufuatilia majibizano kama una point za nyongeza za kimantiki zilete.

Tumedadavua dhana nzima ya "nchi kubwa" ilivyo pana kuzidi ukubwa wa eneo tu.

Kuna sehemu nyingi za wazi hii nchi kuna mahali nimenunua hekari 100 kwa laki moja moja nafanya kilimo na bado maeneo yapo ya wazi

Nchi bado inatudai tuendelee kuzaa
 
Kuna sehemu nyingi za wazi hii nchi kuna mahali nimenunua hekari 100 kwa laki moja moja nafanya kilimo na bado maeneo yapo ya wazi

Nchi bado inatudai tuendelee kuzaa
Una teknolojia gani kulima? Unalima nini?

Kwa nini unafikiri tunahitaji kuongeza watu beyond replacement rate wakati watu waliopo wengi ni masikini na hawana kazi?

Unaangaliaje ukubwa wa nchi bila kuangalia teknolojia?

Ukiwa na nchi kubwa ambayo watu bado wanakata miti ili kupata kuni na kuifanya nchi iwe jangwa kwa haraka sana, bado utataka kuongeza watu kwa kasi waongeze kasi ya nchi kuwa jangwa?

Ukiwa na nchi kubwa ambayo kila ongezeko la uzalishaji unalolipata linafunikwa na ongezeko la watu kwa kasi sana, kiasi kwamba, badala ya kuendelea mbele kiuchumi, unarudi nyuma, bado utasema nchi kubwa sana tuzaane tu?
 
Sitaki kukujibu "kishabiki (kwa Tanzania), wala Kishamba/kipumbavu", kwa sababu umeuliza maswali mengi yanayohitaji mjadala makini (ambao huwezi kuupata humu JF).

Kwa nini nchi za Kiafrika, zinafananafanana, hata zile zilizobadili serikali; kama hiyo mifano uliyoiweka hapo juu!

Sijui kama hii ndiyo sababu unayotaka sote tuitumie kwa hapa Tanzania ili tuendelee na CCM, kwa vile kubadili vyama hakuna manufaa? (Naweka hiyo alama, sijui kama hiyo ndiyo unayolenga kwa andiko lako hili).

Sitaeleza nionavyo mimi, kuhusu hayo maswali uliyo uliza hapo. Lakini sikubaliani na hiyo dhana unayoilenga kuhusu kubadisha tawala na maendeleo ya nchi Tatizo siyo kubadili serikali/tawala na vyama; tatizo ni vyama kama hiyo CCM ilivyo sasa na kuendelea kubadilika ikitoka kwenye misingi yake na kuporomoka katika malengo yake.
Watanzania na pengine waafrika tutakosea hwasa kama tutakuwa tunapambana na immediate causes of our economic problems na kuacha kupambana na underlying na basic causes za shida zetu. Basic causes ya shida zetu ni kukosekana kwa usawa katika upatikanaji wa technology, bei, mitaji na masoko ya bidhaa zetu. Kiongozi yeyote wa siasa anaetaka kufanya kitu Cha tofauti na kiongozi au Chama kingine lazima atoe majibu ya namna ya kuyatambuka matatizo ya upatikanaji wa technology, bei za haki kwa bidhaa zetu, masoko huru na mitaji. Vinginevyo ni uongo TU wajemeni kusema nichagueni mimi muone nchi ya asali na maziwa.
 
Watanzania na pengine waafrika tutakosea hwasa kama tutakuwa tunapambana na immediate causes of our economic problems na kuacha kupambana na underlying na basic causes za shida zetu.
Ni sentensi nzuri, lakini kiuhalisia, utaachaje kuhangaika na matatizo yaliyopo sasa kiuchumi?

Ni kama ugonjwa, mtu kapata ugonjwa, ni lazima ashughulikie tatizo hilo la ugonjwa sasa hivi, ili aweze kuendelea na maisha.

Haina maana kwamba kushughulikia matatizo ya sasa ya kiuchumi yanasababisha kufanya mipango ya muda mrefu na kujiandaa vizuri ili kuitekeleza hiyo mipango, ikiwa ni pamoja na hiyo teknolojia unayoizungumzia, ambayo mimi nairundika kwenye kuwepo ubora katika mfumo wa elimu yetu. Watu walio andaliwa vizuri, wana elimu nzuri na ujuzi hawawezi kukosa kujua umuhimu wa teknolojia.
Kiongozi yeyote wa siasa anaetaka kufanya kitu Cha tofauti na kiongozi au Chama kingine lazima atoe majibu ya namna ya kuyatambuka matatizo ya upatikanaji wa technology, bei za haki kwa bidhaa zetu, masoko huru na mitaj
Nitakubaliana na wewe katika hili kama maana yako ni kuhusu kiongozi mwenye dira na maono kuhusu nchi anayoiongoza. Asiwe kiongozi wa maneno matupu na huku akifanya kila kitu kuhujumu hayo anayodai kuyataka kwa nchi yake.
 
Back
Top Bottom