Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu una roho ya dhahabu Mungu akuzidishie Mimi binafsi nalibeba hili.Sasa mchizi wa JF nakupa idea nyingine, nunuwa ardhi uswahilini ambako bado Ardhi inauzwa kwa thamani ndogo jenga community swimming pool kubwa halafu ndani yake weka kapub kadogo na something like circus ya michezo ya Watoto, wekeza hii kitu kwenye community tofauti tofauti according to your research
Utapiga pesa mpaka basi, na hii ni permanent investment.
Bongo kuna tatizo la community kukosa maeneo yao ya kufurahia maisha zaidi ya watu kuwekeza bar tu kila corner.
Uzuri wa Bongo almost ni summer time mwaka mzima kwahiyo swimming pool ni biashara inayolipa sana.
Mleta mada sifa yako kuu niliyoigundua kwenye mabandiko yako ni kwamba huna hasira za haraka wala jaziba.Ok, nimetoka katika family popuar ambayo ilikuwa na weza kusema watu wa watu, hivyo wazee wangu walikua na marafiki wengi , tukajenga mahusiano na kama undugu na familia nyingi sana, hivyo hizo familia zote ni kama ndugu zangu sababu ni majirani na tumishi pamoja.
Kwanini nina uliza sababu kama unavyo ona hapa nimeuliza teari umeshaanza ni hisi lada mimi ndio the killer, hivyo hivyo , hatuja zoea ulizana masuala haya face to face ,hivyo nisinge weza uliza members wa hizo familia , ila hapa kwangu ni rahisi kuuliza na kujua sababu bado ninajiuliza kama justice was served.
Wa kisure ila pande zingine za nchi... 🤣 🤣 🤣 🤣Si ni kama wewe tu au[emoji23] wa kisure
Fanya hii kitu utakuja kunikumbuka, na kwa mtu mwenye mzunguko mzuri wa pesa Kujenga swimming pool kubwa si gharama kubwa sana, pub ya kijanja unapata designer mzuri anakufanyiwa design ya kijanja anakutolea 3D image.Mkuu una roho ya dhahabu Mungu akuzidishie Mimi binafsi nalibeba hili.
Ahahah, Dah! Hao huyo Judy namjua yupo hadi leo siku hizi yupo Mwenge hata juzi nilionana nae hapo MwengeYes Buzweiriri mama ya mkewe alikua halfcast wa kizungu, Bella yuko Sweden and Milly yuko UK, anita or Norah mmoja aliolewana somebody kw aukoo wa Rupia, ilkua bonge la harrusi ,ilifanyika Kilimanjaro Hotel Poolside, maharusi wakaaka katika swimming pppi kuliwekwa a flating stage hapo , harusii ilikua na vigogo wote , mwingine aliolewa na jama wa gambia aor Guniea kitu kama hicho .
Aisee , kuna rfiki yangu hapo kwa TEMU alikuwa naitwa Mapinduzi , sijui yuko wapi , mara nasikia sijui alifariki longtime , sijui kama ni kweli, dada yao alikua Mkubwa wa miaka mingi ila ndio nilikua nampenda ,nyumbani waka wa wananitania mchumba wangu, mimi nikiwa Nussery school hapo nilikua na mpenda sana huyo alikua anaitwa Juddy , mpaka leo na muwazaga now anweza kuwahata ana miaka 60 huko .
Kabla ya Temu kwnye hiyo nyumba kulikua na boss mwingine wa Police alikuwa anaitwa Nguruwe sijui nao wako wapi hao jamaa.
Ebwana itabidi unipe contact zake, nmetafute , sio kimapenzi ila tuu ni mjulie hali kama mwana Obay mwenzangu lol. nimefurahi sana kusikia yuko salama . ukionana naye msalimie sana mwambia kuna katoto kalikua kanakupenda sana zamani hahahahahaAhahah, Dah! Hao huyo Judy namjua yupo hadi leo siku hizi yupo Mwenge hata juzi nilionana nae hapo Mwenge
Nadhani unazungumzia familia ya Galinoma sio?
Mungu akuzidishie Sana.Fanya hii kitu utakuja kunikumbuka, na kwa mtu mwenye mzunguko mzuri wa pesa Kujenga swimming pool kubwa si gharama kubwa sana, pub ya kijanja unapata designer mzuri anakufanyiwa design ya kiwanja anakutolea 3D image.
Kuna kitu Wabongo hatujakipa kipaumbele ni michezo ya Watoto, ndio sababu siku za sikukuu watu wanajazana beach hawana pa kwenda, sasa hizi huduma ukiwasogezea kwenye Kata zao utapiga pesa mpaka utashangaa, na kiingilio unaweka bei ya kawaida tu lakini wanaingia watu wengi.
Kuna kipindi Joto la Dar likipamba moto watu watakuwa wanashinda kwenye kiota chako.
Kuna pesa nyingine hapo unapiga kukodisha swimming dress za kike na za kiume buku mbili mbili tu, hapo napo pana pesa ya ajabu.
Asante sana , nimekuja gudua maishani kwenye real life watu hunienda sana kwa hilo ,nashukuru Mungu sana kwa ninipa hali hiyo .Mleta mada sifa yako kuu niliyoigundua kwenye mabandiko yako ni kwamba huna hasira za haraka wala jaziba.
Bravo!
Magu alikua kama wengine tuu yani kulikua na Mawaziri wengi tuu Obay so haikua ajabu kumuona wala kuwa kama a family friends , baada ya kua raisi ndio akawa big deal .lolKumbe mpaka familia ya JPM ilikuwa na family friends?
Shikamoo kaka[emoji28][emoji28][emoji28]Viwanja vyangu vyote hivyo.
I was out and about.
Maandazi Road ndiyo mama akikuita ukisikia tu "mtoto wangu mzuri..." unajua hii safari ya maandazi road inafuata hapa.
Unalitafuta Toyota Stout la TZA enzi hizo ulichanganye mafuta.
Haile Selassie ndiyo kuanzia St. Peters mpaka IST na Coco Beach, parties za mabalozi na kwa Warioba kama zote.
Mpaka nyingine siwezi kusema hapa.RIP Baba T for lifting me up in the compound.
Kilima nyege hapo nashuka kwenda kwa Bibi Masaki meeting up with my Geneva cousins to catch up, I make a left tMsasani Road nafikiri hapo, to the Bakilanas, na ubalozi wa Ireland huko, nyumba ya Mzee Bakilana ndiyo ipo mwisho wa Mzinga Way, tunatoka parties za alipokaa Mtei tunahamia kwa paries za Bakilana, tunakwenda kupita kwenye kilimanyege chenyewe. Tunaamua, tuende parties za Mzee Malocho, IST, Coco beach, za kwa Marcel Komanya au za balozi Mahiga? parties za posta au za bandari?
Au tunarudi Msasani Road kwa Ronald Mutie Mengi na kulianzisha Oysterbay Hotel huko na ufirauni wa Abbas Mwinyi?
Leo nimeamua tu kuepuka kikombe hiki, nikitaja mengi sana kuna wasiojulikana watanijua mpaka jina.
Hao jamaa walikaa US zamani na walipo rudi wakaa kaa Upanga , hivyo hatukuwa nao pamoja , na kipindi hicho ukiwa waziri sio big deal kivilee so , wao sijui walikua wana hang out wapi, ila nadhani walikua ni wa toto wa Upaga, ,iaka unavyo jua watoto wa Upanga na wa Obay ulikua kama hauchnganyuki ni wachache sana tulikuwa tuna changanyika nao labda kina Baraka Shelukindo (Na party zake) kina Mao Lwangisa , haya kina Joseph KUsanga hatuku hang nao ,Sisi tuli wamind mademu zao na sisters zao , hahahahaha alikua wana hasira na sisi kinoma . lolSijaona mnawazungumzia watoto wa Benjamin Mkapa au hawakuwa sehemu ya wana osterbay miaka hiyo?.
Halafu huyo Mapinduzi alishafariki mkuu, tena kitambo kidogo, alifariki 2007 kama sio 2008Ebwana itabidi unipe contact zake, nmetafute , sio kimapenzi ila tuu ni mjulie hali kama mwana Obay mwenzangu lol. nimefurahi sana kusikia yuko salama . ukionana naye msalimie sana mwambia kuna katoto kalikua kanakupenda sana zamani hahahahaha
Yeah, Lulu was a crush of mine, the very early years, tell me more.
Hapana, Idi hakuja kunichukua, dereva wetu alikuja kunichukua, mwalimu Ndosi alikuwa katuchelewesha kutuachia darasani, Idi na kiherehere chake akamfuata dereva wetu kujua anamsubiri nani, akaja darasani kwetu na kumuambia mwalimu Ndosi kuna watoto wanasubiriwa na madereva hapo nje. I thought that was so personable, from then, nobody could talk bad about Idi in my books.
Nkuruvi kuna dada anaitwa Mwanaidi I went there with.
Watu wanataka kujua stories za Magilani na food evenings za watoto wa kishua.
Kuna dada alikuwa anaitwa Halima, Mzanzibari, alikuwa anakaa Uganda Avenue Oysterbay, opposite na kwa Balozi Fulgence M. Kazaura aliyekuwa Chancellor wa UDSM, alisoma SR. Alikuwa anakaa next to balozi wa Zimbabwe.
Alitesa sana vijana siku hizo. Kina Santa na Mwita walikuwa shingo feni kila akitembea kama model mtaani.
Yes , ni huyo alikua Magereza, Mama Mwanguku alikua pia mwalimu wetu , nilikutana naye siku fulani miaka ya nyuma alikua hajazeka ana fanana vile vile , ila bahati mbaya nasikai alifariki kama miaka miwili iliyo pita .Hii ilikuwa kwa Mwanguku (mkuu wa magereza) right?
Wale kwao hapa karibu na Morogoro Stores, gardens zao zilikuwa tended na wafungwa siku zote tu.
Halafu nimewakuta gardeners wa kutoka jela kwa former Prime Minister Warioba tena, nikajua kumbe wale gardeners waliosemwa kwenye package ya viongozi wa taifa ni wa kutoka magereza.
Lakini wale wafungwa waliokuwa wanaangalia bustani kwa Warioba walikuwa wanapata good time sana.
Dah aisiee nime umia sana , siku wa nataka kuamini alifariki sababu niliwahi sikia na nikadhani ni sio habari sahihi so nilikua nina hope bado yuko hai, alikua rafiki yangu mkubwa sana primary school , tukaja potezana , sikuwahi msikia tena mpaka nilipo mtafuta ndio nikapata habari kafariki ila habari zilikua hazina uhakika dah ,asante kwa taarifa , R.I.P. my dear friend Mapinduzi.Halafu huyo Mapinduzi alishafariki mkuu, tena kitambo kidogo, alifariki 2007 kama sio 2008
Nadhani ni huyo unayemzungumzia, kama ni yeye basi ndio hivyo mwamba alisha rest in peace
Alimuoa Shangazi yangu, alikuwa na roho nzuri sana, kipindi hicho mimi mdogo nilikuwa nakaa na Shangazi yangu nilikuwa najiuliza mwamba kwani anafanya kazi gani? Maana alikuwa anabadilisha mandinga sio mchezo, Leo akirudi na Gari na kesho atarudi na lingine
✍️🤝🙏👏👊💪👊👍Fanya hii kitu utakuja kunikumbuka, na kwa mtu mwenye mzunguko mzuri wa pesa Kujenga swimming pool kubwa si gharama kubwa sana, pub ya kijanja unapata designer mzuri anakufanyiwa design ya kiwanja anakutolea 3D image.
Kuna kitu Wabongo hatujakipa kipaumbele ni michezo ya Watoto, ndio sababu siku za sikukuu watu wanajazana beach hawana pa kwenda, sasa hizi huduma ukiwasogezea kwenye Kata zao utapiga pesa mpaka utashangaa, na kiingilio unaweka bei ya kawaida tu lakini wanaingia watu wengi.
Kuna kipindi Joto la Dar likipamba moto watu watakuwa wanashinda kwenye kiota chako.
Kuna pesa nyingine hapo unapiga kukodisha swimming dress za kike na za kiume buku mbili mbili tu, hapo napo pana pesa ya ajabu.
Aisee umenikumbusha sana , kipindi hicho nilikua hata sijui wazee wana fanya kazi gani hapa ndio nina shangaa kumbe waze walikua na nafasi hizo , hata Mzee wangu ilikua late sana kuja kujua ana fanya kazi gani , sijui kwanini nilikua sina time ya kujua hilo.Hatari.
Let me remember all the girls. The streets, the homies, the stories. From my times.
Kuna dada mmoja alikuwa anakaa karibu na lighthouse kule Toure Drive, kwa Jaji Nyalali, alisumbua sana.
Tulikuwa tunakwenda karibu na club ya Wamarekani walikuwa wanakwenda sana kuangalia movies.
Kuna siku nyumba yao ilipigwa na radi, I wonder if it was because of the lighthouse.
I think it was Lulu.
Nilikuwa naenda na mshua nilikuwa mdogo sana. Mshua alikuwa anakaa na Judge Bomani, Judge Nyalali na washua wengine wanakata issues ambazo mimi hata sizielewi wakati huo.
Halafu kulikuwa na Mary Mosha hapa karibu na ubalozi wa Marekani wa Laibon. Alikuwa anasoma Forodhani. Baba yake alikuwa DG wa TANESCO, Mzee Mosha akaamua kuhama pale kwa sababu alisema ubalozi wa Marekani ulikuwa unawaangalia mpaka ndani.
Halafu kulikuwa na the Abebe sisters, Salaita na yule mwingine mdogo wake nafikiri yupo Las Vegas siku hizi. Anaitwa Maisara.
Halafu down the road Laibon kulikuwa na Arthur Lema na mdogo wake Brenda, baba yao likuwa DG breweries. Brenda was hot, but she was like a little sister to me.
Baba yao alivyotoka Breweries alienda kufanya kazi Nairobi for six month akarudi na a flashy red car. Akaenda kuwa DG wa Tanganyika Packers.
Arthur alipelekwa shule Ireland akanywa school fees zote, baba yake akampeleka Los Angeles California. Akasoma akarudi Tanzania kuendeleza mashamba yao.
Ule mtaa wa Laibon kulikuwa kuna nyumba ya Mwinyi, basi siku nyingine tukitoka shule tunakaa kuna kijiwe kona ya Kaunda, tunauona msafara wa Mwinyi anarudi nyumbani, anatupungia mkono.Mwinyi was cool to the kids on the corner.
Siku nyingine Mzee Mwinyi anaalika jirani kwenda kucheza naye bao, kuna mzee mmoja alikuwa anakaa nyuma ya nyumba yake alikuwa CEO wa NBC, karibu na kwa Speaker Adam Sapi Mkwawa, mtoto wake alikuwa rafiki yangu, walikuwa wanaitwa sana kwa Mwinyi kula kashata na kunywa kahawa.
Kuna siku Salama Mwinyi alikuwa ananiringishia sarafu mpya ina picha ya baba yake, nikapiga kofi, a message kwamba I don't care that your father is the president. Akataka kwenda kunisemea, lakini rafiki yake akamwambia huyo Kiranga ni kichaa, ukimsemea ndiyo utazidisha ugomvi. That is how I got away with slapping the president's daughter in the face. I am not proud of that, especially since my philosophy of not hitting women now.
Siku moja nikaamua kuwachemsha tu ubalozi wa Marekani. Nilitaka tu kuingia ubalozi wa Marekani na kuwauliza maswali.
Nikaingia. Kufika getini, yule Marine akaniomba ID, nilikuwa na wallet ina picha ya paka. Akaiangalia, akasema huyu ni paka wako? Nikasema ndiyo. Akafurahi sana. Apparently he was a cat person. Huyo paka hata hakuwa paka wangu, it was a stock photo.
Nilikuwa na documebts za watu wa kampuni za Marekani wanataka watu kutoka nchi za nje waende kufanya kazi Marekani. Nikawa nawaluliza wale watu wa Ubalozi, hawa Wamarekani tutawajuaje kama ni watu genuine au matapeli? Yule Consular wa Ublozi wa Marekani hakuwa na jibu. Kwanza aliniangalia kama haamini nauliza swali lile, inaonekana alikuw ahajapata kuulizwa swali lile na hakuelewa kama nimetumwa na serikali au vipi. Akaniambia atanipa mtu wa kunisaidia. Yule mtu alinizungusha ule ubalozi wa Marekani Laibon mpaka nikajua huyu ananizungusha makusudi nisijue ramani ya jengo. Mwisho wakanifikisha kwa mtu aliyeniambia kwamba Ubalozi wa Marekani Tanzania ni mdogo sana na hauna labor attache, kwa maswali yangu walihitaji nipate majibu kutoka kwa labor attache wa ubalozi wa Marekani Nairobi Kenya, nikapata mambo mengine nikaacha kufuatilia.
Mtaa huo pia walikuwa wanakaa kina Said, Idi, na wakina Janguo wengine.
Idi alikuwa na shobo sana, lakini siku moja alinionesha a very human side of him. Deereva wetu alikuja kunichukua shule, Muhimbili Primary (nilianza Muhimbili kwa sababu ya kukaa Upanga) halafu darasani mwalimu alikuwa katuchelewesha kutoka, yule derava hakujua la kufanya, Idi akajipa jukumu la kuja darasani na kumwambia mwalimu kwamba kuna dereva ananisubiri ameshangaa hatujaachiwa kuondoka darasani, mwalimu akaturuhusu kutoka, kutoka siku hiyo Idi Janguo akawa rafiki yangu.
Mtaa huo wa Laibon nakumbuka kina Chambi Chachage, kina Humphrey Mbise, Salama Mwinyi alikuwa anakuja kwenye nyumba yao ya Laibon siku moja moja, lakini mara nyingi akikaa Ikulu.
Siku moja natoka shule nikakutana na Salim Ahmed Salim akitembea kufanya mazoezi, alikuwa na bodyguars wake wachache tu, akatupa hi kawaida tu..
Kuna binti mmoja wa Adel, I forgot her first name, alikuwa anasoma Jangwani, baba yake alikuwa Permanent Secretary kwenye one of the key ministries, nilikuwa naongea naye sana kwenye simu halafu hanijui mimi ni nani.
Kuna siku tumeenda Ubalozi wa Indonesia kwenye party, kule Coco Beach, nikatokea naongea na mtoto wa balozi anataka sana kujua Kiswahili, alikuwa anasema anataka sana kujifunza Kiswahili, kinafanana sana na lugha yao, kilichofuata hapo sitaki kuhadithia.
Those were the days.
Ndugu zake ambao nawafahamu ambao wapo hai hadi Leo, ni huyo sister yao Juddy, Rose, Vicky na kaka zao wengine sijajui vizuriDah aisiee nime umia sana , siku wa nataka kuamini alifariki sababu niliwahi sikia na nikadhani ni sio habari sahihi so nilikua nina hope bado yuko hai, alikua rafiki yangu mkubwa sana primary school , tukaja potezana , sikuwahi msikia tena mpaka nilipo mtafuta ndio nikapata habari kafariki ila habari zilikua hazina uhakika dah ,asante kwa taarifa , R.I.P. my dear friend Mapinduzi.
Dah masikitiko makubwa aisee ,ghafla namna hiyo , dah , Mungu Maeke Mahali pema peponi Amen.Ndugu zake ambao nawafahamu ambao wapo hai hadi Leo, ni huyo sister yao Juddy, Rose, Vicky na kaka zao wengine sijajui vizuri
Mama yao ndio anakaa hapo Mwenge hata juzi Jumamosi nilipita kuwasalimia
Halafu Mapinduzi alifariki kama utani, alitoka tu kwenye sherehe jioni akarudi nyumbani bahati mbaya mke wake ambaye ni Shangazi yangu alikuwa hayupo, so nyumbani alikuwa Dada wa kazi tu
Sasa alivyorudi home baada ya muda kidogo akaanza kukohoa Damu, hali ilivyozidi kuwa mbaya Dada wa kazi akachukua simu na kuwapigia ndugu zake, kaka zake wakafika na kumuwahisha hospitalini, Kwa bahati mbaya mgonjwa akakata moto njiani[emoji22]
Kifo chake nae kilikuwa Cha kutatanisha sijui hata alikula nini, maana ilikuwa ghafla Yani katoka kuongea na mkewe muda sio mrefu Dakika tano nyingi tunaambiwa mtu kafariki