Vifurushi vya intaneti 'visivyo rasmi' kwa kampuni za simu

Nitafanya hivi pia, wadau wengi walishauri hawa ni wakwenda nao mperampera mpaka kinaeleweka
Lengo la kuandika haya malalamiko ilikuwa ni kujua kuwa ni mfumo wa kampuni ndio wenye kusua sua katika utekelezaji wa huduma zao au ni watu wa chini ndio wanaokwamisha mchakato na uongozi haujui.

So nikajilipua ili kama walikuwa hawajui namna mambo yalivyo basi wajue na kama walikuwa wanajua basi lawama ziende kwa kampuni kwa kuwa na utaratibu mbovu.




Baada ya kuandika hivyo nikapokea email yao ambayo ni hii hapa chini


Baada ya kuwatumia namba ya simu wakanijibu


Nikatumiwa email kutoka kwenye branch yao ya kusini iliyopokea maagizo kutoka HQ


Baada ya lisaa limoja kupita nikapigiwa simu na surveyor kuwa yupo njiani anakuja maeneo nilipo.

Nikamuuliza maswali surveyor kuwa baada ya wewe kutoka hapa huduma nitarajie kuipata kwa muda gani? akaniambia mpaka wamalizane na waliowahi kabla yangu.

Hapo ndio nikashangaa, nikamuambia mimi nimeanza miaka miwili kufuatilia swala la fiber hao unaowasema wamenitangulia hata miezi 6 hawajafikisha.

Sasa kwanini mimi niliyekuwa wamwanzo niwekwe pending na watu ambao wamekuja baada yangu?

Mara surveyor alete vikwazo ambavyo havina msingi eti eneo langu lipo mbali na ilipoishia fiber hivyo kutakuwa na process ndefu kidogo kwasababu italazimika ziwekwe nguzo.

Nikamuambia mbona hilo sala unalolisema wewe lilikuwepo miaka ya nyuma na ndio sababu ya mimi kushindwa kuchukua fiber nika request Copper?

Kwasababu mwaka juzi TTCL imeingia mkataba na TANESCO kuhusu kushea nguzo ili kufanikisha usambazaji wa internet kote nchini bure inayofika kila sehemu na ndio maana mkaita faiba mlangoni kwako?

Akaniambia ndio huwa wanatumia nguzo za TANESCO ila hutegemeana na situation. Mimi sikuridhika na majibu yake ikabidi niandike email tena


Baada ya hii email nikapokea simu kutoka kwa yule surveyor akinilaumu kwanini nimetuma email tena kulalamika vitu ambavyo tumeongea, sijui aliambiwa nini.

Nikamjibu nikamuambia isingekuwa busara kutorudisha mjesho kwa watu ambao wamekuwa msaada kwenye swala hili.

Lakini hata hivyo nilikuambia kuwa nimeambiwa niwape mrejesho so ulikuwa una taarifa kamili za hiki nilichoenda kuandika, otherwise kama kulikuwa kuna vitu hukutaka wavijue ungeniambia kuwa hiki na hiki usiseme. Na mimi ningekuuliza kwanini

Kwasababu swala la nguzo ni swala ambalo lipo nje ya uwezo wakoso malalamiko yangu kuhusu hilo jambo hayakuwa na effects yeyote kwako kwasababu wewe i mtumishi unayepokea maagizo, kama maagizo yao uliambiwa nguzo za TANESCO zipo limited basi haiwezi kuwa shida mimi kusema kuhusu hilo swala.
 
Nimekupata vyema sana mkuu, kwa hatua hii wasipokuja kufunga itakua uhuni mkubwa sana, tuendelee kuwashambulia hawa jamaa, kongole nyingi sana
 
Nimekupata vyema sana mkuu, kwa hatua hii wasipokuja kufunga itakua uhuni mkubwa sana, tuendelee kuwashambulia hawa jamaa, kongole nyingi sana
Hivi juzi Ijumaa nilimcheki surveyor ambaye alisema niwe namuuliza yeye kujua wapi mchakato umefikia.

Akaniambia Jumatatu kuna mtu atakuwa anachora mchoro.

Sasa mimi hiyo Jumatatu ntamcheki nikiona ananipa majibu ya series, nitafunga safari mpaka ofisini kwao jumatano.

Nikifika huko nitaongea kila kitu ili kama dalili za ubabaishaji kutoka kwa mawakala wao wanaowatuma wajue.

Nikiona na hapo hakuna kitu wamefanya, narudi kwenye email yao kuwaandikia kila kitu.

Kwasababu hata kwenye page yao ya twitter watu wamekuwa wakilalamika ishu hii hii ya ubabaishaji.
 
WAtakamilisha na hakika mkuu huduma itafika tu kwa hapo ulipofika pazuri sana
 
Kazi wanayo[emoji2][emoji2]
 
Mrejesho TTCL

Baada ya yule surveyor siku ya Ijumaa kuniambia ikifika Jumatatu ataniambia kuhusu mchakato ulipofikia.

Jana nilisubiri mpaka saa 10 jioni sikuona simu yake wala meseji. Nikaamua kumcheki mwenyewe hapo ilikuwa ni majira ya saa 16:49.

Alipopokea simu kwanza hakujua anaongea na nani mpaka pale nilipomkumbusha.

Akaniambia kwanini sikupiga simu tangu asubuhi kumkumbusha....nikamwambia "kwasababu uliniambia utanipa mrejesho sikuwa na wazo kuwa asubuhi umesahau ila nilipoona mpaka inafika jioni imekuwa kimya ndio nikajua utakuwa umesahau"

Akaniambia muda huu niko nje ngoja niingie ndani kuuliza halafu nitakupa majibu. Hapo hapo nikamuambia basi ukiuliza unijulishe usisahau akasema poa.

Nikaona muda unazidi kwenda bila kuona simu wala meseji, na huu muda kikawaida ofisi zinakuwa zimefungwa so nikajua tu amejisahau ikabidi nimpigie tena.

Nampigia simu ikaita bila kupokelewa nikaaamua nimsikikizie huwenda yuko mbali na simu au yupo busy.

Nilipoona mpaka inafika saa 19:30 bado kimya nikamuandikia meseji
 
Kazi ipo
 
Baada ya dakika 20 naye akajibu meseji

Nikamjibu



Nikamfahamisha kuwa kesho ambayo ndio leo nitafika ofisini kwao ili nipate uhakika zaidi

Leo sasa kabla sijaondoka kwenda ofisini kwao nikapiga simu tena kwa surveyor ikaita lakini haikupokelewa.

Nimefika ofisini kwao nikamkuta mwenzake ambaye alikuja naye siku ya survey.

Nikamuuliza vipi mchakato umefikia wapi. Huyu akaniambia eneo langu connection ya B.O.Q imejaa hivyo wataalamu wapo katika mchakato wa kufunga zingine, zikikamilika watanijuza.

Nikamuuliza kuhusu uhakika wa siku ambayo hiyo process ya kufunga hiyo connection itakamilika.

Akaniambia yeye hawezi kujua kwasababu hilo jambo lipo nje ya uwezo wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…