Vifurushi vya intaneti 'visivyo rasmi' kwa kampuni za simu

Vifurushi vya intaneti 'visivyo rasmi' kwa kampuni za simu

Screenshot_20240216-132024_Pixel Launcher.png

Tanga tuna vitu vyetu Unique, Fiber ya Bahoza 45,000 kwa mwezi 5mbps speed.

Hapo imeping kenya 21ms tu. Ukiping dar hadi 13ms
Screenshot_20240216-132615_Pixel Launcher.png
 
Samsung wana os yao nyengine inaitwa Tizen na LG wana os yao nyengine inaitwa Web os, os zote mbili hazikubali app za android.

Kwa Samsung kuna stremio store incase unataka app ya movies na iptv zipo app zake pia sema inabidi link ujitafutie mwenyewe kama za Kununua ama za bure.

Kwa LG watu hutumia lampa kama alternative ya Stremio, hii pia hutumika kwenye proprietary os nyengine kama Vidaa ya Hisense, inabidi uwe na jackett na Torrserve kuangalia movies na series, kwa iptv ni kama juu inabidi uwe na link zako.
Mkuu kwa uzoefu wako ipi ni kampuni bora linapokuja swala la android smart tv, samsung, hisensi, tcl nk..? na kuna tofauti gani kati ya andriod tv za kawaida na zenye google tv
 
Mkuu kwa uzoefu wako ipi ni kampuni bora linapokuja swala la android smart tv, samsung, hisensi, tcl nk..? na kuna tofauti gani kati ya andriod tv za kawaida na zenye google tv
Google tv ndio android TV ni muonekano tu, na Hisense, Samsung na LG sio android TV wana os zao wenyewe, Hisense ni vidaa, Samsung ni Tizen na LG ni webos.

TCL, Sony, Haier, Philips etc wanatumia Android TV.

Tv ikiwa haina Android tv ndio watu wanaweka hizo tv box.
 
Google tv ndio android TV ni muonekano tu, na Hisense, Samsung na LG sio android TV wana os zao wenyewe, Hisense ni vidaa, Samsung ni Tizen na LG ni webos.

TCL, Sony, Haier, Philips etc wanatumia Android TV.

Tv ikiwa haina Android tv ndio watu wanaweka hizo tv box.
Kuna jamaa yangu mmoja kakutana na jamaa anasajili line maalumu za halotel but huwezi kupiga wala kupokea simu. Hiyo ni ya internet tu.


Week gb 4 kwa 5000

Mwezi gb 18 kwa 15,000

Mwezi gb 38 kwa 30,000
 
Tayari wamekuja na saizi ndo wanasepa.

Niliomba namba ya fundi lakini walichoniambia ni kwamba kuna mfumo ambao ni randomly katika kumteua fundi wakuja kufanya installation

Ipo idara inayojitegemea kwa ajili ya kuteua mafundi hivyo wamedai hata wakinipa namba hawana uhakika kama huyo fundi ndio atayekuja siku ya kufanya installation

Kaniambia kuwa survey wamefanya na wanaeda kuiwasilisha ikafanyiwe tathmini za mahitaji ya vifaa

Akanitajia na jina la ajabu sijui O.B.P.U kuwa ni miongoni mwa vitu vinavyohitajika kwa ajili ya kufunga fiber.

Ila kuna kitu amenichanganya aliponiuliza mimi nimuambie wapi zimeishia nyaya zao za fiber.

Yani yeye muhusika wa kampuni hajui wapi nyaya zimeishia anataka kufahamu kupitia mimi? Nimeshangaa

Ikabidi na mimi nimpe majibu kuwa imeishia mita 200 kutoka hapo japo sina hakika na hayo majibu.

Akaniambia ooh hili eneo lako lipo mbali na waya za fiber kwa hiyo kutakuwa na ugumu kidogo.

Ugumu unatoka wapi wakati serikali ilitangaza kuwa imeingia makubaliano na TANESCO kuwa wapitishe nyaya zao kwenye nguzo zao?

Sasa hapo ugumu unakujaje?

Akasema tutaangalia.

Nikamuuliza kuhusu uhakika wa siku ambayo huyo fundi atakuja kwa ajili ya kufanya installation.

Akasema itategemea na foleni jinsi livyo, kwasababu kuna watu tangu wiki iliyopita tuliwafanyia survey kwa hiyo vifaa vikiwasili lazima waanze wao kupatiwa huduma.

Nikamuambia kama ndio hivyo basi mimi ndio nayetakiwa kuanza kuhudumiwa kwasababu nimeanza kujaza fomu tangu mwaka juzi, so hao watu kivyovyote vile watakuwa wamenikuta.

Akasema poa.

Nikamuambia kesho majira ya saa 8 mchana nitakuoigia simu kukuulizia mrejesho. Akasema sawa.
Kaka vp process inaendaje? Mm leo waneniambia nguzo sita zinaitajika
 
Kaka vp process inaendaje? Mm leo waneniambia nguzo sita zinaitajika
Nilibwagana nao kitambo

Wahuni wale wana uongo uongo mwingi sio wa kuwaamini.

Nguzo sita za nini kwani hapo hakuna nguzo za TANESCO?

Hapo ndio wanakukataa kimtindo kwasababu TTCL iliingia ubia na TANESCO ku share nguzo kwa ajili ya kupitisha fiber cable.

Sasa nguzo sita zinakujaje?

Miyeyusho sana hao majamaa
 
Back
Top Bottom