Vijana asubuhi na mapema wako vijiweni kujadili mambo ya mpira, tutafika kweli?

Take it easy bro....hakuna nchi ambayo watu wote wapo serious ndio maana nyie wasomi mmepewa jukumu la kufikiri kwa niaba ya nchi...
Umewasahau waliopo guest na bar..
Tunakumbushana tu. Nchi haiwezi kujengwa na wachache na vijana ndiyo wanapaswa kuwa mstari wa mbele kufanya kazi na shughuli za uchumi.

Hii tabia ya kukaa vijiweni na hao unaosema wako bar na guest house sasa hivi ndiyo maana nchi ipo hapa ilipo maana vijana wanaomaliza shule wanakuta kaka na dada wanaamkia mpira, pombe na ngono siku za kazi.

Burudani ni muhimu lakini lazima kuwe na kipimo. Hata nchi zilizoendelea wapiga soga na pombe asubuhi wapo ila asilimia kubwa ya taifa watu wanafanya kazi na inawahamasisha vijana wao kufanya kazi kwa bidii ili kujitegemea na kumudu gharama za maisha. Hapa nchini kijana anajua hata asipofanya kazi anaweza kwenda kwa mjomba na akapewa chai.
 
Hii nchi inamasimango xnaa yaani hadi mnaoenda kazini mnawaonea wivu wapiga soga majobless
Halafu wao wamo humu wanapiga hizo soga wabongo konyo sana
 
Mkuu hao ndio mtaji wa amani uliyonayo leo....
Wakiacha hayo mambo na wakawa serious na mambo ya nchi, hapatakalika...kwahyo kila kitu kipo kimkakati
 
FANYA YAKO.angalia maisha yako.mimi Sasa hivi nipo pembeni ya bwawa nimekaa tu.kwa hyo tusifatiliane
 
Nilivyosoma huu uzi niliamua kuondoka....ila kuna ndezi amesema aziz ki inawezekan akaend simba,
Narudi kubishana naye kidogo
 
Nilivyosoma huu uzi niliamua kuondoka....ila kuna ndezi amesema aziz ki inawezekan akaend simba,
Narudi kubishana naye kidogo
Mnajipa presha ya bure tu.kama hamna hela ya kumlipa muacheni aende
 
Kwanza tambua kila mtu ana definition yake ya mafanikio.
Mie mafanikio kwangu ni kuweza kufika miaka 80 nikiwa na afya ya kuweza kupiga threesome na warembo wa miaka 25 bila kuchoka
 
Sasa hivi nchi yetu imejiweka kwenye mtego kwa kutaka kuwa waandaji na wenyeji wa AFCON, matokeo yake mabilioni ya pesa yatatumika kujenga viwanja na miundombinu. Wakati bado kuna mtoto anakaa chini darasani, mama mjamzito anajifungulia nyumbani.

Sipingi ujio wa AFCON ila kama nchi tunapaswa kujiuliza vipaumbele vya taifa letu ni nini ili kuboresha maisha ya mtanzania: elimu na afya ni sekta zinazohitaji pesa nyingi ielekezwe huko.

Je, mpira unanyanyua maisha ya watanzania masikini kwa pamoja?
 
Sasa wee unaona aziz ki anaenda wapi kazier chiefs au mamelodi?
Mi naona anaweza kwenda Kaizer Chief, anataka usd 20,000 ku sign mkataba mwingine kabla ya yote, naona hataki mkataba tena, hivi hio usd 20k ni ya nini?
 
Inawezekana hapa ndipo tushafika tayari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…