Vijana kachukueni Pasipoti zenu Uhamiaji mtawanyike Duniani; kusubiri ajira na uteuzi ni utumwa wa fikra

Vijana kachukueni Pasipoti zenu Uhamiaji mtawanyike Duniani; kusubiri ajira na uteuzi ni utumwa wa fikra

Passport watakwambia laki na 50.
Lakini kitambulisho Cha uraia unapewa bure[emoji856]
 
Asante kwa kupasua jipu, Kinshasa Congo kuna fursa nyingi mno, ni vyema vijana wakaanza kutoka Tanzania na kutawanyika kwenye nchi jumuia Afrika mashariki.

Mfano mzuri Congo wanahitaji sana dagaa na samaki sangara kutoka huku kwetu ndani ya muda mfupi tu utajiona umefika mahali ukianza biashara hii
Kabla sijaona huu uzi nilikuwa naongea na jamaa yangu kwa njia ya simu yupo Tanga na Pangani anasimamia vyombo vya uvuvi vya jamaa zake,alichonieleza ni kuwa kule wakongo wanakwenda sana kuchukua samaki na dagaa,lakini hasa dagaa hawa baharini wanaitwa zanzibar fish kitu kama hicho anasema wanapakia tandamu kwa tandamu wanunuzi wakubwa ni wakongo.So nakubaliana na wewe nikiunganisha na taarifa aliyonipa jamaa yangu.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Asante kwa kupasua jipu, Kinshasa Congo kuna fursa nyingi mno, ni vyema vijana wakaanza kutoka Tanzania na kutawanyika kwenye nchi jumuia Afrika mashariki.

Mfano mzuri Congo wanahitaji sana dagaa na samaki sangara kutoka huku kwetu ndani ya muda mfupi tu utajiona umefika mahali ukianza biashara hii
Nipe hii connection mzee kwa mtaj Wa milion 1 nikiwa na gunia 7 naweza peleka huko Dagaa?
 
Kabla sijaona huu uzi nilikuwa naongea na jamaa yangu kwa njia ya simu yupo Tanga na Pangani anasimamia vyombo vya uvuvi vya jamaa zake,alichonieleza ni kuwa kule wakongo wanakwenda sana kuchukua samaki na dagaa,lakini hasa dagaa hawa baharini wanaitwa zanzibar fish kitu kama hicho anasema wanapakia tandamu kwa tandamu wanunuzi wakubwa ni wakongo.So nakubaliana na wewe nikiunganisha na taarifa aliyonipa jamaa yangu.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
Ndiyo muende tatizo vijana sahv wanaishia kuongea tu

Ova
 
Passport watakwambia laki na 50.
Lakini kitambulisho Cha uraia unapewa bure[emoji856]

Hapo Kwenye Passport watakuambia Unasafiri?
Wanamaanisha Yaani Tayari unataka kwenda sehemu? Leta Uthibitisho!
Sio Eti Upewe halafu Uanze Kutafuta Ajira[emoji851][emoji851]Hawakupi Aisee tena wanasema Passport ni Mali ya Serikali.
Labda Sasa Hivi wawe wanebadilisha Huo Utaratibu!
 
Mhe. RAIS ameifungua nchi, SI Kwa wazee Bali Kwa vijana. Wakenya wamejaa Tanzania Kwa ajili ya matembezi ,biashara, ajira nk. Sisi Watanzania tumejazana Dar na tunajipongeza Kwamba tumeiona Dunia. Hapana vijana badilisheni fikra, mtizamo na mikakati, wazeni kuvuka mpaka, wazeni kufanya biashara za kuvuka mpaka, wazeni kuajiriwa Duniani.

Mnatafuta distinction za Nini kama fikra zimeishia dar? Maisha ya Dar ndiyo yakufanye usote ukisoma bila kulala? Unapata first class anateuliwa lower second? Unapata first class ujui hata mwonekano wa passport, hapana tukatae utumwa tutembee tuache mji upumue.

Naandika haya baada yakuona tatizo la ajira nchini, hakuna namna utumishi wa umma ulio na uwezo wa kuajiri less than one milioni utafanikisha kiu ya wataka ajira. Acheni kupoteza muda, ondoeni fikra za kupata life Tanzania pekee wazeni nje.

Vijana wakitoka Kwa wingi watapata ujira nje na kutuma fedha zitakazotumika kama mitaji Kwa ndugu zao , vijana wakitoka Watanzania watapata pakufikia HUKO nje. Tutoke

Dar imejaa kila mwanafamilia nchi Hii, hakuna mwenye hofu ntafikia wapi dar maana kila Kijiji kina mtu dar, kwanini tusiamue kuwa na mwanafamilia kila mji Duniani? Tunaweza tuanze Sasa. Tutoke

Tumfate Mkuu wa Uhamiaji atupe pasipoti zetu ambazo amekabidhiwa akae nazo akisubiri tufike watupe, tumpunguzie jam mama Samia Kwa kusambaa kuliko Sasa kila wakati tunampigia kelele atuajiri. Tutoke.

Kama tulivyo wakarimu ndivyo na wenzetu walivyo, tuondoe hofu maana Mabalozi wapo Duniani kote wanalipwa fedha kutulinda tunapoonewa. Tutoke.

Kampeni Hii iwe chachu ya watawala kuwakumbusha vijana wajibu wao wa kutoka , iwe kampeni ya vyuo kutoa elimu ya kujitegemea HUKO nje, ndani tumejaa. Iwe kampeni ya nchi katika kukuza Diplomasia na kupanua mapato yatokanayo na Watanzania waishio nje. Tutoke.

Tunao madaktari na Manesi, tunao vijana wa IT ambao kwa wingi wao tumeshindwa kuwaajiri. Tuwasaidie watoke wakafanye kazi nje mwisho tutawaita wakiwa tayari wamebobea na nimadaktari bingwa. Vijana tokeni
Daaah, umeandika vizuri sana. Wazo hili lingefanyiwa kazi hakika lingeleta matokeo chanya. Ni kweli wapo vijana ambao ni smart sana kichwani lakini wamekosa mahali pa kuzitumia akili zao, ila zipo nchi zenye opportunities zinahitaji vijana kama hawa. Wakiwapata hawa wanawatumia ipasavyo na hivyo kuleta tija kwao na kwa vijana wenyewe. Kwa kuwa zipo nchi zinazohitaji rasilimali watu (Australia, Canada, nk), basi tuwe na idara inayoshughulikia masuala ya kuwapeleka vijana kufanya kazi nje kwa makubaliano maalumu (kati ya vijana na idara husika). Idara hii tuiite 'export brains'.
 
Back
Top Bottom