Vijana kujifunza kuhusu siasa ni muhimu sana

Vijana kujifunza kuhusu siasa ni muhimu sana

Ejolisi

Member
Joined
Aug 26, 2022
Posts
57
Reaction score
87
Wazo hili nimelipata baada ya kupata maoni tofauti tofauti kutoka kwa baadhi ya vijana wa kitanzania tena wasomi kuhusu mchango wao katika siasa na hali halisi iliyoko kwa sasa.

Inasikitisha kuona kwamba hata wenye elimu na mwanga hawana muda wala uelewa wowote, wenye chachu na hamasa ya masuala ya uongozi na utawala ni wachache sana. Wengi wanadai kwamba hawana haja ya kujua siasa na kusahau kuwa siasa ndio inayotoa tafsiri ya mifumo yote ya nchi na ni kwa namna gani yatekelezwe.

Mabadiliko na maendeleo yanaletwa na watu wanaojua nini kinaendelea kwenye nchi, mifumo imekaaje, wapi pamepwaya. Vijana suala la kusema siasa haituhusu ni kwamba inatuhusu sana tena hari hii ipandikizwe mpaka kwa watoto.
 
Yafaa nini kijana kupoteza nguvu yako kuwa mwanasiasa kwenye nchi ambayo raia qamezoea kuibiwa kura kila siku.

Hizo energy si nitumie kupambania maisha yangu na wanangu
 
Yafaa nini kijana kupoteza nguvu yako kuwa mwanasiasa kwenye nchi ambayo raia qamezoea kuibiwa kura kila siku.

Hizo energy si nitumie kupambania maisha yangu na wanangu.
Fikiria vijana wote nchi nzima tuseme ivo, na maana yangu ni kwamba sio uwe politician at least mtu ujue nini kinaendelea kiongozi ni nani anawajibika wapi haki zangu ni zipi.
 
Yafaa nini kijana kupoteza nguvu yako kuwa mwanasiasa kwenye nchi ambayo raia qamezoea kuibiwa kura kila siku.

Hizo energy si nitumie kupambania maisha yangu na wanangu
Siasa inaleta effect kwenye hayo mapambano yako ya kiuchumi!
Wafanyabiashara wengi Kama alivyo Rostam, wanawini kwa sababu wanatembea na beats za siasa!

Wengi wamepoteza nguvu, uchumi, mitaji kwa sababu ya siasa!

Maendeleo ya Taifa pia mtu mmoja mmoja, huchagizwa ama huzoroteshwa na siasa!

Vijana wakiifahamu siasa vizuri, Ni mwanzo wa kupatikana kwa siasa Safi, kwa maana hawatakuwa tayari kukubaliana na makanjanja wa siasa katika uongozi!
 
Back
Top Bottom