Vijana wa Arusha kuuona uhuni na usela ni ujanja kunazidi kulitafuna jiji, usalama umepungua, maadili yameshuka, serikali haina msaada

Vijana wa Arusha kuuona uhuni na usela ni ujanja kunazidi kulitafuna jiji, usalama umepungua, maadili yameshuka, serikali haina msaada

View attachment 2707633

Kunahitajika PROGRAMU ya dharura kuliokoa hili jiji

Vijana wengi wahuni ni wazawa wa hapa hapa Arusha na matokeo ya kuukuta utamaduni wa kutukuza uhuni tangu wakiwa wadogo, imeshakuwa ndani ya mfumo wa maisha wa vijana wengi kwamba ili uonekane mjanja basi uwe mhuni wa kunywa pombe kali, kuvuta bangi ama uwe mhalifu.

mapikipiki haya ya wanakimbiza vibaya mno, ajali kila siku, wamejaa mount Meru na nkoaranga hospital wamevunjika vunjika miguu,.Bodaboda za kutaftia riziki wanalazimisha ziwe pikipiki za michezo, ukienda kwenye magroup yao haya ya kudandia pikipiki kuna "pumzika kwa amani / rip" nyingi sana.

vijana wanazidi kuutukuza ulevi wa hayo ma k-vant na bangi, sina shida na matumizi ya vilevi ila wao wanavitumia kupita kiasi.

Makundi ya vijana wengi ni magenge ya vijana wanaoishi bila future, wanafanya vingi bila kujali madhara wala kesho.

Suala la kupigana beto (visu) nalo halipo nyuma, Sime na visu vimekuwa vitu ambavyo vinazidi kuzoeleka kutumika sio tu kwenye uporaji bali hata kwenye mabifu ama ugomvi baina ya vijana, nilikua naangalia clip moja hata msanii wa huko anauvuma kwa sasa Fidovato analalamika vijana wanapigana sana beto.

Wizi nao hauna dalili ya kupungua, watu wanaporwa kikatili sana inabidi utii amri lasivyo utavurugwa maini na beto, bodaboda wanaibiwa pikipiki mpaka kuuwawa, ujambazi nao upo wa kuvamia matajiri, kwa ufupi kuna famjlia zinajulikana kabisa wanaishi mjini kwa shughuli hizo lakini ndio wanapewa heshima maana uhuni unaonekana ujanja.

Ajabu ni kwamba hata polisi ni kama vile wamefumbia jicho ama jitihada wanazofanya ni ndogo sana, ni kama vile wamezila na kujikatia tamaa wamewaacha wenye mji wafanye watachojua wao with little interference
Shida yako nn wakifa ww unaumia nn?
 
Well ...

Kama ndivyo mbona nanjilinji BETO na ZUNA hazitembei sana kama chugga?!! [emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Unajua, niliwahi kuskia hizi nyama nyekundu wanazokula binadamu Zina athari kiasi flani wanakuwa kama wanyama wa mwituni.

Lakini kwa watu wanaokula samaki pwani pwani huko wanakuwa na ukarimu flani hivi, sjui kama ni kweli au laa.
 
Well ...

Kama ndivyo mbona nanjilinji BETO na ZUNA hazitembei sana kama chugga?!! [emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Chuga pako peace arawa! Hizi mambo nilishuhudiaga miaka ya 90s huko!
Uhuni uliopo saivi ni WA kiduanzi,bangi machalii wanayovuta saizi ni low quality halafu wanavuta na maunga
Nenda mianziani uone
Huo unaoona ni uhuni sidhani kama ni uhuni

Ni lifestyle Yao tu na mazingira waliyoyakuta kama meno yao
 
Shida yako nn wakifa ww unaumia nn?
[emoji15][emoji15][emoji1787][emoji1787]

Kwani suala ni kufa mkuu ?!!

Kufa kila mtu atakufa....

Kwani huu uhai tuliopewa hauna thamani ya kuishi KIUPENDO wa "Rastafarianism" ama "ubudha"....hivi "chaos" mashambani inaweza kuzalisha MAZAO YA KUTUSHIBISHA ?!! [emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Dah , mnaikosea Sana Bangi , Huu ni udhalilishaji. Huku ni kuinyanyapaa Kwa makusudi kabisa.

Mkunazi Njiwa

Kama MTU ni mpole , akivuta bangi au akinywa kileo kitadhihirisha Kuwa yeye ni Nani, Akiwa mpumbavu na mkatili yote yatadhihirika tuu.

Machalii WA chuga ni by nature wakorofi
 
Unajua, niliwahi kuskia hizi nyama nyekundu wanazokula binadamu Zina athari kiasi flani wanakuwa kama wanyama wa mwituni.

Lakini kwa watu wanaokula samaki pwani pwani huko wanakuwa na ukarimu flani hivi, sjui kama ni kweli au laa.
Kuna ukweli ndani yake....

Ndio maana "Rastafarians" hawali nyama....

Na mikoa inayokula sana nyama kuna tabia zinashabihiana [emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
[emoji15][emoji15][emoji1787][emoji1787]

Kwani suala ni kufa mkuu ?!!

Kufa kila mtu atakufa....

Kwani huu uhai tuliopewa hauna thamani ya kuishi KIUPENDO wa "Rastafarianism" ama "ubudha"....hivi "chaos" mashambani inaweza kuzalisha MAZAO YA KUTUSHIBISHA ?!! [emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Badili approach Mkuu.
 
Back
Top Bottom