Vijana wanawezeshwa vipi kujiajiri

Vijana wanawezeshwa vipi kujiajiri

Ambapo nitakuwa nimeitumikia serikali kwa muda wa miaka 10 tangu niajiriwe mnamo mwaka 2015
 
Tunaotaka tutoke hii Jela Tushauriane humu, je tukusanye mtaji sasa bila kufanya ujasiriamali na tutakapoacha tu kazi ndio tuanze rasmi ujasiriamali? Ama tuanze sasa hivi kufanya kazi na ujasiriamali ili tu-taste ladha ya ujasiriamali kabla hatujaacha kazi? (Ila hata mambo yakiwa magumu kwenye ujasiriamali kipindi tupo kazini na tunafanya ujasiriamali, kuendelea na kazi sio option). Kubaki Jela haiwezi kuwa option kisa kuna dona na maharage ya bure, bora kuwa uraiani ule mlo mmoja wa maharage na ugali kwa mwaka mmoja ili uje kula asali na maziwa kwa miaka mingi ijayo.
nadhani kama upo jela pambana kukusanya mtaji meanwhile anzisha ujasiriamari mdogo uendenao mpaka pale utakapoamua kuondoka jela
usitamani kukaa jela zaidi ya miaka mitano iwe pungufu ya mitano
 
Inasikitisha kuona wengine wanatamani kuingia angali wengine wanataka kutoka
 
Bado kitambo kidogo niachie kazi...ki ukweli nimechoka kufanya kazi huna amani ni sawa na kuishi na mke mliyeshindana bora nikafuge ngo'mbe wa maziwa miradi niipendayo!
 
Katika maisha yangu mpaka sasa na kwa umri huu niliajiriwa mara moja,.sikuwahi kufurahia maisha ya kazi yangu aisee nilijiona mtumwa waziwazi doh,.lakini katika hayo nilijifunza vitu..sasa niko kusimamia malengo/maono na ndoto zangu kwa muda mwingi na kwa nguvu zangu zote nikiwa nimezielekeza katika hayo..safari ni taaaam[emoji4][emoji4]nilijiona nimecheleeeewaa kumbe aah,..Ahsante Jehovah.
 
Mtaani kugumu...... Haya ndio Majibu ya walio wengi kwenye ushauri wa kuacha kazi, Kama unataka kuacha acha usiombe ushauri, Nakuomba ufanye kautafiti. Tafuta watu kama kumi ambao wako mtaani na unawaamini, waombe ushauri.

Kama wakitokea wawili wakakubaliana na wazo lako njoo nidai vocha ya 500(joke)

Kimsingi haya maamuzi yanategemea tu utashi wako, Unapokua na Biashara huku bado uko kwenye ajira watumishi huwa wanakupiga sana, mwisho wa siku biashara inakufa na ndoto yako ya kuacha kazi inakufa

Mimi nakushauri anagalia mfuko wako na uwe na uhakika wa biashara ambayo unataka kufanya, Kumbuka challenges hazipo maofisini peke yake hata kwenye biashara pia kuna challenges.

Biashara ambayo unaweza kuanza nayo kama bado hujabuni biashara jaribu kuangalia Mazao, Mazao hayana hasara jaribu ku avoid perishable things kama viazi na mboga mboga.

Mazao kama mahindi yakiharibika utauzia wanaotengeneza byakula vya kuku.

suala kubwa ni mfuko wako na utayari wako wa kuishi kigumu.
Umesema kitu sahihi, mara nyingi ukiwa kwenye ajira huku ujasiriamali watumishi wanakuumiza, hii ndiyo changamoto kubwa kwa aliyeajiriwa na kufanya uhasiriamali kwa sababu muda wa kusimamia uwekezaji wako unakuwa mdogo saana! Labda kama umeoa/kuolewa hivyo mmoja wenu ahusike kwa asilimia nyingi zaidi wakati mnajiandaa kuacha kuajiriwa. Haya yameshanikuta zaidi ya mara moja [emoji17]
 
Great, nilishaacha kazi ya Ualimu mara mbili, nikarudi kwa kazi nyingine ila pia roho yangu inaniambia kuwa ni Lazima niache kazi ili niwe na kitu ambacho ni lasting.... kazi zina muda, kazi za watu zinazeesha, zinaleta magonjwa ya stress na kukuminya sana kufikiria nje ya box. Nashukuru kwamba nakarinia kuvuka daraja hili, sitarudi nyuma this time MUNGU anisaidie. Kuna kitabu nakisoma kipo kwenye Playstore kinaitwa THINK AND GROW RICH aaaghhhh kinanitia nguvu sana, I encourage you guys mkisome pia.

Hivi vitabu vipo vingi na vya bure
Lazima tubadilike, lazima tubadilishe our Life style, inawezakana lakini ni lazima tujikane kwanza, lazima tujishushe, lazima tuwe commited.

Thank you
Kingine ni nidhamu ya woga kwa tulio wengi, binafsi naandaa mazingira ya kujiajiri wakati bado nimeajiriwa, mambo si mepesi kiivyo lakini inawezekana ikiwa umefanya uchaguzi sahihi kulingana na wito unaousikia ndani yako. Binafsi napambana kuweka miundombinu itakayonipatia fedha ya kula na kujikimu mahitaji yangu muhimu kama baba anayetegemewa na familia na kisha nafanya uamuzi wangu mzima.
 
dedication kwenu;
retire young, retire rich by R.Kiyosaki...
ni miongoni mwa maamuzi magumu ambayo ni sahihi.
ni kosa kuacha kazi ujiajiri akilini mwako ukiwa na wazo mambo yakigoma nitarudi kuajiliwa.
unaweza kuja kuaibika. Hiyo mission ni kama movie ya The Hardway The only way, makomando wanatua na ndege iliyowaleta inalipuliwa kuwadhihirishia hawana option zaidi ya kushinda pambano msituni maana hakuna usafiri wa kuwarudisha.

ukifanya maamuzi hayo mapema, utapata faida ya Muda mrefu ila lazima upitie bonde la uvuli wa mauti ili kukuandaa kukabiliana na kupata na kukosa maishani. bonde hilo huwarudisha wengi kwenye ajira wakiogopa gharama ya kujiajiri.
Hahaha asante, kiukweli ili uonekane ni lazima uwe umefanya kitu cha tofauti
 
Kingine ni nidhamu ya woga kwa tulio wengi, binafsi naandaa mazingira ya kujiajiri wakati bado nimeajiriwa, mambo si mepesi kiivyo lakini inawezekana ikiwa umefanya uchaguzi sahihi kulingana na wito unaousikia ndani yako. Binafsi napambana kuweka miundombinu itakayonipatia fedha ya kula na kujikimu mahitaji yangu muhimu kama baba anayetegemewa na familia na kisha nafanya uamuzi wangu mzima.
Mkuu kukata tamaa ni kosa la jinai

Kuweka miundo mbinu ni kutengeneza njia sahihi

Kujiajiri ni sehemu ya kutimiza unacho kiamini

Kuajiriwa ni sehemu ya kutengeneza mandalizi ya kwenda unapo amini panatakiwa uwe

Amua kwa busara tekeleza kwa uafanisi
 
Ndugu zangu. Swala LA kuacha kazi linahitaji kujipanga sana, huwa siwashauri watu wakurupuke kwani yaliyonipata sipendagi na wengine yawapate
Kuna wazo huwa naliwaza kuhusu ajira na kujiajiri, kwanza kujiajiri kutokana na ujuzi ulionao mf:- dereva wa gari aliyeajiriwa kuamua kuacha kazi ya kuajiriwa na kununua gar yake na kufanya taxi (kuikodisha) na kuendesha mwenyewe (uber) au kujiboresha kwa kuongezea status ya fani yake na kuwa na ushindani mkubwa katika soko la ajira hivyo kuwa mchaguzi wa aina fulani ya kazi itakayo mpatia muda wa kusimamia mradi wake na bado ikamlipa vizuri [hii ni katika kutafuta ujasiri wa kifikra wa kuanza kujiajiri] na mwisho kuwa na mtaji wa kutosha na taarifa kamili ya kile unachotaka kukifanya.
 
Aisee, maandalizi umeyafanya kwa muda gani mkuu

Mkuu sijajiandaa kihivyo,

Nimekuwa mjasiliamali kwa muda sasa nikiwa kazini,

Nimekuwa nikijihusisha na kilimo cha matunda lakini napata hasara sana,

Lakini hiyo hasara haitokani na ubovu w bidhaa la hasha ni usimamizi mbovu

Watu wengi nnao waamin mpaka leo ndo wengi wao wananiliza,

Kimahesabu kwa nikifanya kilimo kwa mara moja naweza pata pesa ya mshahara wa mwaka mzima,

Kwanini niendelee kubaki kazini wakati naona kuna sehemu naweza kupata pesa ya kutosha nzuri tu,
 
Vitabu vingine vizuri ni E-Myth kinaongelea kuhusu kuanzisha MFUMO WA BIASHARA ambao ndio kiini cha mafanikio kwenye biashara. Kingine ni 21 Secrets of Self Made Millionaires, kuna Richest Man in Babylon, pia kipo The millionaire Next Door, Get Rich Your Own Way n.k

Ukivisoma hivyo huwezi kubaki kama ulivyokuwa mwanzo
Halafu kitu kingine kinachoweza kuwa ni changamoto wakati mwingine lakini, ni namna ya kuhamisha mazingira ya mwandishi wa kitabu kutoka kwao na kuyaleta katika mazingira ya kiafrika ama kitanzania ili mawazo hayo yaweze kuendena na wewe
 
Mkuu umenitia moyo sana nmepanga baada ya mwaka niache kazi nijiajiri,Jana nilikuwa naongea na aunt yangu alinikatisha tamaa sana akasema mwanang sikushauri uache kazi kabisaaa,km umeamua kufanya biashara fungua asimamie mwingine uendelee na kazi
Lkn kazi yangu inachosha nafanya kazi na matusi juu,kuna wakati nalia
Kwa hili andiko lako limenitia moyo
Kwa nia thabiti nitaweza
Huyo Aunt yako hajui unayoyapitia. Anataka uendelee kubeba huo msalaba wa moto (kuajiriwa) shingoni.
 
Mkuu ni kweli mziki wake ni mnene. Imagine sasa hivi ukivyoajiriwa ukichalewa kutofika kazini mwisho wa mwezi mshahara upo pale pale, lakini ukichelewa au kutofika kazini kwenye kazi yako mwenyewe ina maana tayari pato ulilotarajia kulipata limeshapungua.

Cha msingi ukiamua Kujiajiri na baadae kuajiri lazima uwe committed 100%
Changamoto ingine ni mambo ya kuigana, unataka kuwa kama fulani wakati wewe siyo huyo fulani! Ni vizuri kufanya kile unasikia kabisa ndani yako hasa wakati ukiwa na utulivu ili upate kijitathimini mwenyewe
 
Back
Top Bottom