Hili jambo linanifikirisha sana.
Sababu hasa ni nini.
Kijana wa Kitz akipata hata Getto tu basi humo Mademu watajaaa.
Atabadirisha mademu kila sikh, hapo geto lina Tv, Kitanda cha chuma na Godoro la Nchi 10. Na zile taa za rangi rangi.
Ukilinganisha na Vijana wa Kitz asili ya Waeabu na Wahindi ni watulivu sana. Wanamiliki Biashara na Makampuni ya Kwenda. Lakini huwezi kuwasikia.
Hawasikiki kwenye kashfa za Ulevi, uzinzi wala za hovyo hovyo.
Kijana wa Kibongo au Mwingine asili ya Afrika akitoa hata Wimbo mmoja tu uka Hit aisee mtamjua tu hata asubuhi anakula nini na analala wapi. Kutwa kupost hadi Boxer zake.
Je hii ni laana?
Mhindi na Mwarabu akipata pesa na biashara anatulia kuboresha familia yake na uchumi zaidi. Lakini sisi Watz ni kuongeza michepuko kila siku kukimbizana na Kesi za Fumanizi mitaani.
Tuna wajibu wa kubadilika na kujifunza kwa wenzetu waliofanikiwa
1. Wanadamu wengi Wanafanana.
Itakuwa hauishi au kushinda mitaa ya hao unaowazungumzia.
Ila wanazo tabia zote za Watanzania
Tofauti ni kuwa wao hawapo Huru, nchi hii bado kuna Watanzania weusi wengi huamini hao waarabu na wahindi sio Kwao. Utawezaje kujirusha kwenye nchi ambayo majority wanawaona ninyi sio kwenu.
2. Kubadilisha wanawake hata Waarabu au Wahindi wanafanya hayo.
Ushahidi ni uwepo WA machotara wengi maeneo wanayoishi hao waarabu na wahindi.
Au unataka majina ya watu mashuhuri ambao ni matokeo ya uzinifu?
3. Nenda kwenye Casino, Kule m
mjini au Osterbay, Masaki na Mikocheni utaona mambo wanaofanya hao ndugu zetu Waarabu na Wahindi.
Kingine,
Pesa za Kurithi hazinaga Mbwembwe.
Mtu karithi Mali anawezaje kujivunia yeye ni Legendary au Mwamba au Hustler?
Wahindi na Waarabu wengi wao pesa Zao ni za Kurithi, wanategemea familia zao. Hivyo wapo chini ya udhibiti Mkali.
Wabongo wengi waliotoboa unaowaona kwenye mitandao ya kijamii au popote wengi wao ni ma-legendary, Miamba, Hustlers kutokea chini KABISA.
Watu waliokataliwa, watu waliotelekezwa na wazazi na jamii, watu walionyimwa Fursa lakini wakapambana wakatoboa unataka wasiwe Proudly kwa mapambano Yao?
Mtu kama Diamond, au hao kina chief godlov, kina Masanja, kina Mpoki, kina Dotto Magari.
Hao ni watu waliodharauliwa, waliokataliwa, Leo wametoboa unataka wakae Kimya?