Vijana Wenzangu, Connection za Maisha zipo Bar na Kwenye Viwanja!

Carlos The Jackal

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2017
Posts
25,725
Reaction score
78,589
Usikae tu home na vijiwe viisvyo maana.

Hata kama sio Mlevi, Toka nenda Kiwanja ambacho unajua wastaarabu wanakaa.

Huko ukutane na RC, DC, RAS, DAS, DED na Ma CEO mbalimbali. Hawa watu typically ni Walevi, ni wanywaji Pombe haswaa, nahuko Niko wanakutana kupeana michongo.

Sio lazima unywe, wewe nenda hakikisha una Hela mfukoni. Alafu ukifika Agiza Juisi hata ya Azam.

Chungulia chungulia mazingira, Muagizieee Mzee Fulani yule aliyekaa pale , au wazee Fulani walokaa pale , au Jamaa fulan wanaokunywa vitu mdogdogo wakionekana wanajadili!

Muagize tu Muhudumu, Kamuongezee yule Mzee pale, akikuuliza, mwambie Yule kijana palee!!

Hapo utajenga Uhusiano na watu bila kujua na ndo Connection iyo!

Nimewaibia Siri!
 
Bar Kuna madili ya ovyo .. Connection zipo LinkedIn ila madogo hawataki wao kulamba lips TikTok na Instagram then ndo wanajifanya watoto wa town.

Kusema la haki nimekutana na watu wengi wa maana Facebook kushinda mitandao yote..
Uko sahihi kabisa. Facebook kuna magroup ya maana mno. Utakuta group yupo hadi kiongozi mkubwa wa serikali na ukipost ana-comment.
 
Ni kweli.

Usikae vijiwe vya vijana wa hovyo kiasi kwamba likitokea tukio mtaani basi nyie ndio washukiwa wa kwanza au polisi wanaanza na nyie.

kakae bar ila sio za vichochoroni. Michongo ipo huko.
Huna ajira halafu unakaa ndani. toka ukutane na watu.
 
Huko ndo kuwa chawa kwenyewe! Kuna gharama kuilinda koneksheni. Hao uliwataja wana mishahara, posho, milungura na upgaji mkubwa. Hawanywi tena serengeti wala konyagi.

Je unao uwezo wa kuwalewesha kwa mapombe ya hadh yao ya bei mbaya?

KAMA UNATAKA MICHONGO KUWA NA KONTENTI KICHWANI NA UCHANGIE MIJADALA KWA WELEDI.
 
Ccm wote ni wezi, rushwa na ubadhirifu. Je ndio michongo unayoongelea?
Nchini kwetu, hakuna fursa za kibiashara halali, wafanyabiashara wanauoweza kupata bila ya kuiibia na kuifuja nchi kwa kupitia 'wazalendo'?
 
Najua watu wenye connection zenu mtapita kusoma Uzi huu

Natafuta kazi yenye sitaha hasa zinazohusu usimamizi wa project au Office zenye mtandao mpana.

Wasifu wangu ni huu:

Nina maarifa hasa mambo ya sayansi ya afya

Naweza kusoma, kuandika, kuzungumza lugha mbili kuu; kiswahili na English

Ninaweza kuandika maandiko ya miradi, kuandaa mpango kazi na kuitekeleza bila usimamizi wa karibu.

Nina uwezo mzuri wa kufafanua mambo kwa lugha nyepesi na bila kumboa anayenisikiliza.

Sina tabia ya wizi, uaminifu, heshima na kupenda kuwajibika ni sehemu ya maisha yangu

Aliye interested , usiache kunijulisha

Note: Najisikia huru nikifanya kazi na mtu mwenye uzoefu mkubwa ambaye yeye ndo awe leader kwenye eneo hilo. Mimi anitumie kama officer mtendaji.
 
Please take it from me maisha ya bar sio maisha... Labda ukutane na watu sahihi sana.. Ni kweli unaweza kupata connection nyingi lakini kwa asilimia kubwa mapato yake yakaishia kwenye starehe pombe wanawake na mambo ya kishenzi
Ni kama laana fulani... Watu tuliokuwa tunapeana connection 10+ years back wengi ni marehemu au wamechoka ama wanaumwa[emoji848][emoji2827]
 
Unasema unajua kuzungumza na kuandika lugha ya kiswahili kwa ufasaha...

Sasa uliposema "bila KUMBOA anaekusikiliza" ulimaanisha nini? Hiyo KUMBOA ni lugha gani?
 
Hata usipaniki, wengi wanakunywa mapombe ya kawaidaaa kabisaa
 
Mkuu Mshana , Ukiwa mwenye uzoefu umenena , siwez kupinga .
Mimi sio Mlevi, na haitokaa Mimi kunywa pombe, , kidogo Ulevi wangu ni mbususu

Walakini nimekua na Tabia ya kutoka nakwenda viwanja kupunga upepo nakushangaaa watanzania.

Sio Bar za uchochoron ambazo ni Kuna madanga ya Buku ten ,na wanahitaji pombe tu.

Ni sehem ambazo ni za starehe hivi, muziki laivu bendi, Kuna nyama choma ya Kila aina n.k.



Hawa watu wenye konekishen, hawapendi Bar za uswazi na Wana mambo ya ovyo Giza linapoingia , ila Sasa unatulia unasoma mchezo .
 
Kule bar kuna maroho yanayomeza pesa.. Nilikuwa mwendaji mzuri sana wa bar connections nyingi sana pesa ilikuwa inakuja bila taarifa kutumia laki 5 kwa wiki kipindi hicho haikuwa shida.. Ila sijui zile pesa zilikuwa zinaenda wapi
 
Nichangie mijadala wapi mkuu? I mean kwenye forums zipi? Or una maana comments za kawaida?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…