Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Mimi wa kwangu nilikuwa nadownload katuni namwekea kwenye simu anaangalia sasa siku moja nikamnyima akaniambia siku nikifa simu yangu itakuwa yake, sema tulikuwa wawili angelikuwa na mtu ningejua ameambiwa na hapo ana miaka 4 tu.
 
Mwanangu nakaa mbali nae ULA hakuna MTU anampenda kama Mimi hata kama hatujaonana mwezi mzima akiniona tu he is happy to the fullest,hahaha shobo na watu wengine,unaweza kumbeba na atabki amekuangalia tu anacheka akiamua Mwenyewe..
 
Wangu ana mwaka na nusu ila ana vituko vingi sana na pia anajitahidi kuongea. Mama yake kaendanaye kijijini kwa bibi siku ya pili kaaza kulia anadai tv. yeye huwa anaita tii
 
Hahaaa. I could talk about my kids the whole day.

Yule mkubwa wa almost 5 years ni mpole na ana hurumaaa. Pia anapenda sana ufugaji na ameshajua kuchanganya vyakula vya kuku. Anawajua kuku wake wakiumwa, anajua kuandika numbers kwenye kila yai linalotagwa na kuliondoa bandani. Pia anajua kufatilia aina ya kinyesi cha kuku kama ni cha kawaida ama ni cha kuumwa.

Mdogo wake anaekaribia miaka 3 ni mtundu na mbabe. Yeye anapenda magari na ufundi. Yaani umuoneshe video ya magari kwenye simu imekula kwako huna jinsi ya kujitoa atakavyotupa tantrums.

Wengi hupenda kusema nampendelea yule mkubwa lakini sio kweli. Ni rahisi kumuonea kutokana na sura yake ya kipole na huruma aliyonayo so nikisikiaga nywiiii amelia basi nageukaga chui. Because the lil man can surely take care of himself.

Huyu mdogo atakuwa amekufanana kwa asilimia kubwa sana...!
 
Watoto katika hatua zao za ukuaji na kujifunza wanakuwa na mambo flani flani ya kufurahisha sana yaani mwanao anaweza kukuvunja mbavu balaa.
Mfano
1. Mwanangu (1.5years) anaweza kuwa anatazama TV akisikia unaongea na simu au umeweka music kwenye simu anakimbia kuja kuangalia simu hata kama TV ilikuwa na TV program ya katuni nzuri kiasi gani[emoji23] [emoji23] [emoji23]

2. Ukitaka alale we nenda kitandani weka music kwenye simu yako atakuja mwenyewe hata kama alikuwa anakwepa kulala[emoji23]

3. Anaheshimu simu yangu kama kituo cha polisi ila ya mama yake kashaipasua ukiiona utajua mama yake anafanya kazi idara ya miamba (geology)[emoji23]

4.Kupenda safari akiona mtu anatoka tu anaanza kuaga bye bye akijua nayeye anahusika na safari[emoji23] [emoji23]

5. Chakula kikiwa tayari, kabla sijaitwa kula yeye akiona mambo yako tayari anakuja kunipigapiga mgongoni(hajajua kuongea) akiashiria msosi tayari basi ukipotezea anaenda anarudi mpaka utakapoinuka[emoji23] [emoji23]

6. Mwanangu anatabia flani kama wivu, akiona naongea na mama yake mara nimemshika mkono tunaongea kama jambo la siri anakuja fasta analia anataka mama yake ambembe[emoji23]
Nadhani hajajua kwamba mama yake ni mke wangu[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Hivi ni baadi ya vituko vya watoto mdau ongeza vya mwanao
Watoto wanaleta raha sanaaa
View attachment 521347
Jembe langu lina maswali flan ya kichunguzi sana halafu ana kumbukumbu ukimwambia kitu inabidi uwe makini kuna siku atakuumbua,mbaya zaidi au nzuri anapenda sana ishu za kijeshi jeshi, kuna siku tunaangalia maadhimisho ya Muungano gwaride linapigwa ye katulia tuuuliiiii duuh baadae nmkuta nje kashika gongo kaweka begani anapiga kwata na sauti za kikakamavu "mbeeeleeee tembeeeaaaa.....nyumaaaaa geeeukaaaaa"....

Moja ya maswali aliyowahi kuniuliza nilienda nae benk ATM kutoa hela akaangalia mchakato ulivyo baadae akaniuliza "hivi baba zile hela kuna mtu ndani anazitoa au zinatokaje?" hahahahaaa

Siku nyingine Aliuliza hivi mvua inatoka wapi? au Mungu anamwaga maji? daah

Kubwa kuliko alikua anacheza na wenzake wakamtania "mwangalie kichwa chake" duuh karudi amekasirika analia anasema "baba hiki kichwa sikitaki niletee kingine" Ilibidi niuvae ubaba kumtuliza.

kua na mtoto au watoto ni faraja sana....
 
Wangu ilikuwa nikivaa mzura(boshori/kofia ya baridi) huwa ananikimbia na hataki hata kuniona. Anajilaza kifuani kwa mamayake anaficha uso kabisa. Akiulizwa nini, ananyoosha kidole na kusema mtu...mtu. Nikiwa bize sitaki anisumbue naivaa tuu. Kuna kipindi nikaiweka kitandani akawa kila akitaka kuingia chumbani anachungulia na akiiona haingii. Alivyokuwa mkubwa mkubwa (3yrs) akawa kila akiiona anaichukua na kwenda kuitupa. Hata soksi zangu kama zina rangi nyeusi kama lile boshori akiziona anaenda kuzitupa nje.
 
Na dogo ana miaka 4..... Huchoki kuwa nae ana penda story anapenda compyuter zaidi ya kula.... Amesoma mwaka mmoja tu kaacha shule...... Wame mpeleka shule ya mambo ya IT... Shule za kawaida anakwambia haelewi chochote
 
Hakuna raha duniani kama mtoto. 0.8yrs lakini akiona tangazo lolote itv hata kama alikuwa anafanya nini, ataacha na kuangalia. Tangazo la tigo akimuona Joti lazima acheke, ukiongea na simu hata kama alikuwa analia, lazima atanyamaza, ukiweka loud speaker atacheka hadi raha..
 
ni 4yrs ..akiudhiwa tuu... ni kilio na kilio chake anakuangalia usoni huku machozi yanamwagika.....anasubiri umbembeleze....ukijifanya kumpotezea anaongeza sauti ya juu zaidi...[emoji1] [emoji1] [emoji1] ...lazima umbembelee....hakawii kunyamaza....
 
Wangu ana 4yrs last week walikuwa kwenye exam ya midterm kwa elimu yake ya kindergarten sasa mwalimu akaandika vitu amabvyo hawajawahi kusoma aisee aligoma kuufanya huo mtihani mpaka akaenda mama yake siku iliyofuata ikabidi afanye kama special mbele ya mama yake na kumbembeleza kwa sana tu.
Hii ya huyu imetisha wangempa sapp tu.
 
Wa kwangu akiona paka anawaambia uchindwe kwa jila LA Yesu
Hahahaaa wangu anapenda kuwaonea sana nyau akimuona popote atamshika masikio na kumnyanua juujuu au mkia afu anamnyanyua hamuogopi hata kidogo..very interesting na mengine kibao afanyayo..watoto raha
 
Back
Top Bottom