Viongozi kumi (10) Bora Tanzania

Viongozi kumi (10) Bora Tanzania

Mkuu sidhani kama ni kweli Mwinyi amefanya mengi kama aliyemfuatia.Jaribu kupeleleza utakubaliana nami.Pia sidhani Mwinyi anaweza kuwa amefanya mambo makuu zaidi ya Chifu Mkwawa,Au Nyerere au Magufuli.Mwinyi huenda akafaa nafasi nyingine lakini kwa hapo hajawafikia.Jaribu kuchunguza,Utakubaliana nami.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Mwinyi ndio raisi bora kabisa kuwahi kutokea katika nchi hii na ubora wake hautafutika hadi dunia inaisha maana waliomfuata wote wanaendelea na mfumo wa uchumi aliyo uacha Mwinyi yani CAPITAL RISIM hakuna aliyethubutu kurudi katika mfumo wa uchumi wa SOCIAL RISIM

Ila Mimi nilichogundua watu ambao hawajui Mwinyi alifanya nini katika nchi hii

1) Alikuwa hajazaliwa hivyo hajui tofauti ya maisha ya watanzania kabla Mwinyi hajawa raisi na baada ya Mwinyi kuwa raisi

2) Alikuwa anaishi kijijini maana mabadiriko ya kiuchumi ukiwa mjini especially Dar unayaona vizuri na unayaishi kila siku tofauti na mtu aliyeko kijijini

KWA UFUPI TU
Kipindi Mwinyi anakabidhiwa nchi Watanzania

1)walikua hawana nguo za kuvaa na viatu / akaleta nguo za mitumba na viatu

2)kulikua hakuna chakula yani unga wa mahindi, ngano na mchele / akafungua milango waganya biashara walete ndipo walipo ibuka kina Dewji na Bakharesa

3) kulikua hakuna mafuta ya taa na ilikua siku mkisikia yanakuja katika duka la mtaani kwenu mnakaa foleni kutwa nzima na chupa zenu mkononi / Mwinyi alienda Queite tazizo la mafuta likaisha kabisa

3) kulikua hakuna sukari alipaingia zikaanza kuja gali za ugawaji kila kata kwa wiki Mara moja gali likija mnakaa foleni na mgambo anakusimamieni na kuchukua mwisho kilo mbili nakumbuka zamu yetu ilikua J5 mwisho tatizo likaisha kabisa

4) kulikua hakuna viwanda na makampuni ya watu binafsi wakaruhusiwa kuanzisha

5) kulikua hakuna shule za private akaruhusu wenye uwezo wanzishe shule za private
Kabla ya shule za private ilikuwa mwanao akikosa nafasi za shule za serikali hata kama unayo pesa mwanao hawezi kusoma

6) kama mnaendesha vi private car sasa hivi basi mjue Mwinyi ndio aliyeruhusu vije

Sasa mlivyo mambumbu mnamsifia mkapa kwamba alikusanya kodi vizuri bira ya kujua kwamba hiyo miundombinu iliyomfanya Mkapa aweze kukusanya kodi Mwinyi ndio aliyeijenga

Binafsi nawaheshimu na nawakubali maraisi wote walifanya ambacho walitakiwa wafanye katika vipindi vyao ila Mwinyi ndio mbora wao sidhani kama kuna mtu anaweza kushangilia barabara na madaraja wakati akiwa hana basic need
 
Watu walioishi vipindi vyote vya utawala kama ss nawashangaa sana kutothamini juhudi za mzee Mwinyi .
Mzee Mwinyi alianza kuchafuliwa nyota na mtangulizi wake kwa kumdhihaki, kumponda na kumkejeli kwa kila alilolifanya iwe baya au zuri. Na kwa vile wengi walimuheshimu na kumuamini mtangulizi huyo basi yakajengeka mazoea na propaganda za kuonesha kuwa Mwinyi hakufanya kitu. Mabaya yote ya mtangulizi wake pamoja na yale machache ya kwake mwenyew Mwinyi( kama binadam) akabebeshwa Mwinyi, alafu yale yote mazuri aliyofanya/leta Mwinyi akapewa Mkapa ndio maana mleta mada anakwambia eti Mkapa ndio kafanya mambo makubwa zaidi ya Mwinyi na kwamba Mwinyi hakustahili kuwepo ktk list hii. Ukweli ni kwamba mtangulizi alitaka Mwinyi aongoze nchi kupitia mawazo yake yeye, kitu ambacho Mwinyi alikikataa. Mwinyi aliona kuongoza nchi kwa style ya mtangulizi wake huenda kungesababisha mapinduzi kama jinsi alivyotaka kupinduliwa huyo mtangulizi.
 
Tanzania imebahatika kuwa moja ya nchi iliyopata kuwa na viongozi bora kabisa Afrika na hata duniani kwa ujumla.Viongozi hao wamepata kuwa na mchango mkubwa Tanzania na hata kwa bara la Africa. Tunaona mifano ya Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambaye amepigania uhuru si kwa nchi ya Tanzania tu bali amekuwa na mchango mkubwa katika harakati za uhuru kwa nchi jirani kama Afrika Kusini, Zambia na Msumbiji.

Tanzania pia imepata kuwa na wanaharakati na wapigania uhuru mahiri walioweza kuitwaa nchi kutoka katika kucha za wakoloni. Tunaona wapigania uhuru na wanaharakati kama Kinjekitile Ngwale, Bwana Abushiri na Bibi Titi Mohammed. Viongozi kama Mtemi Isike, Chifu Mirambo, Mangi Meli na wengineo wengi ambao walikuwa viongozi wa kimila walikuwa mstari wa mbele katika mapambano ya uhuru na hatimaye kuikomboa na kutupatia Tanzania hii tunayoifurahia leo.

Bila kupoteza muda, Naomba niweke orodha fupi ya viongozi waliopata kuongoza Tanzania walioacha alama kubwa na historia ya kipekee kwa ubora wao na uwezo wao wa kiuongozi ambao pasi na shaka uliacha alama kubwa kwa watanzania.

Kwa sasa nitaweka orodha tu kwa kifupi ila nitarejea kuelezea kila mmoja kwa undani zaidi.Pamoja na kuongeza orodha mpaka kufikia kumi (10) Bora.

Viongozi watatu (3) bora kuwahi kuwepo Tanzania.

1. Mwl.Julius Kambarage Nyerere (Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
View attachment 1752017

2. Edward Moringe Sokoine ( Waziri Mkuu wa Tanzania 1977–1980 na 1983 - 1984)
View attachment 1752018

3. John Pombe Magufuli (Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
View attachment 1752024

Nyongeza;

4. Chief Mkwavinyika Munyigumba Mwamuyinga (Mkwawa) - Chifu wa kabila la Wahehe
View attachment 1752029


5. Benjamin William Mkapa (Rais wa Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
View attachment 1752030
Namba 4 tupa mbali haituhusu labda kama ulilenga hii thread isomwe na kabila fulani
 
Kama kigezo ni lazima tuchague kutoka hiyo list basi mimi ninao wawili tu

Mwalimu pamoja na Sokoine - Huyo number 3 mtoe hapo hastahili kuwepo !!

Mkwawa alikuwa kiongozi wa Wahehe, hakuwahi kuwa kiongozi wa kitaifa - yeye ataingia kwenye kinyanganyiro cha WATEMI hodari - tunao wengi tu kama kina Kijigitile, Mirambo, Isike, Lugusha nk
 
Mzee Mwinyi alianza kuchafuliwa nyota na mtangulizi wake kwa kumdhihaki, kumponda na kumkejeli kwa kila alilolifanya iwe baya au zuri. Na kwa vile wengi walimuheshimu na kumuamini mtangulizi huyo basi yakajengeka mazoea na propaganda za kuonesha kuwa Mwinyi hakufanya kitu. Mabaya yote ya mtangulizi wake pamoja na yale machache ya kwake mwenyew Mwinyi( kama binadam) akabebeshwa Mwinyi, alafu yale yote mazuri aliyofanya/leta Mwinyi akapewa Mkapa ndio maana mleta mada anakwambia eti Mkapa ndio kafanya mambo makubwa zaidi ya Mwinyi na kwamba Mwinyi hakustahili kuwepo ktk list hii. Ukweli ni kwamba mtangulizi alitaka Mwinyi aongoze nchi kupitia mawazo yake yeye, kitu ambacho Mwinyi alikikataa. Mwinyi aliona kuongoza nchi kwa style ya mtangulizi wake huenda kungesababisha mapinduzi kama jinsi alivyotaka kupinduliwa huyo mtangulizi.
Mkuu umemaliza kila kitu na naludia kusema 80% wanaomuona Mzee Mwinyi mbaya ni watoto/vijana waliozaliwa miaka ya tisini na kuendelea lakini kiukweli Mwinyi aliikuta Nchi hii ina hali mbaya kwelikweli
Nakumbuka mwaka1983 nilikoswakoswa kukamatwa na (JKT) kwa kosa la kuuza Dawa ya mbu(tena vipande vipande) kwa kuonekana mlanguzi vijana walikuwa wanakamatwa na kupigwa(mpaka wanajeruhiwa) kwa kosa kuuza sigara tu(SM,SPORTSMAN,EMBASSY au SIGARA KALI) alikuwa akikutwa na paketi mbili za hiyo bidhaa atakiona cha mtema kuni

Ninachokiona sasa ni nguvu kubwa inayotumika sasa kumsifu Magufuli hata kwenye mabaya na nguvu hiyo ndio imetumika sana kwa Nyerere kumsifu sana hata kwenye mabaya
 
Viongozi bora ambao hawakuwahi kuwa Marais

Oscar Kambona

Edward Sokoine

Salim Ahmed Salim

Mark Mwandosya
Nashangaa, huyo Salim Ahned Salim hatajwi tajwi, sijui kwa vile VIJANA WA LEO hawakushuhudia utumishi wake!?
Hata Nyerere alikuwa anamkubali sana, mpaka kufikia kupewa Uwaziri Mkuu. (Kwa vile ni Mzanzibari, sijui kama alistahili kuwa Waziri Mkuu wa JMT! )
 
Mwinyi ndio raisi bora kabisa kuwahi kutokea katika nchi hii na ubora wake hautafutika hadi dunia inaisha maana waliomfuata wote wanaendelea na mfumo wa uchumi aliyo uacha Mwinyi yani CAPITAL RISIM hakuna aliyethubutu kurudi katika mfumo wa uchumi wa SOCIAL RISIM

Ila Mimi nilichogundua watu ambao hawajui Mwinyi alifanya nini katika nchi hii

1) Alikuwa hajazaliwa hivyo hajui tofauti ya maisha ya watanzania kabla Mwinyi hajawa raisi na baada ya Mwinyi kuwa raisi

2) Alikuwa anaishi kijijini maana mabadiriko ya kiuchumi ukiwa mjini especially Dar unayaona vizuri na unayaishi kila siku tofauti na mtu aliyeko kijijini

KWA UFUPI TU
Kipindi Mwinyi anakabidhiwa nchi Watanzania

1)walikua hawana nguo za kuvaa na viatu / akaleta nguo za mitumba na viatu

2)kulikua hakuna chakula yani unga wa mahindi, ngano na mchele / akafungua milango waganya biashara walete ndipo walipo ibuka kina Dewji na Bakharesa

3) kulikua hakuna mafuta ya taa na ilikua siku mkisikia yanakuja katika duka la mtaani kwenu mnakaa foleni kutwa nzima na chupa zenu mkononi / Mwinyi alienda Queite tazizo la mafuta likaisha kabisa

3) kulikua hakuna sukari alipaingia zikaanza kuja gali za ugawaji kila kata kwa wiki Mara moja gali likija mnakaa foleni na mgambo anakusimamieni na kuchukua mwisho kilo mbili nakumbuka zamu yetu ilikua J5 mwisho tatizo likaisha kabisa

4) kulikua hakuna viwanda na makampuni ya watu binafsi wakaruhusiwa kuanzisha

5) kulikua hakuna shule za private akaruhusu wenye uwezo wanzishe shule za private
Kabla ya shule za private ilikuwa mwanao akikosa nafasi za shule za serikali hata kama unayo pesa mwanao hawezi kusoma

6) kama mnaendesha vi private car sasa hivi basi mjue Mwinyi ndio aliyeruhusu vije

Sasa mlivyo mambumbu mnamsifia mkapa kwamba alikusanya kodi vizuri bira ya kujua kwamba hiyo miundombinu iliyomfanya Mkapa aweze kukusanya kodi Mwinyi ndio aliyeijenga

Binafsi nawaheshimu na nawakubali maraisi wote walifanya ambacho walitakiwa wafanye katika vipindi vyao ila Mwinyi ndio mbora wao sidhani kama kuna mtu anaweza kushangilia barabara na madaraja wakati akiwa hana basic need
Ni kweli bro nakubaliana na wewe wale wasio jua nchi hii aliitoa wapi na akaifikisha wapi aidha walikuwa hawajazaliwa au walikuwa wanaishi kolomije

Hilo la foleni ya mafuta ya taa na sukari nalikumbuka vizuri sana maana kipindi hicho ndio nilikua katika umri wa kutumwa tumwa sukari

Siku ya kuja mafuta dukani Kwa mpemba zinapangwa chupa kuanzia dukani hadi mtaa wa pili mafuta yakisha fika Kila mtu anasimama ilipokua chupa yake
 
Hakuna cha 10 bora wala nini yote yanafanywa kumtafutiwa Jiwe room aonekane kwenye rank za juu!

Kwa matendo dhalimu aliyofanya jiwe hastahili hata kuwemo top 10! Taratibu mtazoea tu kuwa hatunaye tena na hatutakuja kupata kiongozi evil kama yeye!

Poleni sana MATAGA
Madhara ya kumpa Zito au Lisu akushikie akili ndio haya
 
Kaikosea hii 3 Bora, ilibidi iwe hivi

01. Nyerere
02. Mwinyi
03. Dr. JK
 
Mbona hukumuweka mzee Mwinyi ambae ametutoa katika hali ya kupiga mswaki na mkaa, kusimama juani kusubiri nusu kilo ya mchele tena mdundiko, kwenda harusini au kweny kasherehe na suruali iliyojaa viraka, chachacha kuwa ndio style ya viatu vya watoto wa mjini.

Nafikiri Mwinyi alistahili kuwa ktk list hii maana amefanya mengi ya maana ktk nchi hii, hata Mkapa kaja kakuta kila kitu kawekewa mezani na yeye akatelezea mle mle kama ganda la ndizi.

Kabla ya Mwinyi ilikuwa ukikutwa na dawa ya mswaki tu au sabuni ya kuogea basi asubuh mgambo wanakuja kuizunguka nyumba yako kwa kosa la kuhujumu uchumi wa nchi
Du!
 
Kwangu mini kama historia haikuwa manipulated Mzee Mwinyi ndio kiongozi bora wa muda wote nchi hii.

Aliikuta nchi kwenye depression kubwa lakini akaisongesha na hakuwa na ujivuni wala visasi na pengine ndio sababu Mungu amempa maisha marefu.

Mzee Mwinyi Mungu wangu ninayemwabudu katika Kristo Yesu akutunze akushibishe siku akujalie afya.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Mleta mada ni mzaliwa wa miaka ya 90 ukijumlisha na matango pori aliyolishwa huko alipoandikia uzi huu, ndio maana hakuweza kuuona mchango wa Mwinyi. Hapo ilitakiwa Mwinyi awe nafasi ya pili kwa vile ya kwanz siku zote huwa anapewa Nyerere. Mkapa angepokezwa kijiti na Nyerere huenda mpk miaka ya 2000 watu wangekuwa bado wanapiga miswaki ya miti, wanafulia majani ya mipapai, redio au taarifa ya habari watu wangekuwa bado wanaenda kusikiliza kwa mjumbe, chai ya mkono mmoja nk. Mkapa alikuwa na chembe chembe ya utawala wa Nyerere kwahiyo mengi ambayo angeyakuta kwa Nyerere na yeye angeyafanya yale yale au kwa lugha nyingine angetawala kwa style ile ile ya Nyerere. Ndo maana nasema Mkapa leo kuonekana amefanya mazuri ni kwa sababu alikuta Mwinyi ashamtengenezea na kumpa yeye amalizie vichache vilivyobaki
 
Nashangaa, huyo Salim Ahned Salim hatajwi tajwi, sijui kwa vile VIJANA WA LEO hawakushuhudia utumishi wake!?
Hata Nyerere alikuwa anamkubali sana, mpaka kufikia kupewa Uwaziri Mkuu. (Kwa vile ni Mzanzibari, sijui kama alistahili kuwa Waziri Mkuu wa JMT! )
Mkuu Je, Unadhani Salim Ahmed Salim alikuwa bora kuliko Sokoine?

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom