Viongozi wa SADC wasalimu amri wa Kagame! Wakubali kuondoa vikosi vyao CONGO DRC. Huu ni ushindi kwa Kagame na hatari kwa mataifa yanayomzunguka

Ye anapiga Combat ili kupiga picha! Mwenzake akipiga Combat yuko kazini kuwapa maarifa na morali askari wake.

We're fucked up!
Kunawatu hawajui nini maana ya uongozi. Unakuta mtu anasema Tanzania tuna jeshi bora afrika hivi unadhani kagame kasomea political science and administration ? Kuna vitu vinatokea vinaishushia hadhi jeshi sana. Mabasi ya jeshi kubeba madiwani au wajumbe wa CCM. Amiri mkuu wa majeshi ubaliambia jeshi lijiandae na uchaguzi are serious ?
 
Maamuzi ya SADC kusitisha misheni zake mashariki mwa DRC yamulikwa kwa kina

View: https://m.youtube.com/watch?v=tDZaTqwP9YkUmoja huo wa mataifa 16 ya SADC ulipeleka ujumbe wake huko Desemba 2023 kusaidia kupambana na uasi wa waasi wa M23.

Katibu wa Muungano wa Kitaifa wa Maveterani wa Jeshi la Ulinzi wa SA Bw. Pikkie Greeff, na mwandishi na mchambuzi wa Afrika Bw. Joseph Ochieno wanajadili hili kwa kina zaidi
 
Nchi za SADC wanajeshi wake dhaifu sana, hawa wanalopigania, nchi ile si yao.
 
Ye anapiga Combat ili kupiga picha! Mwenzake akipiga Combat yuko kazini kuwapa maarifa na morali askari wake.

We're fucked up!
Mkuu ukilamba asali tena utaanza kusifia kama kipindi cha DP W? Hii sudden change in perspective uliyomo saivi imesababishwa na nini?
 
Maono ya rais mstaafu Joseph Kabila yamezingatiwa

TOKA MAKTABA :

23 February 2025

View: https://m.youtube.com/watch?v=FEiyHSsFXjMDRC Crisis needs more than a military solution.

"Given the history of its member states, Sadc should know better.The grievances of the Congolese people against their government must be addressed"

-Joseph Kabila in the Sunday Times opinion column writes.
 
TOKA MAKTABA :

Jeshi imara la South Afrika tangu 2016 misheni zake Congo zimeshindwa pamoja na kuwa wana zana kali za kisasa :

View: https://m.youtube.com/watch?v=x6BYYyukjDIHii 𝘀𝘁𝗼𝗿𝘆 ilirushwa mara ya kwanza 𝟭𝟴 𝗦𝗲𝗽𝘁𝗲𝗺𝗯𝗲𝗿 𝟮𝟬𝟭𝟲.

Akisindikizwa na helikopta maarufu ya Rooivalk mfano wa ngome yenye ulinzi uliosheheni silaha kali , Carte Blanche anasafiri hadi kambi ya kijeshi iliyotekwa hivi majuzi ndani ya misitu ya tropiki kaskazini mwa Beni katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

John Webb anapata ruhusa ya kipekee kuvifikia vituo vya mstari wa mbele vya jeshi la South Africa SANDF katika eneo maarufu la liliopachikwa jina la kuogofya la Pembe Tatu ya Mauti (Triangle of Death) katika Mkoa wa Kivu Kaskazini tunapowatembelea wanajeshi wetu walio mstari wa mbele katika vita dhidi ya waasi wa ADF.

Tunakutana na wanajeshi ambao uMauti umeshindwa kuchukua roho zao katika uwanja wa vita na vile vile katika majukumu muhimu ya usaidizi wa mapigano, na marubani wa SANDF wanaofanya kazi kama sehemu ya kitengo cha anga cha Umoja wa Mataifa ambao wamekuza sifa ya ustadi na ujasiri wa kufika maeneo haraka kupambana na adui.

Carte Blanche pia anakutana na Jenerali wa SANDF Derrick Mgwebi ambaye aliteuliwa kuongoza operesheni ya jumla ya Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini DRC - ambayo bado ni Misheni kubwa zaidi ya kulinda amani duniani.

View: https://m.youtube.com/watch?v=x_SYts84EGM
 
Silaha hizo zote za majeshi ya SAMIRDC yaani SADC itabidi ziachiwe M23?
 
Hawa ndo wachambuzi sasa. Ona wanavvyosema kwa uwazi kuwa haijasemwa sababu ya msingi kwa nini wanatoa vikosi vyao. Wanasema kabisa Je mission imefeli? na kumbuka hii ni television ya Taifa ya South Africa.

Tanzania huku tuna Television ya Taifa ila huwezi sikia mijadala ya maana namna hii! Tuna waandishi @ Pascal Mayalla sijui kina Balile na Sammy Awami ila huwezi kuwasikia wakifanya mijadala ya maana kama hii.

Hili Taifa letu limeshakufa saivi tusubiri kuzikwa tu. Kwenye Historia ya JWTZ kwa mara ya kwanza tunafeli mission ya nje ya nchi baada ya miaka mingi kupita( Ikumbukwe mission ya kwanza tulifeli ni ile ya Liberia ambayo tuliondoa vikosi vyetu baada ya kuuliwa askari wetu).

Jeshi kuwa chawa wa wanasiasa na TISS kufeli kiintelejensia ndo matokeo ya tunayoyaona sasa. Badala ya kujikita kwenye weredi wa shughuli zao wamejikita kwenye kuwa matoy ya CCM na haya ndo matokeo yake.
 
Silaha hizo zote za majeshi ya SAMIRDC yaani SADC itabidi ziachiwe M23?
Na hawasemi tu. Hiyo Withdrawal ni moja ya masharti ya M23 na Kagame.

Kagame ndo alianza kuhoji kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Afrika Mashariki Kuwa majeshi ya SADC yanafanya nini Mashariki mwa Congo?

Statement ya Kagame ilifuatiwa na mfululizo wa demands za M23 kuwa vikosi vya SADC viondoke Congo. Demands hizi zikitolewa kwenye statements rasmi za M23.

Pia kuna taarifa zilienea sana kuwa Bikosi hivi vya SADC vilijuwa vimetekwa nyara na vkkosi vya M23 na Rwanda na walikuwa hawawezi kufanya lolote lile bila ruhusa ya hao watekaji wao huko Congo.

Kuondolewa kwa hivi vikosi ni ushindi kwa Kagame na ushindi mkubwa kwa kikundi chake cha M23.

Pia kuondolewa kwa vikosi hivi ni ujumbe rasmi kuwa huku Afrika hatuna strong and smart leadership. Viongozi wa huku hawajui maana ya Uongozi na maana ya nafasi zao kama Viongozi. Wamejikita katika kutumia majeshi yao na intelligence zao katika kujisimika kwenye madaraka ila sio kwa faida ya watu wao na nchi zao.
 
Kagame na Museven don't joke. Wanajua mission zao na wako serious kwenye kuzifanikisha. Wao wana ndoto ya kuyatengeneza Mataifa yao kuwa imara kijeshi na kiuchumi ili kutawala Afrika. Na wanatimiza kweli ndoto hizo.

Kagame alijua SADC hakuna strong leadership kuwa wapambania madaraka tu pale alipoombwa ba Ufaransa kwenda Kaskazini mwa Msumbiji kupatuliza.

Na alituma vikosi vyake kweli na akapatuliza wakati SADC walishindwa kufanya hayo.

Kagame anaijua sana SADC na anajua vyama vya ukombozi wa Afrika ambavyo vingi ndo vinatawala nchi za SADC vimeishiwa think tanks wa kuongoza vizuri kwenye karne hii ya Ushindani, Sayansi na Teknolojia na kujikitq katika ku politicise majeshi yao na intelligence agencies zao ili viwasaidie kuendelea kubaki madarakani.



Kagame anajua hizi nchi za SADC hasa zinazoongozwa na vyama vya ukombozi nyingi ziko kwenye blink of collapse kutokana na kutojikita kwenye kujijenga vizuri ki intelligensia na kijeshi. Hivyo aliset vizuri mission yake ya kuingia Congo.


Haya ndo matokeo tunayoyaona sasa.
 
Sasa wewe unataka liendelee kukaa ili iweje,ilihali Trump & Elon Musk wamisha sema watawalinda Kongo kwa mabadilishano na madini???.
 
Mkuu sio issue uimara wa majeshi ya SADC,Hapo ni issue ya economic war.Anayeleta matatizo yote Congo ni Rwanda kwa kupitia mataifa ya USA & UE.sasa USA amerudi kwa upande wa 2 kujifanya mtakatifu kutaka kumsaidia Congo-sasa ww unataka majeshi ya SADC yaendelee kuwepo ili iweje???
 
Akina Mnagangwa walipata Nchi wakiwa na Mugabe kwa njia hizo hizo za M23, Rwanda walipata nChi kwa njia hizo hizo za M23.
Iganda M7 na wenzake walipata Nchi kwa njia jizo hizo za M23.

Nini kipya ambacho wangekuja nacho?
 
Kwanza majeshi ya SADC yameruhusu vipi Loophole ya Trump kuja?
 
Simila Case ya Mobutu versus Patrice Lumumba.
 
Jeshi limekuwa jepesi sana. Acha Kagame awafundishe nini maana ya Jeshi imara.
Mzee kwa sasa sio muda mzuri sana wa kuonyesha ubabe..uchaguzi unakuja na huwezi jua what was next. Africa nzima inatokota moto kuanzia Ethiopia mpaka South Africa
 
Mzee kwa sasa sio muda mzuri sana wa kuonyesha ubabe..uchaguzi unakuja na huwezi jua what was next. Africa nzima inatokota moto kuanzia Ethiopia mpaka South Africa
Uchaguzi ndo nini? Kama mna mifumo mizuri ya kidemokrasia mnahofia nini?

Kwa Taifa lenye akili na maarifa uchaguzi unazuia shughuli za masingi kufanyika?
 
Rwanda na Uganda wanavyopigana hawana concerns za kiuchumi? Ni nyie tu mlio na concerns za kiuchumi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…