Viongozi wa Simba Hongereni sana kwa kucheza hili vizuri, Ila Bodi mmejaa Vibaya sana


Hilo la mechi kutokuchezwa kabisa sidhani, itashangaza likitokea.

Kutegemeana na kukamilika kwa uchunguzi wa hayo matukio yaliyoletwa na afisa usalama wa michezo ambayo hayajawekwa wazi, ni either:
1. Mechi kurudiwa
2. Simba kunyang'anywa point 3 na faini au vyote
3. Yanga kunyang'anywa point 3 na faini au vyote

Kinyume na hapo bodi ya ligi itakuwa imejiacha utupu mno.
 
Ukiona maamuzi yanachukua muda mrefu kutolewa, niamini mimi nikikwambia watakuwa wanasoma upepo wa ligi.

Sioni Yanga au Simba akipewa point za mezani hasa kwa sababu bodi yenyewe iliahirisha mechi yenyewe baada ya malalamiko ya Simba.

Kama watafanya maamuzi ya kuipa point 3 timu moja wapo basi watafanya hivyo pale watakapoona maamuzi hayo hayaendi kuathiri msimamo wa timu ipi inayoenda kuchukua ubingwa.

Kama watafanya maamuzi ya mechi kurudiwa ni pale itakapoonekana Simba na Yanga wanaendelea kupishana point 1 au 2 na hivyo mechi hiyo inaweza kuamua bingwa na timu itakayokuwa nyuma itaidai na kuitaka hiyo mechi.

Kulingana na msimamo wa ligi utakavyoendelea kuwa, sitashangaa ligi kuisha bila mechi hiyo kufanyika na timu zote mbili kuridhika.
 
Mkuu, kuna jambo tunamiss. Bodi hawawezi zuia mechi sababu Simba hajafanya mazoezi tu. Kanuni zinakataa.Kuna mambo hayajawekwa wazi.

Simba si wajinga kususia mechi sababu ya mazoezi wakijua kanuni haziwabebi, lazima kuna matukio yametokea ambayo wanajua ikianza kesi watayatumia kujilinda na hii nchi ukikaa vibaya kiongozi unaweza tengwa na taaisi ukatupiwa msala wewe kama wewe hivyo hakuna kichaa wa kujitoa ufahamu.

Kuna sababu zinazowekwa mbele na kuna sababu halisi zilizo nyuma ya pazia.

Ukumbuke, hapa huongelei maslahi ya Simba na Yanga tu, kuna third parties wanaosubiri hatma ya maamuzi, na wana haki ya kudai fidia kutegemeana na maamuzi.

Assume hakuna mechi, unakuja na taarifa gani inayojitosheleza kuhalalisha hilo bila kuwajibishana?
 
Huu mzigo ambao tff na bodi ya ligi wameuchukua kutoka Simba watajua wanaenda kuutua wapi. Hapa inatakiwa wandae ushahidi wa kutosha kwann waliahirisha mechi.
Huo ushahidi wa kuutoa wapi sasa wakati wao ndio wenye mamlaka?
 
Nakubaliana na wewe kabisa. Mimi nilichofanya ni kufanya kautabiri tu ka maamuzi yanayoweza kuja kuchukuliwa based on jinsi ninavyojua siasa zetu za mpira zilivyo.

Ukiingiza ishu za fidia jambo linakuwa complicated zaidi.
 
Nakubaliana na wewe kabisa. Mimi nilichofanya ni kufanya kautabiri tu ka maamuzi yanayoweza kuja kuchukuliwa based on jinsi ninavyojua siasa zetu za mpira zilivyo.

Ukiingiza ishu za fidia jambo linakuwa complicated zaidi.
Kabisa mkuu, hapa hatuongelei mechi ya namungo vs kagera yenye thamani chini ya M30.

Pima thamani ya mechi halafu uone kama kuifuta isitokee tena kwa sababu ya mazoezi tu ni jambo jepesi.
 
Kabisa mkuu, hapa hatuongelei mechi ya namungo vs kagera yenye thamani chini ya M30.

Pima thamani ya mechi halafu uone kama kuifuta isitokee tena kwa sababu ya mazoezi tu ni jambo jepesi.
Ila pia sioni taasisi inayoweza kuamua kukomaa na mambo ya fidia. Hawa Azam, NBC, CRDB, nk. wote ni wadau wasiotaka kujiingiza kwenye migogoro ya kisheria na hizi timu. Tukiongelea vikampuni vidogovidogo ambavyo vimepewa vizabuni vya hapa na pale navyo sioni vikiamua kutunisha msuli, labda kama kuna watu waamue kusimama nyuma yao. Mashabiki hawa wa kudai fidia za 10K sijui 100K ndiyo kabisa hawana ubavu huo.

Fikiria ni kesi ngapi za madai zinazohusu hizi timu zinakufa juu kwa juu kabla hazijafika mbali?
 
Reactions: Tsh
Simba haiwezi kunyang'anywa points 3 kwa sababu hajatekeleza kusudio la kugoma kwa vile mechi imeahirishwa,Yanga pia hawezi kunyang'anywa points 3 labda agome kucheza kwenye tarehe itakayopangwa.Bodi ya ligi wajanja,wametunga kanuni (ya 34:2(1.3) inayowapa haki ya kuahirisha mechi ikiona inafaa.Hapo Yanga hawana ujanja.
 

Attachments

  • Screenshot_20250309-213158.png
    251.2 KB · Views: 1
Reactions: Tsh
Kwaiyo chanzo cha sakata zima ni simba kuogoa kucheza na yanga?
 
Simba mnavyotetea maamuzi ya TFF kama vile mechi ikiahirishwa mna uhakika wa kushinda
 
Labda kama hili tukio lina baraka za serikali kwa maslahi ya kisiasa kinyume na hapo viongozi ndo wana hilo balaa.

Sikia boss, Ukiona kuna pesa zimewekezwa sehemu, halafu pakatokea maamuzi yaliyoleta hasara na watu wakanyamaza uje mzee wa boma serikali kuu au mwanasiasa mwenye nguvu ana jambo lake hapo, kinyume na hapo lazima kesi zianze watu wapate pesa za kuendesha kesi.
 
Upo sawa boss.
 
Hatupeleki timu. Madunduka yakipewa ushindi tutaenda kuudai CAS.
Safari hii tuko tayari kuuza ng'ombe kwa kesi ya kuku.
Tutatafuta hata wanasheria wa kimataifa.
Harambee ya buku buku itaanzishwa kwa wapenzi na wanachama.
Hersi anataka ubunge hawezi kubishia au kugomea huo mchezo na mind you mgeni rasmi atawekwa kimkakati hachomoi
 
Bodi ya Ligi ya Tanzania haina weledi ni saws na sanamu, (figure heads), Simba wanajua vizuri Bodi ya Ligi, Simba kama taasisi hawakuwa makini
 
Huu mzigo ambao tff na bodi ya ligi wameuchukua kutoka Simba watajua wanaenda kuutua wapi. Hapa inatakiwa wandae ushahidi wa kutosha kwann waliahirisha mechi.
Watasema kulikouwa na viashiria vya uvunjifu wa amani kutokana na makomandoo wa Yanga kuifanyia fujo Simba na hata barua yao ya kuahirisha mechi kuna para ilieleza kuwa kutokana maelezo ya afisa usalama wa mechi amabaye alikuwepo kwenye tukio hilo, yote kwa yote hili fupa gumu sana labda walete wale fisi wenye madoa meupe toka hifadhi ya Katavi walioandaliwa kumla Sativa hadi fuvu la kichwa kufuta ushahidi.
 
Ila hii kesi itakuwa ngumu pale bodi ya ligi ikiamua kuwapa Yanga point 3 halafu Simba wanaenda CAS wanatoa ushahidi wa mechi kuahirishwa.
 
Ila hii kesi itakuwa ngumu pale bodi ya ligi ikiamua kuwapa Yanga point 3 halafu Simba wanaenda CAS wanatoa ushahidi wa mechi kuahirishwa.
Yaani hi kimakonde tunasema ukichimama nchale na ukikaa nchale na uchiteme wala wala uchimumunye hadi kwa jumbe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…