Viongozi Wote Walio Karibu au Wana Uwezo wa Kumfikia Rais

Viongozi Wote Walio Karibu au Wana Uwezo wa Kumfikia Rais

Kalamu

Platinum Member
Joined
Nov 26, 2006
Posts
12,096
Reaction score
15,393
Wanao wajibu wa kumweleza rais ukweli wanavyouona wao kwa msukumo wa uzalendo wao kwa nchi yao.

Maswala mazito, kama hili la Bandari yanapotokea nchini na kuwa na mwonekano wa kuwagawa wananchi katika makundi yanayovutanai, siyo mambo ya kunyamazia, hasa kwa viongozi wa ngazi za juu mbalimbali waliomo serikalini na ndani ya chama cha Mapinduzi.

Kwa bahati mbaya katika nchi yetu hatunayo mifano mingi ya aina ya watu wa namna hii, lakini tunaweza kumtaja Oscar Kambona, na pengine hata Abood Jumbe kama mifano husika.

Inaeleweka, siyo jambo sahihi kwa viongozi hawa kujitokeza hovyo hovyo mbele za wananchi na kuanza kuropoka hovyo kuhusu misimamo yao katika jambo linalojadiliwa.

Lakini kamwe, hapawezi kukosekana njia za kumfikia kiongozi wao mkuu na kujadili naye dukuduku zao kuhusu wanayoyaona wao katika jamii kuhusu mwelekeo wa jambo hilo linapoonekana kuleta mtafaruku ndani ya nchi.

Kwa hiyo, viongozi hawa, wanao wajibu mkubwa, kwanza kwa kiongozi wao, lakini hasa hasa kwa wananchi kuwa wawazi kabisa juu ya hali wanavyoiona wao, na kueleza msimamo wao juu ya swala husika.

Wakishajieleza kwa huyu kiongozi wao, na bado maoni yao yakawa hayatiliwi maanani, lakini dhamira zao zikiwa bado ni hasi juu ya jambo zima linavyofanyika; ni wajibu wa hawa viongozi kujitokeza mbele na kujieleza waonavyo wao. Huu ni wajibu wao kwa wananchi na kwa taifa lao.

Sasa mimi ninajiuliza baada ya kufikia hapa tulipofika na hii Bandari, huku serikali wakisema wananchi hawana elimu; na hao wanaotoa elimu wakizidi kuonekana kama vioja, je hawa viongozi wetu ambao dhamira zao zinawasuta juu ya jambo hili wao watafanya nini? Kunyamaza kimya ndilo suluhisho na salama kwao?

Kamwe siamini kuwa hakuna watu wa aina hiyo katika ngazi mbali mbali serikalini na ndani ya chama.

Watakaa kimya wakiwa na matumaini kwamba jambo lenyewe litalazimishwa kwa nguvu za dola na liwalo na liwe?

Inanibidi nitoe angalau mfano mmoja, hata kama sijui huyu mtu anasimamia wapi katika swala zima la Bandari..

Huyu "Profesa aliyeokotwa Jalalani" kwa namna alivyojipambanua wakati wa Magufuli, ni vigumu sana kuamini kwamba sasa hivi kabadilika na kuunga mkono hatua hizi zilizochukuliwa hadi kuwepo na makubaliano ya Tanzania na Dubai kuhusu bandari zetu chini ya masharti yaliyomo ndani ya IGA.

Ni vigumu pia kuamini kwamba, yeye, kama mshauri wa Rais wa sasa, kama inavyofahamika, kwamba hakuwa na ushiriki, au ufahamu wowote juu ya jambo hili. Na kama hakuwa na ufahamu wowote hadi lilipojitokeza mbele za wananchi, hali hiyo yeye ataiona vipi, kama mshauri?

Huyu Profesa analo lipi tena la kupoteza katika maisha yake kwa hapo alipofikia, kiasi kwamba aogope hata kule kutamka tu lolote analoona ni kwa msukumo wa uzalendo kwa nchi yake! Bado anasubiri kuteuliwa kuwa waziri?

Nimetumia mfano wa Profesa Kabudi, lakini ipo mifano mingi sana ya viongozi hawa wanaoonekana kutoweka uzalendo wao mbele, kuitetea nchi yao dhidi ya kitu kingine chochote kwa ubinafsi wao pekee.

Nitawataja tu akina Majaliwa (Kassim); akina Lukuvi; Mawaziri mbalimbali, wabunge, n.k..

Huko kwenye chama nasikitika sina hata mmoja wa kumpa heshima ya kumtaja hapa.
Naona ni kama wote ni watumishi wa Mwenyekiti tu, wasiokuwa na utashi wowote juu ya jambo lolote.

Inasikitisha sana.
 
JamiiForums-787880945.jpg
 
tukubali tu, mwanamke hawezi kuwa Rais, hivi mnaona kuna nini kinaendelea pale, semeni tu ukweli.
Mkuu 'chapwa24', sijui/sielewi ulicho andika hapa, kama ni kumhusu yeye mwenyewe Samia Suluhu, kama mwanamke asiyekuwa na uwezo wa kuwa rais, au maana yako ni kuwa wanawake wote kwa jinsia yao hawawezi kuwa marais?

Kama maana yako ni hii ya pili, kamwe siwezi kukubaliana nawe. Kuna mifano ya wanawake walioweza kabisa kuongoza nchi zao vizuri; hata wakati nchi hizo zilipoingia kwenye misukosuko waliendelea kuwa imara.

Kwa hiyo, kama unamzungumzia Samia Suluhu, kutokuwa na uwezo wa kuwa rais, mzungumzie yeye kama yeye, na wala siyo kwa sababu ya jinsia yake.

Hata hivyo, maana ya kuwa rais si kwamba anafanya kazi zote yeye na maamuzi yote huyo huyo. Ndiyo maana kuna wasaidizi wengi kila eneo la serikali wenye uwezo wa maeneo yao.
Kuwa na uwezo wa kuongoza ni pamoja na kujua namna nzuri ya kuwatumia hawa wasaidizi, ili kiongozi aweze kufikia maamuzi mazuri.

Sasa, kama rais mwenyewe anakuwa na wasaidizi na inakuwa ni yeye anawaburuza wasaidizi hao, huku wakiogopa kumshauri waonavyo wao juu ya maamuzi yake, hapo ndipo panakuwa na chimbuko la mada hii. Hawa wasaidizi wanapaswa kumweleza kiongozi wao, bila ya hofu, na kama akiendelea kukaidi ushauri wao, ni muhimu wasaidizi hawa wajieleze kwa wananchi kulinda uzalendo kwa nchi yao.
 
Wanao wajibu wa kumweleza rais ukweli wanavyouona wao kwa msukumo wa uzalendo wao kwa nchi yao.

Maswala mazito, kama hili la Bandari yanapotokea nchini na kuwa na mwonekano wa kuwagawa wananchi katika makundi yanayovutanai, siyo mambo ya kunyamazia, hasa kwa viongozi wa ngazi za juu mbalimbali waliomo serikalini na a Mwenyekiti tu, wasiokuwa na utashi wowote juu ya jambo lolote.

Inasikitisha sana.
Huyu amefanya hivyo makusudi ili watanganyika tuvunje muungano kwa nguvu.
 
Kubadili au kufuta mkataba FAKE na BATILI ni jambo moja.

Kurudisha Mzigo ni jambo jingine!!!
Kwa nini wasijijue wenyewe waliobeba mzigo, kuliko kuitumbukiza nchi kwenye matatizo?
 
Mkuu 'chapwa24', sijui/sielewi ulicho andika hapa, kama ni kumhusu yeye mwenyewe Samia Suluhu, kama mwanamke asiyekuwa na uwezo wa kuwa rais, au maana yako ni kuwa wanawake wote kwa jinsia yao hawawezi kuwa marais?

a hofu, na kama akiendelea kukaidi ushauri wao, ni muhimu wasaidizi hawa wajieleze kwa wananchi kulinda uzalendo kwa nchi yao.
Angalia Elen Jonson wa Liberia, nguli aliyefanya kazi world bank miaka ya kutosha, anayejua uchumi, ni kitu gani amekifanya LIberia baada ya kukabidhiwa nchi? Mungu mwenyewe hakuwaumba hawa wawe marais. simple and clear.
 
angalia Elen Jonson wa Liberia, nguli aliyefanya kazi world bank miaka ya kutosha, anayejua uchumi, ni kitu gani amekifanya LIberia baada ya kukabidhiwa nchi? Mungu mwenyewe hakuwaumba hawa wawe marais. simple and clear.
Lakini hujamtaja Angela Merkel wa Ugerumani, Magreth Thatcher au Indira Gandi, wala Golder Meir wa Israel, au kwa kuwa hawa hawakuwa wanatokea Afrika?

Mpe kazi hapa huyu waziri wa Mambo ya nje uone kazi itakavyofanyika.
 
Lakini hujamtaja Angela Merkel wa Ugerumani, Magreth Thatcher au Indira Gandi, wala Golder Meir wa Israel, au kwa kuwa hawa hawakuwa wanatokea Afrika?

Mpe kazi hapa huyu waziri wa Mambo ya nje uone kazi itakavyofanyika.
huyo ndo hamna kitu kabisa. nchi za ulaya watawala hata wawe wanawake, sio wao huwa wanatawala, ila katiba zao na sheria na raia ndio wanatawala. ila nchi za africa zinahitaji mwanaume atawale, huu ni ukweli usiopingika. na 2025 watanzania changamkeni, acheni kuzubaa.
 
huyo ndo hamna kitu kabisa. nchi za ulaya watawala hata wawe wanawake, sio wao huwa wanatawala, ila katiba zao na sheria na raia ndio wanatawala. ila nchi za africa zinahitaji mwanaume atawale, huu ni ukweli usiopingika. na 2025 watanzania changamkeni, acheni kuzubaa.
Duh!

Kumbe? Haya nieleze hawa "wanaume" walikokwisha tufikisha. Tumesogelea karibu na Ulaya?

India ni ulaya, eti!

Hii 'argument' yako haina mashiko yoyote.
 
Duh!

Kumbe? Haya nieleze hawa "wanaume" walikokwisha tufikisha. Tumesogelea karibu na Ulaya?

Hii 'argument' yako haina mashiko yoyote.
wewe nahisi utakuwa sio mwenzetu. au unavaa sketi mbona unaongea kama huna marinda? kwenda huko.
 
wewe nahisi utakuwa sio mwenzetu. au unavaa sketi mbona unaongea kama huna marinda? kwenda huko.
Sikiliza.
Huwa svumilii ujinga ujinga hapa.
Kama ndio kwanza unabalehe, na hali hiyo mpya inakupa matatizo kichwani mwako, basi chunga sana unapojadili kitu nami. Sina uvumilivu kabisa na uchizi.

Umeelewa?
 
Wanao wajibu wa kumweleza rais ukweli wanavyouona wao kwa msukumo wa uzalendo wao kwa nchi yao.

Maswala mazito, kama hili la Bandari yanapotokea nchini na kuwa na mwonekano wa kuwagawa wananchi katika makundi yanayovutanai, siyo mambo ya kunyamazia, hasa kwa viongozi wa ngazi za juu mbalimbali waliomo serikalini na ndani ya chama cha Mapinduzi.

Kwa bahati mbaya katika nchi yetu hatunayo mifano mingi ya aina ya watu wa namna hii, lakini tunaweza kumtaja Oscar Kambona, na pengine hata Abood Jumbe kama mifano husika.

Inaeleweka, siyo jambo sahihi kwa viongozi hawa kujitokeza hovyo hovyo mbele za wananchi na kuanza kuropoka hovyo kuhusu misimamo yao katika jambo linalojadiliwa.

Lakini kamwe, hapawezi kukosekana njia za kumfikia kiongozi wao mkuu na kujadili naye dukuduku zao kuhusu wanayoyaona wao katika jamii kuhusu mwelekeo wa jambo hilo linapoonekana kuleta mtafaruku ndani ya nchi.

Kwa hiyo, viongozi hawa, wanao wajibu mkubwa, kwanza kwa kiongozi wao, lakini hasa hasa kwa wananchi kuwa wawazi kabisa juu ya hali wanavyoiona wao, na kueleza msimamo wao juu ya swala husika.

Wakishajieleza kwa huyu kiongozi wao, na bado maoni yao yakawa hayatiliwi maanani, lakini dhamira zao zikiwa bado ni hasi juu ya jambo zima linavyofanyika; ni wajibu wa hawa viongozi kujitokeza mbele na kujieleza waonavyo wao. Huu ni wajibu wao kwa wananchi na kwa taifa lao.

Sasa mimi ninajiuliza baada ya kufikia hapa tulipofika na hii Bandari, huku serikali wakisema wananchi hawana elimu; na hao wanaotoa elimu wakizidi kuonekana kama vioja, je hawa viongozi wetu ambao dhamira zao zinawasuta juu ya jambo hili wao watafanya nini? Kunyamaza kimya ndilo suluhisho na salama kwao?

Kamwe siamini kuwa hakuna watu wa aina hiyo katika ngazi mbali mbali serikalini na ndani ya chama.

Watakaa kimya wakiwa na matumaini kwamba jambo lenyewe litalazimishwa kwa nguvu za dola na liwalo na liwe?

Inanibidi nitoe angalau mfano mmoja, hata kama sijui huyu mtu anasimamia wapi katika swala zima la Bandari..

Huyu "Profesa aliyeokotwa Jalalani" kwa namna alivyojipambanua wakati wa Magufuli, ni vigumu sana kuamini kwamba sasa hivi kabadilika na kuunga mkono hatua hizi zilizochukuliwa hadi kuwepo na makubaliano ya Tanzania na Dubai kuhusu bandari zetu chini ya masharti yaliyomo ndani ya IGA.

Ni vigumu pia kuamini kwamba, yeye, kama mshauri wa Rais wa sasa, kama inavyofahamika, kwamba hakuwa na ushiriki, au ufahamu wowote juu ya jambo hili. Na kama hakuwa na ufahamu wowote hadi lilipojitokeza mbele za wananchi, hali hiyo yeye ataiona vipi, kama mshauri?

Huyu Profesa analo lipi tena la kupoteza katika maisha yake kwa hapo alipofikia, kiasi kwamba aogope hata kule kutamka tu lolote analoona ni kwa msukumo wa uzalendo kwa nchi yake! Bado anasubiri kuteuliwa kuwa waziri?

Nimetumia mfano wa Profesa Kabudi, lakini ipo mifano mingi sana ya viongozi hawa wanaoonekana kutoweka uzalendo wao mbele, kuitetea nchi yao dhidi ya kitu kingine chochote kwa ubinafsi wao pekee.

Nitawataja tu akina Majaliwa (Kassim); akina Lukuvi; Mawaziri mbalimbali, wabunge, n.k..

Huko kwenye chama nasikitika sina hata mmoja wa kumpa heshima ya kumtaja hapa.
Naona ni kama wote ni watumishi wa Mwenyekiti tu, wasiokuwa na utashi wowote juu ya jambo lolote.

Inasikitisha sana.
Swali fikirishi hivi kiti cha spika kikipwaya nini hufanyika
 
Swali fikirishi hivi kiti cha spika kikipwaya nini hufanyika
wabunge wanazo taratibu za kumwajibisha spika mbovu, ikiwa ni pamoja na kumwondoa madarakani.

Lakini kwa bahati mbaya sana, siyo kwa bunge kama hili tulilonalo sasa hivi.
 
wabunge wanazo taratibu za kumwajibisha spika mbovu, ikiwa ni pamoja na kumwondoa madarakani.

Lakini kwa bahati mbaya sana, siyo kwa bunge kama hili tulilonalo sasa hivi.
Nimekuwa namsikiliza matamshi yake mengine duu mpaka nimejifunza mengi kuhusu hawa tunao wapa dhamana
 
Huyu amefanya hivyo makusudi ili watanganyika tuvunje muungano kwa nguvu.
Kusema kweli ni vigumu kukataa haya uliyoandika hapa, kwani hata mengi mengine anayofanya mbali ya hili la Bandari ni kama hilo ndilo lengo mahsusi analotegemea litokee.

Lakini nadhani watu makini tayari wamekwishamstukia, kwa hiyo hatafanikiwa kuuvunja muungano kamwe.
 
Back
Top Bottom