Viongozi Wote Walio Karibu au Wana Uwezo wa Kumfikia Rais

Don't be the first to say the Queen is naked!
Mfalme hapingwi Afrika!
 
Duh!

Kumbe? Haya nieleze hawa "wanaume" walikokwisha tufikisha. Tumesogelea karibu na Ulaya?

India ni ulaya, eti!

Hii 'argument' yako haina mashiko yoyote.
Acha ubishi Samia is an incompetent President!
 
na kama akiendelea kukaidi ushauri wao, ni muhimu wasaidizi hawa wajieleze kwa wananchi kulinda uzalendo kwa nchi yao.
Mkuu wamwambie nini na wao wanalinda ugali wao na matumbo yao? Sana sana wataogopa kupoteza vibarua vyao km ikionekana wana mawazo tofauti na yeye, wazungu wanasema 'never outshine your Master'
✍️
 
Acha ubishi Samia is an incompetent President!
Ona na wewe, unarukia tu jambo usilojua limeanzia wapi?
Umesoma wapi nilipoanadika kuwa Samia ni rais bora. Nionyeshe sasa hivi nilipoandika kwenya mada hii kuwa Samia ni rais "compitent".
Hizi bangi zinawaharibu vichwa vyenu kwelikweli.
 
Mkuu wamwambie nini na wao wanalinda ugali wao na matumbo yao? Sana sana wataogopa kupoteza vibarua vyao km ikionekana wana mawazo tofauti na yeye, wazungu wanasema 'never outshine your Master'
✍️
Nafahamu hili ndilo tatizo kubwa sana kwa hawa tunaowaita "viongozi" sifa ambayo hawaistahili kabisa.

Kuna mambo ambayo hawatakiwi kuwa na msimamo tofauti na ule uliofikiwa katika maamuza ya pamoja, kichama, au ndani ya serikali katika Baraza la Mawaziri.

Katika ngazi ya vikao hivyo huko kwenye chama au serkalini ndiko kunakotakiwa kuwa na mijadala moto moto sana ndani kwa ndani, hadi wanafikia maelewano ya pamoja, ambalo wote kwa ujumla wao wanakuwa pamoja kulitetea.

Lakini inavyoonekana nyakati hizi, hata vikao hivi havifanyi majadiliano ya aina hii. Mara nyingi ni uamzi tu aliokwishafanya mwenyekiti wao/rais na kuja kuwafikishia taarifa tu hawa wajumbe bila ya kushirikishwa na bila ya mjadala wa maana wa kufanya maamuzi juu ya jambo husika.

Huu mkataba wa Bandari ni mfano halisi wa haya ninayoeleza hapa, la sivyo kusingekuwepo na kelele nyingi kiasi hiki

Ni katika hali ya namna hii ndipo washauri wa kweli wa rais, wanaotumwa na uzalendo wa nchi yao wanapopaswa kumweleza kiongozi huyo misimamo yao, bila kujali hayo maslahi yao binafsi. Uzalendo una thawabu kubwa zaidi kuliko maslahi binafsi haya yanayowalaza akili hawa watu.
Watu hujitoa mhanga kufia nchi yao, kama vitani, bila kujali maslahi yao binafsi, itakuwa kucha kazi, ambayo pengine itapatikana nyingine nzuri zaidi na maisha kuendelea mbele?

Mbona Edwin Mtei aliacha Ugavana wa Benki, na maisha yakaendelea mbele!
 
" ... Wananchi hawana elimu, na wanaozidi kutoa hiyo elimu wakionekana vioja"

Hiyo caught hapo juu inaonesha vile tunachezewa na wajinga, wanaotudanganya hatuna tunalofahamu kuhusu ule mkataba wa hovyo, lakini kumbe, hao wanaotuambia hatufahamu kitu, wao ndio wajinga kabisa.

Hapo ndipo tunapoamua kwamba, hatuna sababu tena kuendelea kuwasikiliza hao wajinga, ambao baada ya kuona hatuelewi ujinga wao, wakaja na ujinga mwingine wa udini, nao tukaupuuza, sasa nao kama wanataka kuja na ujinga wa kumlaumu Nyerere kwa kila jambo, huu nao wakijaribu ndio utapuuzwa vibaya kabisa.

Vyema watambue tu, hili sasa sio taifa la wajinga walilozoea, hili ni taifa la watanganyika tofauti, werevu, wenye uwezo wa kuhoji, na kuhitaji majibu ya msingi sio vioja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…